Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

ILIPOISHIA:
Mage hakutaka kuuliza swali lingine alinyanyuka na kutoka kuelekea kwa mama Colin kutaka kujua sababu ya safari yake ya Afrika ya Kusini na kwa sababu gani hakurudi na Colin. Alitoka hadi kwenye gari na kuchukua aina ya Toyota Harrier na kuelekea kwa mama Colin, aliendesha kwa kasi ili kuwahi kupata taarifa.
SASA ENDELEA...



Alipofika alipaki gari kwenye maegesho, kwa shauku ya kuyajua ya Afrika Kusini hakufunga hata mlango wa gari. Alitembea mwendo wa haraka hadi mlango wa kuingia ndani. Alibisha hodi na kukaribishwa na mama Colin aliyekuwa amekaa na mama Cecy wakiangalia mkanda wa video huku wakinywa vinywaji.
“Karibu ma mkwe,” mama Colin alisema.
“A..a..sa..”


Alishindwa kumalizia sentesi ambayo ilikatikia njiani baada ya jicho lake kutua kwenye kioo cha runinga alichokiona mbele yake.
Alimuona Cecy katika vazi la harusi akiwa na Colin katika suti ya gharama, alikaza macho kama yanataka kudondoka.


“Maa..a..ma.”
“Vipi mkwe?”
“Huyu si Colin?” alisema huku akinyoosha kidole.
“Ndiyo.”
“Na..na..huyu si Cecy?”
“Ndiyo.”
“Hii si..si..harusi?”
“Ndiyo.”


“Wameoana lini?”
“Leo ni siku ya nne toka waoane na sisi tumerudi jana usiku kutoka huko.”
“Mmh! Si kweli, haya ni maigizo tu ili kuniumiza roho.”
“Kukuumiza roho ili iweje? Na picha zao hizi hapa.”


Mage alizichukua albamu akiwa haamini anachoambiwa, aliifungua na kuanza kuangalia picha mojamoja huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio. Kila ukurasa alioufunua uliupasua moyo wake alijikuta machozi yamefunika macho na kushindwa kuona picha.


Alihisi mapigo ya moyo yakiongeza kasi pumzi zikamjaa na kutoka kwa shida, kiza kizito kilitanda mbele yake kilichoendelea hakukijua. Mage alianguka kama mzigo akiwa amepoteza fahamu, kitendo kile kiliwashtua sana. Walijikuta wakitaharuki ilibidi wamchukue na kumkimbiza hospitali kisha kumjulisha mama yake.


Kwa vile huduma ile haikuwepo alitakiwa kupelekwa Afrika Kusini haraka kwani walisema ugonjwa ule ikiwa atapata matibabu ya haraka anaweza kupona.
***
Mage alisafiri na mama yake mpaka Afrika Kusini katika Hospitali ya Milpark iliyopo katika Jiji la Johannesburg. Alipokelewa na kuanzishiwa matibabu mara moja, madaktari walifanikiwa kufanya upasuaji uliochukua saa tatu kuondoa damu zilizovuja baada ya mshipa kupasuka.


Baada ya upasuaji kwenda vizuri alirudishwa kwenye chumba maalumu chini ya uangalizi ya madaktari bingwa. Taarifa za Mage kuumwa zilimfikia Colin aliyekuwa katika mji wa Port Elizabeth.
“Mpenzi nasikia Mage anaumwa ameletwa hospitali ya Milpark, Johannesburg,” Colin alimwambia Cecy aliyekuwa akicheza game kwenye Ipad.


“Maskini mke mwenzangu nini kimemsibu?”
“Nasikia kapata mshtuko baada ya kuona video na picha zetu za harusi.”
“Maskini, Mage alikuwa kama fisi aliyeamini siku moja mwanadamu atadondosha mkono.”
“Namshangaa kutaka kufa wakati anajua mimi ni wa nani.”
“Wa Cecy.”


“Najiuliza bila Cecy, Colin leo ningekuwa wapi?”
“Anajua Mungu si sisi wanadamu ambao hupokea matokeo.”
“Asante mpenzi wangu kwa kuyaokoa maisha yangu, huwezi kuamini baada ya kuachwa ghafla na Mage nilijawa na mawazo mengi na kujiona nina mapungufu.”


“Asante niseme mimi uliyoyapa majibu maswali yangu kama kuna siku maji yatapanda mlima.”
“Nina imani huu ni muda muafaka wa ku-renew mkataba wako na makapuni yote ya mavazi ya majarida. Waliniuliza afya yako nikawaambia hujambo kabisa hivyo wameomba tupange siku ya wao kuja ili uendelee na kazi yako.”


“Mpenzi moyoni mwangu nimepanga kwanza nikae na mume wangu kwa mwaka mzima ndipo nifanye kazi nyingine.”“Cecy si tumeshafunga ndoa wasiwasi wako nini?”
“Sijaifaidi raha ya ndoa kazi ipo tu, kama wameweza kunisubiri muda wote waendelee kusubiri.”
“Makubaliano ya awali ni kwamba tutakuwa tupo pamoja katika kazi zako zote kwa vile mimi ndiye meneja wako.”


“Mmh! Kama hivyo sawa.”
“Mmh! Bado tu una wasiwasi wa kuibiwa?” Colin alimtania.
“Si umesikia mtu kataka kufa baada ya kusikia umeoa, vipi niwe mbali nawe? Nikisikia upo na Mage ningekufa mimi.”
***
Baada ya kuwajulisha siku ya kuonana na Kampuni ya Ebony walifika katika Hoteli ya The Beach na kuingia mkataba mpya wa miaka miwili. Pia kampuni ya maonesho ya mavazi na urembo nayo iliingia mkataba mpya na makubaliano ya kuanza kazi baada ya miezi mitatu.


Mage naye alitoka hospitali akiwa na afya njema, mama yake alipotaka kujua sababu ya mshtuko ule, alimweleza ukweli kuwa baada ya kuona harusi ya Colin na Cecy alipata mshtuko wa ajabu kilichoendelea hakujua mpaka alipozindukia Hospitali ya Muhimbili akiwa amepooza upande mmoja.
“Unasema nani kaoa? Sijakuelewa vizuri,” mama Mage alishtuka kusikia Colin kaoa.
“Colin, mama.”


“Kama ni kweli basi mwanangu achana na mawazo ya Colin, Mungu atakupa mume wa kweli.”
“Mama hata mimi nimejifikiria hivyo lakini Colin nilimpenda sana.”


“Si kweli, ulimpenda Hans, Colin anapendwa na Cecy kwa hiyo waache na ndoa yao.”
“Ndiyo mama, japo nilikuwa na nia mbaya kwa Cecy, lakini kuanzia sasa sitashughulika na Colin wala Cecy nami nasubiri ndoa yangu.”


“Hilo ndilo neno la kijasiri mwanangu.”
Baada ya Cecy kumaliza mapumziko alianza kazi rasmi, mwaka mmoja baadaye alishika ujauzito na kusubiri muda wa kujifungua. Mage naye alipata mchumba na mambo yalikwenda kama yalivyopangwa.


Siku ya harusi akiwa anajiandaa kwenda kanisani anapata habari zilizomshtua moyo na kufanya apoteze fahamu kuwa mpenzi wake Hans yupo huru baada ya kushinda rufaa yake.


*****************************************MWISHO***********************************


Baada ya kuwa safari ndefu hatimaye chombo kinatia nanga, mambo ya kujifunza kutokana na simulizi hii yako mengi ngoja nianishe machache tu, 1. mapenzi ya kweli hayaangalii hali ya mtu awe na pesa asiwe na pesa, 2. tuthamini hisia za mtu anayekupenda, 3.usimfanyie unyama mwenzio hasa wa kimapenzi aliyoyafanya Mage kwa coliny ndo yaliyomtesa mpaka mwisho. Mwisho wa yote mpende akupendae asiye kupenda chapa lapa

Imeanza kwa utata ila itaisha vizuri japo milima na mabonde yatakuwepo
 
WAKILI WA MOYO...SEHEMU YA 1

Maumivu ya moyo hayana msaidizi na moyo wa kupenda hauna subira, kilichojificha moyoni huwa sawa na mfungwa asiye na kosa lakini hajui kujitetea. Siku zote anayependa kama muhusika hajui kama anapendwa huwa mateso ya kujitakia.

Cecilia msichana alinayetoka katika familia ya maskini anampenda Colin mvulana aliye katika familia ya kitajiri mwenye mchumba anayetaka kufunga naye ndoa. Anajikuta akiumia kila akimuona, pamoja na kuonekana jambo hilo kama maji kupanda mlima lakini msichana Cecy anauapia moyo wake kuwa atauwekea wakili na kuweza kushinda kesi ya maumivu ya mapenzi.

Je, atafanikiwa? Kuyajua yote ungana tena na mtunzi mahiri katika hadithi tamu ya mapenzi ili upate uhondo mwanzo mwisho.
TWENDE KAZI.....

Mama Cecy alishangaa kumuona mwanaye amerudi mapema huku sinia likiwa limejaa ndizi. alimalizia kupuliza moto wa kuni kisha alitoka jikoni huku akifuta machozi kwa upande wa khanga kutokana na moshi wa kuni kumuingia machoni. Alimtazama binti yake aliyekuwa amekaa chini huku ameshika tamaa na machozi kumtoka.

"Cecy nini tena mama?" alimuuliza huku akimsogelea.
"Mama hata nashindwa kujielewa sijui ni kwa nini inakuwa hivi?" alisema huku akiondoka mkono shavuni bila kufuta machozi.

"Una lingine au ni lilelile za siku zote?"

"Kuna lingine lipi mama yangu! Hata sijui kwa nini nimejiingiza kwenye mateso ya kumpenda Colin mtu ambaye hayajui mapenzi yangu kwake."

"Lakini kwa nini mwanangu unapenda kuota ndoto za mchana, wewe na Colin wapi na wapi kama mbigu na ardhi."

"Najua mama utasema hivyo lakini katika mapenzi hakuna kitu kama hivyo, nakuapia kwa Mungu Colin atakuwa mume wangu wa ndoa."

"Cecy mwanangu hebu achana na kujishugulisha na masuala ya mapenzi, hebu jiangalie ulivyo na alivyo Colin. Kwanza mwenzako hand same."

"Hata mimi beutiful girl," Cecy alijibu kwa kujiamini huku akinyanyuka na kujishika mkono kiunoni kujionesha kuwa ni mrembo.

"Mwenzio ana elimu ya chuo kikuu wewe darasa la saba la kufeli, mwenzako anatoka kwenye familia ya kitajiri wewe pangu pakavu tia mchuzi. Kingine ambacho kinafanya usiweze kabisa kumpa ni kuwa Colin ana mchumba na mipango ya harusi ipo karibuni sasa huyo Colin yupi wa kukuona?"

"Mama nina uhakika kwa asilimia mia Colin kunioa," Cecy alisema kwa kujiamini.

"Wee mtoto una wazimu? Au kuna mganga kakudanganya, maana siku hizi ushirikina hauna mtoto wala mzee."

"Mama katu mapenzi sitayaendelea kwa mganga, ila nitayapigania kwa nguvu zote."

"Kipi hasa kinakupa jeuri ya kusema hivyo?"

"Ipo siku nitakwambia lakini amini ndoa ya Colin na Mage haipo ila mimi ndiye mke wake."

"He he he heee, usinichekeshe miye, kwa nini unasema hivyo?" mama Cecy alicheka mpaka machozi yakamtoka.

"Mage hampenzi Colin."

"We umejuaje?"

"Ni historia ndefu mama."

Cecy alianza kumuhadithia mama yake sababu ya kuamini siku moja Colin atakuwa mpenzi japokuwa hajawahi kumtamkia kitu kama hicho hata siku moja.

Alianza toka siku ya kwanza kumuona Colin, Mage msichana aliyetoka katika familia ya kimaskini elimu yake ya dalasa la saba shuleni alikuwa mmoja wa wasichana wabuluza mkia.
Baada ya kufeli kwenye mtihani wa mwisho aliamua kufanya biashara ya ndizi kwa kupita mtaani kuuza. Japokuwa alikuwa maskini lakini alijipenda sana.

Baada ya kuuuza ndizi siku za mwanzo alinunua nguo nzuri ambazo alizivaa kila alipozunguka mkaani kuuza ndizi zake. Kitu kilichopelekea apendwe na wateja wengi kutokana na umalidadi wake na heshima kwa wote akiwemo mama Colin ambaye alikuwa mnunuzi wake mkubwa.

Nyumba ya mama Colin ilikuwa ndiyo iliyokuwa ikinunua ndizi nyingi kitu kilichomfanya Cecy aongeze mtaji. Mama Colin alitokea kumpenda sana na kumwita mkwe.

Siku moja alipitisha ndizi kama kawaida bila kujua kama nyumba ile ina kijana mzuri aliyekuwa nje amerudi baada ya kumaliza masomo yake. Baada ya kufika nje ya geti alibonyeza kengele na mlinzi alimfungulia mlango na kuingia ndani.

"Mwambie mama mkwe leo nimeleta ndizi za ukweli," alimwambia mlinzi aliyekuwa amemzoea sana.

"Mamkweee," Cecy alipaza sauti kama kawaida yake kila alipofika.

Mara alitoka mama Colin akiwa katika muonekano wa mtoko.
"Ha! Ma mkwe safari ya wapi tena?"

"Nampeleka mchumba wako mjini."

"Muongo, yupo wapi?"

Siku zote Cecy alipokuwa akipeleka ndizi alitaniwa na mama Colin kwa kuitwa mkwe japokuwa hakuwahi kumuona huyo mwanaume. Kila siku alikuwa na hamu ya kumuona japokuwa alikuwa akitaniwa.
"Jana usiku na ndege."

"Waawooo," Cecy aliruka juu kama anamfahamu.

Ghafla alinyamaza baada ya kumuona mvulana mzuri tenamtanashati akitoka ndani. Alibakia kama kapigwa shoti ya umeme kwa jinsi alivyosimama kwa mshangao kidole mdomoni.
"Colin umemuona mchumba wako niliyekuandalia?" mama Colin alitania.

"Nimemuona mzuri," Colin alisema huku akimtazama Cecy aliyekuwa bado amesimama.

"Cecy umemuona Colin?"

"Ndi..ndi..yo," Cecy alipatwa na aibu na kushindwa kuzungumza.

"Sasa mkwe, msichana wa kazi atachukua ndizi sisi tuna safari ya mjini."

"Sawa mkwe."

Mama Colin alifungua pochi na kutoa noti ya elfu tano na kumpatia Cecy, wakati huo Colin alikuwa akilisimamisha gari pembeni ya mama yake. Mama Colin alifungua mlango wa gari wa nyuma na kuingia.
"Bai mchumba," Colin alimuaga Cecy aliyekuwa ameingiwa aibu.

"Bai," Cecy alisema huku akiangalia pembeni.

Geti lilifunguliwa na gari lilitoka nje kuelekea mjini na kumuacha Cecy akitoa ndizi kwa msichana wa kazi kisha alitoka na kuendelea kufanya biashara kama kawaida.
****
Safari ya mama Colin na mwanaye ilikuwa kwenda nyumbani kwao Mage msichana aliyemchagua kuwa mke wa mwanaye. Alimuona siku moja alipokuwa na mama yake walipokutana na shoga yake Super Market, wakati akiwa katika manunuzi ya bidhaa muhimu.

"Ha! Shoga za siku?" Mama Colin alimsemesha mama Mage.

"Nzuri shoga, za kupotezana?"

"Mmh! Nzuri, vipi Colin bado hajarudi?"

"Anarudi mwezi kesho mwishoni."

"Shikamoo," Mage alimwamkia mama Colin.

"Marahaba, hujambo mama?"

"Sijambo."

"Monika, binti yako?" mama Colin alimuuliza shoga yake.

"Ndiyo amemaliza chuo kikuu Mlimani anasubiri ajira."

"Nimempenda sana, unafaa kuwa mke wa Colin."

"Tena wataendana wasomi kwa wasomi," mama Mage aliunga mkono.

"Anaitwa nani?"

"Mage," Mage alijibu mwenyewe.

Tokea siku ile wakawa wakiwasiliana hata kutembelea huku wakisubiri muda wa Colin kurudi toka masomoni ili wapange mipango ya ndoa. Mama Colin alimpenda sana Mage kwa umbile lake nzuri na heshima aliyoionesha siku zote kwake. Naye mama Mage alifurahi mwanaye kuolewa na Colin kutokana na kumfahamu vizuri.

Siku Colin aliyofika hakutaka kuwajulisha, kesho yake alimpeleka nyumbani kwao Mage bila taarifa ili wafanye surprise. Familia ya kina Mage ilikuwa ikikaa Kigamboni walikwenda hadi kwao na kupiga honi nje ya geti. Wakati wote huo Colin alikuwa hajui anakwenda wapi.
Baada ya geti kufunguliwa Colin aliliingiza gari ndani na kwenda kulipaki kwenye maegesho. Mama Mage alitoka nje baada ya kusikia gari likingia ndani na kujiuliza nani amekwenda kwake bila taarifa. Alishtuka kumuona mama Colin akiteremka kwenye gari.

"Waawooo jamani, ha! Colin siamini jamani karibu mwanangu," alikuwa akimfuata mama Colin kumkumbatia lakini aligeuza baada ya kumuona Colin na kwenda kumkumbatia.


Itaendelea...............
 
Back
Top Bottom