mwana ally
JF-Expert Member
- Jan 30, 2014
- 363
- 119
Haaa mapendo jamani!""!!acha tuu..Omba yasikukute
Nahisi huyo bint Cecy atagongwa na gari then jamaa amkimbize hospt afu huko atakuja kutana na Mage afu kitanuka...just prediction!
Wakili wa Moyo-22
ILIPOISHIA:
Cecy leta ndizi mbili.
Kwa vile taa ziliruhusu, aliliondoa gari na kwenda kulipaki kituo cha mafuta cha Magomeni, alilizima na kutoka nje. Kwa vile Cecy alikuwa amevuka barabara kwenda kuuza ndizi maeneo ya hospitali, alimtuma kijana mmoja aliyekuwa akiuza miwa.
Samahani mkubwa, naomba kamwambie yule msichana alete ndizi kumi.
Yule kijana alimfuata Cecy aliyekuwa ametua beseni lake chini akiuza ndizi, alipofika alimwambia
This is very interesting story indeed!!!Nice Work.
Wakili wa Moyo-22
ILIPOISHIA:
Cecy leta ndizi mbili.
Kwa vile taa ziliruhusu, aliliondoa gari na kwenda kulipaki kituo cha mafuta cha Magomeni, alilizima na kutoka nje. Kwa vile Cecy alikuwa amevuka barabara kwenda kuuza ndizi maeneo ya hospitali, alimtuma kijana mmoja aliyekuwa akiuza miwa.
Samahani mkubwa, naomba kamwambie yule msichana alete ndizi kumi.
Yule kijana alimfuata Cecy aliyekuwa ametua beseni lake chini akiuza ndizi, alipofika alimwambia
This is very interesting story indeed!!!Nice Work.
Daaaahh!!!
Wakili wa Moyo-23
ILIPOISHIA:
Najua mama yangu alimpenda Cecy lakini si kuwa mke wa mwanaye bali msichana mzuri anayejiheshimu. Inawezekana kigezo cha elimu ndicho kilichomfanya mama yangu amtafute Mage, nina imani kama Cecy angekuwa na elimu kama ya Mage basi angekuwa chaguo la kwanza la mama.
SASA ENDELEA...
Wasiwasi mkubwa wa mama ulianzia siku alipomuona Cecy kapendeza, naweza kusema aliwashinda wote waliokuwa kwenye sherehe yangu. Kilichomshtua zaidi ni baada ya kunikuta na picha ya Cecy aliyokuwa amependeza sana. Aliamini kabisa ni mpenzi wangu hivyo akaamua kujihami kabla mambo hayajaharibika kutokana na harusi yetu kuandaliwa kwa fedha nyingi.
Lakini hakutakiwa kuchukua uamuzi aliochukua bila kuniuliza mimi japokuwa nilimweleza sababu ya kuwa na picha ile. Ila napenda kuwaeleza kitu kimoja kuwa, sitauacha upendo wa Cecy upite hivihivi, najitolea kumsomesha ili aongeze elimu na ujuzi.
Baada ya elimu hiyo, nitafanya naye kazi ndani na nje ya nchi ambayo naamini itamweka katika maisha mazuri na ramani ya dunia. Pia nitahakikisha naijenga nyumba yenu katika hadhi ya kisasa pia mama nitakufungulia mradi ili muendeshe maisha yenu, Colin alieleza nia yake nzuri kwa Cecy na mama yake.
Asante baba..
Mama nani kamwambia sisi tuna shida ya vitu hivyo? Kama kilichonitesa nimekikosa, sihitaji kitu kingine toka kwako, Cecy alimkatisha mama yake na kumjia juu Colin kwa kauli yake.
Cecy mimi na wewe nani mwenye kosa, ulilolisema leo ungelisema mapema tusingefika huku, Colin alijitetea.
Muongo! Colin hata ningesema ingekuwa sawa na kazi bure kwa vile tayari mama yako aliishakuchagulia mwanamke, Cecy alisema kwa hisia kali.
Kabla ya kutoa uamuzi ningechagua.
Mimi na Mage unampenda nani?
Nawapenda wote, ila kwa sasa Mage kwa vile ndiye tupo katika mipango ya ndoa.
Kwa kauli hiyo naomba tukomane, kila mtu ashike hamsini zake ukinikuta njiani nipite kama nguzo ya umeme, Cecy alisema kwa hasira.
Cecy kuwa na adabu, heshimu anachokisema mwenzako...Baba kama una nia hiyo ifanye faida hataiona leo, lakini baadaye atakushukuru.
Sawa mama nimekuelewa, Cecy punguza hasira nina nia nzuri na wewe, uzuri wako nitaulinda na baadaye utakuingizia fedha nyingi na kumsaidia mama. Utauza ndizi mpaka lini?
Cecy hakujibu kitu aliinama chini, Colin alimsogelea na kumbembeleza kitu kilichomfanya Cecy aangue kilio na kusema:
Colin nisamehe kwa yote, hujui kiasi gani penzi lako lilivyouathiri moyo wangu, najua nilikupenda bila kushauriana na moyo wangu. Mnaweza kuniona mdogo lakini nami nina hisia za mapenzi kama wengine, Cecy alisema huku akimtazama Colin kwa macho yaliyojaa machozi.
Najua Cecy, isingekuwa mipango ya harusi ningeweza kufanya chochote ili ujue nauthamini upendo wako.
Sawa Colin nimekuelewa.
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda, Colin aliaga kuwahi nyumbani. Alikwenda kwenye gari na kuwaletea laki moja, walimshukuru naye aliondoka kuelekea nyumbani. Njiani alijikuta akimuwaza Cecy msichana mdogo lakini alikuwa jasiri kuzielezea hisia zake japo aliamini mama yake asingemkubali kutokana na uduni wa maisha na kukosa elimu.
Kwa upande mwingine aliamini kabisa kutokana na kasi ya mabadiliko duniani, Mage ndiye mwanamke sahihi kwake. Kwani aliamini maisha ni zaidi ya mapenzi kwa vile maisha yakiwa vizuri kila kitu kinakwenda. Aliamini kwa umbile adimu la Cecy angeweza kuifanya kazi yake vizuri ya maonesho ya mavazi.
Kitu kikubwa aliamini Cecy kama atapata twisheni ya kingereza, ataweza kuongeza uwezo wake hata kusafiri nchi za nje kufanya kazi ya maonesho ya mavazi pia kupata tenda ya kupamba majarida. Aliamini akimtumia vizuri Cecy, kampuni yake itafika mbali na yeye kujitengezea kipato kikubwa.
Alipanga kuwekeza fedha nyingi kwa Cecy baadaye angevuna fedha nyingi kwa kuamini alikuwa na kitu cha ziada ambacho wasichana wengi hawakuwa nacho. Japokuwa alikuwa na wasiwasi na kikwazo cha mama yake, lakini kwa vile yupo kikazi alijua mama yake angemuelewa tu.
Alipanga ndani ya wiki mbili nyumba ya kisasa ya kina Cecy iwe imesimama huku akimtafutia twisheni nzuri ili kuijua lugha haraka.
Alipanga kufungua duka mbele ya nyumba yao ambalo litawafanya waingize kipato kila siku. Kutokana na kuzama kwenye mawazo ya kumuwaza Cecy, alijikuta akimsahau Mage mpaka alipofika kwao.
***
Alipoingia ndani alikutana na mama yake ambaye alishangaa kumuona mwanaye akiteremka kwenye gari.
Colin unatoka?
Colin ilibidi amweleze mama yake kilichotokea, baada ya kumsikiliza alimuuliza:
Colin mwanangu umemfanya nini mtoto wa watu?
Mama sijamfanya kitu chochote kama nilivyokueleza.
Mage si mjinga kulia tu na kukataa kuzungumza na wewe wakati mlikuwa pamoja?
Yaani sijui kitu labda uulize wewe utapata jibu.
Nitauliza, lakini Colin kuna kitu unanificha haiwezekani Mage aondoke bila kukuaga kisha akatae kuzungumza na wewe wakati usiku mmelala pamoja?
Mama piga simu uulize labda utagundua kitu.
Mmh! Sasa nimepata jibu, mama Colin alisema huku akitikisa kichwa kama kakumbuka kitu.
Jibu gani?
Maana lazima kuna kitu Mage amegundua kuhusu wewe na Cecy, nasema hivi ndoa ikivunjika Cecy atanitambua.
Mama unamuonea bure mtoto wa watu, toka siku ile ya sherehe sijaonana na Cecy, Malki alidanganya.
Muongo umemkataza asilete ndizi ili mkutane sehemu nyingine. Colin Mage akinieleza kuwa amegundua una uhusiano na msichana mwingine pagala lao nakwenda kulitia moto sasa hivi.
Mama kwa nini unanihukumu kwa kosa nisilofanya, nimekueleza piga simu uulize unaanza kutengeneza mawazo yako. Cecy amekukosea nini mpaka kumchukuia hivyo, ni wewe ndiye uliyekuwa naye karibu?
Mama Colin hakusema kitu, aliingia ndani kuchukua simu ili ampigie Mage kujua amepatwa na nini.
***
Baada ya Colin kuondoka, mama Mage alimfuata mwanaye chumbani aliyekuwa amezama kwenye dimbwi la mawazo juu ya hali ya Hans na familia yake ilipomtenga na kumuona kama kinyesi. Moyo ulimuuma na kujua hakukuwa na haja ya yeye kwenda hospitali pia kumuacha mchumba wake, mumewe mtarajiwa akiwa amelala na kuondoka bila kumuaga.
Alijilaumu kwa kitendo chake cha kumpita Colin bila kumsemesha, alijiuliza atamfikiriaje. Alijiuliza ndoa yake ikivunjia na ijulikane sababu ya Hans mwanaume asiye na mapenzi naye ataiweka wapi sura yake. Lakini alijiuliza angesimama na kuzungumza na Colin angemwambia anatoka wapi na kwa nini hakumuaga?
Akiwa katika mawazo hayo, mama yake aliingia na kumkuta amejilaza chali huku ameukumbatia mto wake na macho yake yalikuwa yakiangalia darini.
Mage..Mage.
A..a..bee.
Mbona sikuelewi mwanangu?
Mama nahitaji msaada wako najua nimechanganya madawa.
Nikusaidie nini?
Sijui Colin atanielewaje maana nilichomfanyia si kitu kizuri.
Kwa kweli hatua tuliyofikia huku vikao vikienda vizuri halafu mwenzako abadili uamuzi sijui sura zetu tutaziweka wapi?
Hapo ndipo ninapochanganyikiwa, mama kitendo walichonifanyia familia ya kina Hans, sitakisahau.
Umeona eeh, nilikueleza toka zamani familia ile ilikuwa haikupendi kama ungeolewa na Hans ndoa yako isingedumu. Mungu amekuletea mwanaume wa maisha yako unamchanganya.
Mama nimeisha fanya kosa naomba msaada wako, nitamweleza nini Colin anielewe.
Wala usiwe na wasiwasi, kamwambie kuwa ulimtuma Brenda cheni ambayo ulipanga kumpatia kama surprise umekuta hajaitengeneza na kujikuta umekasirika na kuanza kulia.
Mmh! Atanielewa? Naona kama utetezi mwepesi.
Walaa, ye anajua ulikuwa kwa Brenda, nilimwambia kuna kitu mmeshindwa kuelewana ndiyo maana ulirudi katika hali ile.
Mmh! Basi ngoja nifanye hivyo.
Wakiwa katikati ya mazungumzo, simu iliita. Ilikuwa ikitoka kwa mama Colin.
ITAENDELEA....................