Mimi sikupingi hata kidogo uenda tuko pamoja kwenye mambo mengi tu. tatizo langu mimi ni kwa nini kwa kila jambo unampinga DK sababu ya kusema kuwa eti anawagawa wana kyela hiyo ni ya kitooto kabisa. Siasa ni mchezo kura zinagawa watu hata iwe 80-20. Ningejua unampinga ingekuwa powa. Nilikuuliza unataka kugombea ubunge kyela ukang'aka haya tupe sababu za kuwa kinyume na DK kwa kila kitu husemi sasa tukubebeje. Mimi siitaji tips yoyote ninaporudi nyumbani siendi kujenga gorofa kule!
kama umetoa misada kwenye afya na shule hongera kwani huo nimtizamo wako. Sasa unataka kusema kuwa matatizo ya afya na shule yameisha kwa sasa? kama yako vile vile haukuwa msaada bali pozeo hilo. na mimi sio mzee wa mapozeo (tempo.. Solutions) mimi naamini katika kutatua tatizo na siyo kupoza maumivu. hapo atuko pamoja. Je huko UK umeshaaona watu wakigawa hiyo misaada kama yako? na matajiri wako kibao wenye mihera sasa hujajiuliza wanamatatizo gani kama wewe uko njia sahihi?
Kunionesha kuwa unamjua ilikuwa lazima utaje mazambi ya baba yake? hakuna lingine positive la kuweza kunionesha kuwa unamjua kama vile labda ni brain, HB na n.k. Ndugu yangu kwako wewe kuiba peke yake ndiyo problem, ukiwa mzinzi, dhuluma, uchawi na mengineyo siyo shida na hayo yanafanywa sana na maskini. Mimi niliweka hili kwa kukutega tu nilitaka kujua kama kweli unahoja na chuki yako na DK au wivu tu. kwa jinsi ulivyoonekana kumbe hata rafiki zake unawachukia kwangu ni kipimo tosha kuwa una lako jambo. marafiki zako wangapi ni wezi mbona huwataji humu?
Wewe kama ni mjamaa kivyako vyako mimi kwangu ujamaa ni evil! Lucifa's philosphy period! na kwenye hili sibishani hata kidogo kwani siitaji mjadara kwenye kanuni za Mungu hata kidogo.
halsafu mimi sio CCM hata DK kura yangu hapati na wewe pia kama utagombea maana naona wameshakuvunja nguvu hupati pia. Mimi ni kati ya wale asilimia ndogo tunaona kuwa tupo hapa kwa sababu ya CCM.
Private massage sijibu!
Shalom,
Kabla ya kulaumu wengine tuambie wewe umefanya nini? Kama mtu amejenga ghorofa si huyo afadhali angalau vijana wamepata ajira kuliko bingwa wa kuongea kwenye mtandao au wanaoiba Tanzania na kuhamishia huku nje?
Mimi nimekupa sababu za kutofautiana na Mwakyembe, badala ya kutoa sababu zako unaanza maneno ya kejeli. Toa hoja zako kwanini unaona Mwakyembe anafaa na sio kunishambulia mimi. Lakini kwasababu umeamua kunifanya mimi ni hoja wacha nikuvae na kukupa ukweli wako.
Si afadhali wanaosaidia shule na hospitali kuliko nyie mnaopeleka wazungu fake kwenda kudanganya wananchi eti mtasaidia huku ni utapeli tu? Vipi wale uliowapeleka safari iliyopita wamefanya nini? Ni kweli huhitaji tips zangu maana mwekezaji tapeli toka lini akataka kujua taratibu? Mnawakusanya vijana wa vikoba na kuanza kuwadanganya, aibu kweli kweli!
Kwanza hata hizo solutions za kudumu unazozisema uwezo wa kuzifanya unazo? Toka lini anayetegemea mke kuishi akawa na uwezo wa kusaidia wengine? Mkuu achana na ujinga wa kuzunguka huku na huku kutapeli watu, fanya kazi. Unasema ujamaa unauchukia, huku ishi yako inategemea fadhila za wengine? Usituzuge hapa mkuu, tunakufahamu ipasavyo.
Kama mimi nimekwisha kweli ungehangaika humu kwenye net kufuatilia hoja zangu? Una wasiwasi gani mpaka utumiwe hivyo? Unakubali utumiwe ili tu jina lako litokee kwenye reports, utambulishwe kwa spika. Kama unataka kufika bungeni si gombea kwa nguvu zako?
Mimi si nilikuruhusu umtaje huyo mzazi wangu? Najua hauko informed; hunijui. Taja lolote unalolijua kuhusu wazazi wangu. Hata hao marafiki zangu wataje, nimekupa ruhusa maana sina cha kuficha.
Vipi zile shares za kwenye upepo umewauzia Wakorea? Hiyo ndio miradi endelevu? Mnachukua ardhi ya watu maskini halafu mnawauzia wageni? je mbona matatizo ya umeme bado yapo pale pale? Si mungejiita tu kwamba nyie ni watu wa property or land management?
Kama una matatizo na mimi kugombea ubunge basi nenda kabadili katiba ya TZ na iwafanye wabunge waliopo wawe wa kudumu. Je wote wanaopinga hoja za Mwakyembe hapa wanataka kugombea ubunge Kyela? Ubunge haugombewi JF, kama ubunge ungekuwa unashindaniwa JF basi CHADEMA wangeshinda Busanda.
Kama hujui huku wenye pesa wanatoa sehemu ya pesa zao kusaidia wenye shida. Hata huko uliko akina Bill Gates wanatoa pesa kibao kusaidia miradi mbalimbali ya kusaidia maskini. Mmeshindwa hoja mnaanza kuingiza majungu ya kwamba wanagawa pesa. Pesa ulizozipata kwa kuchapa kazi utagawa kwa watu kwenye vijiwe? Labda mnaopata pesa za utapeli au za kwenye siasa ndio mna uwezo huo.
Hata ukibeza hatuwezi kuacha maana tunaona vijana wanaofaidika. Wewe utawajua wapi hao vijana wakati unachoweza ni kutumia influences za wanasiasa ili kuidanganya serikali ikupe nafasi ya kuwekeza?
Ila mkuu tunajua utapeli wako, tafuta kazi ujitegemee na sio kutegemea mke kama mgonjwa. Utawekeza TZ huku huna mpango wowote; acha kudanganya watu kwa utapeli.
Unafikiri Tanzania inahitaji Wazungu kuendelea? Tumia akili yako kwenda kuwekeza nyumbani kwani huo utapeli hautakufikisha popote.
Kama projects zangu zinakupa kiwewe, basi subiri na zingine zinakuja tena kwa kasi mpya. Mtachukia mpaka mpasuke mwaka huu, hata mukwamishe vipi tutaendelea kufanikiwa tu maana hatumwibii mtu.