Engineer
Asante kwa analaysis yako, ila ninaomba ushauri , kwa uzoefu wako wa siasa za Kyela una dhani ni nani atafaa zaidi ya Mwakyembe, Kuiwakilisha Kyela. Because is good to start thinking of someone who will have credibility than Mwakyembe and I believe you can help us on that, naomba uje na few names tuwajadili na tuwafanyie vetting .
Leokweli
Mwakyembe bado ni nafuu sana kuliko wengine ninaowajua mimi kwenye hii mihangaiko ya siasa za Kyela. Ni nafuu kuliko Mwakipesile, na ni nafuu kuliko hao jamaa wengi wa Dar bora awe tayari kukubali kwamba amefanya makosa kung'ang'ania migawanyiko ya watu na awe tayari kukutana na makundi yote. Huyo kijana mwingine wanayemsema mimi simfahamu zaidi ya kusikia tu na hata ukiwauliza hao wanaompigia debe au wanaompinga utagundua walio wengi hawamjui zaidi ya kujua miradi yake.
Anachotakiwa kufanya Mwakyembe ni kuwa mkweli, hata pale anaposhindwa akae na kuwaambia wananchi kwanini ameshindwa. Aache kulia lia kwenye kila kitu kusingizia watu wengine. Alianza na Mwakipesile kila siku, akaja na Mwanjala, akaja na Rostam na sasa ni huyo kijana.
Ajenge ngome yake Kyela kwakuwa na watu wa kumsaidia anapokuwa mbali na sio kutegemea hawa wapambe ambao hakuna wanachojua zaidi ya kushinda kwenye vijiwe. Pale ofisini kwake awe na mtu wa kushughulikia matatizo ya watu na yale yanayomshinda ndio yaende kwa mbunge. Katibu wake sasa hata hajui nini kinaendelea.
Ajiepushe na hizi pesa za michango ya wananchi, kazi yake sehemu kubwa iwe kuchangisha na kusimamia utekelezaji wake lakini sio yeye kuwa mbele katika kuzitoa na kuamua zitumike wapi. Ni rahisi sana kujikuta unachafuka shauri ya hizi pesa za watu kama hauko makini.
Muhimu kuliko yote awe mkweli; ni bora useme ukweli hata kama utakupeleka gerezani kuliko kukamatwa ukidanganya. Kwa mfano kuna kuna wakati aliwaambia baadhi ya wajumbe wa kata ya Matema kwamba ameacha pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya shule kwa mfanyabiashara mmoja pale mjini na amempa maelekezo diwani (mama mmoja) akachukue. Kumbe kulikuwa hakuna ukweli wowote; viongozi wa ile kata kidogo wamkabe koo huyo mama wakiamini amechukua pesa na kula. Ukweli ulipojulikana, mbunge akawa amejichafulia kwa hao wajumbe wote.
Pia aache kuwa na wapambe wale wa Dar ambao kila mtu anajua ni mafisadi. Wewe unapigana na ufisadi huku unashinda na akina Kifukwe ambaye hata wananchi wa kawaida vijijini wanajua ni fisadi. Lingine ni dharau ya elimu, ukiongoza wananchi wasio na elimu inabidi dharau kuhusu elimu uzifiche kabisa. Ukimtukana mmoja kwamba huna elimu, wale wengine wanajiangalia na wao na kuona pia hawana elimu.
Hivi unategemea CCM kuna msafi mle? Tofauti tu kuna wengine ni nafuu kidogo kuliko wenzao.
Lengo langu si kuwachagulia wana Kyela mbunge ila kutoa taarifa juu ya haya yanayotokea huku. Kama nitaendelea kuwepo, hata akija mwingine itakuwa hivyo hivyo.
Ni mwendo mdundo mpaka kileweke!