Nemesis
JF-Expert Member
- Feb 13, 2008
- 5,536
- 4,532
Mods kuna uwezekano wa kuunga hii na ile ya mrema apata ajali?
Mkuu, Mrema naye kapata ajali? Mrema yupi?
Mods kuna uwezekano wa kuunga hii na ile ya mrema apata ajali?
Mkandala,
Naona umeadika Samwel ila umechukua maneno yake na yangu.
Ni mie nilisema kuwa nazifahamu kesi mbili/tatu tayari ambazo nina imani Mafisadi mwakani WANAWEZA kuzitumia kummaliza Mwakyembe. Nimeandika kabisa hizo kesi zote mbili na sikuzificha. Kesi ya kwanza aliiandika kwa kurashia FMes hapahapa JF na kama sikosei iko kwenye hii thread. Ukitaka zaidi waweza kumuuliza. Kesi ya pili inafanana sana na hiyo, sema ya kwanza ilifanyika Dar na ya pili imekuja kujianika bila kukusudia kwenye mazishi ya mama yake.
Kesi ya tatu hiyo hata wewe unaifahamu na siyo siri ingawa mie niseme nilikuja kuipata humuhumu ndani na hiyo ni wakati wa Uchaguzi Zenji (Utawala wa Mkapa). Sijawahi ifahamu vizuri ila ina uhusiano na kipigo kilichotembea Zenji.
Sasa si unaona zote tunaziweka hapa ili kumpa muda ajiandae? Kama tungelikuwa hatumpendi unavyofikiri, tungelikaa kimya. Nimesema tangu mwanzo kuwa Mwakyembe ana uwezo mkubwa ila anajiharibia mwenyewe.
Mkandala, tatizo la Mwakyembe anataka kujifanya Rostam wa Kyela. Yaani lazima uwe na yeye tu na akisikia ulienda kwenye party kwa Mwakipesile (Boiler la kutupwa) basi siku hiyohiyo unakuwa mbaya wake. Analazimisha uwe na marafiki anaotaka na uhusiano na watu wale tu unataka. Ukifanya kivyako basi kwishieni. Ni sawa aje hapa akute mmekubaliana na Zitto juu ya jambo fulani basi hapohapo urafiki kwisha. Anakuwa kama Mwanaume mwenye wivu. Kila akiona mke wake kasimama na mwanaume basi ugomvi. Namhurumia huyo mwenyekiti wa CCM aliyemfanya mali yake na jamaa hajui hata afanye nini maana anaendeshwa na Mbunge na huku sheria/katiba ya CCM inamdai afanye vile. Nafikiri binadamu ili uishi na wengine lazima ujifunze kuwaamini. Vinginevyo, nenda kashike chaki.
Juu ya MAFISADI kama watataka kummaliza, nina imani wanazo kali zaidi ya hizi tunazozifahamu sisi hapa. Si uliona kwenye swala la umeme, walimtekenya kidogo na akaanza kuhaha kila sehemu?
Juu ya kupaka watu, juzi kampaka kijana mmoja aliyeko UK kuwa analeta mambo jambo. Na kibaya zaidi, imetoka kwenye geazeti la MAJIRA ukurasa wa mbele wakat jamaa yuko busy na Mabox yake UK, huku analimwa eti anataka kugombea. Haya magazeti nayo sijui yakoje, habari ya MBEBA mabox mnaiweka ukurasa wa mbele, kisa makala ya Mwakyembe? Na kwa ufupi ni kuwa alishaanza muandama jamaa siku nyingi sana. Na amekuwa akija hapa kwa kutumia jina la LAZARUS MTINDI (Soma nyuma jumbe zake - Ninaamini kwa asilimia 90 kuwa ni yeye). Ila jamaa wa UK naona mwisho atafikia sasa achoke na aamuwe kwenda kugombea. Akishaamua kufanya hivyo basi usiwe na wasiwasi, NITAKUJULISHENI <> kama ninataka kwenda kugombea (heeee Sikonge...🙂
Hizo sababu mbili kwa kweli zimekaa vibaya sana. Itabidi kumtafuta Dr. mzuri sana wa Plactic Sugery ili kuondoa hayo makovu aliyojiwekea. Mwakyembe alimtoa Mwakipesile kwa kumtolea uvivu na madudu kibao na moja wapo likiwa hilo la kugawa watu. Yeye anafanya hayohayo.
Anyway, madudu mengine sintayaweka kwa hisani ya ndugu zangu wa Kyela. Ila siku ikifika basi nitayaanika. Ila lazima ujuwe kuwa kama kuna sehemu mwakani uchaguzi utakuwa katika hadhi ya KIMATAIFA, basi Kyela utakuwa namba 1. Hapa hatuongelei pesa ila mbinu za kivita. Watu watakaa chini na kuchora Algorithm ya kushinda.
Mkuu, huyo unayemweleza, si Mwakyembe ninayemfahamu kwa karibu na kwa siku nyingi. Ni Mwakyembe uliyemuunda wewe kujifurahisha na wana JF ambao ni extremely ill-informed. Cheers!
...Walituaminisha? unafikiri hili ni suala la kufikirika.......please calm down ndugu yangu, yaani mpaka leo unafikiri tu issue ya Richmond ni yakufikirika.......unadhani ingekuwa ya kufirikirika kina EL, Karamagi na ''Bangusilo'' wangekubali kirahisi kuachia ngazi?walituamiisha kuwa RICHMOND NI KAMPUNI FAKE na serekali imeilipa mamilioni kampuni hiyo
Hiyo kesi inaendelea wapi.....kisutu, mahakama kuu.....please help hapa! na Mwakyembe ameonyesha vipi kuwa ni mwongo au nani kathibisha huo uwongo wake mkuu?kwa kesi hii inayoendelea mwakiembe ameonyesha kuwa si mkweli
Khaaa! we ni mbongo au umehamia hivi majuzi....yaani umesahau hata yale malipo ya Ths 152m per day ambayo hata Tanesco walikiri kuyalipia?kwani imethibitika mpaka sasa kuwa RICHMOND hawakulipwa hata senti moja na serekali,na ni kampuni halali iliyosajiliwa Tanzania. IMEDANGANYA
Kama unasema Mh. Mwakyembe alishindwa kuthibitisha kauli yake kuwa Mh.Zitto kapokea hela toka dowans, Je. Mh. Zitto yeye alithibitisha wapi na vipi kwamba kamati ya kina Mwakyembe walipokea posho kinyume na utaratibu? au mambo ya double standards?zitto kupitia Tz Daima alituonyesha wa Tanzania kuwa Mwakiembe yeye na kamati yake walilipwa pesa za ziada na tanesco na kupewa posho zilizo kinyume na utaratibu.
Acha kuunda meneno yako mjomba....wengi tulimsikia kupitia ITV yes, hakuconfirm kuwa ajali ile iliundwa...yeye alisema, kama ilikuwa planned basi the planner was very smart..........!angalia maneno yake haya hapa:Akiwa kitandani aliweza kutuambia watanzania kupitia ITV na NIPASHE kuwa aligongwa kwa nyuma,na ajali hiyo ni kuundwa
Mh. Mwakyembe:
``...Mimi ni Mkisto, nimemuachia Mungu hayo, nimesema Mungu kama hiyo, kilichotokea leo, ni binadamu alikipanga basi namshitakia yeye, na kama kilichotokea ni ajali, basi tumuachie Mungu. Lakini kama kilichotekia kilipangawa basi huyo aliyepangwa kufanya hivyo ni mtaalam wa hali ya juu sana maana jinsi alivyoigonga ile gari, kupoteza mwelekeo, mimi kwa kweli nimeiona hiyo, hayo matukio, kwenye sinema tu.``
Uwongo wa mwakyembe ni upi? yaani mtu aliyekuwepo kny tukio na kamati ambayo haikuwepo wakati tukio linatokea.....hivi wewe unatoa benefit of dought kwa yupi....kamati au Mwakyembe aliyekuwepo pale?ingawa kamati ya IGP imethibitisha kuwa taarifa za mwakiembe ni za uongo na hazina ukweli ajali hiyoimetokana na uzembe wa dereva
wake.
Wewe inaonyesha hukuwahi kuwa na imani yoyote na Mwakyembe, vinginevyo ungejaribu kuwa obejective kidogo kwenye comments zako!wana jf nimejaribu kuonyesha haya kutokana na imani yangu kwa mwakiembe kuanza kupotea baada ya kuona kila alofanya linakuja kuonekana jambo na kuletea maswali juu ya alicho kifanya,
Kwa kweli Mwakyembe na ukweli ni vitu viwili mbali mbali kabisa. Anajua kweli kutafuata ukweli wa wengine lakini yeye sio msema ukweli?
Pia wiki mbili zilizopita wakati anafungua tawi la CCM Kyela alitamka bila hata kutoa ushahidi mmoja kwamba kuna milioni 400 zimetengwa kummaliza kisiasa Kyela na tayari milioni 5 imepewa kata moja. Akaanza kumhusisha kijana mmoja bila hata kutoa chembe ya ushahidi kuonyesha huyo kijana ana uhusiano hata mdogo na hao anaowaita mafisadi.
Kwa kweli Mwakyembe na ukweli ni vitu viwili mbali mbali kabisa. Anajua kweli kutafuata ukweli wa wengine lakini yeye sio msema ukweli?
Kwa taarifa zenu tu tayari halmashauri ya wilaya inashughulikia malalamiko ya madiwani kwamba michango kwa ajili ya Kyela kupitia NGO ya akina Mwakyembe (KDF) haijafika Kyela. Wajumbe wameomba atafutwe mtu huru kuchunguza pesa zilizochangwa tokea 2006 mpaka leo, mbunge anapiga chenga na toka aunde hiyo KDF hajawahi hata siku moja kutoa mahesabu yake kwenye halmashauri ya wilaya.
Mwulizeni hilo na muone kama atakanusha. KDF inaongozwa na yeye na wezi wengine akiwemo Kifukwe aliyefukuzwa kazi kwa ufisadi Nordic na pia mtunza fedha ni jamaa mmoja alikuwa mkurugenzi wa fedha na utawala NMB, naye kafukuzwa kazi kwa wizi.
Hawa CCM wote ni mafisadi tu, kama kuna wasafi ni wa kuhesabika lakini Mwakyembe sio mmojawapo.
wana Jf baada ya kutokea ajali ya Mh mwakiembe nimejaribu kufatilia baadhi ya matukio yalo muhusu mh huyu.
A; richmond case.
nimeangalia na kufatilia kesi inayoendelea kuhusu richmond kutokana na riporti ya mwakiembe bungeni walituamiisha kuwa RICHMOND NI KAMPUNI FAKE na serekali imeilipa mamilioni kampuni hiyo,kwa kesi hii inayoendelea mwakiembe ameonyesha kuwa si mkweli kwani imethibitika mpaka sasa kuwa RICHMOND hawakulipwa hata senti moja na serekali,na ni kampuni halali iliyosajiliwa Tanzania. IMEDANGANYA
Pia wiki mbili zilizopita wakati anafungua tawi la CCM Kyela alitamka bila hata kutoa ushahidi mmoja kwamba kuna milioni 400 zimetengwa kummaliza kisiasa Kyela na tayari milioni 5 imepewa kata moja. Akaanza kumhusisha kijana mmoja bila hata kutoa chembe ya ushahidi kuonyesha huyo kijana ana uhusiano hata mdogo na hao anaowaita mafisadi.
Kwa kweli Mwakyembe na ukweli ni vitu viwili mbali mbali kabisa. Anajua kweli kutafuata ukweli wa wengine lakini yeye sio msema ukweli?
Kwa taarifa zenu tu tayari halmashauri ya wilaya inashughulikia malalamiko ya madiwani kwamba michango kwa ajili ya Kyela kupitia NGO ya akina Mwakyembe (KDF) haijafika Kyela. Wajumbe wameomba atafutwe mtu huru kuchunguza pesa zilizochangwa tokea 2006 mpaka leo, mbunge anapiga chenga na toka aunde hiyo KDF hajawahi hata siku moja kutoa mahesabu yake kwenye halmashauri ya wilaya.
Mwulizeni hilo na muone kama atakanusha. KDF inaongozwa na yeye na wezi wengine akiwemo Kifukwe aliyefukuzwa kazi kwa ufisadi Nordic na pia mtunza fedha ni jamaa mmoja alikuwa mkurugenzi wa fedha na utawala NMB, naye kafukuzwa kazi kwa wizi.
Hawa CCM wote ni mafisadi tu, kama kuna wasafi ni wa kuhesabika lakini Mwakyembe sio mmojawapo.
mkuu heshimaa..Pole sana fred
Kuna wakati nilishasema humu kuwa Mwakyembe anaishi kwenye dampo, wakati yeye aliposema kuwa Rostam anaoga maji taka. kumbuka.CCM ni dampo!
1.Ni mwanasiasa, kama wengine wowote wale popote pale duniani
2.Ni mwana-CCM watafanya lolote yeye na chama chake kusema lolote au kuwatwist watanzania
3. Analinda jimbo lake kwa chama hicho hicho anachopiga kelele kuwa kuna mafisadi!
Sasa sijui ni lini alishawahi kuwa na credibility!
Viongozi wote wanaojiita wasafi na yet wako ndani ya CCM ni wanafiki!, hawana ujasiri, waoga, wanapenda vyeo, fedha na kutaka chama chao kiwabebe kwa namna yoyote ile!
Nashangaa baadhi ya watanzania kuingia kwenye huu mkumbo vikiwemo vyama vya upinzani!
Nimekuwa ni kiwauliza Chadema mnamsifiasifia Mwakyembe je huko kyela mtamsimamisha mgombe wa Chadema hiyo 2010!!!! hayawezi kujibu yanabaki yanatoa macho!
Hii sio yanga na simba, we need to be strategic!
SIJAONA MSAFI CCM!!!, ANGALAU MREMA ALIONYESHA NJIA!! wote wako kukilinda chama , chama kile kile tulichokipa miaka 40 lakini wameshindwa kazi!
mkumbo huu wa kuwagawa CCM wasafi na wachafu umewakumba wengi wakiwemo wapinzani pasi kujua CCM wasafi ni CCM na CCM wachafu wote ni CCM.
Top yote ya CCM ni walewale akina Rostam, Lowassa, Karamagi!!!!!!!! n.k
Hey mbona tuliaminishwa hapa kuwa Mwakyembe ni shujaa, kamanda, mpiganaji, kiboko ya mafisadi nk.
Kulikoni tena?