Godbless Lema na kitabu Nchi ya wasioona(The country of the blind)

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,574
13,311
Kulikuwa na hekaya kuwa huko juu milimani kuna bonde ambalo wakazi wake wote ni vipofu. Siku moja mpanda milima mmoja kwa bahati mbaya aliteleza na kuporomokea kwenye bonde refu sana. Bonde lililokuwa limezungukwa na milima iliyosimama wima pande zote. Bahati akakuta kuna watu wanaishi. Akakumbuka hekaya za kuwepo kwa bonde la vipofu milimani huko. Akili yake ikamkumbusha msemo, KWENYE NCHI YA VIPOFU MTU MWENYE JICHO MOJA NI MFALME.

Basi akawa na mawazo mengi ya jinsi atakavyowaongoza watu wale na kuwafundisha mambo mengi. Lakini baada ya kukutana na watu wenyewe, ni kweli wote walikuwa vipofu, lakini walikuwa na utaratibu wao mzuri wa maisha walioufuata. Maisha yao yote hawakuwahi kusikia habari ya kuona. Bwana yule alipoanza kuwaeleza habari za kuona wakamuona kama kachanganyikiwa.

Alipowaambia kuwa mchana ndiyo muda mzuri wa kufanya kazi na si usiku walimuona punguani kabisa. Walimwambia kuwa usiku ndiyo muda sahihi wa kufanya kazi sababu hakuna joto, joto linapoanza asubuhi ni muda wa kulala. Kwao tofauti ya mchana na usiku ilikuwa ni joto wala si uwepo wa mwanga.

Na hata walipopapasa macho yake na kuona yanachezacheza walimuona kuwa ni kiumbe duni sana. Basi akawa ndiye kiumbe anayedharaulika kuliko wote kwenye bonde lile. Na maneno KWENYE NCHI YA VIPOFU MTU MWENYE JICHO MOJA NI MFALME yakawa mwiba kichwani mwake.

Mwishowe wakaamua wamtoboe macho, maana waliona kuwa yanavyochezacheza yanasababisha na akili yake nayo iwe inachezacheza.

Bwana yule angetumia njia gani ili kueleweka na vipofu wale?
Nchi ya wasioona..png
 
Kulikuwa na hekaya kuwa huko juu milimani kuna bonde ambalo wakazi wake wote ni vipofu. Siku moja mpanda milima mmoja kwa bahati mbaya aliteleza na kuporomokea kwenye bonde refu sana. Bonde lililokuwa limezungukwa na milima iliyosimama wima pande zote. Bahati akakuta kuna watu wanaishi. Akakumbuka hekaya za kuwepo kwa bonde la vipofu milimani huko. Akili yake ikamkumbusha msemo, KWENYE NCHI YA VIPOFU MTU MWENYE JICHO MOJA NI MFALME.

Basi akawa na mawazo mengi ya jinsi atakavyowaongoza watu wale na kuwafundisha mambo mengi. Lakini baada ya kukutana na watu wenyewe, ni kweli wote walikuwa vipofu, lakini walikuwa na utaratibu wao mzuri wa maisha walioufuata. Maisha yao yote hawakuwahi kusikia habari ya kuona. Bwana yule alipoanza kuwaeleza habari za kuona wakamuona kama kachanganyikiwa.

Alipowaambia kuwa mchana ndiyo muda mzuri wa kufanya kazi na si usiku walimuona punguani kabisa. Walimwambia kuwa usiku ndiyo muda sahihi wa kufanya kazi sababu hakuna joto, joto linapoanza asubuhi ni muda wa kulala. Kwao tofauti ya mchana na usiku ilikuwa ni joto wala si uwepo wa mwanga.

Na hata walipopapasa macho yake na kuona yanachezacheza walimuona kuwa ni kiumbe duni sana. Basi akawa ndiye kiumbe anayedharaulika kuliko wote kwenye bonde lile. Na maneno KWENYE NCHI YA VIPOFU MTU MWENYE JICHO MOJA NI MFALME yakawa mwiba kichwani mwake.

Mwishowe wakaamua wamtoboe macho, maana waliona kuwa yanavyochezacheza yanasababisha na akili yake nayo iwe inachezacheza.

Bwana yule angetumia njia gani ili kueleweka na vipofu wale?
View attachment 2537558
🤣🤣🤣🤣 acha kusingizia maskini wa watu. Wangemtoboaje wakati walikuwa hawaoni? Kama asingekuwa taahira, angeachana nao kwani alikuwa anashindana na ukweli kama wewe na Lema wako.
 
🤣🤣🤣🤣 acha kusingizia maskini wa watu. Wangemtoboaje wakati walikuwa hawaoni? Kama asingekuwa taahira, angeachana nao kwani alikuwa anashindana na ukweli kama wewe na Lema wako.
Lema asichukulie poa watu ambao 'hawaoni' kama yeye. Aende nao polepole. Watamtoa macho awe kama wao.
 
Back
Top Bottom