Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,011
- 144,371
Kwa mtazamo wangu, pamoja na Godbless Lema na familia yake kupewa hifadhi ya kisiasa nchini Kenya, Lema na familia yake watakuwa salama zaidi iwapo wataishi nje ya region hii ya Afrika Mashariki na zaidi wakiwa Ulaya,Marekani au kwingineko licha ya ukweli kuwa hadhi ya ukimbizi aliopewa nchini Kenya inatosha kumhakikishia usalama wake.
Hivyo, ninaamini Tundu Lissu akiwa nchini Ubelgiji, anaweza kufanya mipango /kushawishi nchi za ulaya hasa Ubelgiji atakokuwa anaishi, kuhakiisha Lema na familia yake wanahama nchini Kenya na kwenda kupata hifadhi katika mojawapo ya nchi za Ulaya,Marekani au katika nchi nyingine tofauti na Kenya ambapo anaweza kukaa kwa muda tu.
Ni imani yangu pia Lissu atafanikisha mambo mengi ya kusaidia wapinzani wenzake pamoja na vyama vya upinzani akiwa huko ughaibuni-anakwenda kuanzisha movement za kusaidia mabadiliko akiwa huko Ulaya pasipo kuvunja au kukiuka mashariti ya kupewa hifadhi katika nchi za watu.
Muda utaongea.
Hivyo, ninaamini Tundu Lissu akiwa nchini Ubelgiji, anaweza kufanya mipango /kushawishi nchi za ulaya hasa Ubelgiji atakokuwa anaishi, kuhakiisha Lema na familia yake wanahama nchini Kenya na kwenda kupata hifadhi katika mojawapo ya nchi za Ulaya,Marekani au katika nchi nyingine tofauti na Kenya ambapo anaweza kukaa kwa muda tu.
Ni imani yangu pia Lissu atafanikisha mambo mengi ya kusaidia wapinzani wenzake pamoja na vyama vya upinzani akiwa huko ughaibuni-anakwenda kuanzisha movement za kusaidia mabadiliko akiwa huko Ulaya pasipo kuvunja au kukiuka mashariti ya kupewa hifadhi katika nchi za watu.
Muda utaongea.