Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:😛eace:

hakuna muda wa kujibizana na mtu safari hii......
hata wakitukana sisi hatuongei.......ni mbere kwa mbere Mura.....
wanadhani sisi ni karunguyeye......

 
sasa nimeamini chadema mnapenda damu hata mawakala wenu mumewaua ili mpate sympathy

ongeeni weeeee.......mkimaliza mnyamaze.......
mmezoea kuanzisha fujo.......ili ionekane ni Chadema.......
sasa hivi tunatumia formula ya......ukipigwa kofi upande wa kulia....geuza na kushoto......

 
Jamani lazima tuhakikishe ushindi wa CDM Arusha. mie ntatoa 50,000/- vile vile
 
Hivi waungwana wenzangu naomba tusaidiane hapa kuhusu mchakato mzima wa kesi iliyopelekea kutenguliwa kwa Mh. Godbless Lema kuwa mbunge wa Arusha. Msingi mkubwa kabisa wa kesi kama ilivyoripotiwa ktk vyombo vya habari ni kuwa kulikuwa na udhalilishaji wa kijinsia na matumizi ya lugha chafu dhidi ya mpinzani wake wakati ule. Sasa mimi nauliza vp kuhusu matumizi ya lugha chafu ktk uchaguzi mdogo wa Arumeru mashariki!!!!!? Watanzania tunajifunza nini?
 
Chaguzi ndogo na kesi mahakamani ni gharama kubwa sana,magamba hawa wanatuumiza wafanyakazi kwa matumizi mabaya ya kodi zetu.Binafsi nalipa kodi ya moja kwa moja sh175000 kila mwezi achilia mbali VAT ktk manunuzi mbalimbali nitakayofanya kwa mwezi,hizi ndzo pesa magamba wanazochezea.
Naamini kama tungekuwa na tume ya uchaguzi yenye watu wenye akili zinazo fanya kazi haya yote yasingejitokeza,hivi sasa kuna kesi nyingi tu za kupinga matokeo ya uchaguzi wa2010,na pengine tukaona chaguzi ndogo kama matokeo ya kesi hizi arusha ukiwa ni mfano tu.Tume ya uchaguzi ilipaswa kuyaona haya kabla ya kampeni na wakati wa kampeni hivyo wagombea waliokiuka kanuni wangeshaenguliwa.
kama watanzania tuelewe kwamba hatuwezi kupata maendeleo ya kweli kama kila uchwao tunawaza kampeni za uchaguzi.

hizi kampeni ni gharama kubwa na ni kodi zetu,kesi mahakamani pia ni gharama na ni kodi zetu pia.inapasa kama kweli Lema alikiuka kanuni na hivyo ni haki kwa yeye kuvuliwa ubunge,basi na wasimamizi kutoka tume waliokuwa najukumu la kusimamia kampeni wawajibike na wagharamie uchaguzi mdogo endapo utafanyika kwa kufilisiwa.

Wito kwa wapenda maendeleo ya kweli,2015 tuchague na tushawishi achaguliwe mtu mwenye akili ambaye wastaafu wataachwa wajipumzikie na sio kuteuliwa kuwa wenyeviti na wakurugenzi wa tume na pia tuwe na tume makini ambayo itawaona wanaokiuka kanuni na kutuepusha na chaguzi ndogo ambazo zinaepukika.
 
Huyu ushenzi wake ni upi mkuu? mbona anaonekana ni mstaarabu sana! nampa heshima zangu kwa heshima ya Marehemu Hayati sokoine!

kwa hiyo si kwamba unampa heshima yeye binafsi bali kwa heshima ya baba yake....???!!!!

Mkuu..... nchi inatakiwa iendeshwe na viongozi wenye uwezo na sifa binafsi ambao sisi waongozwaji tutawapa heshima wao binafsi kwa uwezo na sifa zao njema, hatuhitaji viongozi ambao hawatoweza kujisimamia isipokuwa kwa kutumia majina ya wazazi wao.....
 
Mjengwa umesema vyema lakini huku mtaani watu,hawaelewi mahakama ndio imeamua bali serikali ya ccm imempokonya mh.lema ubunge kwa hila.katiba iko pale je inafuatwa kama inakiukwa?katiba inaruhusu serikali kuua wananchi wake?wale waliouwawa arusha,nyamongo,songea na leo geita?hakuna uhuru wa mahakama judge mkuu kuhudhuria semina elekezi ambayo imeandaliwa na raisi dodoma maana yake nini?anatekeleza maagizo ya serikali,ukweli ni kuwa mahakama zetu zimeoza mno,na mahakama ya kweli ni wananchi.ikulu imeshindwa kukanusha mambo mangapi?kwa nini hili wamejitokeza haraka ,ukweli unajulikana nape nauye alishasema watashinda na lema ataangushwa,lakini pia january makamba alimpigia simu mh.g.lema kabla hukumu haijasomwa kuwa unavuliwa ubunge,kwa nini tusiamini wakati huyu alikuwa mwandishi wa jakaya mrisho kikwete?alizipata wapi habari?hili suala wanasheria watatafsiri wanavyotaka lakini mtaani tunajua lilipangwa halijatokea kwa bahati mbaya wasubiri hasira za wananchi tu kwani ndio mahakama ya kweli.
 
Hahahaha maskini ccm! Hata walete wabongo wote arusha, watachagua chadema jamani magamba hamsikii
 
kweli mkuu,haya mambo utafikiri mpira wa miguu bongo matokeo hupangwa mezani sio uwanjani!
 
Huu ni mchezo wa paka na panya. CCM wangeshinda Arumeru mashariki Lema asingepokonywa nafasi yake. Nahisi JK anapanga karata kwamba EL na RA wamalizie mitaji yao kwenye chaguzi ndogo ili 2015 amuweke anayemuwazia yeye kwani hawa wenye meno watakuwa hawawezi kungata tena!:shock:
 
Maggid elewa kuwa LEMA si mjinga, amekuwa main character wa hili saga. We unachambua baada ya tukio, yeye ame-connect dots. We unapita juu ya daraja ukiona mwanga, ye kapita ndani ya tunnel kuona vya gizani na hatimaye mwanga at the end of tunnel. Ungemuuliza sababu na pia kwa nini NAPE alitoa kauli kuwa 'lazima kesi imtie kidole' !?
 
Hii itakuwa Kufuru ya Mwaka!! Pia Itakuwa ni Kuwadhalilisha Wana Arusha!! Huyu Binti Yupo Mjengoni Tayari!! Halafu awazibie Wengine Kisa Watu wanataka Kuabudu Usulutani? Aliyefanya mambo Makubwa ni Baba yake!! Na yeye ajitahidi kwa njia yake ila Usulutani na Kurundikiana Vyeo Hiyo Haikubaliki!!
 
Ndugu zangu,


Kuna kila dalili, kuwa tunakokwenda ni kubaya. Tumefika mahala sasa, kuwa kwenye siasa tunaingiza hulka za ushabiki wa Simba na Yanga. Hii ni hatari kwa taifa.


Jana alhamisi, kabla ya jua la saa sita mchana, habari zililipuka na kusambaa kote nchini; Mahakama imemvua Ubunge Godbless Lema.


Ni ukweli, Godbless Lema ni mbunge kijana na maarufu sana hapa nchini. Lakini, imefika wakati Watanzania tukubali na tuamini, kuwa Mahakama inafanya kazi kama mhimili huru wa dola hata kama kunahitajika, kupitia Katiba mpya ijayo, kuboresha mhimili huo ili uaminike zaidi.


Ni kwa mantiki hiyo, kuwa mahakama ni mhimili huru wa dola, tumeshuhudia hata Serikali ikifikishwa Mahakamani na hata kushindwa kesi. Tumeshuhudia , katika historia ya nchi hii, Wabunge wa CCM , bila kujali majina na umaarufu wao wakifikishwa mahakamani na kushindwa kesi.


Kwa Godbless Lema, kutoa hadharani madai kuwa Rais wa nchi anahusika na hukumu yake ni kauli ya bahati mbaya sana anayopaswa yeye mwenyewe Lema, na chama chake, kuacha kuendelea kuitoa, haina mantiki. Inaidhalilisha Mahakama. Ni kauli iliyotolewa kwa haraka na isiyo na tija kwa taifa.


Tukubali kwa sasa, kuwa kule Arusha hukumu imeshatolewa. Kuna fursa pia ya kukata rufaa ya hukumu hiyo kwenye Mahakama iliyo juu zaidi. Hakika, kwa Godbless Lema na chama chake, huu ni wakati kutafakari hukumu hiyo na kuona ni namna gani ya kwenda mbele kisheria au kisiasa.


Haiwezekani kwa sasa kudai kuwa CCM inahusika na hukumu hiyo. Wakati kimsingi CCM imepata 'hasara nyingine ya kisiasa' kwa matokeo ya hukumu hiyo. Kwa anayechambua kwa undani sana, hukumu ya Lema ya kuvuliwa ubunge imekuja katika wakati mbaya sana kwa chama tawala, CCM.


Ni hukumu inayomtangaza na kumwongezea umaarufu Godbless Lema na chama chake cha Chadema. Leo, bila kufuatilia mwenendo wa kesi husika, kuna wanao-sympathy na Godbless Lema na Chadema, wakiamini CCM imetumia Mahakama kumhujumu Godbless Lema na Chadema. Na kama Lema atasimama tena kuwania kiti hicho, basi, yumkini kura zake zitaongezeka maradufu. Lema ana hakika ya kura nyingi pia za ' kuonewa huruma'.


Na ukweli mwingine ni huu, katika nchi yetu kwa sasa kuna kundi jipya la wapiga kura. Hawa naweza kuwaita " Wapiga kura dhidi ya hali iliyopo"- Aina hii ya wapiga kura inaundwa kwa idadi kubwa na waliokuwa wapiga kura wa CCM katika chaguzi za miaka ya nyuma na ambao sasa hawaridhiki na hali iliyopo ndani na nje ya chama chao.


Ndio, hawa ndio waliokuwa wapiga kura wa CCM na ambao sasa wanawachanganya sana CCM. Ndio hawa waliompigia kura Nassari Arumeru, ndio hawa waliowahakikishia viti vya udiwani Chadema kule Ruvuma, Mwanza na Mbeya.

Maana, ni wapiga kura wa kundi hili unaoweza kuwaona wakijaa kwenye mikutano ya kampeni za CCM, lakini, kwa vile hawapati majibu ya maswali yao ya namna gani CCM na Serikali yake, si tu itakavyorekebisha, bali inavyorekebisha sasa ' Hali iliyopo', basi, siku ya kupiga kura wanatumbukiza kura zao kwa wapinzani.


Ndio, ni ukweli pia , kuwa ' Ndani ya nyumba ya CCM' kwa sasa hakuna amani na utulivu. Makundi na mbio za kuelekea kwenye Urais 2015 zinawaacha wana-CCM wakivurugana wenyewe kwa wenyewe.


Focus sasa haiko kwenye kutekeleza ahadi lukuki walizowaahidi wapiga kura kwenye kampeni zilizopita. Kwa sasa kuna wenye kufikiria hatma zao za uongozi. Kuna waliojikita kwenye mnyukano wa kimakundi kwenye vita ya kuelekea Urais wa 2015. CCM ya sasa inaonekana kuwa mbali na wananchi na kero zao zinazowakabili. CCM ya sasa imeacha kuwa ' Kimbilio la Wanyonge' kama wakati mmoja alivyopata kukiri Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa. CCM ya sasa ni kimbilio la ' wenye nacho' wakiwamo wafanyabiashara.


Ndio, CCM imeanza kulipa gharama ya wananchi kutoridhika na ' Hali iliyopo'.


Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo

Hiyo ni tafsiri yako na wote tunaaminishwa hivyo kuwa mahakama ni muhimili huru,lakini uelewe kuwa hii ni nadharia tu ila ukija kwenye vitendo mahakama haiko huru kama unavyoeleza.ndio maana tunadai katiba mpya,hata jaji mkuu othman chande kuna siku alikiri kuwa mahakama ya tz haiko huru.sasa tukuamini wewe maggid au jaji mkuu?jaji mkuu kuna siku alizungumzia uwepo wa kamati ya nidhamu ktk mahakama zinazomhusisha mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya ambayo inasababisha mahakama kutokuwa uhuru kimaamuzi...........anyway sina lugha nzuri ya kuelezea hili ila wataalum wa sheria wanaweza kuelezea vizuri.
 
itisheni kikao cha viongozi wa ccm na familia zao halafu mteue mgombea wenu.

Tunachosubiri huku arusha ni kuizika ccm kama tulivyofanya arumeru pale makaburi ya ngarasero.
 
nimepitia threads nyingi na sehemu nyingi ili kuona mawazo ya wanachadema na viongozi wao. Nilichoona ni kuwa hawaaamini kama mahakama imetenda haki. Bali si hilo tu wamediriki kuhisi kuwa ati mahakama imeamuriwa na ikulu kufikia maamuzi yaliofikiwa


nimesikitishwa sana na watu ambao siku zote hujihesabu makini kwa kauli zao za kuhusisha ikulu na mahakama katika maamuzi.

Inawezekana hukumu haikuwa tamu kwao, na wanahisi hawajatendewa haki, na ndio maana kwenye sheria kukawa na haki ya kukata rufaa ili kuhakikisha haki inatendeka. Kwa hio ndugu zangu wa chadema kama mnahisi haki haijatendeka fateni taratibu za kisheria kudai haki zenu badala ya kuhubiri chuki na uongo


ndani ya chadema mna wanasheria wengi tu, watumieni ktk kuhakikisha haki inatendeka. Na si kuwa nyny mkishinda tu haki imetendeka mkishindwa haki haijatendeka huko ni kutokuwa watu wa haki.
sawa ridhiwan kikwete lakini mahakama ya kweli ni wananchi,fanyeni mpango kutengua na urais babako!
 
Mabadiliko ya kweli hayatapatikana mahakamani, bali kwa wana wa nchi hii watakapoamua uamuzi wa haki. Hivyo nimetambua busara ya wana CDM kwa kutambua hilo kwa kutokata rufaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom