Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Huu si ndio usultan niliokuwa naulalamikia? Utendaji wa baba wa mtu unawezaje kuwa kipimo cha mtoto wake? Wameamua kumtoa kafara tu huyu dada wa watu, kama kweli wanampenda na kumjali si wangempa uenyekiti wa chama chao hapo Arusha?
 
Siyoi has a super super job that pays him handsomely... Acheni *****

Janjaweed,
Sasa alifuata nini kwenye Ubunge kama ana hiyo Super Job inayomlipa vizuri? Ukweli ni kwamba kazi aliyonayo haimtimiziii mahitaji aliyoachiwa na Baba yake. Mzee Sumari kazaa nje ya ndoa watoto watatu ambao wote wapo under 19 years. Wakati Sumari anakufa Sioi aliachiwa jukumu la kuhakikisha hao watoto anawasomesha vizuri hadi wafike Chuo Kikuu. Sasa ukichanganya na majukumu ya familia yake, Mzigo alionao Sioi ni mkubwa sana. Apewe tena nafasi ya kujaribu Arusha Mjini.
 
Kama CCM walishindwa kujifunza Arumeru sasa watapata somo Arusha Mjini.
 
Walete watoto wote wa marais, mawaziri wakuu, wote wataangukia pua.


Hata wakimfufua Baba yake agombee kwa CCM hatoboi! watu wanafikiri watu wa Arusha ni kwamba Godbless ni mzuri sana kuliko wote? hapana ni kwamba CCM hata imsimamishe nani kupitia ccm hawezichukua, na sasa ndiyo wametengeneza hasira kali kwa wananchi kuhusu hili jimbo. aje tu kuchafua jina lake
 
Kama CCM wanafagilia kusimamisha mwanamke kwani ni lazima wamsimamishe Mtoto wa kigogo?
Kwanini wasimpendekeze Katherine Magige?

Huyu naye anatoka zile familia zenye copyright ya kutawala watanzania?
 
nnguu007,

..Joseph Sokoine amepigwa marufuku Tanzania na Edward Lowassa.

..adhabu yake ya kuishi nje itaisha pale Edward Lowassa atakapouchoka ubunge wa Monduli.

Haaaa,kumbe Lowasa ana uwezo wa kuwapa BAN watanzania wasirudi nyumbani?
OMG
 
Huyo dada namfahamu ni mshenzi sana na sijui alipateje pataje ubunge wa viti maalumu kupitia Monduli!!!!

Akigombea huyo hata kama CDM ikisimamisha kivuli, kivuli kitashinda tu na siyo yeye tu hata JK akija hapa atashindwa maana hata kura zar urais Arusha hazikutosha dhidi ya Dr. Slaa.

Hapa kwenye red. Hebu funguka zaidi.
 
Nakumbuka sana siku Lowassa alipokuja kumpigia kampeni AICC kupitia viti maalum.
Wamama walilalamika sana kitendo cha Lowassa kuja kumpigia kampeni hawara wake. Tena walidai kuwa Lowassa anataka kuwaweka hawara zake tu, maana Jimbo la Arusha alifanikiwa kumpitisha hawara mwingine ambaye ni Batilda.

Lowasa kidume eeehh???:shock:
 
Hivi ni vizazi hivyo tu vyenye karama za uongozi?? Tunachoka jamani majina, koo, familia zile zile!!
 
Acha ile Dada yake alikuwa Miss World Africa Nancy Sumari; Dada Mwingine Mwimbaji kasaini na SONY alikwenda Chadema kugombea Ubunge Chadema hawakumpa sababu alijiunga sababu ya Ubunge akarudi CCM kwa kishindo na kupokelewa na Kikwete pamoja na baba yake kabla hajafariki... sasa wadogo zake gani anasomesha???

Wote wanajitegemea na wana pesa...

acha kuchanganya mambo nancy na nakaaya baba yao mwingine kabisa na sioi baba yake ni mwingine, hayo ni majina ya ukoo tu... Inaweza kuwa sumari mdogo na mkubwa.
 
nnguu007,

..Joseph Sokoine amepigwa marufuku Tanzania na Edward Lowassa.

..adhabu yake ya kuishi nje itaisha pale Edward Lowassa atakapouchoka ubunge wa Monduli.

Kwa nini Joseph Sokoine amepigwa Marufuku na Lowasa?
EL ana uwezo gani wa kumpiga marufuku Mtanzania asije nchini kwao?
 
Janjaweed,
Sasa alifuata nini kwenye Ubunge kama ana hiyo Super Job inayomlipa vizuri? Ukweli ni kwamba kazi aliyonayo haimtimiziii mahitaji aliyoachiwa na Baba yake. Mzee Sumari kazaa nje ya ndoa watoto watatu ambao wote wapo under 19 years. Wakati Sumari anakufa Sioi aliachiwa jukumu la kuhakikisha hao watoto anawasomesha vizuri hadi wafike Chuo Kikuu. Sasa ukichanganya na majukumu ya familia yake, Mzigo alionao Sioi ni mkubwa sana. Apewe tena nafasi ya kujaribu Arusha Mjini.


mmh haya tukae mkao wa kula, tutayajua mengi sana hapa.
 
kwa kuwa magamba wana mpango maalum wa kutumia mahakama ili kuchukua jimbo la arusha.
Naomba kuwasilisha ombi maalum kwa cdm.

Uwezo wa lema katika kujenga chama ni mkubwa sana,vile vile uwezo wake katika kampeni zinazohitaji purukushani ni mkubwa mno.wana cdm watakubaliana nami kuwa lema kwa kiasi kikubwa amefanikisha ushindi wa nassari kule arumeru hivyo lema ni mtu muhimu katika kukuza chama.

Tumpe lema operation ya kukomboa waliolala.tumpe kazi zofuatazo:

1.kuhakikisha jimbo la arusha linarudi cdm kwa ushindi mnono

2.kuhakikisha jimbo la monduli,simanjiro na arumeru magharibi yanachukuliwa na cdm hapo 2015

3.kuhakikisha cdm inapata wanachama wapya kutoka vyuo vya elimu ya juu au ufundi,wamachinga,wauza nyanya na madereva toyo hasa vijana.

Chadema tumieni makosa ya ccm kuiadhibu,muwezesheni lema abomoe kambi ya ccm kaskazini najua atafanikiwa.
 
Mkuu Nanyaro nashukuru umeni PM nimesave hiyo namba nitakutafuta nikirudi Arusha.
 
kwanza nashukuru sana jaji alietoa hukumu kwani alijua wazi nini wanachadema wanasubiri,ccm wanahela ya mchezo,badala ya kutatua kero za wananchi angalau waweze kufikiriwa 2015 wao wako kwenye malumbano na chadema,kamwe technic wanyotumia chadema ccm hawawezi,wao chadema wako kikazi zaidi na ccm wako kimalumbano zaidi,sasa basi mwanya mwingine wakuikosoa serikali kwenye kampeni za ubunge wa arusha.lema atabakia kuwa lema tu.kwa hasira za wanaarusha kuwaonyesha majaji na serikali kuwa wao ni majaji namba moja serikali na majaji ndo wanafuatia ni kwenye box la kura.serikali ijaribu kufikiria kabla ya kuchukua hatua.
 
ccm inapoteza rasilimali kubwa kwa mambo yasiyo na msingi hizi pesa zitakazo tumika kwenye kampeni si zingejenga hospitali nyingi tu nchini
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom