Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Tunakwenda kutoa adhabu kwa CCM kitu ambacho kitavunjavunja hushangai hawashangilii jimbo kuwa WAZI.Wanajua kikombe hiki cha CDM lazima wanywe!
 
Mimi sijui kama hili swala litaenda bila mtu kupata risasi ya Kifua au mgongo. Risasi zinapata kutu stoo ya silaha kanda ya Arusha. Wanafaham kua damu haitamwagika bure ila wanalazimisha.
 
Kama mbwai mbwai tu, chadema ikate rufaa.

Huyu jaji anadhihirisha wazi bila kificho kwamba ametoa hukumu isiyo halali kama kweli kifungu alichokisoma mbele ya kadamnasi sicho alichokiandika kwenye ruling yake, na kwa namna hiyo atakuwa ameidhalilisha sana mahakama na kuishusha mno hadhi yake, na kwa hali hiyo anaifanya mahakama iendelee kutoaminiwa na wananchi.

Ni jambo ambalo halikutarajiwa kwamba ubunge wa Lema utenguliwe halafu asizuiwe kugombea, tangu mwanzo nilikuwa sijaamini taarifa hiyo kwakuwa ccm wanaamini mwiba mchungu kwao ni lema, kwahiyo ni lazima wamuweke benchi. Lakini uzuri mmoja wa arusha ccm hawawezi kushinda ubunge hata lema asipogombea.
Nimeanza kuwa na mashaka na wewe.
 
hizo gharama za uchaguzi zingeweza nunua madawati huku chamwino,bahi,kongwa,mpwapwa na wilaya mpya ya chemba.
 
zipo fununu kwamba fungu la fedha za uchaguzi mdogo Arusha mjini halitakuwepo katika siku 90 hivyo uchaguzi unaweza kuchukua muda zaidi kama ilivyo kwa wale madiwani wa chadema waliofukuzwa lakini hadi sasa wanaendelea na majukumu yao.
 
Nahitaji kusoma nakala ya Hukumu kama nitaona kuna dalili za CCM kuingilia kwa mchakato wa kesi husika, nitajitoa rasmi CCM na kujiunga na CHADEMA.
Haiwezekani kila mahala panajisiwe kwa ajili ya interest ya kundi la wachache, hata mahakama iliyotakiwa kuwa mzani na kimbilio la wote inajisiwe?? Hapana, nahitaji niisome hiyo hukumu...kabla ya kufanya maamuzi.
 
Aibu moja haijaisha CCM wanajiingiza katika aibu nyingine. Unaweza kununua mahakama zote duniani lakini huwezi kununua nguvu ya umma
 
Yaani huku ni kupoteza pesa na kumfanya lema aonekane mtu wa vurugu, mbadhilifu na asiye leta maendeleo A-town ila kwa hili ccm watashndwa sababu wanachomfanyia lema ni kinazidi kuwa bomoa, mfano viongozi wao waliofanya kampen Arumeru ndo walio ipaiza cdm na wanacho kifanya sasaivi ni kuwapa cdm umarufu pamoja na lema...
Giza haliwezi kutawala nuru.
 
Nimepokea sms toka kwa jamaa yangu wa karibu ambaye ni kada mkubwa wa magamba kanidokeza kuwa kuna tetesi chama kimejipanga kumrejesha mgombea mwanamke na chapuo linamwendea Mbunge wa Viti maalumu Ndugu, Dada yetu Nameloki Sokoine. wadau mwasemaje? je huyu dada katolewa kafara ama magamba wanategemea kutumia historia ya baba ya binti huyu, waziri mkuu kipenzi cha watanzania Hayati edward moringe sokoine kwa manufaa yao? sielewi!
 
ili kutoa simanzi ya kufiwa na baba yake?Wana arusha wamesema hata kama Chadema watasimamisha jiwe na CCM wamsimamishe Kikwete CHADEMA itashinda!!!
 
Anazuiwa kwa sababu gani? Kuna suala la kutumia rushwa kama hukumu ya Waryoba dhidi ya Wassira?

Mkuu Kimbunga,
Safari hii utabiri wa Mwanakijiji umekwenda alijojo...

Alisema Lema atashinda kesi hiyo ya uchaguzi ana 99%99.

Hakasahau kuwa masuala ya sheria hayana uhusiano na utabiri.
 
nimepokea sms toka kwa jamaa yangu wa karibu ambaye ni kada mkubwa wa magamba kanidokeza kuwa kuna tetesi chama kimejipanga kumrejesha mgombea mwanamke na chapuo linamwendea mbunge wa viti maalumu ndugu, dada yetu nameloki sokoine. Wadau mwasemaje? Je huyu dada katolewa kafara ama magamba wanategemea kutumia historia ya baba ya binti huyu, waziri mkuu kipenzi cha watanzania hayati edward moringe sokoine kwa manufaa yao? Sielewi!


nadhani hajasahau mafisadi walichomfanya baba yake, au anafikiri wamechoka kutoa kafara? Nitamsahangaa sana akikubali kutolewa kafara!
 
Hakuna damu kumwagika, Kamanda mbowe kesha tuambia tukae kwa utulivu ili dunia waone kuwa CDM ni chama makini. tunawasubiri ccm kwenye uchaguzi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom