Gwankaja Gwakilingo
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 1,996
- 617
mwerevu yamtosha ishara
Mh.Godbless Lema ndani ya miaka miwili tu, ameweza kufanya mambo makubwa lakini watu wamekuwa wakifikiri tofauti kwakuwa hawajui majukumu ya mbunge ni yapi...!
1.Godbless Lema Kupitia mradi wake wa ARDF ameweza kusomesha watoto na kulipia ada zaidi ya 1000, sidhani kama kuna mbunge ndani ya bunge la Tanzania amefikia rekodi hiyo..! na tena hana hata mfadhili zaidi ya yeye mwenye kujitolea pesa zake za ubunge ambazo alipewa kwaajili ya kununulia gari..!
2.Godbless Lema amekuwa kiongozi wa kwanza kwenda Gerezani na kujua kitu gani kinachoendelea Huko gerezani..,baada ya kusema bungeni manyanyaso wanayopata wafungwa, jinsi hata wafungwa wa kike wanaishi gerezani bila hata kupewa pedi...!
3.Godbless Lema ameweza Watanzania kujua jinsi gani kulivyokuwa na uozo jeshi la polisi, ambako watanzania wengi wemekuwa wakibambikiziwa kesi bila sababu za msingi...!
Jamani ni vigumu GODBLESS LEMA baada ya kufanyiwa mizengwe na CCM kwenye harakati zake za kuwatumikia wananchi..,mfano kwenye uchanguzi wa Meya mh.Mbunge alipigwa kama mwizi na polisi baada ya uchaguzi wa umeya kufanyika bila halali, na vile vile SERIKALI YA MAPINDUZI KWA MAKUSUDI walizuia MAANDAMANO YA CHADEMA ili POLISI KUINGILIA NA KUFANYA FUJO KWA KUPIGA MABOMU WANANCHI...!
CCM NDIO WANAPENDA FUJO NA MATUTSI, KWA KUTUMIA JESHI LA POLISI, NA WABUNGE WAO WAMEKUWA WAKITUMIA PESA KUWALAGHAI WANANCHI TOFAUTI NA MH.LEMA ANAPIGANIA HAKI, KULIKO KUMPA MTU ELFU KUMI ALAFU KESHO HANA KITU, KULIKO HAKI ITAMLINDA MTU MAISHA YAKE YOTE
CCM mmeshaanza kuhaha na kuanza kampeni kwamba Lema hafai, hiyo mbinu katumieni kwenye kampeni labda itwasaidia angalau msipate 0.Baada ya kuenguliwa ubunge wa Arusha,sasa bwana GODLESS LEMA anakabiliwa na pigo lingine kubwa ambalo wadadisi wa mambo wanaamini linaweza likamfanya ashindwe kutetea kiti chake na hivyo kushindwa kuingia bungeni! PIGO hilo linahusiana na yeye kuwaambia WANAARUSHA tangu achaguliwe miaka miwili iliyopita ameshawafanyia nini wanaARUSHA mpaka sasa? LEMA amekuwa akihaha huku na huko,kushiriki maandamano yasiyo na TIJA baada ya kujikita katika kuleta maendeleo na kutimiza ahadi, inadaiwa mpaka sasa lema hajafanya chochote arusha, utalii umeshuka kutokana na maandamano yake ya mara kwa mara,hili kwa kweli ni PIGO SANA KWAKE NA CHAMA KWA UJUMLA!
MYTAKE: KAMA CHADEMA WANAWEZA WAMSIMAMISHE MTU MWINGINE ARUSHA
Hata mumsimamishe Slaa, hampati kitu hapa. CCM tumejipanga kulichukua hili jimbo hata kwa bilion 900. Mtajibeba!!!
Lema alishajua ni jinsi gani kesi ilivyokuwa imepangwa na dhahiri uhamuzi ulikuwa ni mahakama kumpiga chini kwa vyovyote vile:
Akiongea via Star TV mara baada ya hukumu kutolewa Lema ameeleza yafuatavyo ktk kudhibitisha hilo.
1. Lema amesema; kabla ya kwenda mahakamani asubuhi amepitia ofisini kwake kama kawaida lkn alishangaa kukuta kundi la askari polisi zaidi ya 50 wakizunguka ofisi yake kana kwamba kuna jambazi wanamvizia- swala hilo limemfanya afikilie kwamba hao askari polisi tayari walikuwa na majibu juu ya hukumu na wakiamini kuwa haitawependezesha wapiga kura hivyo kuhamua kuweka ulinzi mkali.
2. Wakati wko Bungeni Lema alimtakia Waziri mkuu kwamba amesema uongo Bungeni; jambo ambalo lilimfanya Mh. Lukuvi amwambie Lema kwamba hana nidhamu na kwa vile kesi yake hiko Mahakamani basi watatafuta namna ya kumwadabisha.
3. Mh. Rais mwaka 2007 alimuita Lema na kumuomba agombee Ubunge jimbo la Arusha mjini kupitia tiketi ya CCM jambo ambalo Lema hakuliafiki na tangu siku hiyo mahusiano hayakuwa mazuri kati ya Lema na viongozi wakuu wa CCM.
4......
Kwa kauli yake Lema anasema hawezi kutishika na huu uhamuzi uliojaa mizengwe; kwa vile mahakama haijamuzuia kugombea tena, nafasi aliyonayo nayo ni kubwa kuendelea kuwatumikia wananchi wa Arusha. Lakini anashangaa kwanini Judiciary Machinery inaingiliwa na State Machinery.
Wembe gani!
Mkitaka CDM ifutike mumcague agombee tena! Wale madiwani 5 wa CDM waliofukuzwa tutawatumia vyema this time maana walikuwa na bifu na LEMA
itakuwa ni busara kwa CDM kutokata rufaa kwani uchaguzi ukirudiwa mwendo mdundo