Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Sioni haja ya kukata rufaa tusubili uchaguzi mwingine hao magamba watakuwa wamejimaliza wenyewe chama kisiofie gharama wakereketwa tutachangia waseme badget yao ya uchaguzi huo pale watakapokuwa wamekaa sawa.
 
Hili lilikuwa wazi sana kuwa Lema atavuliwa ubunge, kitendo cha Batilda Burian kutokutokea kutoa ushahidi na Jaji kufunga bila shahidi mkuu huyo kutokea mahakamani ilikuwa ishara tosha.
Pamoja na Majaji kula viapo vya kutenda kazi yao vizuri, Jaji Mkuu MH. Chande alinukuliwa akilalamika Serikali kuingilia Mhimili huo muhimu na matokeo yake ni hayo.
Pesa za walipa kodi zitatumika tena kwenye uchaguzi mdogo wakati umaskini umetukalia kooni.

Shahidi Mkuu ni Batilda kivipi?

Batilda hawezi kuwa shahidi mkuu kwa sababu hana kawaida ya kuhudhuria mikutano ya Lema, kwa hiyo hana uhakika na alichokisema Lema katika mikutano yake ya kampeni
 
Kaka umeniibia mawazo yangu utafikiri ulikuwepo na mimi,hiyo hukumu naisubiri sana kwa hamu
 
Nilisikia kama Hakimu alipewa kitita cha kutosha ili kutoa hukumu ya aina hiyo. Tatizo la mahakimu na polisi wetu huwa hawaoni aibu hata kidogo kupindisha sheria ilimradi waweze kulinda maslahi ya CCM. Sasa mtashangaa hukumu ya jimbo la segerea hapo Miltoni mahanga atakapoonekana hana hatia.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Tulianza na mungu na tutamaliza na mungu,tuwe na moyo wa subira wana jf na chadema kwa ujumla na watanzania wapenda haki,
 
Duh. Big soo! Hizi by-elections zinatuharibia uchumi
 
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"][/TD]
[TD="class: buttonheading, align: right"] Send to a friend[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Thursday, 05 April 2012 10:56[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Arusha imetengua matokeo ya ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini hivyo kumvua ubunge Godbless Lema wa Chadema. Taarifa zaidi soma gazeti la Mwananchi kesho[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Tanzania mahakama zote ndo zilivyo!hakuna haki,nimekua nikifuatilia sn,kwa ukaribu mkubwa hii kesi ya mh lemah,mim sina shahada ya sheria lakin hakuna ushahid wowote uliopelekea hata kwa mbali mh lema kuachishwa ubunge. Ukitaka kuamin haya, embu tizama na ufuatilie kwa ukarib ktk kesi ya mh Tundu Lisu na hiyo ya Mh JohnMnyika ndo utagundua hila ya ccm,hakika mim nataman kumdhuru mtu yeyote wa ccm
 
Naunga mkono wenzangu, hakuna haja ya kukata rufaa, acha hukumu iwe kama ilivyo ili turudi kwenye uchaguzi, naamini CCM hawawezi kupata kitu wanajisumbua tu
 
mbona ya Lema imeenda fasta? tunaomba na ya kigoma mjini ifanywe fasta hivohivo. maana mshindi hakuwa serukamba alikuwa mgombea wa cdm. sasa itakuwaje kisheria maana Batrida tayari ni balozi na yuko kenya? je sheria inamruhusu kuwa balozi na mbunge at the same time?
Uchaguzi utarudiwa
 
Hukumu inasema anaruhusiwa kugombea tena,tunaomba mpaka mwenyekiti wa chama c.c.m nae awe kwenye kampeni uchaguzi huo mdogo!hakuna kukata rufaa turudi kwenye chaguzi
 
Nadhani sheria imechukuwa mkondo wake, Jaji wa kwanza Lema alimkataa alikuwa hana imani nae Jaji wa pili katenda haki.
 
Tusubiri uchaguzi. Kuna mdau anasema kwa vile mda umeenda, kuna uwezekano wa arusha kukosa mwakilishi mpaka hiyo 2015
 
its okey, kifuatacho ni kusimama na kujipukuta vumbi kisha tusonge mbele, tunamtanguliza Mungu na ccm itaibika tena
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom