Katika pitapita yangu, nimekumbuna na hii kwenye Forum za Watanzania:
MABOMU KIKOSI CHA JESHI 511 GONGO LA MBOTO
· Mimi nimeona mwanga mkali nauona nikiwa hapa ubungo nikafikri labda kuna kituo cha mafuta kinaungua moto huko tabata kumbe ni Gongo la moto imelipuliwa???
· USIOMBE KUSIMULIWA ONA MWENYEWE KAMA VILE MUVI FULANI HIVI, jIji linarindima kwa sauti ya kutisha ya mabomu inasikika.
· Tayari redio zinatangaz na TV, KUMBE GHALA LA SILAHA LIMELIPUKA HUKO JESHINI Gongo la Mboto.
· Nimepiga simu kwa shemeji yangu, akiwa kazini, ametoka mbio kwenda nyumbani gongo lamboto, anasema hali ni mbaya sana, amekimbilia nyumbani kuangalia USALAMA WA FAMILIA, amekuta hakuna watu nyumba zote zimehamwa, watu wanakimbia ovyo ovyo, hajuin familia iko wapi, kibaya zaidi aliacha watoto na houseirl, nyumba za karibu zimesawazishwa ardhini. Anasema atanipigia baadae.
· Nilipofuatilia kwa simu baadae akawa hapatikani kwenye simu, sijui kilichompata mpaka hapo kesho nitakapo kwenda huko nitajua.
· Rafiki yangu mwingine anasema jamaa zake walikimbilia kanisa la karibu, bomu bomu limewafuata na watun saba wamekufa humo ndani na watu 40 wako mahututi.
· Kisukuru nao huko tabata bomu limetua na haijajulikana watuy wangapi wamekufa.
· Mwanga mkali na anga la jiji lilikuwa jekundu kwa mlipuko wa mabomu maeneo ya huko Vingunguti, hgongola mboto , Airport.
· Watu wangi kutoka eneo la Mombasa, banana wanakiimbia mchaka mchaka mkuelekea mjini.
· Ni kama vile ambush ya kivita maeneo hayo, mabomu yanalipuka hovyo hovyo maeneo hayo, watu wamechanganyikiwa wanakimbia ovyo hawajui waendako ili mradi tu kuliepuka eneo hilo.
· Hakuna usafiri tena wa kwenda huko Magari yote ya wakaazi wa huko tokea mjini hayaendi huko, hakufikiki usiku huu.
· Watu wamezuiwa kurudi huko, wamezuiwa kulaa kwenye viwanja vya uhuru Dar.
· Ukonga Mageraza: Boumu limedondoka karibu na gereza, wakati watu wanakimbilia uwanja wa magereza mbele yao likadondoka bomu , watu wanaelekea kichanganyi mbele yanaendelea kundoka kwenye nyuma za karibu, hapo kila mtu anaangalia wapi akafiche kichwa chake.
· Vibaka nao ndio peak ya mavuno yao.
· Majeshi yanasaidia kuzima moto mitaani, lakini pia Serikali inawaomba wanachi waondoke katika maeneo hayo kiasi cha umbali wa kiliomita 10 tokansehemu ya mlipuko wa silaha hizo.
· Majeshi yoteya polisi yameamuliwa kuelekea huko kutoa msaada kuokoa watu na mali usiku huu.
· Mabomu mengi ne yameingia kwenye nyumba za watu na bado hayajalipuka
· MAWASILANO YA SIMU NA WATU WA E NE HILO YAMEKUWA MAGUMU. SIJUI NDUGU ZANGU WATAKUWA HAI MPAKA ASUBUHI HII
· Taarifa zaidi zinaendelea...kesho.
· Ni saa saba hii usiku naomba nikalale.
Swali BINAFSI:
Tulipendekeza na kushauri serikali ya Kikwete kuwa ghala za silaha zihamishwe zitoke kwenye makazi ya watu kutokana na somo tulilolipata kule Mbagla. MABOMU YA MBAGALA!!!
Kuna organization au uongozi wowote uliofuatilia uhamishwaji wa silaha hizo??
Bado maghala ya jeshi ya Lugalo, MBWENI,Makongo/ Mwenge, nyuma ya chuo Kikuu nk
Hii ni hujuma au bahati mbaya??UZEMBE AU NI MAKUSUD??
Tukio la mwaka ule liliongelewa sana na watu walipiga sana kelele juu ya maghala ya silaha na utunzwaji wake, je tulifikia wapi??
Hili ndilo jeshi letu la karne hii la wasomi.........
Bado tutaendelea kujiua wenyekufa kabla hatujaenda vitani
Usiku mwema