Inasikitisha kuona wachangiaji wengi kwenye hii forum wakichukulia ajali iliyotokea Gongo la Mboto kisiasa.
Pamekuwa na wachangiaji wanaothubutu hata kuhusisha chama cha siasa au ufisadi na milipuko hiyo.
Si ustaarbatu kukurupuka na kutoa majumuisho yasiyo na mantiki. Kulilaumu jeshi au serikali kabla ya kujua chanzo cha milipuko hiyo ni kukosa busara. Wengine wanajidai wanajua hata umri wa mabomu yale, yalivyohifadhiwa na mambo mengine ya taaluma za kijeshi ambazo si kila mtu anazijua.
Tuwe na subira. Kama itagundulika kuwa ni ajali, ieleweke kuwa ajali ni ajali, hata kama ilitokea Mbagala yaweza kutokea pengine pia, hizo ndo ajali.
Mtaalam mmoja wa milipuko amenieleza kuwa mlipuko kama ule unaweza kusababishwa na mambo mbali mbali. Inawezekana ikawa kweli ni umri wa mabomu, au shoti ya umeme au uzembe wa mtu mmoja au hujuma kutoka kwa watu wabaya kama baadhi ya wanachama wa chama cha siasa wanaotaka Tanzania isitawalike.
Tuache kupotosha mambo, tusubiri wataalam wafanye kazi yao na umma utataarifiwa tatizo lilikuwa nini.