Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Hadi muda huu hakuna tv station iliyofanya uzito wa hili janga so sad, ni bongo fleva tu, hivi ingelipuka kambi ya upanga wangekaa kimya? Tatizo ni wanahabari??wamiliki?? Au hadi wapate ruksa baada ya kuchuja. Daaah nnahasira, then kova anasema uvumi, uzushi unawachanganya wananchi, si watoe tamko la kueleweka?? I wish wahanga waunganishe hadi ikulu. Time will tell.
 
hizo mil 90 walizopewa Kila mbunge kununulia ma VX, sizingetumika kununulia madawa, na kutoa fidia kwa waathirika wa mabomu
 
wenye kuvaa kijani ngoja tuone . Si ndio mko huko . Tulisema ccm maafa hamkusikia
 
At last iam a bit happier maana nimewasiliana na ndugu zangu wote ndio wanajikongoja kurudi majumbani kwao baada ya kuona hali inatuliatulia.
Thanx Jesus!
 
Poleni sana kuna nyumbna iko kinyerezi imeungua ni nyumba mpya haina hata miezi 2 tangu wenyewe wahamie poleni sana Mdoe Family....poleni sana....
 
Its a matter of zamu tu hapa dar. Makambi ya jeshi yamesambazwa jiji zima

mbagala
lugalo
gongo
Kigamboni
mabibo
lugalo
kawe
mgulani
mwenge
kurasini

Umesahau na Kunduchi mtongani. Likilipuka la huko au Lugalo na yuleeee wa.z.r. wa kulindana huenda atakumbwa na hilo litakuwa funzo.
Ee Mwenyezi Mungu tupe Rehma zako na tuepushe na majanga haya.
 
Kwa hiyo watu wanaenda kulala uwanja wa taifa!
 
jamani, what a country!? kila mtu duniani atakua anashangaa kama mimi na maswali mengi juu ya hilo. sijasikia kitu kama hicho katika nchi jirani. tanzania tumekosa nini!? wahusika wa jeshi wanafanya nini? intelijensia?
 
Hivi Kamanda Kova alipowataka wananchi warejee majumbani kwao alimaanisha nini hasa? Manake nimeshindwa kabisa kumuelewa kusudio lake..
 
Back
Top Bottom