Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

majeruhi wengi sana pamoja na maiti zinapelekwa mortuary hospitali ya amana.
Radio iman
 
Mi nishachoka nakwenda lala.... nisubiri utumbo wa kesho:angry::angry::angry:
 
Wajameni haya maswala ya kulipuka mabomu na baruti za jeshi kunakotokea kila siku ni uzembe wa wahusika! mbona linachukuliwa ati kama ni bahati mbaya? kivipi kila kitu chini ya serikali ya Kikwete ni bahati mbaya tuuu... rushwa bahati mbaya... mabomu Mbagala bahati mbaya...tahadhari haikuchukuliwa na watu wanalala nje mpaka leo... yatafuatia kambi ya jeshi Mgulani, then Changanyikeni, then Kigamboni naomba yaanzie Kigamboni maana ni karibu na Ikulu ili washtuke na hisia za hila za ugaidi kutaka kuhatarisha maisha ya presidaa labda sikio la kufa litaskia dawa! wahusika wata-act kulinda usalama wa wananchi!

Huu uzembe inapaswa watu wajipime mapema....! Ama siku jiji zima litaungua moto!
 
shida hawa wanajeshi wanaondolewa katika shughuli zao za jeshi na ku monitor usalama katika maghala ya zana za kivita wanaletwa katika kutetea wanasiasa na kutisha wapinzani. Matokeo yake ndiyo hayo. Sasa intelligensia ilikuwa wapi kama haingalii mahali nyeti kama yanapotunzwa mabomu na zana nzito nzito? Inteligensia feki inayojua yatakayotokea kwenye maandamano ya Cuf Buguruni na Arusha ikashindwa kujua yatakayotokea Mbagala na Gongo la Mboto. Mabomu yana pita muda wake hawana habari, mengine yanapangwa vibaya wahana habari, hawachukui hatua za kiusalama mapema. Wapi taarifa za safety audit na vipi juu ya safety inspections??? Twambieni sasa. Si tayari kuna mtoto mmoja hatumwoni wengine wote wamepatikana baada ya kupoteana kwa masaa matatu. Tanzania, Tanzania!!!!!Q!
 
Na hakika jinsi mabomu na missile zilivyokuwa zimehifadhiwa ni mwelekeo PUGU. KISARAWE n.k hivyo wanaJF wa mwelekeo huo(PUGU, KISARAWE, PUGU KAJIUNGENI n.k) tupeni yanayojiri, maana lazima yatakuwa hayakuelekezwa UPANGA, FERRY au O"BAY
 
Kova anasema TBC kwamba askari wote wa polisi wameitwa kazini na wako barabarani hata wale wa intelijensia! My foot!
 
Kova anatoa macho TBC,

Anasema kuna watu wanavumisha eti watu wanakimbia hovyo na watoto wamepotea

pumbafuuuu

Usingizi umekata, ati asemajeeeeeeeee.....!!!! huyu jamaa vp lakini, ile VX v8 ndo inamfanya aseme yote haya bila kujali ukweli wa mambo?
Yeye kafika kwenye eneo la tukio au anaota tuuuuu
 
Polen wahanga wote wa Gongola mboto, watoto wamepotezana na wazazi. Hv hii serikali c inakitengo cha maafa ofisi ya waziri mkuu au ndio hadi kesho?? Jamani kila cku semina za emergency preparedness. Halaf Kova nae anatuchanganya !! Aaah hii nchi bana
 
Haiwezekani bwana Tanzania ni nchi ya AMANI NA UPENDO mbona raia wake hawachukui hatua kama hawapendezwii!!! :coffee::coffee::coffee:
 
Kova anasema TBC kwamba askari wote wa polisi wameitwa kazini na wako barabarani hata wale wa intelijensia! My foot!

Muulize yeye yuko wapi????? itakuwa hao wenzie mxsiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Dah nina hasira hata kumeza maji nashindwa!!! Zile milioni 90 kawasaidieni basi waathirika wa mabomu!!! Hii nchi kwakweli inakera
 
saa hizi wanachakachua majibu ya kutuletea kesho kwa runinga, na kama wataunda tume itaundwa
 
Tuta pigwa siasa tu. Viogngozi wata ahidi kufanya uchunguzi, waathirika wata ahidiwa vijisenti. Wananchi wakiongea sana itaanzishwa "kamati". Do you expect anything new?
Only it would sound if someone stepped down!
Hata wakilipa bilioni moja moja kwa wathirika, kama hawana sense ya kuwajibika ni sawa na kuitupa chooni!
At least thats what we wait to see!
 
Hivi pale lugalo hakuna silaha, kama zipo siku zikilipuka si itakuwa kizaazaa...
Bila kusahau na pale Upanga,
Nawashauri wakazi walio karibu na hayo makambi wakae kimagutu kama si kuhama hayo maeneo
 
Back
Top Bottom