Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Waungwana nipo mitaa ya hapa jet lumo mabomu ktk ghala ya polisi ya ukonga yanalipuka yani angani kuna mataa kama ya baruti au mafataki,lol tz tunaenda wapi?

Acha kutudanganya polisi hawana mabimu mkuu!!!
 
Bila kusahau na pale Upanga,
Nawashauri wakazi walio karibu na hayo makambi wakae kimagutu kama si kuhama hayo maeneo

Afu Opposite kuna Ile hospitali inaitwaje tena???
 
Lugalo ikilipuka nayo sijui itakuwaje au hapo lugalo hawaweki mabomu. hizi kambi zihamie mbali na makazi ya watu
 
Huu ni UVUNJIFU WA AMANI usio na kiwango na ambao haujawahi kutokea katika nchi ye yote ile (kwa uelewa wangu), Mabagala na sasa Gongo la bongo. Ndoo maana tuliambiwa mwaka jana MAAFA.
 
Its a matter of zamu tu hapa dar. Makambi ya jeshi yamesambazwa jiji zima

mbagala
lugalo
gongo
Kigamboni
mabibo
lugalo
kawe
mgulani
mwenge
kurasini
 
saa hizi wanachakachua majibu ya kutuletea kesho kwa runinga, na kama wataunda tume itaundwa

Mhusika mi nasema hivi...! Nimeshachoa kuona kodi yangu inavyotumika vibaya na TUME zako, sitaki tena tume ninataka mawajibiko.
Hizo tume baki nazo mwenyewe zitakusaidia ktk maisha yako binafsi sisi hazitusaidiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
kuna bomu limeruka mpaka mbagala na kuua mtoto.
Clauds FM
 
Hii serikali bana!!! Nimesikia Radio One saa hii kuwa wamefungua Uwanja wa Taifa ili watu wa maeneno ya Gongo la Mboto wakalele huko!!

Wanaenda kulala bila nguo wala nini!!!
 
Hajui mipaka yake, kazi sio kuwa na ofisi tuu na gari zuri la kutembelea

Naona anatakiwa kuitizama Contract yake ya kazi na kuielewa vyema
Utafikiri yeye ndio Mwamunyange eti ni ajali,ajali anaijua anafikiri hayo ni madawa ya kulevya au ujambazi,same thing in two years halafu unasema ajali
 

Hisani ya Kituni na Dedichijr wa Youtube
 
Last edited by a moderator:
Najaribu TBC haipatikani!!!

Inteligencia gani tena... my foot this country...
 
If we have no clue on how to store explosives we should not own them.

It is not about owning .....but rather a case of an irresponsible government that harbors irresponsible individuals.

Safari hii umma lazima ushinikize watu kuwajibishwa na kama JK hatawajibisha yeyote, then hii itumike kushutumiza wabunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na uongozi wake.

Katawala kwa miaka 5 lakini bado nchi ni giza, mashirika ya umma yanakufa (TRC, ATC, TANESCO, THA n.k), inflation inazidi kupanda, elimu inadidimia kupita kiasi, wanafunzi wanfeli, wahujumu uchumi ndio wenyeviti wa kamati za bunge, halafu sasa mabomu yanaendelea kulipuka na kuua watu. Hivi kweli tuna uongozi?
 
Hii serikali bana!!! Nimesikia Radio One saa hii kuwa wamefungua Uwanja wa Taifa ili watu wa maeneno ya Gongo la Mboto wakalele huko!!

Wanaenda kulala bila nguo wala nini!!!
Wawapelekee na huduma ya kwanza sio unaenda kulaza watu kwenye uwanja kama vile unalaza ng'ombe kwenye zizi
 
Mkono wa mtu moyo na kanga na viatu seems ni vya mwanamke vimeonekana
Source Radio One
 
Mhusika mi nasema hivi...! Nimeshachoa kuona kodi yangu inavyotumika vibaya na TUME zako, sitaki tena tume ninataka mawajibiko.
Hizo tume baki nazo mwenyewe zitakusaidia ktk maisha yako binafsi sisi hazitusaidiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
tume lazima iundwe...
 
Back
Top Bottom