Gari ya nyonya damu kwa waliosoma miaka ya 90

Gari ya nyonya damu kwa waliosoma miaka ya 90

Mnakumbuka na ile usipokula mchicha unaambiwa Mandela anakuja kukunyonya damu
 
Kijijini kwetu ilikuwa balaa. Siku mmoja padri alisimamisha land rover katika msitu kuwapa lifti kinamama walikuwa na mizigo ya mapeasi walikimbia vibaya sana chini ya gema la barabara kwa woga, sijui kipi kilisalimika kati ya viungo vyao na mapeasi. Mzungu alisikitika sana. Binafsi niliamini huo uvumi enzi hizo lakini walipomtuhumu baba yangu kuwa ananyonya damu kwa kuwa tu ameweka rangi nyekundu kwenye sakafu nikaachana na huo upuuzi japo nilikuwa shule ya msingi. Eti Mumiani...
 
Kijijini kwetu ilikuwa balaa. Siku mmoja padri alisimamisha land rover katika msitu kuwapa lifti kinamama walikuwa na mizigo ya mapeasi walikimbia vibaya sana chini ya gema la barabara kwa woga, sijui kipi kilisalimika kati ya viungo vyao na mapeasi. Mzungu alisikitika sana. Binafsi niliamini huo uvumi enzi hizo lakini walipomtuhumu baba yangu kuwa ananyonya damu kwa kuwa tu ameweka rangi nyekundu kwenye sakafu nikaachana na huo upuuzi japo nilikuwa shule ya msingi. Eti Mumiani...

hahahaha
 
Hahaha dah kitambo sana .... Ila mi hilo gari sijawahi kuliona kusema kweli , alafu nilikuwa napenda sana lukopa bajia za mwalimu wa somo la historia
 
Hahaha dah kitambo sana .... Ila mi hilo gari sijawahi kuliona kusema kweli , alafu nilikuwa napenda sana lukopa bajia za mwalimu wa somo la historia

hilo gari halikuwepo nbi uzushi uliotungwa ili watotimo tuwe tunawai kurudi nyumbani
 
Morogoro mjini kulikuwa na Mzee mmojaanaitwa Kararambe alikua mzungu akipita na 110 yake tunakimbia eti mnyonya damu. Duuh ilikuwa balaa
 
Morogoro mjini kulikuwa na Mzee mmojaanaitwa Kararambe alikua mzungu akipita na 110 yake tunakimbia eti mnyonya damu. Duuh ilikuwa balaa

landrover ilikuwa gari za kuogopa izo..
 
  • Thanks
Reactions: ilu
nakumbuka enzi hizo simu ndo za mkononi ndo zinaingia ...kujaza vocha ni kwa dola tu..unajaza dola..!!simu nyenyewe Siemens dole gumba..

Enzi za Tritel kumbe bado wanyonya damu walikuepo...!!!!
 
Yaani weewee tunaenda mashine za misufin pale ukikuta Land rover ya Kalalambe yule nusu nusu umwage unga duuuu

!
!
mashine za misufini aisee kitambo sana, kulikuwa na pori nyuma ya mashine kipande cha sabato. Mimi nilikuwa nakaa sultani area kipindi hicho na shule nilikuwa pande za mbuyuniiii. Tulikuwa kama tumetoroka kwenda kuwinda ndege pande zile mmoja wenu anaweza kuanzisha tu kalalambe huyo ni mbio mpaka balaaaa. Hahahahahahaha nouma sana mwana.
 
Wakaja kusema et wana kioo ambacho ukikiangalia tu kina kuvuta unawafuata mwenyewe basi ilikuwa mkianza kukimbizana hakuna kuangalia nyuma unaogopa hicho kioo.
 
hahaha.. Kipindi hko kelele nyingi darasani halafu kimya kikipita kidogo mnahisi shetani kapita katikati yenu
 
maeneo ya dodoma huo mchezo ulikuwepo kweli kulikuwa na hao wa2(wachuna ngozi na wanyonya damu)na baadhi ya wa2 walipoteza maisha, wengn walinusurika ikiwem mm mwnyw.. balaa.
 
Aisee nishachomokea dirishan sana! Sikuwa na muda kabisa wa kupita mlangon .....kweli nimekumbuka mbali leo!
 
Aseee! Umenikumbusha mbaali. Sio miaka ya 90 hata ya 80 mambo hayo yalikuwepo..Nakumbuka kuna siku tukasikia nyonya damu inakuja, bila hata ya kuiona tulitoka darasan kwa kiwewe nakumbuka tulibanana mlangon nilipotoka hapo nilipata maumivu ya kifua wiki nzima.. We acha tu
 
Back
Top Bottom