sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Usije kujidanganya hata siku moja kwamba mwanamke atakupenda kuzidi watoto au mtoto wake, tena yule wa kwanza huwa ana nafasi yake maalum huwezi mwambia mwanamke chochote kuhusu mtoto wa kwanza aliejifungua, huyu ndie anampa heshima kwa mara ya kwanza kuitwa mama.
Na ndio hapa tunapotoaga onyo kwamba linapokuja suala la ku date ama kutaka kumuoa single mom hakikisha sana umemchunguza vizuri mwanaume mwenzako aliemtunga mimba ya kumpa mtoto wa kumpa heshima ya kuwa mama, mapenzi ya mama kwa mtoto atafanya chochote kwajili ya furaha ya mtoto, mtoto akitaka aonane na baba yake mama yupo tayari kujishusha hata kama hawaelewani na mzazi mwenzake, mama yupo tayari kufanya chochote ilimradi tu aone mtoto wake ana furaha.
Kama mwanaume mwenzako bado ana kiu na huyo mwanamke ama anataka kukukomoa basi ni rahisi sana amtumie mtoto kupasha kiporo na huyo unaemwita mke wako, zuia wawezavyo lakini mbele ya mtoto mama atapata upenyo na ukibana sana basi utaja kuona upande wa mkeo ambao hujawai kuuona mithiri ya tetea anavyojitoa mhanga kupigana na mwewe bila kujali kazidiwa nguvu , hata awe mpole ataliamsha dude ambalo hukuwahi kuliona !! huko kwa mwenzako akishaweza kujua kuntumia mtoto basi hio ndio sarafu yake ya kuweza kum controll mkeo, hata kama mwanamke hapendi lakini atafanya kama sharti la kutimiza wajibu wake ili mtoto aweze kuwa karibu na baba yake.
Na ndio hapa tunapotoaga onyo kwamba linapokuja suala la ku date ama kutaka kumuoa single mom hakikisha sana umemchunguza vizuri mwanaume mwenzako aliemtunga mimba ya kumpa mtoto wa kumpa heshima ya kuwa mama, mapenzi ya mama kwa mtoto atafanya chochote kwajili ya furaha ya mtoto, mtoto akitaka aonane na baba yake mama yupo tayari kujishusha hata kama hawaelewani na mzazi mwenzake, mama yupo tayari kufanya chochote ilimradi tu aone mtoto wake ana furaha.
Kama mwanaume mwenzako bado ana kiu na huyo mwanamke ama anataka kukukomoa basi ni rahisi sana amtumie mtoto kupasha kiporo na huyo unaemwita mke wako, zuia wawezavyo lakini mbele ya mtoto mama atapata upenyo na ukibana sana basi utaja kuona upande wa mkeo ambao hujawai kuuona mithiri ya tetea anavyojitoa mhanga kupigana na mwewe bila kujali kazidiwa nguvu , hata awe mpole ataliamsha dude ambalo hukuwahi kuliona !! huko kwa mwenzako akishaweza kujua kuntumia mtoto basi hio ndio sarafu yake ya kuweza kum controll mkeo, hata kama mwanamke hapendi lakini atafanya kama sharti la kutimiza wajibu wake ili mtoto aweze kuwa karibu na baba yake.