Form 4 na wengine, angalieni hapa!

Form 4 na wengine, angalieni hapa!

Muulize nini anataka afanye kwanza alafu ukipata jibu utajua jinsi gani utamsaidia......au kama vipi Mtafutie msingi wa pesa ajiajiri mwenyewe(mfanyabiashara) au mrudishe tena form 4
 
Samahani mkuu....lakini mimi binafsi nina historia mbaya na matokeo mabaya ya kuwasomesha wajomba zangu....yaani wote wameniangusha....kama sio kunibwaga....ninachokushauri ni kuwa umuulize mara mbili mbili au hata mara kumi kumi kuwa kweli ana nia ya kusoma kweli au analeta maskhara...hasa kwa mazingira ya huku mjini na hao boda boda waliojaza huko mitaani unaweza ukaletewa mjukuu badala ya cheti cha form four....huyo mwenye miaka 17 unayemuona mdogo kwa vijana wa boda boda na makonda wanamuona kama mjane anayehitaji kuliwazwa.....

Tafakari chukua hatua......
Haaaaa umeongea ukweli mtupu....hawa boda boda,makondacta na madereva ni shidaani
 
ELIMU HAINA MWISHO,hata hawa walifeli bado kuna fursa nyingi katika ugunduzi na ubunifu,wasikate tamaa,mtaji wa akili wanayo.
 
Jaribu kumdadisi na kuona nini anapenda au anaweza kufanya. Mfano kama ni kushughulika sana na vifaa vya umeme, electronics, mechanics, painting, biashara dukani au chochote kile ambacho anaweza kufanya kama kipaji chake.

Lakini kama anaajiweza kimasomo mtafutie shule sekondari aanze form three huenda alikosea mahala akapata alichokipata.

Kusoma sana nako ni kuzuri ila huenda akajiajiri baada ya muda mfupi kuliko kupoteza muda mwingi na shule.

Penye nia pana njia, kama hana nia na ufundi au biashara possibility ya kusoma itakuwepo. Mdodose!
 
Mpeleke chuo cha ufundi. Ukitaka chuo kizuri n mp nitakuelekeza
Chuo gani kinapokea zero aise!! Acheni masihara bana. Huyo kama anataka kuendelea na elimu ni lazima arudie tu, tena ikibidi form one. Hakuna ushauri mwingine bora! Au afanye QT Lakini kwa msuli mpana then aendelee ikiwa Mungu atamsaidia.
 
Hata mimi nilikuwa nawaza hivi mkuu, asante
Akasome kwanza QT, kama atafeli tena ndo aende ufundi, kuwa na elimu ya taaluma Fulani halafu vyeti vya basic education vinasoma zero au kwa maneno mengine hunavyo kabisa si jambo jema. Msihakie Maisha, mpelekeni mtoto QT then atafaulu
 
Ongea nae kwanza upate mtizamo wake kwanza kuhusu kurudia mtihani au kwenda kusomea kazi.
Kama kurudia mpe QT
Kama course zipo nyingi mfano
Ususi.upambaji.urembo
Hotel management
Computer graphic designs
Kozi zifuatazo atamaliza ila kazi itamsumbua kwani watadai cheti cha kidato cha 4
Secretarial studies
Record management
Human Resources
Business Administration
etc
Sawa, Lakini utafika wakati wa kujiendeleza mkuu, unadhani itakuwaje?! Matatizo ya sasa tuyasolve kwa muono wa miaka kadhaa ijayo siyo kusolve tatizo la sasa tu!
 
pia nami nahitaji msaada dogo langu kapata iii~25 ana 'c' ya history 'c' ya kiswahili na 'c' ya biology masomo mengine ana 'd' je anaweza kwenda kidato cha tano,?
Kama alisoma chemistry Amepata nini? If ana D, alternative zipo. Aende vyuo vya afya akaanze na certificate
 
Pole sana Mkuu!
USHAURI WANGU
1. Muulize anapenda nini.
Katika maelezo yake kama unashindwa kumuelewa anapenda nini basi fanya yafuatayo.
2. Mpeleke shule aanzie na masomo ya Form III kwa mwaka huu na mwakani apige NECTA. Dhumuni la kuanza Kidato cha 3 ni kujipanga zaidi, na Kidato cha ndani ndo msingi mzuri wa kufanya vema kidato cha 4. Wakati anarudia hakikisha unamtafutia sehemu inayotoa elimu bora. Pia na wewe uwe mfatiliaji sana kwake, uwe na namba hata za walimu na unawapa ela ya vocha ili wakufatilie zaidi. Wakisema wanahitaji tuition basi fanya hivyo. Mtoto aliyepata O mpaka aje kupata IV yenye D walau 5 sio kazi rahisi Mkuu. Pia nitapendekeza asome Sayansi, Sayansi inalipa sana Mkuu huko mbeleni, tofauti na Arts.
3. Akimaliza Form IV peleka Chuo, achana na mambo ya Advances, kupitia Form IV akienda chuo na kupata Diploma kama ya sayansi hivi anaweza akaajiriwa. Hapa atakupunguzia mzigo Mkuu, Diploma za Sayansi zinauzika maana mtu anakuwa na maarifa mengi tuu, akiendelea Degree akitokea Diploma haitamsumbua sana kama mtu aliyetokea Six.


***** KILA LA HERI MKUU *****
 
Nina uncle wangu kapata matokeo mabaya sana, ambayo sikuyategemea na wala yeye hakuyategemea ila all is well.

Nimekuja kwenu wakuu kuomba ushauri, najua wapo na wengine wengi watakaofaidika na ushauri huu.

Lengo langu nataka asome. Ni options zipi ambazo zinaweza kumsaidia akaendelea kupata elimu kwa hii div 0 yake, binafsi sijakata tamaa na hata yeye nitamshawish asikate tamaa. Ni binti wa miaka 17 alikuwa huko moshi sasa nikamchukua tupo nae hapa Dar
Muozeshe tu mkuu
 
Mleta uzi kwenye elimu siasa pembeni,, huyo mtoto mrudishe shule aweze kuwa na certificate,, from there ndo aende hata huko ufundi,,,, coz hata ck moja hatuwez kukupa tender while you have got no academic
 
tatizo anachotaka yeye ni kuendelea na form five na six....sasa ndo nashindwa elewa kama ata chaguliwa au vipi...
 
13 mega pixel,

Kwanza pole sana, hususani kwa huyo mtoto!! Nimeona ushauri wa watu mbalimbali huku wengi tu wakishauri umpeleke ufundi. Binafsi sikushauri umpeleke ufundi mtoto mwenye sifa za Darasa la Saba!
  • Kwanza kabisa usimfokee, na kama umeshafanya hivyo basi jirudi kwake! Kwavile Waafrika tuna viburi kiasi cha kwamba hatuoni kwamba tunalazimika kuwaomba msamaha watu wanaokula ugali wetu, basi unaweza kumuomba msamaha in other way round kama vile kuanza kumchangamkia as if nothing happened. The idea behind is to make her not to feel like amefanya serious crime ambayo haiwezi kuwa repelled. Akishaona upo nae, hata kurudia mtihani atakuwa tayari.
  • Two, kwanini unasema hukutegemea na wala mwenye hakutegemea kwamba angepata zero? Je, ulikuwa unafuatilia matokeo yake vizuri? Kama ulikuwa unafuatilia kwa karibu, je alikuwa anasoma shule ya aina gani? Ukitaka kufahamu aina ya shule, kama mwenyewe huifahamu vizuri basi angalia ufaulu wa wanafunzi wengine. Mamia ya shule zetu huwa wanapata Division IV darasa zima lakini kabla ya hapo usidhani kwamba hapakuwapo wakali wa darasa ambao wao piga ua wapo kwenye 5 bora na walikuwa wanapiga paper ile mbaya! Kumbe kimsingi walikuwa wanaongoza darasa la wajinga na walimu walikuwa wanatoa paper zinazokidhi viwango vya darasa la wajinga! Kwahiyo ikiwa binti yako alikuwa anasoma darasa la wajinga; hapo hakuna suala la "hakutarajia kupata Zero.... hiyo ilikuwa given."
  • Ukijiridhisha hayo, jaribu kutafiti level yake ya written English. Hili suala la kizungu ni jipu kwa watoto wa O-Level na tatizo zaidi ni kwamba kinawaondolea confidence. Kimsingi ninaposema level yake ya kizungu ni ile confidence aliyonayo kutumia lugha... I don't care how grammatically correct she is. Ukiona hapo kuna shida, mpeleke pale British Council. Si kwamba akitoka pale ndo atapiga ile ya Queen Lizzy, not at all but suala la yeye kwenda kusoma Kiingereza kwenye madarasa ya wenye lugha kutamjengea confidence! Atakuwa anatiririka huyo na ma-broken kibao lakini huku mwenyewe akidhani yupo right! This's all what's needed. Mtu mwenye broken English lakini ana confidence ni much better kuliko mwenye good English but hana confidence ya ku-communicate. Na huyo akishajiona amesoma English course, hamu ya kurudia mtihani atakuwa nayo.
  • Baada ya yote hayo; hapo hakuna cha VETA wala nini... mrudishe mtoto darasani. Mtoto unaweza kumpeleka sehemu kama VETA angalau akishahitimu na kuwa na cheti cha Form IV na sio Darasa la Saba. Kama mfuko wako upo vizuri na unaongea na watu; jaribu kumtafutia shule ambayo atakuwa anaingia darasani kama wenzake lakini kwa yeye atakuwa anajiandaa as a private candidate. Back then Jitegemee walikuwa wanafanya hivi... mimi mwenyewe wakati tupo O-Level kidato cha IV, tulisoma na msichana ambae nae alikuwa anajiandaa as a private candidate ingawaje pale shuleni hili halikuwa jambo la kawaida sana but penye connection, nothing is impossible. Ukipata shule ya hivyo, hapo hakuna cha hakutegemea Zero wala nini; aanze tu Form III. Kufeli kwa kutogemea hakuzidi masomo mawili... unakuta mtu alikuwa fit sana kwenye Biology lakini paper inarudi F ingawaje masomo mengine amefaulu! Lakini mtu umekula F mwanzo mpaka mwisho na masomo yenyewe ali-sit kwa siku tofauti tofauti... dah, ngoja niishie hapa manake naona naongea lugha kali sana!!!
 
Back
Top Bottom