Foleni za magari ni maisha bora - Kikwete

Rais Jakaya Kikwete ametamka hadharani kuwa foleni kubwa za magari jijini Dar es Salaam ni ishara tosha kuwa sera yake ya kuleta "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania" sasa imeanza kutoa matunda kwani Watanzania wengi zaidi wamemudu kununua magari chini ya uongozi wake.
Badala ya kukiri kuwa msongamano wa magari unaoleta athari kubwa kwenye uchumi wa nchi, unatokana na serikali yake kushindwa kuwekeza pesa kwenye miundombinu na kujenga fly-overs, Rais wetu mpendwa anasema kuwa foleni barabarani ni ishara ya neema.

Nalipongeza sana gazeti ya MAJIRA kwa kufanya umakini mkubwa na kuripoti habari hii.
Matamshi haya ya Rais yanadhihirisha jinsi alivyokuwa na upeo mdogo wa kufikiri na kuongoza nchi.

Kwa maana hiyo, anataka Watanzania wafurahie foleni au wavumilie tu kwani ndiyo matunda ya maisha bora hayo.
Yeye haoni kabisa kuwa foleni hizi ni ishara kuwa serikali yake imeshindwa kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo zaidi.

Barabara hizi zimejengwa tangu enzi za Mwalimu wakati population ya Dar ikiwa ni watu laki 5 tu. Leo Dar ina zaidi ya watu milioni 4 na miundombinu ni ile ile ya zamani.

Baada ya kutoa matamshi haya mazito. Rais Kikwete sasa tunaambiwa anaenda tena ulaya kwenye shopping spree.

Safari hii anaenda Spain kuwapongeza kwa kushinda kombe la dunia ili akapewe jezi na kupiga picha na kina David Villa, Puyol, Iniesta, Xavi, Torres na Cesc Fabregas.
Pia, atafanya mazungumzo tena na Rais wa Real Madrid ili awalete kina Jose Mourinho, Ronaldo, etc waje kutalii Tanzania kwa pesa zetu sisi wote wapiga kura.

Baada ya kupiga picha na kutoa zawadi za vinyago kwa kina Drogba, Kaka, Robinho, Valdes, Luis Fabiano, etc. Sasa Rais yupo Spain kuongeza collection yake ya picha na jezi za football stars wengine.

HUYU NDIYE RAIS WETU NA SISI NDIYO WANANCHI TUTAKAOPIGA KURA ZA KUMPA MIAKA MITANO ZAIDI YA KUVURUGA NCHI YETU
 
Wasomi, wanasiasa wamkosoa JK


PostDateIcon.png
Tuesday, 20 July 2010 04:46
Na Makumba Mwemezi
SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete kueleza umma wa Watanzania kwamba ongezeko la magari na kero ya msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam ni dalili ya maisha bora, wanazuoni na wanasiasa nchini wameikosoa kauli hiyo na kuilaani vikali.
Wamesema kauli hiyo ni dalili tosha kwamba CCM imekosa mwelekeo halisi ya maendeleo ya nchi hivyo haistahili kuendelea kutawala kwa kuwa haina dira ya kubali maisha ya Watanzania.

Mhadhiri katika kitivo cha Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. Bashiru Ally aliliambia Majira kuwa ni aibu kwa kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa nchi aliyebeba dhamana ya taifa zima.
Alisema ongezeko la fedha, majumba ya kifahari kwa watu wachache na foleni za magari jijini Dar es Salaam hakuwezi kuchukuliwa kama kipimo cha maisha bora kwa kuwa hivyo si vigezo vinavyopaswa kutumiwa kupima kiwango cha maendeleo katika nchi yoyote duniani.
Alisema maisha bora na maendeleo yoyote katika nchi yanapaswa kupimwa kwa kuzingatia ongezeko la watu, upatikanaji wa ardhi, siasa safi na uongozi bora mambo ambayo bado ni ya taabu na yanayozua migogoro mikubwa nchini.
"Kauli hii inanikumbusha kauli ya hayati Korimba (Horance), kuwa CCM haina dira wala mwelekeo, huwezi kupima maisha bora ya mwananchi wa Masasi au Kagera kwa kuangalia foleni za magari Dar es Salaam, laiti kama Mwalimu (Nyerere) na Sokoine (Moringe) wangekwepo leo kauli hii ingewapandisha presha," alisema Bw. Bashiru.
Alisema ni vema Rais Kikwete akaangalia uwiano wa ngezeko la foleni hizo na uboreshaji wa miundombinu hususan barabara, shule na mfumko wa bei za bidhaa na thamani ya fedha ambavyo vimekuwa vikiporomoka kwa kasi katika kipindi cha uongozi wake.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. Freeman Mbowe, alisema kauli hiyo inaonesha jinsi serikali ya CCM isivyokuwa na jambo la kujivunia kwa wananchi katika kipindi chote cha miaka mitano iliyopita.
Alisema kimsingi msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam inasababishwa na ukosefu wa miundombinu ambayo chimbuko lake ni uongozi mbovu ulioko madarakani.
Alisema kinachotokea Dar es Salaam si kuboreka kwa maisha ya wananchi bali ni ongezeko la tabaka kati ya walionacho na wasio nacho hasa masikini walioko vijijini hali ambayo inasababisha ongezeko la watu mijini wasiokuwa na ajira wala mahali pa kulala.
"Foleni za magari Dar es Salaam si dalili ya maisha bora, na kama ukifanya utafiti utagundua kuwa foleni kubwa ni katika baadhi ya barabara zinazoelekea kwa matajiri wachache ambao baba, mama na watoto kila mmoja ana gari lake, sasa maendeleo ya watu wachache huwezi kuyatumia kupima kiwango cha maisha ya Watanzania wengine," alisema Bw. Mbowe.
Naye Mhadhiri Mwandamizi katika Kitivo cha uchumi na Biashara Chuo Kikuu cha Dar Salaam, Profesa Humphrey Moshi, alisema si sahihi kwa rais wa nchi kupima maisha ya Watanzania wachache wengi kwa kutumia mfano wa watu wachache wenye uwezo wa magari.
Alisema licha ya ukweli kuwa ongezeko la idadi ya watu wanaomiliki magari linaweza kutumika kuonesha ongezeko la kipato kwa wananchi lakini haikuwa sahihi kwa kiongozi wa nchi kupima maisha ya Watanzania kwa kuangalia wenye uwezo wachache walioko Dar es Salaam.
Alisema Dar es Salaam ni mji wa kibiashara wenye viwanda, mashirika na taasisi karibuni zote za serikali ambazo katika shughuli za kawaida zinahitaji usafiri wa magari, hivyo kuna uwezekano kuwa foleni kubwa husababishwa na magari ya taasisi, hizo lakini si mabadiliko ya maisha ya Watanzania.
"Magari mengi si ya watu binafsi, idara nyingi za serikali ziko hapa, kuanzia ikulu, bunge, wizara zote, taasisi binafsi, mashirika ya dini, viwanda na wafanyabiashara mbalimbali ambao ndio wamiliki wa magari, sio wananchi wa kawaida, sasa huwezi kusema kuwepo kwa foleni za magari ya idara hizi ni maisha bora kwa wananchi," alisema Prof. Humpherey.
Alisema maendeleo yanapimwa kwa kuangalia maisha ya jumla si ya mwananchi mmoja mmoja, ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezo wa kuzalisha mali wa wananchi, thamani ya fedha, kiwango cha elimu na uimara wa sekta za viwanda na kilimo, na si kuangalia msongamano wa magari yaliyokosa barabara za kupita.
Akihutubia wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mkutano wa kuwatambulisha wagombea urais, mgombea mwenza na Rais wa Tanzania Visiwani katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Rais Kikwete alisema ongezeko kubwa la magari na kusababisha msongamano wa magari ni mijawapo ya dalili za maisha bora.
 
Na ifahamike wazi kwamba Tanzania haina magari mengi. Tanzania nzima ina magari laki tatu. Hiyo ni chini ya nusu ya magari ya mji wa Johannesburg peke yake.

Tanzania ni mojawapo ya nchi zenye magari machache sana duniani. Msongamano unaoonekana Dar es Salaam unatokana na kutokuwepo barabara. Na vichochoro anavyojenga Kikwete kama kile cha kutoka Namanga kwenda Masaki si barabara. Aache utani.

Ni aibu kwa Rais kusema hovyo namna hii.
 
ukinyanyua mkono linauma, ukishusha linauma!!! huyu kiongozi wenu sijui kama afya yake ya ubongo ni njema (samahani kama mtu atakwazika) This sickens

tehetehetehe ...hahahahaha...ihihihihihihi.....hohohohohohoho...! ama kweli kiwete ni jipu la kwapa

nicheke ni nenepe mie...! kiwete u need to be serious kwa kweli....otherwise u gonna kill this fragile economy...!
 
Tokyo, Moscow, Los Angeles, Shanghai, Sao Paolo, London, Paris, Mumbai, Bangkok, ni baadhi ya miji yenye maendeleo ya miundombinu ya barabara lakini bado kuna misongamano ya kutisha barabarani.

3088635961_ae4ee28a5e.jpg

Wakazi wa huko wanahimizwa kutumia usafiri wa wengi. Watu wa familia moja, kwa mfano, wanapokuwa wanaelekea maeneo mamoja wanashauriwa kutumia gari moja badala ya familia moja kujilimbikizia na kutumia magari mengi.

Dar-es-Salaam hatuna hata mabarabara ya kutosha kama ya miji mingine yenye magari mengi na matatizo ya msongamano halafu bado tunaambiwa tuongeze magari. Ni ushauri mbovu wa kupotosha.

Beijing wanashauriwa na serekali yao kununua magari zaidi na zaidi ili uchumi wa nchi uendelee kukua na ajira ktk viwanda vya magari pamoja na support industry zisipotee. Lakini kodi za gari kwa mwaka zinaongezwa, mafuta yanapanda bei na siku za kuliweka gari barabarani ni siku sita kwa wiki. Ni mategemeo miaka ijayo watu watashauriwa kuendelea kununua magari kwa wingi lakini hawataruhusiwa kuyaendesha zaidi ya siku tatu kwa wiki ili kumpa kila mtu ingalao fursa ya kuendesha mara chache kwa wiki. Kama wewe mbishi na unaendesha basi faini dola 15 na huwezi kwepa CCTV maana kila kona na kila mita chache zipo.

Ni wazo zuri kushauri watu waendelee kununua magari lakini tatito ni kuwa serikali yake JK pamoja na yeye mwenyewe hawana uwezo kafanya sehemu yao ya kazi. Watu watanunua magari, je ni kweli serikali ya CCM itajenga mabarabara maake maji tu yameshinda miaka 50 plus baada ya Uhuru kiasi kwamba Dar nzima watu wanatumia maji ya kujichimbia kisima? je ajira zipi zinaongezeka tokana na wingi wa magari TZ, mapato ya serikali tokana na faini na kodi za magari je? ni kiasi gani? Miundo mbinu ingeundwa ya kutosha faini tu za magari zingeweza kutatua mahitaji ya Polisi wote nchini pia na kujenga miundo mbinu ya maji Dar nzima. Mpaka Mbagala kumejengwa barabara ya MSAADA, sasa angalia serikali ya JK isivyokua makini, humo hata lori la uzito wowote laruhusiwa kupita, mwaka tu mabonde barabarani. Nabaki najiuliza yaani serikali yetu hamna wawezacho hata kutunza tu walichopewa bure hawawezi je kujenga wataweza.

Pamoja na uzuri wa wazo, lakini yote ya JK yanakuwa ni usanii kwa sababu serikali yake ni ya kisanii. Ni kusema, sema tu. Sawa na mmoja aliyesema ukiwa na watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora basi nchi itaendelea - sasa utashangaa huyo alikosa kitu gani kuendeleza nchi yake alipoukwaa Uraisi maana siasa safi na uongozi bora vyote vilikua chini yake.
 
Hawa jamaa huko nyuma walisema magari ni anasa na waliweka amri ya kutoendesha
gari ndogo binafsi siku za Jumapili kuanzia saa nane mchana mpaka saa kumi na mbili asubuhi
Jumatatu. Mabasi, malori, mabasi na pick ups yaliruhusiwa ndiyo kwa maana kuna wakati
nchi hii ilikuwa na pick ups nyingi kuliko gari nyengine. Hawajakumbuka kuweka miundo mbinu
ya barabara za kutosha katika jiji la Dar Es Salaam.
Hivi sasa magari sio mengi ila hakuna barabara za kutosha. Kinachotakiwa kuwe na barabara pana
zenye kupitisha magari manne kila upande na baadhi ya hizo wangezifanya za kwenda upande mmoja.
 
Beijing wanashauriwa na serekali yao kununua magari zaidi na zaidi...
Ya kweli hayo kaka?

Beijing to extend restriction on car use
Mon, Apr 05, 2010
China Daily/Asia News Network

BEIJING - The restriction on car use in the national capital will be extended for another two years starting April 11, as traffic jams are still one of the city's most serious problems, the municipal government announced on Friday.

Beijing sees cyclists as saviours of polluted city
JONATHAN WATTS
January 27, 2010

BEIJING: After wrestling for years with Beijing's appalling traffic and pollution problems, city planners have come up with an old-fashioned solution: bicycles. Municipal officials want...

Beijing To Levy Environmental Tax On Car Owners
February 1, 2010

Zhang Yanyou, the deputy director of the Beijing Development and Reform Commission, has disclosed to local media that Beijing may soon levy an environmental tax on car owners in the city...

Beijing Extends Car Restrictions
8 April 2009 - 7:00am

A slightly watered-down version of the traffic reduction methods the Chinese city of Beijing instituted in Summer 2008 to reduce congestion and pollution during the Olympics has been extended for another year. "The measures take a fifth of the city's 3.61 million vehicles off roads each weekday, according to the Beijing Traffic Management Bureau...

Cars crowd Beijing roads again
CHINA.ORG.CN

With the tremendous increase of vehicles and the weakening effects of vehicle restrictions, traffic jams have resumed and become more serious in Beijing. Some experts advise that the local government should take more effective measures to ease the congestion.

Beijing Extends Car Restrictions for Another Year
by Elizabeth Balkan on April 6, 2009
in Autos, International, Transport

Beijing authorities have announced that driving restrictions will be extended another year, as part of the city’s overall strategy to reduce airborne pollution and traffic congestion, according to reports from China’s state-run media. The plan hopes to take 930,000, or roughly 20%, of Beijing’s over 3.6 million vehicles off the road each weekday.

Beijing mayor says city faces serious pollution
BEIJING | Mon Jan 25, 2010 12:56am EST

BEIJING (Reuters) - Beijing's mayor Guo Jinlong said on Monday that the Chinese capital faces an "extremely serious" pollution problem, unveiling a target for "blue sky days" below the number achieved for all of 2009. Beijing is frequently enveloped in foul-smelling smog, the result of a private car boom on the back of breakneck economic growth...
 
Siamini kama kiongozi wetu (ambaye ni mchumi) anaweza kutoa kauli ya ki-layman kama hii. Kama ni kweli alitamka hayo basi moja kwa moja hastahili kuendelea kuwa kiongozi wa nchi hii inayohitaji mapinduzi makubwa ili kupiga hatua ya maendeleo. Inasikitisha kwamba CCM hawajauona udhaifu wa mtu huyu na kuthubutu kumpitisha bila kupingwa kuwa mgombea wao wa nafasi nyeti ya urais. Tena huyu ana nafasi kubwa ya kuchaguliwa kuwa Rais kwa miaka mingine mitano kwani Watanzania wengi bado wapo usingizini. Inabidi tufunge na kusali ili Mungu atupitishie mbali 'kikombe hiki'.
 
Atuambie yeye kajenga barabara ngapi Darisalama sio atajenga.....kujenga fyover mbili ni sawa na kumvalisha kofia na chupi mtu aliye uchi halafu ukasema kavaa nguo.....
 
duh.. ni wapi hasa huko? labda sijaelewa maana ya kujilimbikizia magari.


Ni kweli wakuu, kitendo cha watu kujilimbikizia magari ndo kuliko lifikisha jiji hapo.
We unakuta familia inawatu sita na wote hao asubuhi wanatoka na magari wengine ofisni wengine shuleni, unategemea nn!

Nakumbuka mwaka 90s Kampuni mmoja ya Japani waliwapiga marufuku wafanyakazi wao wapatao 5000 kwenda na magari yao binafsi kazini, nakushauriwa watumie mabasi ya kampuni.
 
Lakini hata kama mngekua ni nyie kwenye kipindi hichi tunachoelekea uchaguzi mngesemaje?

Afu mbona hamkujitokeza kuchukua form za uraisi? au mnaogopa mkwara wa sheikh?
 
Ukitaka kujua kama kuwa na magari mengi Dar ni dalili ya watu kuendelea waulize makondakta wa daladala. Hawaishi kuwatukana madreva wenye magari madogo barabarani kwa kuwaambia kwamba wanaringia magari ya mikopo tu! Ni wazi, magari mengi Dar hayatokani na maendeleo ya watu bali mikopo toka kwenye mabenki na maofisini.


Great thinker at work.
 
Na ifahamike wazi kwamba Tanzania haina magari mengi. Tanzania nzima ina magari laki tatu. Hiyo ni chini ya nusu ya magari ya mji wa Johannesburg peke yake.

Tanzania ni mojawapo ya nchi zenye magari machache sana duniani. Msongamano unaoonekana Dar es Salaam unatokana na kutokuwepo barabara. Na vichochoro anavyojenga Kikwete kama kile cha kutoka Namanga kwenda Masaki si barabara. Aache utani.

Ni aibu kwa Rais kusema hovyo namna hii.

....kama hio idadi ya magari 300,000 ni sahihi tanzania nzima......% ngapi ni ya serikali,NGOs,balozi,UN,company cars???
 
labda mkulu kaangalia hapo chini:

This is a list of the top ten countries for total number of motor vehicles owned.
Rank Country Total # of Motor Vehicles Owned Notes: 1
22px-Flag_of_the_United_States.svg.png
United States 229,500,000
-
22px-Flag_of_Europe.svg.png
European Union 211,600,000
2
22px-Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg.png
China 176,000,000 [22] 3
22px-Flag_of_Japan.svg.png
Japan 68,900,000
4
22px-Flag_of_Brazil.svg.png
Brazil 59,000,000 [23] 5
22px-Flag_of_Germany.svg.png
Germany 44,804,760
6
22px-Flag_of_Italy.svg.png
Italy 34,048,983
7
22px-Flag_of_France.svg.png
France 31,951,079
8
22px-Flag_of_Russia.svg.png
Russia 32,050,386
9
22px-Flag_of_the_United_Kingdom.svg.png
United Kingdom 26,034,225
10
22px-Flag_of_Spain.svg.png
Spain 21,977,778

List hii haina tofauti sana na top ten ya nchi zenye biggest economy


1.USA
2.JAPAN
3.GERMANY
4.UK
5.
6.
 
Wakuu,
Kila nikiwa kwenye foleni iwe ni Dar, Mwz na ARS huwa nakumbuka moja ya kauli tata za jk kwamba msongamano wa magari Dar ni kiashiria tosha kuwa jitihada zake za kuboresha maisha kwa kila mtanzania zimezaa matunda. Kwa mantiki hiyo, yeye kama rais, anajisikia furaha zaidi na amani moyoni anapoona misururu mirefu ya magari barabarani. Ama kweli, watanzania tunaye rais.
 
Habari wana Jf, nimepata wazo kuhusu jinsi ya kuweza kupunguza foleni barabarani na hata kutokomeza kabisa, sasa naomba msaada hapo je ni nani anayehusika na suala hili ikiwezekana nipate contacts zake ili niweze kuwasilisha maoni yangu kwake.
 
Back
Top Bottom