Filimbi za matundu 8 zimepotelea wapi?

... hivi nyie madogo huko mashuleni huwa mnasomaga vitu gani? Umewahi angalau kusoma hadithi au kusikia stori ya "Mpiga Filimbi wa Hamelini"? Ndio hizo filimbi anaulizia mleta mada raslimali.

Kuna uzi hapa kwa hisani ya Mshana Jr unazungmzia kitu hicho hicho, Mpiga filimbi wa Hamelin! Deliver every promise. Tumshukuru Rais kwa kumbadilisha waziri wa elimu maana yalikuwa mjanga!
Vitabu kama hivyo sijui hata kama vipo mashuleni siku hizi!
 
Mchina ametoa za plastic.
Ninaziuza dukani kwangu.
Mikoani natuma.
Unataka ngapi?
Bei 1 ni 1k TSHS
 
... na za bati pia zipo; hao jamaa (mgambo na sungusungu) wakizining'iniza shingoni wanajihisi ni alfa na omega! Halafu ni kama kanuni fulani hivi mifukoni lazima wawe na kadi fulani iliyochoka mbaya! Ha ha ha! Mkongwe johnthebaptist anajua sana hizo mambo.

Hizo wanaongelea zile tulitumia kupiga kukiwa na tukio au wakiwa wanapandisha na kushusha bendera ya Taifa.

Hizi za ala nyingi zilikua za bati, siku hizi wanaleta za plastic.

Vitu kama hivyo licha ya kuwa burudani vilichangamsha ubongo na kuongeza ubunifu. Ilihitaji kujifunza kuipuliza vizuri na kupangilia vidole ipasavyo ili zitoe mlio unaotakiwa.
 
Hizo wanaongelea zile tulitumia kupiga kukiwa na tukio au wakiwa wanapandisha na kushusha bendera ya Taifa.

Hizi za ala nyingi zilikua za bati, siku hizi wanaleta za plastic.

Vitu kama hivyo licha ya kuwa burudani vilichangamsha ubongo na kuongeza ubunifu. Ilihitaji kujifunza kuipuliza vizuri na kupangilia vidole ipasavyo ili zitoe mlio unaotakiwa.
... kabisa! Leo madogo kutwa kushinda Insta na FB hawajui kingine. TEHAMA kwa upande mwingine imeleta majanga hasa kwa vinchi kama vya kwetu. Vijana hawashugulishi brains to the maximum kilichobaki ni kuchat upumbavu tu huko whatsap na sms.
 
Shule Za Msingi Zilikuwa Zinatumika Kwenye Bendi Hasa Wakati Wa Asubuhi Kwenye Ukaguzi
 
Hawa wajukuu hawataweza kuzipuliza
... madogo wenyewe hawa mlo wao kiepe yai la broiler kwa sana na fanta chupa zenyewe mnazichezea siku hizi? Toto la kiume linashindana wowowo na manyonyo na dada zake? Bure kabisa!
 
Habari wakuu.
Kwa wale ambao wamesoma elimu ya msingi miaka ya 80 watakuwa wanakumbuka tulikuwa na bendi za gwaride la shule na tulikuwa tukitumia ngoma na zile filimbi zenye matundu manane. Hizi filimbi nakumbuka zilikuwa zinatolewa na serikali kwa ajili ya mashule na pia zilikuwa zinauzwa kwenye maduka mitaani.

Tulikuwa tunafundishwa namna ya kutumia ala hii ya muziki. Ni miaka mingi sijawahi tena kuiona ala hii ya muziki ikiuzwa mahali popote. Kwa mwenye kujua kama bado zinapatikana anijulishe ni wapi. Nakumbuka zilikuwa bei rahisi sana maana zilitengenezwa kwa mrija (pipe) ya bati na kipande cha mti kwenye sehemu ya kupulizia upepo. Miaka ile nadhani bei ilikuwa kama shilingi kumi hivi!
Zipo ila kwa uchache sana.
 
Mchina ametoa za plastic.
Ninaziuza dukani kwangu.
Mikoani natuma.
Unataka ngapi?
Bei 1 ni 1k TSHS
Ngoja niangalie hapa Arusha Kuna mahali nimeelekezwa nikikosa nitakutafuta. Niachie mawasiliano pm.
 
... madogo wenyewe hawa mlo wao kiepe yai la broiler kwa sana na fanta chupa zenyewe mnazichezea siku hizi? Toto la kiume linashindana wowowo na manyonyo na dada zake? Bure kabisa!
😂😂😂
 
Halafu mi nilikuwa fa'la sana ujue!

Eti ndo nilikuwa mkali wa kupiga filimbi, dah!!!

Sema hapo juu nimesoma kuhusu filimbi za miti... dah, hizo sikuwahi kuziona aisee!! Sasa ile hollow walikuwa wanafanya fanya vp kwa mfano kuitengeneza?!
Ukijujua kupiga filimbi saxophone haikusumbui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom