Filimbi za matundu 8 zimepotelea wapi?

Filimbi za matundu 8 zimepotelea wapi?

Tulizitumia kwenye magwaride mashuleni enzi hizo!
Ilikuwa raha sana enzi hizo. Siku hizi haya mambo naona shuleni hakuna. Hata somo la muziki hakuna. Mtu anaitwa mwanamuziki hata kusoma music sheet hajui.
 
CB7D6B41-77D6-4671-9E92-AAA334AA030D.jpeg

Mimi niliruka sana na aina hii ya flute hadi parade
 
Kumbukumbu yako ni sahihi kabisa. Bati za betri za National!
Yah nlitumia sana

Nlipokuwa nasoma chimala shule ya msingi mbeya nlikuwa napiga sana hiyo

Nikaenda kusoma forodhan shule ya msingi kulikuwa na bendi nlikuwa natwanga sana trumpet kwenye bendi ya shule na filimbi

Ova
 
Habari wakuu.
Kwa wale ambao wamesoma elimu ya msingi miaka ya 80 watakuwa wanakumbuka tulikuwa na bendi za gwaride la shule na tulikuwa tukitumia ngoma na zile filimbi zenye matundu manane. Hizi filimbi nakumbuka zilikuwa zinatolewa na serikali kwa ajili ya mashule na pia zilikuwa zinauzwa kwenye maduka mitaani.

Tulikuwa tunafundishwa namna ya kutumia ala hii ya muziki. Ni miaka mingi sijawahi tena kuiona ala hii ya muziki ikiuzwa mahali popote. Kwa mwenye kujua kama bado zinapatikana anijulishe ni wapi. Nakumbuka zilikuwa bei rahisi sana maana zilitengenezwa kwa mrija (pipe) ya bati na kipande cha mti kwenye sehemu ya kupulizia upepo. Miaka ile nadhani bei ilikuwa kama shilingi kumi hivi!
Baada ya Bongofleva kuja wanunuzi wa zana za muziki walikosekana.
 
Ilikuwa raha sana enzi hizo. Siku hizi haya mambo naona shuleni hakuna. Hata somo la muziki hakuna. Mtu anaitwa mwanamuziki hata kusoma music sheet hajui.
Ni kweli kabisa! Haya mambo hayapo kabisa siku hizi! Mfumo wetu wa elimu kwa sasa unachangia kwa sehemu kubwa kuua vipaji na ubunifu wa watoto wetu! Kuna wakati natamani enzi zile lakini ndiyo hivyo tena!
 
Halafu mi nilikuwa fa'la sana ujue!

Eti ndo nilikuwa mkali wa kupiga filimbi, dah!!!

Sema hapo juu nimesoma kuhusu filimbi za miti... dah, hizo sikuwahi kuziona aisee!! Sasa ile hollow walikuwa wanafanya fanya vp kwa mfano kuitengeneza?!
 
Yah nlitumia sana

Nlipokuwa nasoma chimala shule ya msingi mbeya nlikuwa napiga sana hiyo

Nikaenda kusoma forodhan shule ya msingi kulikuwa na bendi nlikuwa natwanga sana trumpet kwenye bendi ya shule na filimbi

Ova
Vipi bado unapiga hizo zana mkuu au umeshazisahau?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom