Feminism kirusi kipya katika jamii yetu

Feminism kirusi kipya katika jamii yetu

Swadaktaaaa
Anafoka Hadi kwenye uandishi .. Sasa ni nyuma ya keyboard live itakuwaje.

Ila nyote mna hoja..

Minority VS majority...
Threat perceived are they real big au Ni just a small threat with no ripple effect in how our society is governed


Na swala la justice linaingilia kati ...

Duniani Kuna maswala Qua trillion to deal with...

Nafikiri Kinyagi ni kidogo ila through media Kinakuwa casted as if it a big enormous Kinyago...

Kuna lots of issues to Discuss and reach a solid and profound conclusion
 
Tuna lots of issues that requires our Energy and attention to deal with...

They have thrown a bone and as dogs we are dealing with it .. huku Nyama wakiwa wanakula wao..

Water sanitation...

Malnutrition

Agriculture
Industrialization

Energy and energy security...

And so many more
 
hatarii hamtaki kuosha vyombo ndo inaleta shida zote hizi 😂😂😂😂😂
 
Moja ya uzi bora kabisa ambao unatoa insightful thoughts kwa jamii kuhusu upuuzi na unafiki uliopo kwenye movement nzima ya women empowerment na feminism kwa ujumla.

Sijamuona comrade Natafuta Ajira hapa bila shaka hajauona huu uzi.
 
Katika mambo ambayo mwanaume hautakiwi kabisa kuruhusu yaingie ndani ya familia yako ni hii itikadi ya feminism, ni hatari sana kwa mustakabali wa familia.

Mtu kama Jadda unaona kabisa huyu ni zao la binti ambaye amekosa malezi ya baba au amelelewa na baba legelege.
 
Kwanza ifahamike kwamba neno feminism lina tokana na neno feminine ambalo ukiperuzi maana yake utakuta ni “having characteristics that are traditionally thought to be typical of or suitable for a woman” na pia utaweza kukutana na maana ikisema “describes qualities, appearances, or behaviours typically associated with women or girls”. Katika hizi maana mbili utaona kwamba neno feminine (adjective) ambalo linatokana na jina (noun) Female limelenga kumtambulisha mwanamke kwa sifa zake za kike kinyume na shughuli za mafeminists wengi wa hovyo kama Jadda et al ambao humtambulisha mwanamke kwa sifa za kiume.

Ukiingia mtandaoni ukatazama maana ya neno “feminist’ na “Feminism” utakutana na maneno kama haya: “a feminist is someone who supports equal rights for women” au “a feminist is a socio-political movement advocating for the equality of the sexes, believing modern societies are patriarchal and unjustly treat women.

Kwa mtu mwenye utimamu wa akili akitazama tu hizi maana yaani maana ya neno jina na neno kitendo haviendani hata kidogo. Yaani kwa asili neno female lina maana ya “wa kike” au “ya kike” lakini iweje tena movement yake yaani feminism iseme ni harakati za kumfanya mwanamke alingane na mwanaume na kuacha asili yake kudai haki za kiume, sawa na mwanaume bila kutumikia au kuwa na wajibu sawa na mwanaume? Make this make sense ndugu zanguni. Ni kichaa tu ambaye ataona hili jambo limekaa sawa sawa na hallina dosari yoyote ya kimantiki.

Hivi kama wanajamii tumeshawahi kujiuliza maswali magumu kama ni haki zipi ni za mwanamke? Au tuhoji hivi, mwanaume ana haki zipi za kimsingi na mwanamke ana haki zipi za kimsingi?

Je, kama mwanaume anapendelewa kihaki je, anapendelewa katika maudhui yapi ambayo mwanamke anaminywa?
Hivi tumeshawasikiliza kwa umakini wanawake wanacholalamika na matakwa yao (sio mahitaji) then kuwatazama wanachokifanya katika uhalisia wakishapewa fursa wanazotaka?

Mimi siungani na hii movement na nina ipinga kama movent haramu kwenye jamii na yeyote anayeisapoti pia anakuwa ni haramu katika hii jamii kushinda hata dawa za kulevya maana dawa za kulevya hazijaleta madhara mabaya kushinda feminism ndani ya muda mfupi.
Unawezaje kuwa na harakati batili inayojinasibu kuwa ipo kulenga kumtetea na kumkomboa mwanamke ila kiuhalisia ime target kushape akili za wanawake kuwa negative katika jamii yao na kuwageuza kuwa kansa ya kuiharibu jamii hiyo hiyo huku kikiacha u’hovyo wa kila aina.
Hebu mtu aniambie faida za feminism na matokeo yake tokea imekuwa introduced miaka ya 1990s?

Ni muda sasa kutambua feminism kama harakati haramu kwa jamii na tuanze kuikemea kwa nguvu zote.

Nimeona pale chou kikuu UDSM wame introduce masomo ya femism ili kuwajaza ujinga mabinti na vijana wetu ambao wanakwenda kupewa elimu ya kuikomboa jamii yao na sio kuigawa katika makundi ya jinsia.

Kama tutaendelea kukaa kimya then tutarajie maasi zaidi kama yanayotokea huko mataifa ya magharibi kama USA, CANADA na United Kingdom ambayo kwasasa yanapitia mvurugiko mkubwa sana wakijamii kwasababu ya uzembe wa kuendekeza ideology za kipumbavu kama feminism katika jamii zao na matokeo yake zimeparanganyua kabisa ustawi na jamii sasa haieleweki ina uelekeo upi.
Faminism kama feminism yenyewe haikuwa na lengo baya hata kidogo, hapa naongelea first wave feminism ile ambayo ililenga kumnyanyua mwanamke kiuchumi,kisiasa,kijamii na kielimu tu basi.

Na aina aina hiyo ya feminism ilipata nguvu sana kwa sababu kila mtu aliisapoti maana ilionekana inaleta matokeo chanya kwenye jamii, kwanza itaongeza nguvu kazi na kuchochea ukuaji wa maendeleo kwa haraka, pili kuwapunguzia wanaume mzigo wa kuendesha familia na pia vile vile italeta mapinduzi kwenye siasa.

Na hakika vugu vugu hilo lilileta mafanikio makubwa sana, ndio tukaona nchi nyingi za ulaya wanawake wakianza kupiga kura,kumiliki aridhi na kupata wataalamu wa kada mbali mbali na kila mtu alifurahi sana hapa tunaongelea habari za miaka 1920s mpaka 1970s hapo.

Mambo yalikuja kuvurugika miaka 1990s pale ambapo extremists walipoigeuza movement kuwa men-hating agenda ambapo walifanikiwa kumshawishi mwanamke aone mwanaume ndio kikwazo cha maendeleo yake na ndiye adui yake namba moja, na hivyo basi hili mwanamke asonge mbele ni lazima mwanaume ashuke chini.. hapa ndio ikazaliwa ile kitu inaitwa "third wave feminism" ambayo kimsingi ndio hii modern feminism ambayo ndio imevuruga jamii yetu mpaka leo kiasi cha kuotesha uadui wa kijinsia.

Na hii modern feminism hata huko ilipoanzia inapigwa vita sana sio tu na wanaume mpaka wanake wenyewe, maana mbali tu na kuleta chuki za kijinsia lakin pia inashusha kasi ya maendeleo ya kijamii.. kuna report ilitoka mwaka juzi nafikiri kwenye chuo cha MIT huko marekani inasema siku hizi ushirikiano wa scholars wa kike na wa kiume umepungua sana na moja ya sababu ni hofu iliyopo baina ya jinsia zote mbili.

Ni bahati mbaya sana watu ambao ni pioneers wa hii modern feminism ni damaged women yaani wanawake wasiokuwa waliochanganyikiwa na wana misandristic elements ndio wamekuwa wasemaji na hakuna cha maana wanachokifanya chenye kujenga zaidi ya kutaka kumdidimiza mwanaume na kumpendelea mwanamke kwenye kila jambo na zaidi ya hapo wametengeneza mazingira ya mwanamke kuutumia uhuru wake vibaya halafu athari zozote zitakazomkuta lawama ashushuwe mwanaume.

Kwa ufupi tu hawa modern feminists wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kupalilia uadui kati ya mwanamke na mwanaume na kuivuruga kabisa jamii kiujumla.

Wamewapa sumu wanawake hasa mabinti sasa hivi wamekuwa wabishi,wakorofi na kujiamini kupita kiasi na wabinafsi kiasi kwamba hata kwenye mahusiano ya kawaida tu kwa mwanaume mstaarabu ni ngumu kuishi nao.

Wamemwaminisha kwamba mwanamke asipokuwa na pesa zake mwenyewe basi ajiandae kunyanyaswa na wanaume hata kama hatoingia kwenye mahusiano na pia vile vile akiwa na pesa zake mwenyewe ni guarantee kwamba hatanyanyasika na hahitaji kuishi na mwanaume, yaan mbali na kumpa mtoto mwanaume hana umuhimu mwingine maishani mwake.

Sasa hivi karibu kila binti nnayekutana nae hata wala ambao hawajaenda shule wanakwambia wanapambana washike pesa zao wenyewe hili waishi maisha yao bila uwepo wa mwanaume.... of course mimi nawasapoti kwenye hili acha watafute hela kisha waishi wenyewe maana kwanza hawaoleki sababu ya mindset zao za ajabu ajabu.

Sasa ni mwanaume gani timamu anataka kuwa na mwanake aliyeaminishwa kuwa adui wake wa kwanza ni mwanaume na akishika pesa ndoa kwake ni option? Mwanamke ambaye ameaminishwa kwenye uhuru jinga kwamba ana uhuru wa kufanya chochote muda wowote mathalani tu hakimdhuru mtu haijalishi hata kama ameolewa?

Binafsi yangu hawa modern women baada ya kudanganywa na hizi modern feminism propaganda acha tu watafute hela kisha waishi wenyewe bila wanaume, wakihisi upweke wafuge mapaka ndio yawe kampani yao.

Kuhusu sisi wanaume tutawaoa wanawake gani? Tukikosa wanawake humu nchini basi tutafanya hata kuimport kutoka nchi jirani kama Malawi ambao bado hawajawa corrupted na huu upumbavu wa modern feminism.
 
Katika mambo ambayo mwanaume hautakiwi kabisa kuruhusu yaingie ndani ya familia yako ni hii itikadi ya feminism, ni hatari sana kwa mustakabali wa familia.
Nakumbuka miaka fulani ya nyuma taifa la Turkey lilijitoa kwenye ile mikataba ya women rights inayosimamiwa na UN, kama kawaida mafeminists a.k.a feminazis kutoka nchi za magharibi walipiga kelele sana.

Mwaka juzi kuna mnigeria mmoja anasoma china alikutana na binti wa kituruki wakaanzishq mahusiano, jamaa alivyoomba mzigo binti akamchomolea akamwambia kwamba siku wazazi wake wakijua amepoteza bikra yake akiwa masomoni na hajaolewa itamletea kesi kubwa sana, baada ya jamaa kupewa hilo jibu akasitisha na mahusiano hapo hapo kama unavyojua tena sisi ngozi nyeusi mahusiano yasiokuwa na sex hayana maana, binti naye akampotezea mshikaji.

So unaweza kuona jinsi gani jamii ambazo zimeukataa upuuzi wa feminism wanawake wao walivyokuwa morally upright.

Same to ngazi ya familia, ukimaintain traditional values tegemea kuwa na familia bora yenye uadilifu wa hali ya juu, ila ukisharuhusu tu feminism basi tegemea binti yako kuanza kurudi saa nane usiku huku akijitetea ana exercise uhuru wake.
Mtu kama Jadda unaona kabisa huyu ni zao la binti ambaye amekosa malezi ya baba au amelelewa na baba legelege.
Watu kama huyo Jadda(kwanza nikionaga hii id navuta picha huyu atakuwa na spirits kama za jadda Pinket wa will smith) huwa ni hatari sana wakiwa kwenye nafasi za maamuzi, vuta picha aina ya mwanamke kama huyo ndio anakuwa kwenye nafasi ya Dorothy Gwajima wanaume na jamii kwa ujumla watakuwaje? Maana huyo anaonekana tu kwa comments zake humu ni pure misandrist.
 
Watu kama huyo Jadda(kwanza nikionaga hii id navuta picha huyu atakuwa na spirits kama za jadda Pinket wa will smith) huwa ni hatari sana wakiwa kwenye nafasi za maamuzi, vuta picha aina ya mwanamke kama huyo ndio anakuwa kwenye nafasi ya Dorothy Gwajima wanaume na jamii kwa ujumla watakuwaje? Maana huyo anaonekana tu kwa comments zake humu ni pure misandrist.
Bila shaka hata iyo user name yake ameitumia baada ya kuwa inspired na uyo Jadda Smith. Mwanamke mwenye maadili na anaijua nafasi yake kama mwanamke kwenye familia na jamii hawezi kutumia user name ya wakala wa shetani
 
Uzi best sana huu mkuu. Ukichunguza Kwa upana ideology nyingi za wanawake Huwa hazielemei kutafuta ukombozi Wala maendeleo yoyote ya kijamii Bali hutaka kuonekana wanaonewa, hii inawasaidia ku play victims Kwa lengo Moja maalum ambalo ni kuiharibu jamii without feeling guilty, kabla ya uharibifu wowote ambao mwanamke hupanga kufanya Kwa matakwa yake hutafuta kuti kavu la kujifichia aonekane hakuwa na options zaidi ya upuuzi atakaoufanya.
This is rarest thought i have ever seen in any intersexual dynamics related discussion, sahihi kabisa the whole issue of the so called women empowerment doesn't realistically intend to uplift women to catch up with men in all sphere of life, rather it is here to give women preferential treatments and freedom from accountability of all sorts of their typical shenanigans.
Pili, wanawake wa kisasa wanatafuta Kila agenda ili kuurasimisha umalaya na njia zote ili kuvuruga mwenendo wa jamii zetu, women don't seek for solutions they'll only find ways for destruction. Fuatilia wanawake wote wanaoshinikiza hizo sera Huwa hawaegemei upande wa kujenga, huwezi kuskia feminist akisema "Mume wangu anaugua ninapambana kulisha familia ili tubaki kuwa strong" never.
Such a golden piece of writtings, mkuu una fikiria sana kwa mapana natamani na hao watetezi wao wangekuwa hata na robo ya fikra ulizonazo.

Kiufupi watetezi wa wanawake wa kisasa wanapambana hasa kuondoa athari zinazotokana na maamuzi ya wanawake wenyewe, haijalishi hata kam ni maamuzi ya kipumbavu, na mara nyingi wakishindwa wanatafuta namna ya kulaumu wanaume. Leo hii kuna wanawake ni waraibu wa dawa za kulevya ukiskiliza watetezi wao wanakwambia huyu alishawishiwa na boyfriend wake na huwezi kuskia watetezo hao hao wakisema wanaume waathirika wa madawa ya kulevya walingizwa kwenye uraibu huo ni mademu zao.
Hoja pendwa za feminist, ni namna Gani ya wanawake wataishi vizuri Kwa kushusha thamani za waumezao na kulea watoto bila wazazi🤣🤣
hahahaha... wao wanaamini kuwa mwanaume ndio adui namba moja wa mwanamke tangu dunia inaanzishwa, na ikitokea wewe ukawa unaishi vizuri na mke wako basi wanatafsiri kwamba mke wako lazima atakuwa oppressed bila ya yeye kujua kama anakandamizwa, hivyo basi watatafuta kadosari kokote kale kaliopo kwenye ndoa yenu na kukatumia kama breaking point hili kumfanya mke wako aone ndoa yenu ni gereza hivyo anapaswa atoke, mashetani sana hawa wamevunja ndoa za watu kibao zilizokuwa na afya.
It kills my smile. Dear ladies hivi kuachika ni achievement!?
Huwa wanapongezana sana baada ya ndoa kuvunjika, huku wakitafuta justifications za kipuuzi sijui bora ndoa iliyovunjika kuliko ndoa mbovu.
Nowadays Feminist wanahisi kama mwanamke kuwa rude, arrogant, careless, lack of social responsibility and accountability will make them be seen as the strongest ladies 🤣🤣.
wow!! hii kitu nimewahi kuisema humu kuna nyuzi moja hivi, wanawake wa kisasa wanatamani kuwa wanaume wanaowachukia.

leo hii mwanaume ukiwa arrogant,narcissistic,mgomvi na non romantic unaitwa majina yote ya ovyo kuwa caveman, psychopath,mshamba na mtu usiyestahili kabisa katika jamii mwenye toxic masculity.

ila sasa mwanamke akiwa na sifa hizo hizo yuko so rude,arrogant,rebellious na mgomvi atakuwa branded kama mwanamke jasiri,imara na shupavu ambaye ni mfano wa kuigwa.

They actually love to be the version of man they hate with passion, in fact they envy men.
It doesn't make any sense kuhisi ata wanaume tunapendelewa hapana, They are just creating the environment Kwa kuweka wanaume kwenye kizuizi Cha kifikra na hisia ili watumie nguvu zetu na jitihada kuyuvuruga wakati wao wanaendeleza dhambi zao zilizovikwa utukufu.
Wanawake wa kisasa ukitenda haki wanaone wamependelewa na ukiwapendelea wanaona ndio umetenda haki.

Nakumbuka kuna taasisi moja hapo kenya walitoa ajira 40 ambapo waliajiri wanawake 27 kati ya nafasi zote 40.

halafu kuna shirika moja la kiserikali walitangaza ajira 15 wakaajiri wanaume 8 na wanawake 7, aisee zilipigwa kelele hizo na wana harakati uchwara wa huko kenya eti wanaendeleza ubaguzi wa kijinsia. Can you imagine?

Yaani hawa wamefanikiwa kuwafanya wanaume wajione ni wenye hatia kwenye kila jambo wasiloliridhika nalo.
Hivi ata hizo haki za binafamu or jinsia Huwa wanafanya women empowerment or gender substitute? What I know is, usawa ni kumpush aliye chini ku catch pace ya aliyejuu ili kuweka uwiano rafiki kutengeneza usawa. Lakini in reality haipo hivyo, what's Happening ni kumuangusha mtoto wa kiume na kumuinua mtoto wa kike Kwa lazima. Sasa hapa nani anapendelewa? Ni yule anayepambana kuweka utofauti au yule anayepewa viwango rahisi kuonekana analeta ushindani? Inasikitisha sana.
Kinachofanyika ni gender reversal kwenye maeneo ambayo yana manufaa kwao na sio kuleta usawa kama wanavyodai.
Huwa nakaa nawaza kuwa kama tu huko nchi za magharibi ambako ata literacy rate ni kubwa na tumeaminishwa wanaelimu na uelewa mpana haya mambo yanaeahukumu je vipi ikikaririwa na dada zetu wagumu wa kujifunza na kukwapua Kila hoja za mitandaoni? Wadogo zetu wakike, dada zetu, wake zetu je watasalimika na Hilo?.
Huko magharibi huu upumbavu ulipoanzia wao wenyewe wameshalionja joto la jiwe kwa mfumo jike waliouanzisha, sasa hivi huko wanaume wamekuwa binadamu wa daraja la pili, na ndio maana hata MGTOW group zimeanzia huko.
Wahusika wa haya mambo wakati mnagawa mataulo ka kike (which is a good thing) muunganishe na hizi elimu za kuwarudisha dada zetu na wadogo zetu kurudi katika tamaduni na uelewa wetu wa kiafrika Kwa kuzingatia Mila,desturi na maadili ya mwafrika.
Hawawezi kufanya hivi, wanajiona na wao wamekuwa wacanada kwamba mwanamke anatakiwa kutetewa kwa expense ya mwanaume mpaka dunia inafika mwisho.

Yote kwa yote hii ni comment bora kabisa kwenye huu uzi.
 
Uzi ufungwe 👏👏👏 mimi ni mwanamke msomi, mpenda maendeleo ila naungana nawe kusema kuwa feminism ni mpango wa magharibi kudhoofisha jamii kutoka nchi zinazoendelea specifically za watu weusi. Hadi hapa nilipofikia, naelewa kuwa I have nothing to prove, I'd rather be a traditional wife. Sijaumbwa mimi kufanya kazi mpaka jasho la mwisho. Siwezi kubeba zege wala nini... Nitaendelea na kazi ila baba mjengo ataendelea kuwa breadwinner
Wow!! Ubarikiwe sana jamani mama Zion( japo hao zionists ndio wametufikisha hapa kwenye huu mvurugano) kwa mtazamo huu ulionao.

Binafsi huwa nafarijika sana nikikutana na mwanamke ambaye bado anathamini traditional values ambazo ndio msingi mkuu wa ndoa na familia imara.

Na siku zote katika dunia hii mwanamke ambaye anakubali kuishi kwenye nafasi yake kama mwanamke ndani ya ndoa ndio anayeishi kwa furaha sana, maana ni rahisi sana mtu kuishi kwa kufuata traditional roles maana zina eleweka tu tangu kuumbwa kwa hii dunia.

Tofauti kabisa na hawa modern wives ambao kwanza wengi wao wana double standards, kuna mahali wanaikubali 50/50 na kuna muda wanaiona haifai, kiufupi ni wanawake ambao wanaishi kwa kuchanganyikiwa sababu wameupokea mfumo sawa/jike bila kutambua kuna privilages za kike watazikosa, ila wao wanataka kubaki nazo, hapo ndio kuchanganyikiwa kunapokuja.

Na pia hata ukichunguza wanawake wanaoishi na uchungu sana moyoni na kuparuana na wanaume mara kwa mara ni wale wapenda haki sawa ambao minds zao ziko corrupted na feminism, na huwa wanachukia sana wakiona nyie traditional women mnaishi kwa furaha kwenye ndoa zenu.

Ubarikiwe sana kwakweli.
 
Bila shaka hata iyo user name yake ameitumia baada ya kuwa inspired na uyo Jadda Smith. Mwanamke mwenye maadili na anaijua nafasi yake kama mwanamke kwenye familia na jamii hawezi kutumia user name ya wakala wa shetani
Kama ni hivyo basi huyu dada atakuwa na matatizo makubwa sana ya kiroho, maana yule jadda pinkett anaonekana dhairi sio mwanamke wa kawaida ni wakala halisi wa shetani mpaka feminists wenyewe wanashangazwa na maisha yake ya kimahusiano, sasa kama yuko inspired na mwanamke wa dizaini hiyo basi ni wa kumuogopa huyu hasa mbele ya mabinti wadogo.
 
Wow!! Ubarikiwe sana jamani mama Zion( japo hao zionists ndio wametufikisha hapa kwenye huu mvurugano) kwa mtazamo huu ulionao.

Binafsi huwa nafarijika sana nikikutana na mwanamke ambaye bado anathamini traditional values ambazo ndio msingi mkuu wa ndoa na familia imara.

Na siku zote katika dunia hii mwanamke ambaye anakubali kuishi kwenye nafasi yake kama mwanamke ndani ya ndoa ndio anayeishi kwa furaha sana, maana ni rahisi sana mtu kuishi kwa kufuata traditional roles maana zina eleweka tu tangu kuumbwa kwa hii dunia.

Tofauti kabisa na hawa modern wives ambao kwanza wengi wao wana double standards, kuna mahali wanaikubali 50/50 na kuna muda wanaiona haifai, kiufupi ni wanawake ambao wanaishi kwa kuchanganyikiwa sababu wameupokea mfumo sawa/jike bila kutambua kuna privilages za kike watazikosa, ila wao wanataka kubaki nazo, hapo ndio kuchanganyikiwa kunapokuja.

Na pia hata ukichunguza wanawake wanaoishi na uchungu sana moyoni na kuparuana na wanaume mara kwa mara ni wale wapenda haki sawa ambao minds zao ziko corrupted na feminism, na huwa wanachukia sana wakiona nyie traditional women mnaishi kwa furaha kwenye ndoa zenu.

Ubarikiwe sana kwakweli.
Asante nashukuru. Nimetoka mbali. Nimejifunza mengi katika maisha nikaja kugundua kuwa this is not how we're meant to live. Sijui hii imekaaje lakini siamini kama katika hali ya kawaida mwanamke anaweza ku thrive akiwa mbali na familia, watoto na jamii. Na hapa siongelei pesa tu but as a whole.

Hii Zion nimetoa kule kwenye kitabu kitakatifu. Zion, the dwelling place of God 😊
 
Back
Top Bottom