Anaitwa Ivan Rakitic (alizaliwa
1988) ni
mchezaji mtaalamu sana ambaye anacheza kama
kiungo wa kati au
mshambuliaji wa
klabu yetu pendwa
Barcelona FC na timu yake ya kitaifa
Croatia.
Rakitić alianza soka huko
Basel na alitumia misimu miwili kabla ya kusainiwa na
Schalke 04. Baada ya kutumia msimu mmoja na nusu
Bundesliga, alisainiwa na
Sevilla mwezi Januari 2011. Miaka miwili baadaye, Rakitić alikuwa nahodha wa klabu ya sevilla na alishinda magoli mengi katika msimu wake wa kwanza. Hapa kama mnakumbuka game yetu ya mwisho ya ligi ilikua dhidi ya Sevilla na huyu jamaa aliwafunga goli letu la nne na hakushangilia kutokana na kwamba wale ni waajili wake wa zamani na aliondoka pale bila matatizonao
Juni 2014, Barcelona na Sevilla walikubaliana juu ya uhamisho wa Rakitić. Alifunga goli la kwanza la Mwisho wa Ligi ya Mabingwa 2015 na akawa mchezaji wa kwanza kushinda Ligi ya Mabingwa mwaka mmoja baada ya kushinda
Europa League wakati akichezea vilabu viwili tofauti....
Huyu jamaa huwa naona nyota yake ni kama ya Busquet tu kutokana na kwamba huwa wanafanya mambo makubwa sana lakini hawaongelewi sana kama wachezaji wengine wanaofanya kawaida na wanaongelewa kila siku, kila kona...
Rakitik kwa sura anaonekana mpole sana sijui maisha yake ya nje ila nahisi atakua hivyo hivyo kama sura yake inavyoonekana, akiwa dimbani huwa ananifurahisha maana mara nyingi anamichezo michafu(Rafu) ambayo huwezi amini kama yeye ndio kafanya, kacheza mechi 517 ana magoli 76, kadi anazo 64 ambazo njano 62 na nyekundu 2(hizo ni takwimu za vilabu vyote alivyowahi kuchezea)
Nilichokumbuka juu yake mpaka kuamua kumuuzisha sura humu jukwaani ni yale magoli yake ya kizazi sana nahisi wote mnayajua kama sio kuyakumbuka ata ukifatilia mechi kadhaa tulizopiga hivi karibuni kama hii dhidi ya Sevilla au ile ya ligi ya mabingwa dhidi ya Tot utakutana na mabalaa yake.....
Poa wakuu jioni njema na maandalizi mema kuelekea game ya EL Clasico..