Fred loong tyme Kaka upo???Niliposikia sikuamini, lakini wanamageuzi hatuna budi kukubaliuana na matokeo haya ya kuumiza sana lakini tusikate tamaa, tawi moja la mti linapokatwa hutoa nafasi kwa matawi mengine mengi kuchipua na hilo ndilo litakalotokea kwa wanamageuzi.. Natoa pole kwa wanafamilia na uongozi wa chama kwa ujumla..
Nipo safarini, nasikia habari hizi mwili unapigwa na ganzi. Nyota imezimika!!Namlilia Regia,
Alitamani kuiona Tanzania ikiwa bora zaidi na ambayo watu wake wanafurahia matunda ya nchi yao kwa haki, usawa na umoja. Tunaposema alikuwa ni mwanaharakati hatutii chumvi. Wengi tumeshuhudia jinsi ambavyo amekuwa ni miongoni mwa wanasiasa ambao wamekomazwa kwenye mitandao hii. Amekuwa jasiri kuliko wanasiasa wengi wakongwe kuja na kupitishwa kwenye tanuru la maoni ya JF na kila wakati ambapo ulifikiria kuwa labda amekwazika na hatorudi tena Regia alirudi na alirudi akiwa mpya kabisa. Aliweza kusimama katika moto bila kuungua na kama aliungua haikuwa rahisi kujua!MMM
Napenda kuchukua nafasi hii nikiwa mjumbe wa H/kuu ya CCM wilaya ya ilala kuwapa pole Viongozi,wanachama na wapenzi wa Chadema kwa msiba wa Mbunge wao wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro Mhe R.Mtema,Mwenyezi mungu awpe nguvu katika kipindi hiki kigumu.