comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 8,227
- 5,949
Uhaini ni kosa la jinai analofanya mtu dhidi nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti.Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini. kifungu 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote akifanya haya atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini:- kujaribu kumuua Rais,
- kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano,
- kusababisha,
- kuwezesha,
- kuchochea,
- kushawishi,
- kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais
- kumwondolea Rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali,
- kupindua serikiali iliyo madarakani,
- kutishia serikali, bunge au mahakama.