Fahamu kuhusu Uchawi wa Mapenzi (Limbwata)

Fahamu kuhusu Uchawi wa Mapenzi (Limbwata)

Mhhhhh?Kazi yote ya nini?Kama upendo upo hakuna haja ya yote hayo

Hata kama upendo haupo, still hakuna haja ya kufanya vitu vya namma hiyo.
Ni bora ukachukua hatua nyingine.

Hivi kweli utafurahi kumuona mumeo anakosana na ndugu zake mpaka mama'ke mzazi kwa ajili yako?? Mbaya zaidi unamfanya zoba anakuwa ni mtu wa vituko tu na hata kutoelewana na wenzie kwa ajili ya mapenzi
tu.......hivi kweli siku ukitoka duniani huyo mtu anaishije?
 
Hahahhah utakua chizi kila mtu na limbwata lake ....
adriyel KICHEKO! kwa mfano kila mwanamke mmoja, tena kila mmoja na kabila lake, akuwekee limbwata lake la kuto huko kwao, best lazima urukwe na akili!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu pmwasyoke hata mimi ktk vitu ambavyo vinanchanganya ni kwa nini wanaume hawatumii hizi techn?
Wao ndio walengwa wanaohitaji kutulizwa ndio maana asilimia kubwa wanao fanya haya ni wanawake…
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha sana tena sana, jamaa yangu kipenzi kalishwa, nimejaribu kumweleza lakini kanibadilikia zaid ananiona mimi kama adui yake tena mkubwa ajabu, amepita humu na ukweli ameupata.

Dadaa zangu uchawi na dawa ya mapenzi ni pumzi na kishindo mkiwa 6£6
 
Jamani mmeshinda poa!

Wanawake / Mabinti baadhi wamekuwa watumiaji wazuri wa limbwata kama
sehemu ya kuongeza chachu ktk mahusiano yao ya mapenzi. Zifuatazo ni
baadhi ya teknolojia maarufu ama niseme pendwa za limbwata. Waweza
kuongeza yoyote ile uijuayo:

Kinyama

Hii kitu kuna siku Mkuu MziziMkavu aliielezea
vizuri tu. Katika hili, kipande kidogo cha nyama mfano wa mnofu mmoja wa
“mshikaki” huwekwa katika maku ya mtaka tiba, kwa muda wa siku
kadhaa kulingana na masharti ama maelekezo ya mganga husika “fundi”,
baadae kinyama hiki hupikwa na sehemu nyingine ya kitoweo kama mboga na
kuliwa. Mlengwa wa limbwata ataathirika mara tu baada ya kula mlo
uliohusiha mboga yenye kinyama hiki! Wanaoipenda njia hii wanasema ni
ngumu sana kumuagua mwanaume alielishwa kinyama

Maji ya mchele:

Hii ni aina nyingine ya teknolojia ya limbwata. Ni kwamba kwa kutumia
njia hii, maji ya kawaida hupelekwa kwa mganga kwa ajili ya kazi husika,
na kisha maji hayo hurudishwa nyumbani, mwanamke mhusika huyatumia maji
ya dawa haya kuoshea maku na baadae huyatumia kuoshea mchele ama
hata kupikia kabisa! Limbwata hili hufanya kazi kwa mlengwa baada ya
mlengwa kula chakula kilichopikwa kwa maji tajwa! Wanaoipenda njia hii
wanasema ni ngumu sana kumuagua mwanaume alienyeshwa maji hayo, na
kwamba ili kumuagua lazima apatikane fundi Yule Yule aliefanya yake!

Kisomo:

Nyingine. Hii haisemwi sana, ni kama siri kubwa, huwa haijulikani hasa
ni aina gani ya “kisomo” hufanyika lakini wateja na wafuasi wa limbwata
la aina hii wanakiri kuwa, mwanaume aliesomewa (msomaji ni fundi
“mganga”) huwa ni zaidi ya kondoo, kwa maana ya kuwa maisha yake yote
yaliyobaki yanakuwa ni yale ya “ndio mzee” kwa mwanamke alietengeneza!
Wanaoipenda njia hii wanasema sio nzuri sana kwa vile fundi mwingine
yoyote anaweza akafanya kisomo kinyume.

Kifaranga:

Hapa mwanamke mhitaji huagizwa na fundi kupeleka kifaranga, na mara
nyingi ni cha kuku. Fundi humfanyia kazi Kifaranga huyu katika karakana
yake, namna fundi anavodili na kifaranga hiki ndio ndio kazi halisi ya
kumuinamisha mme ama mpenzi wa mtu, kifaranga huyu hubaki ktk himaya ya
fundi kwa maisha yake yote, na namna kifaranga huyu anavolelewa na huyu
fundi, na kufuata anavotaka mfugaji, ndio hivo hivo mlengwa
atakavopelekwapelekwa! Njia hii inachangamoto moja kubwa, usalama na
uhai wa kifaranga huwa ni tatizo, na iko subjected to frequent updates!

Jina kuning’nizwa juu ya mti:

Hii inafanana na kisomo. Tofauti ni kwamba, baada ya fundi kufanya kazi
yake, huku jina la mlengwa likiwa limenuiwa, karatasi lililoandikwa jina
hili (jina la mwanaume mlengwa) huenda kuning’inizwa katika moja ya mti
mrefu ambao ni sharti uwe mbali na wanapoishi wapenzi ama wanandoa hao,
wakati mwingine inahusisha mkoa mmoja hadi mwingine! Wanasema
kusipokuwepo na upepo, mwanaume huwa mjanja mjanja, lkn upepo ukivuma
kidogo tu, mwanaume huyu akili huruka na kumuwaza aliemtengeneza! Ili
upone kutoka katika limbwata hili, lazima huu mti utafutwe na kikaratasi
kikatwe, ndio utapona!

Kaburi la mtoto

Hapa kuna vitu hufukiwa. Kama ilivo limbwata la hapo juu, limbwata hili
linahusisha madawa na majina ya mlengwa. Kaburi husika hutafutwa maeneo
ya mbali sana. Madawa na majina ya mlengwa hufukiwa katika kaburi la
mtoto. Hapa huponi mpaka kaburi lipatikane na kazi ifanyike hap!

Unyayo kucha ama kinywele:
Hapa kuna mchanganyiko wa ufundi unaotumika. Wapo wanaotumia mchanga wa
unyayo, wapo wanaotumia kipande cha v.u.z.i, wengine hutumia hata
c.h.u.p.i ya mlengwa, lakini yote kwa yote ni kwamba fundi atadili na
mlengwa kutumia aina mojawapo ya nyenzo hizi! Mafundi wengi inasemekana
ni wataalamu wa kuagua wahanga wa njia hii!

Kazi kwenu wapenda michepuko!

wew mwenyewe umetumia ndo maana unaleta hapa feedback. limbwatani ujanja wangu tu na sio hayo ulotajwa.
 
Last edited by a moderator:
Duuu! Kumbe kuna limbwata ee..koz k ninayo ngoja nijaribu
Kumwekea mwafulani...hivi ni mpaka nimwone sangoma au naeza nunua nyama na kuinuwia mwenyewe?msaada jamani
kazurikazuri kwa wewe mwenyewe hutaweza, kuna teknolojia ya "fundi" inahitajika, wewe jukumu lako ni kupeleka tu kinyama!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom