Face 2 Face with Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo: "Tunafanya Politics of Engagement kwa kuwa Pragmatic on What is Possible"

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,499
113,605
Wanabodi,
Tunakwenda shule ili kufunzwa maarifa, sio kupata akili, akili kila mtu anazo na anazaliwa nazo, ila jinsi ya kuzitumia ndicho tunachopaswa kujifunza na kufundishwa.

Mimi najihesabu ni muelimishaji umma kupitia kipindi changu cha TV, "Kwa Maslahi ya Taifa" na makala zangu za magazeti na humu JF.

Nimeamua kuanzisha darasa la watu kujifunza kwa wengine, hivyo nitakuwa nakuletea makala hizi za Face 2 Face zikihusisha mahojiano na watu mbalimbali kuhusu mada mbalimbali kwa kuwatumia watu hao kufundisha wengine.

Mwalimu wetu kwenye darasa la leo, ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe

Kwanza msikilize na uniambie umeelewa nini ili hicho ulichoelewa wewe uwafundishe na wengine.
View: https://youtu.be/RPpcwlnNJ0A?si=KLISZZ3sCb243xzz

Kwa vile sisi binadamu ni tofauti na tuna uwezo wa uelewa tofauti tofauti, mimi nimejitolea nitakuwa nawafanyia a short summary recaps ili wengi zaidi wafaidike na darasa hili.

Zitto ametufundisha kitu kipya kwenye siasa zetu, badala ya zile politics of confrontations za mikutano, maandamano, mivutano, kupigishana kelele and sometimes kutukanana kwa issues za kisiasa kusababishwa kuvuja kwa machozi jasho na damu, ACT Wazalendo inafanya siasa za politics of engagement.

Zitto Kabwe amesema
" Kwa miaka zaidi ya 30 ya siasa zetu za vyama vingi siasa zetu zimekuwa ni siasa za confrontations, kuandamana, kununa, kususa na hatupati chochote!.
Ukifanya jambo lili lile kwa namna ile ile ukitegemea matokeo tofauti, hapa utakuwa unajidanganya"
"Tumeamua kufanya siasa za engagement ili kuwezesha mageuzi kufanyika. Hiki kinachofanyika hapa ni matokeo ya kazi yetu, tumefanya mkutano Dodoma, tumeshiriki kwenye kikosi kazi, tumetoa mapendekezo, leo tunajadili utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi, hili ni jambo kubwa.

Huu sio mkutano wa kupindisha pindisha mambo, ni mkutano wa kunyoosha mambo kuleta matokeo chanya tunayoyataka.

Ofisi ya Waziri Mkuu imeishatangaza kuna miswada mitatu inapelekwa Bungeni kwenye Bunge la October kujadiliwa
  1. Muswada wa mabadiliko ya Tume ya Uchaguzi kuunda Tume Huru ya Uchaguzi
  2. Muswada wa mabadiliko ya sheria ya uchaguzi
  3. Muswada wa mabadiliko ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Sisi tumeomba iongezwe miswada mingine miwili
4. Muswada wa kuhuishwa tume ya Warioba na kukwamua mchakato wa katiba mpya uliokwama
5. Muswada wa mabadiliko madogo ya katiba ili mabadiliko hayo yapate nguvu ya katiba.

Sisi tunafanya siasa za Pragmatism on doing and getting what is possible"

My Take
Hizi ndio siasa za ukweli, kinyume cha utopian politics".

Paskali
 

Attachments

  • pasco.mp4
    25 MB
Wazalendo inafanya siasa za politics of engagement.
Which kind of political engagement?

Huyu tayari ameshapoteza mvuto kwa kuonesha wazi upande unaouunga mkono. Itikadi zake za kidini, fitina alizofanyia taifa awamu iliyopita zimemshusha viwango!

May be ungewatafuta akina mzee Warioba, Msuya nk au watu wenye uelewa wa masuala ya kisiasa wasio na majina makubwa! Achana na hawa vijana wachumia matumbo!
 
Engagement ipi wakati katiba mpya imeshapotezewa? Hivi unaweza unga mkono elimu ya katiba ya zamani itolewe miaka 3 Tena kwa billion 200? Why wasitoe elimu ya rasimu itakayopendekezwa?

ACT sio kama wako engaging ila hawana choice pona Yao ni maridhiano na CCM otherwise hawawezi pambana na CCM head-on kulinganisha na CHADEMA ambayo haihitaji endorsement ya CCM ili kushinda chaguzi yoyote au kuongeza ushawishi kwa wananchi.
 
Siku zote Zitto namuona mpuuzi tu, hana strategy yoyote, au kama anayo, basi ni ya kipuuzi vile vile, kusubiri kiongozi wa imani ipi aingie ikulu, ili nae aamue afuate mlengo upi, huyo ni mnafiki.

Huyo mnafiki leo anasema hataki kufanya politics of confrontations, za mikutano, maandamano, na nyinginezo kwa sababu anajua aliyepo ikulu ni "mama yake katika imani"

Hiyo ndio sababu iliyomfanya ameamua kuwa laini hata pale anapoona maslahi ya Tanganyika na watu wake yanawekwa rehani na mama yake, akisema nyingine yoyote tofauti na hiyo ni muongo, huyu kiumbe ni wa hovyo kabisa kuwepo kwenye siasa zetu, ni mnafiki, mlafi, anayependa kujipendekeza, wala asiye na msimamo wowote.

Matokeo yake sasa, leo anawaona wabaya, wanaofanya siasa mbaya, wale walioamua kuipigania Tanganyika na rasilimali zake, wale walioamua kutumia njia tofauti ilimradi kufanikisha malengo yao, hasa baada ya kumuona binti kiziwi pale ikulu ameamua kutuzibia masikio, hataki njia ya mazungumzo, ajabu kwa Zitto, huu ni ubaya!.

Mimi Zitto hawezi kunifundisha chochote, labda unafiki tu ikitokea siku nikiuhitaji!.
 
Mimi kiuweli hata sielewi huyo Zitto anazungumzia nini...
Hoja zijibiwe tu....

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Hili litanipita kwangu Zitto hafai sasa na hata milele, in fact you have had the same chain, you're no longer a man of integrity, you lost impartiality approach to issues, you opted to be a coward.
Ni ukweli mchungu kuwa ndege wafananao huruka pamoja. Ilikuwa ni swala la muda tu kwa hao ndege wawili kujitambua kuwa wanafanana na hivyo kuruka pamoja. Zitto na Mayalla? What a combination na sasa tujitayarishe kushuhudia mengi.

Je tumewahi kujiuliza ilikuwakuwaje hadi Rais aliyetangulia aliweza kuishi pamoja na makamu wake bila kutofautiana hata mara moja? Nadhani hili si swali tena kwa watu wanaofuatilia matukio ya sasa kwani sote tunashuhudia kazi inavyoendelea!

The chickens are coming home to roost!
 
Wanabodi,

Tunakwenda shule ili kufunzwa maarifa, sio kupata akili, akili kila mtu anazo na anazaliwa nazo, ila jinsi ya kuzitumia ndicho tunachopaswa kujifunza na kufundishwa.

Mimi najihesabu ni muelimishaji umma kupitia kipindi changu cha TV, "Kwa Maslahi ya Taifa" na makala zangu za magazeti na humu JF.

Nimeamua kuanzisha darasa la watu kujifunza kwa wengine, hivyo nitakuwa nakuletea makala hizi za Face 2 Face zikihusisha mahojiano na watu mbalimbali kuhusu mada mbalimbali kwa kuwatumia watu hao kufundisha wengine.

Mwalimu wetu kwenye darasa la leo, ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe

Kwanza msikilize na uniambie umeelewa nini ili hicho ulichoelewa wewe uwafundishe na wengine.


Kwa vile sisi binadamu ni tofauti na tuna uwezo wa uelewa tofauti tofauti, mimi nimejitolea nitakuwa nawafanyia a short summary recaps ili wengi zaidi wafaidike na darasa hili.

Zitto ametufundisha kitu kipya kwenye siasa zetu, badala ya zile politics of confrontations za mikutano, maandamano, mivutano, kupigishana kelele and sometimes kutukanana kwa issues za kisiasa kusababishwa kuvuja kwa machozi jasho na damu, ACT Wazalendo inafanya siasa za politics of engagement.

Itaendelea...

P
Wewe politics of engagement zilikufikisha wapi?. Ulipata kura moja.
 
Siku zote Zitto namuona mpuuzi tu, hana strategy yoyote, au kama anayo, basi ni ya kipuuzi vile vile, kusubiri kiongozi wa imani ipi aingie ikulu, ili nae aamue afuate mlengo upi, huyo ni mnafiki.

Huyo mnafiki leo anasema hataki kufanya politics of confrontations, za mikutano, maandamano, na nyinginezo kwa sababu anajua aliyepo ikulu ni "mama yake katika imani"

Hiyo ndio sababu iliyomfanya ameamua kuwa laini hata pale anapoona maslahi ya Tanganyika na watu wake yanawekwa rehani na mama yake, akisema nyingine yoyote tofauti na hiyo ni muongo, huyu kiumbe ni wa hovyo kabisa kuwepo kwenye siasa zetu, ni mnafiki, mlafi, anayependa kujipendekeza, wala asiye na msimamo wowote.

Matokeo yake sasa, leo anawaona wabaya, wanaofanya siasa mbaya, wale walioamua kuipigania Tanganyika na rasilimali zake, wale walioamua kutumia njia tofauti ilimradi kufanikisha malengo yao, hasa baada ya kumuona binti kiziwi pale ikulu ameamua kutuzibia masikio, hataki njia ya mazungumzo, ajabu kwa Zitto, huu ni ubaya!.

Mimi Zitto hawezi kunifundisha chochote, labda unafiki tu ikitokea siku nikiuhitaji!.
 
Wanabodi,

Tunakwenda shule ili kufunzwa maarifa, sio kupata akili, akili kila mtu anazo na anazaliwa nazo, ila jinsi ya kuzitumia ndicho tunachopaswa kujifunza na kufundishwa.

Mimi najihesabu ni muelimishaji umma kupitia kipindi changu cha TV, "Kwa Maslahi ya Taifa" na makala zangu za magazeti na humu JF.

Nimeamua kuanzisha darasa la watu kujifunza kwa wengine, hivyo nitakuwa nakuletea makala hizi za Face 2 Face zikihusisha mahojiano na watu mbalimbali kuhusu mada mbalimbali kwa kuwatumia watu hao kufundisha wengine.

Mwalimu wetu kwenye darasa la leo, ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe

Kwanza msikilize na uniambie umeelewa nini ili hicho ulichoelewa wewe uwafundishe na wengine.


Kwa vile sisi binadamu ni tofauti na tuna uwezo wa uelewa tofauti tofauti, mimi nimejitolea nitakuwa nawafanyia a short summary recaps ili wengi zaidi wafaidike na darasa hili.

Zitto ametufundisha kitu kipya kwenye siasa zetu, badala ya zile politics of confrontations za mikutano, maandamano, mivutano, kupigishana kelele and sometimes kutukanana kwa issues za kisiasa kusababishwa kuvuja kwa machozi jasho na damu, ACT Wazalendo inafanya siasa za politics of engagement.

Itaendelea...

P
ACT ni CCM B; so lazima wafanye siasa laini ili kuwafurahisha CCM. Hilo halina ubishi.
 
Zito namkubali anafanya siasa zenye uhalisia, sio wale wanaosema hawatapokea ruzuku iliyotokana na Uchaguzi batili wanashangiliwa, na wafuasi wao baadae wanapokea, wafuasi wao wanawashangilia tena

Wanadai hawatashiriki uchaguzi mpaka kuwe na katiba mpya, na wanashangiliwa na wanachama wao, then baadae wanashiriki bila hiyo katiba kupatikana wanashangiliwa tena na wanachama walewale
 
Hizi ndo "politics of engagement za Zitto na chama Cha ACT"
20220925_003728.jpg
 
Back
Top Bottom