Experience yangu kuhusu betting (Ukamaria)

Experience yangu kuhusu betting (Ukamaria)

1x bet warusi hawa nachezea nikiwa nje lakini
Acha kuanza utapeli na hizo demo account zenu za makampuni ya kirusi.

Nakupa challenge moja, Kama kweli ulikua ukibet hivyo kama ulivyoweka, onyesha hapa account management ambayo huonyesha transactions zote deposit na withdrawals. Nina uhakika asilimia 100 hutaweza kufanya hiki nilichokuambia
 
Nilichojifunza kwenye hii dunia kila mahali kuna michezo mingi yakitapeli watu wakiitaka pesa yako katika namna yoyote ile!, so hivyo tamaa zako zinaweza kukufanya udondokee kwenye faida au hasar japo wengi hudondokea kwenye hasara!, wachache ndo hufaidika.

Nafikiri inahitajika elimu ya fedha hasa kwa vijana wasitumie fedha ambayo inaweza kuwaletea shida kwenye haya mambo!.
 
Sikikiza ww ICT guru kubet hakuna algorithm, kubet ni kama ilivyo shughuli nyingine yoyote, kuna kupoteza na Kuna kupata. Unafikiri wanaowekez kwenye kilimo wote hupata? Au wanaowekeza kwenye madini wote hupata? Au wanaowekeza kwenye usafirishaji wote hupata?

More than 65% ya watanzania wanajishughulisha na kilimo, je ni wangapi wamefanikiwa? Kwa hiyo inabidi watu waache kiliko sababu miaka yote kimeahindwa kuwafaidisha kulingana na muda na nguvu walizowekeza?
Mimi sio guru. Sijui hizo algorithm ila zipo hazifichwi unaweza ukagoogle.

Kila kitu kina risk, ila unapaswa upime risk kabla ya kuichukua. Licha ya bahati, kuna mengi mkulima akiyafanya sawa anapata faida. Kuna nini ukifanya sawa unafaidika na kamari? Hakuna.

Wanaopiga hela kwenye betting ni maquant wenye advanved degrees za hesabu na computer science wanaoweza kuchambua hizo algo, tena wanafanikiwa kwa makundi(syndicates) na bado wanakuambia mbinu zinaisha nguvu haraka kwa kuwa ukishazitumia tu mifumo inaboreshwa.

Hakuna hela rahisi.
 
Kila kitu kina risk, ila unapaswa upime risk kabla ya kuichukua. Licha ya bahati, kuna mengi mkulima akiyafanya sawa anapata faida. Kuna nini ukifanya sawa unafaidika na kamari? Hakuna.
Unasema kuna mengi mkulima akiyafanya sawa anapata faida? So ndio?
Ni lipi hilo ukilifanya sawa sawa kwenye kilimo una uhakika wa kupata faida? kwa hiyo hawa mamilioni ya watanzania waliopo kwenye kilimo kwa makumi ya miaka unahisi hawafanyi sawa sawa? Kila mwaka wanakosea tu?

Wanaopiga hela kwenye betting ni maquant wenye advanved degrees za hesabu na computer science wanaoweza kuchambua hizo algo, tena wanafanikiwa kwa makundi(syndicates) na bado wanakuambia mbinu zinaisha nguvu haraka kwa kuwa ukishazitumia tu mifumo inaboreshwa.
Wanapiga hela kwa mtindo upi? Hiyo algorithm inahusiana vipi na matokeo uwanjani? Kwamba wanakua wanajua arswnal vs man city lazima arsenal afungwe? Au wanakua wanajua man city vs Bournemouth hapo lazima mechi iwe draw?

Hakuna anayejua matokeo ya mpira, ni akili ya kawaida tu inatumika kuwa arsenal yupo nyumbani na ana timu nzuri kuliko burnley hivyo arsenal atashinda. Ni nadra sana matokeo kuja tofauti na hapo
 
Unasema kuna mengi mkulima akiyafanya sawa anapata faida? So ndio?
Ni lipi hilo ukilifanya sawa sawa kwenye kilimo una uhakika wa kupata faida? kwa hiyo hawa mamilioni ya watanzania waliopo kwenye kilimo kwa makumi ya miaka unahisi hawafanyi sawa sawa? Kila mwaka wanakosea tu?


Wanapiga hela kwa mtindo upi? Hiyo algorithm inahusiana vipi na matokeo uwanjani? Kwamba wanakua wanajua arswnal vs man city lazima arsenal afungwe? Au wanakua wanajua man city vs Bournemouth hapo lazima mechi iwe draw?

Hakuna anayejua matokeo ya mpira, ni akili ya kawaida tu inatumika kuwa arsenal yupo nyumbani na ana timu nzuri kuliko burnley hivyo arsenal atashinda. Ni nadra sana matokeo kuja tofauti na hapo
Mkulima ana mengi anayoweza kudhibiti haswa akiwa na nguvu ya mtaji mkubwa. Uhakika haupo ila uzoefu na mikakati husaidia.

Hakuna anayejua hatima za mechi ila mifumo iliyopo imetengenezwa na haya makampuni ili kujifaidisha.

Shida ni kwamba hili ni jambo la kitaaluma sana ambalo mimi na wewe hatuwezi kung'amua ila zipo makala kibao zinazozungumzia haya.
 
Mkulima ana mengi anayoweza kudhibiti haswa akiwa na nguvu ya mtaji mkubwa. Uhakika haupo ila uzoefu na mikakati husaidia.
Nimekuuliza Hawa mamilioni ya wakulima kwa miaka yote Wameshindwa kufanya hayo unayosema ili wapate faida? Kwa miaka yote hii kwa nini hawadhibiti hiko unachosema ili wapate faida?

Hakuna anayejua hatima za mechi ila mifumo iliyopo imetengenezwa na haya makampuni ili kujifaidisha.
Kampuni yoyote huundwa ili kujifaidisha. Kwa hiyo Ulitegemea kampuni ya betting isijifaidishe?
Kampuni ya betting inahusiana vipi na mawazo yako utayoamua kuwa ivory coast itachukua world cup? Wewe kwa utashi wako mwenyewe bila kulazimishwa na yoyote umebet kuwa Ivory coast itashinda world cup, hapo kosa la kampuni ya betting ni lipo wapi endapo utaliwa?

Shida ni kwamba hili ni jambo la kitaaluma sana ambalo mimi na wewe hatuwezi kung'amua ila zipo makala kibao zinazozungumzia haya.
Hakuna jambo la kitaaluma, betting ya mpira wa miguu ipo wazi, mpira unachezwa wote mnauona na matokeo mnayaona
 
20260523_063812.jpg
 
Unasema kuna mengi mkulima akiyafanya sawa anapata faida? So ndio?
Ni lipi hilo ukilifanya sawa sawa kwenye kilimo una uhakika wa kupata faida? kwa hiyo hawa mamilioni ya watanzania waliopo kwenye kilimo kwa makumi ya miaka unahisi hawafanyi sawa sawa? Kila mwaka wanakosea tu?


Wanapiga hela kwa mtindo upi? Hiyo algorithm inahusiana vipi na matokeo uwanjani? Kwamba wanakua wanajua arswnal vs man city lazima arsenal afungwe? Au wanakua wanajua man city vs Bournemouth hapo lazima mechi iwe draw?

Hakuna anayejua matokeo ya mpira, ni akili ya kawaida tu inatumika kuwa arsenal yupo nyumbani na ana timu nzuri kuliko burnley hivyo arsenal atashinda. Ni nadra sana matokeo kuja tofauti na hapo
Labda wana hack mfumo, wanabet baada ya matokeo
 
Mhindi ana kanuni moja tuu ya karne nyingi ya biashara "Pata faida ndogo kutoka kwa watu wengi, wanaonunua kwa muda mfupi".
Kupitia kanuni hiyo, ndipo alipopata wazo la "Sports betting". 😊
Mechi moja au mbili, anaweka "Odds" ya kuwavutia 😋. Watu milioni tatu wanaweka pesa ndogo ila kwa wingi sana.
Mhindi anakaa na pesa zenu zile kwenye system yake. Mechi inaisha wanashinda watu elfu moja. Anawalipa hela zile zile mlizoweka. Wale waliokosa ambao ni asilimia 95% anabaki na jero jero zao kama faida. 😁

Very sad na watu hawakomi
 
Back
Top Bottom