EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
Na swali moja tu kwa Zitto Kabwe.

1. Swali langu kuna uwezekano mkubwa Watanzania tukaingia kwenye uchaguzi mkuu na katiba hii iliyopo kabla ya katiba mpya kuwa tayari. Je utafanyaje kuhusu nia yako ya kugombea urais umri utakuwa umekubana kutoka na katiba iliyopo sasa. Wakati umeishawambia jimboni kwako Kigoma Kaskazini kuwa mwaka 2015 hautogombea tena ubunge utagombea urais.

Swali la nyongeza:

Mkuu Zitto kwa kuwa wewe ni mwanasiasa kijana chini ya miaka 40 na kwa kuwa ulishasema kwamba mwaka 2015 utagombea Urais na wala hutagombea Ubunge. Je ikiwa mwaka 2015 katiba mpya itakuwa haijakamilika ama hata kama ikiwa imekamilika lakini akasema umri wa kugombea Urais ni kuanzia miaka 40 hivyo basi utakuww umetupwa nje ya Bunge na Nje ya Urais. Swali: Je utaendeshaje maisha yako ya kisiasa nje ya Bunge na nje ya taasisi ya Urais?
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru kwa jitihada zako. Ila unaharibu mjadala unapotaka tutume maswali kwanza alafu uyachambue ya kuuliza na kutokuuliz. Kama zito
kaamua kuja kufanya interview acha tumhoji bila kuchuja yeye ndo achague la kujibu. Huo utaratibu wa kuchaguliana maswali upo kwa makanjanja pekee.
 
(1) Yes, Mheshimiwa ZZK je ni ukweli kuwa wewe ni mshauri wa uchumi wa ujerumani. Kama ni ukweli je ni kitu gani kilichokutambulisha hadi kufikia kupewa hiyo nafasi.
(2) Mhe. ZZK mara nyingi unakuwa kwenye ziara za Mhe. Rais wa Tanzania, mnapokuwa safarini huwa unapenda kuongelea nini.

(3) Zitto Zuberi Kabwe unaionaje elimu ya Tanzania, kwanini shule zetu za Msingi zimepoteza umaarufu wake kabisa. Unasemaje kuhusu serikali kukurupuka na kubadili mitaala ya elimu kila mara, kwa mfano huu utaratibu wa mwanafunzi kumaliza 'A' level na kusubiria kwenda chuo kikuu kwa muda wa almost mwaka mmoja na nusu utakuwa na tija gani kwa vijana wetu wa kike. Una ushauri gani kwa serikali yetu.
 
Sote twajuwa kama misingi iliyobuniwa na muasisi wa taifa hili, hayati Kambarage, imevurugwa na chama alichokianzisha mwenyewe. chama cha mapinduzi. CCM ya leo ni ccm ya wahujumu uchumi, CCM ya walanguzi, CCM ya watu wabinafsi walio tayari kuona watanzania wanasota kwenye umaskini, lakini wao (kikundi kidogo cha waTZ) wakiishi maisha ya neema na anasa za kila aina. haihitaji ushahidi wa kimahakama juu ya hili.

Swali kwa ZZK:
===========
anazungumza nini juu ya watanzania wanaoishi maisha ya kuunga-unga, si kwa kupenda bali kwa kutokana na hali halisi kwamba ccm imewajengea mazingira ya kuishi katika hali hiyo; lakini waTZ hawahawa wanaoishi maisha ya kuunga-unga, bado wanakipigia kura chama hichi kilichojaa watu wenye uchu wa kukwaa madaraka na kujineemesha kwa rasilimali za taifa letu?
 
swali kwa muheshimiwa zitto kabwe Je kwa nini kila yanayotolewa na chadema bungeni wa bunge wa chama tawala wanasema ni uongo hata pale inapoonekana ni ukweli? na swali la pili hivi tanzania tuna sera ya nchi kweli au ni ya chama na serikali tu ndio iliyopo? ni hayo tu.
 
1. Mkuu Zitto katika utawala bora inaelekezwa kwamba kuwe na vyombo vya usimamizi yaani oversight institutions kama vile Bunge (na kamati zake) ili kusimamia executive (management). Hapa tunapata dhana ya governance na management. Kwa mujibu wa utaratibu wa corporate governance inabidi oversight institutions zisifanye kazi za kiuongozi ama kiusimamizi wa moja kwa moja wa taasisi za serikali kwani vitashindwa kukosoa.

Lakini mkuu tunaona Wabunge wakiwa kwenye Bodi za Wakurugenzi wa Mashirika ya Umma hapa nchini. Hii inapingana na dhana ya utawala bora. Kumbukumbu zangu zinaonyesha ya kwamba uliwahi kulipigia kelele suala hili lakini sijui kama ulilifikisha mwisho.

Swali:
Je unaonaje kama utajiandaa kupeleka Hoja binafsi Bungeni ili Bunge liazimie kwamba ni marufuku kwa Wabunge kuwa Wajumbe wa Bodi za Wakurugenzi wa Masjhirika ya Umma? Sina hakika kama Wabunge watakubali kwa kuwa ni wanufaika lakini kama utapeleka hoja yako kimahiri sina shaka litakubaliwa.


2. Mkuu Zitto kuna hili suala la Posho mbalimbali ikiwemo posho za vikao. Nakumbuka hapo nyuma uliwasha moto juu ya hizi posho na ukaamua kutopokea posho za vikao vya bunge na hata walipokuambia kuwa utapokea tu kwa kuwa ulikuwa unasini daftari la mahudhurio bungeni uliamua kutosaini.

Haikuishia hapo walikutishia kwamba utafukuzwa bungeni kwa mujibu wa kanuni kwa kuwa utaonekana kwamba hujahudhuria vikao/mikutano kadhaa lakini ulikuja na hoja ambazo naona ziliwazima. Baada ya huo utangulizi naomba kuuliza maswali yafuatayo:


a) Najua msimamo wa Chama chako juu ya posho ni kuzipinga, je Chama chako kinatekelezaje msimamo huo kwa vitendo?

b) Je katika suala hili ulipata ushirikiano wa kutosha toka kwa wapinzani wenzako bungeni?

c) Je ulipata ushirikiano wa kiwango gani toka kwa Wabunge wa CCM?

d) Je hadi sasa hupokei posho za vikao?
 
1.Zitto wewe ni naibu katibu mkuu wa chadema.Mara nyingi matamko ya chama yametolewa na katibu,mwenyekiti,mnyika(tangu kabla hajawa msemaji) na mara chache wanasheria km Lissu,Marando na Prof.Safari.Kwa nini Zitto umekuwa mbali sana na matamko haya mbalimbali ya chadema ukiwa kama naibu katibu mkuu?(Naamini hutojibu ni mgawanyo wa kazi?

2.Unafikiri chadema uliyoiasisi na kujitolea kwa nguvu zote kutaka kiwe chama makini ndiyo hii ya sasa au kuna mabadiliko?Kama kuna mabadiliko ni yepi na unafanya nini kufanya chadema iwe kama ambavyo ulitaka iwe?

3.Unafikiri namna chadema inavyoendesha siasa zake kuna uwezekano wa kushika dola mapema?(2015?).Kama ndiyo kwa nini na kama hapana unafikiri mabadiliko gani yanatakiwa kufanyika kuelekea 2015?
 
Mh zitto kabwe,naibu katibu mkuu chadema taifa.
1. Kwa nini chadema haiwatumii viongozi wa mikoa na wilaya na badala yake inatuma watu toka makao makuu hata kwa mambo madogo madogo ambayo yangemalizwa na uongozi wa ngazi husika?

2.kwa nini chadema imekuwa ikijikita sana ktk operesheni mbalimbali zinazokusanya mamia ya wanachama,lakini inashindwa kuweka taratibu nzuri za malezi kwa wanachama hao wapya,huku si kusuka kamba inayoungua?

3.nipe sababu ya kughairishwa kwa chaguzi za msingi ndani ya chama na endapo katiba imefuatwa.
Asante.
 
ningependa nijue kutoka kwa zzk "urafiki wake na zoka ulianza lini?"
 
kwani kuna ubaya gani bosi kujua mshahara wa mfanyakazi wake?
Kama wewe ni boss lazima utajua tu mshahara wa subordinate wako kupitia utendaji wa kila siku wa kikazi.Sisi ni maboss wa rais lakini ubosi wetu ni tofauti sana kwani ni maboss kinadharia lakini kivitendo sisi tupo mbali sana na huyo rais.
 
Zitto ni kweli hauelewani na Mwenyekiti wako Freeman Mbowe? Inasemekana ndani ya CDM kuna kambi mbili na inasemekana hata hizo uniform zenu kuna namna zinawakilisha makundi.

1. Uniform ambayo shati ni mikono mifupi inawakilisha kambi yako Zitto
2. Mikono mirefu inawakilisha kambi ya Freeman Mbowe
 
Mh Zitto,
katika moja ya hoja zinazojaribu kukiandama chadema na kuleta mtafaruku baina na chama na wananchi ni udini.
kiasi kwamba wanasema hata ukiwa muislama ila ukiingia ndani ya chadema basi unakua huna nguvu tena unabakia
kumbwelembwela tu ili mradi upo.mfano mzuri ni wewe,makamu mwenyekiti bara na prof safari.mpo lakini hamna meno.
na hiyo imeleta sura mbaya kwa chama kiasi kwamba kuna waislam wengi wanakiponda chama kwa madai ni cha kikristo
huku CUF wakidai ni cha kiislam..

swali..
1.Nyie kama viongozi wa chama mnalichukuliaje na mna mikakati gani kutoa huo ukungu wa udini ndani ya chama.
ili zile fikra potofu za udini na ukabila ziondoke?
2.wewe kama naibu katibu mkuu,mbona hatuoni kama una uzito ndani ya chama hadi tunafikilia hiyo nafasi yako ifutwe ibakie ya katibu mkuu tu,unalisemeaje hili?

Mara nyingi sisi wananchi wenye mtazamo hasi hatuamini kama wewe una mchango katika chama kwa miaka ya hivi karibuni hasa kipindi hiki cha M4C,huonekani katika mihadhala na mandamano vijijiji kiasi kwamba waonekana msaliti ndani ya chama..
Swali.
1.wewe unalichukuliaje hili?..
2.ni kwanini hujichanganyi na viongozi wengini wanapoenda huko vijijini?
3.unatuambia nini kuhusu huu mtazamo hasi dhidi yako?
4.NB.usijibu historia yako ndani ya chama bali jibu kwa miaka ya hivi karibuni.kwani huko nyuma tunaujua mchango wako chamani.
 
Nikiona maswali hayajibiwi naanza kuchit chat

You have a point though

Nashukuru for the tag,mwaswali yapo lakini sidhani kama yatajibiwa.I'm pessimistic on this one.

Kuna uwezekano mkubwa nikawa msomaji tu.
 
Zitto Umeoa?? na kama hujaoa Kwa nini??

Unaipenda CHADEMA au CCM??hata kama uko CHADEMA mapenzi yako yanaonekana uko CCM kutokana na kuonekana sehemu mbali mbali za sirini na watu wa CCM wakiwemo wakuu wa Inteligensia wa nchi hii/

Wewe ni UAMSHO au la??kuna taarifa za wazi kuwa unauunga UAMSHO mkono kwa hali na mali na umepenyeza rupia kadhaa kuwasaidia na ndio maana tokea wameanza vurugu hujawapinga wala kutoa kauli kama kawaida yako


Je una penda kuongoza Tanganyika au Tanzania??katika harakati zako za kuongoza nchi inaonekana hutaki kusikia neno Zanzibari ndio maana umeanza harakati ukanda wa Ziwa Victoria na Tanganyika


Unamchukia adui RUSHWA??Mbona uliiponda mitambo ya kampuni ile na baada ya kulambishwa mlungula uliitetea kama sio wewe??

NINA MASWALI MENGI ILA MLETA THREAD UWE NA DISCIPLINE YA KUONGOZA USITULIMIT KWENYE MASWALI KWANI YEYE ZZK NDIO AAMUE ANAJIBU LIPI NA KUACHA LIPI
 
Napenda kumuuliza mheshimiwa Zito Kabwe yafuatayo:-
1. Kuacha kugombea ubunge 2015 ni kumwachia Yared Fubusa, na ni kweli ndiye aliyekujenga kisiasa?

2. Kama ni hapana Yared Fubusa yuko wapi kwa sasa na bado ni mwanachama wa CDM? na vipi mipango yake kisaisa kwa sasa.

3. Kwa ufahamu wa ZITO usalama wa taifa unaisaidia nchi kumaliza matatizo mbalimbali likiwemo la ufisadi? Je bado inastahili kuitwa usalama wa taifa?

4. Kuna haja ya kuanzisha chombo kingine cha usalama wa taifa kama vile marekani FBI na CIA kwaani kimeshindwa hata kuwakamata watz wenye vijisenti nje ya nchi?

5. Mheshimiwa zito kutaka kugombea urais si kwamba ana uchu wa madaraka na unatumiwa na CCM kuwagawa CDM? kwaani Mheshimiwa Dr Slaa aliwakirisha CDM vizuri ktk uchaguzi 2010. pia kura za maoni za wanajamii zinaonyesha kuwa Dr slaa anakubalika kuliko Zito.

6.Kwa nini Mh. Zito amepoa sana kuliko siku za nyuma?

7. Je ni kweli Mh Zito ni rafiki wa karibu wa Mh. Edward Lowasa na Rostm Aziz?

8. Baada ya maisha ya siasa anatarajia kufanya kazi gani kwaani kwa nafasi aliyonayo siyo rahisi kuajiliwa kama mtu wa kawaida?

9. Kwa nini Mh Zito hakutaka kuitangaza Chadema katika mkoa wa Kigoma zaidi ya jimbo lake? kwaani hajawahi kufanya ziara za kichama ktk wilayani kama afanyavyo nje ya mkoa wa Kigoma na ndiyo maana CDM haina wafuasi wengi km NCCR Mageuzi nje ya jimbo lake.

10. Anajua nini kuhusu Ugonjwa wa Dr H. Mwakembe.

11. Kwa nini mkoa wa Kigoma uko nyuma kimaendeleo japo anapigania maendeleo ya Tanzania?

12. Kwa kuwa mh Zito yuko karibu na serikali ya ujerumani ana mkakati gani kutumia nafasi hiyo kuleta maendeleo katika mkoa wa Kigoma.

13. Kwa kuwa mkoa wa kigoma umejaliwa kuwa na rasilimali na watu wachapa kazi ana mpango gani kuwaunganisha wasomi km Prof Yanda, Nkontagu, Mbwiliza, na wengine wengi kutengeneza dira ya maendeleo ya Mkoa ambayo wabunge watapaswa kuifuata.

14. Kwa kuwa kila hoja binafsi zitolewazo bungeni serikali huziteka nyara na kujipa majukumu kuzifanyia kazi na mwisho hakuna matokeo mazuri. Je Mh Zito haoni ni bora kutoa ushahidi kwenye vyombo vya habari ili watu wawatambue kwa majina kwa kuwa serikali itafanya sanaa tu. ukizingatia serikali inahusika.

15. Kwa nini Mh ZITO asipinge ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa kuwa haina tija, kwaani hakuna miundo mbinu kutoka Bagamoyo kwenda bara na nchi za jirani, badala yake fedha hiyo utumike kuimalisha reli ya kati na Tazara na kujenga bandari za nchi kavu Mbeya na Kigoma ili mizigo ikitoka bandarini iende moja kwa moja huko kupunguza msongamano wa mizigo bandarini.

16. Ni lini Tanzania itakombolewa kutoka mikononi mwa mafisadi?
 
Asante na hongera kwa harkati hizi. Mie nilishakata tamaa sku nyingi. I NEVER BELIEVE IN WHAT A LIVING POLITICIAN SAYS, PERIOD!!! Hata angekua ni baba yangu. I am politically active though and I do vote every time, utajiuliza how do I vote for someone i don't believe in. Ninaangalia MATENDO yake tu na bado i get them wrong sometimes.
Well, nitafuatilia kwa umakini mjadala na majibu yake kwa maswali atakayoulizwa. Kisha nitaweka NEGATION kwenye kila jibu,na nina uhakika kuwa kwa sehemu kubwa sana ntapata majibu sahihi (Baada ya negation) kuliko wengi tuu.

MASWALI YANGU KWA Zitto :
  1. Je unaamini kuwa CHADEMA ya SASA HIVI (kama tungefanya uchaguzi leo) ni chama kinachoweza kuaminiwa kupewa madaraka ya nchi yetu? Kama ndiyo,unawaambia nini wale wanaobeza hilo? Kama hapana unaamini nini kinapaswa kufanyika ili kifikie kiwango cha kuaminika na ni nini sehemu yako (Kama una ushahidi wa yale unayoyafanya sasa katika kufikia azma hiyo waweza kuutoa tafadhali) katika kufanikisha hilo?
  2. Watu wengi wanakuona kuwa ni mtu aliyejiweka pembeni kidogo na chama chake,ukiwekeza sana katika harakati binafsi zaidi ya zile za CDM na ambaye waziwazi mwenye ajenda binafsi (pengine ya urais). Unadhani hilo ni la afya kwa mustakabali wa maisha yako ya kisiasa na kwa ule wa CDM? na je unafanya nini kulirekebisha hili?
 
Last edited by a moderator:
Mh.Zitto
1. Uchaguzi wa 2010 ,ni kweli kura za Chadema ,urais, ubunge na udiwani hazikuchezewa mchezo mchafu? je kama ni kweli ziliibiwa tufanye nini 2015, na mambo ya umeya Arusha na Mwanza unaonaje au una mtazamo gani?
2. Upo tayari kugombea ubunge huku Kyerwa (kagera ) kupitia Chadema iwapo hutapata nafasi ya kugombea urais? NI majimbo mangapi unayalea kwa sasa ili yawe chini ya chadema 2015 hasa ubunge
 
Mie sina Cha maswali wala Cha majibu.. Niongee direct Na Zuberi my young brother and I know unaufiatilia Uzi huu Na unajiandaa kujibu maswali ya wananchi Kwa mlengo unaoujua.. AMA kweli au uongo potelea mbali mradi wadanganyika waridhike..

, kumbuka ulipoutwaa Ubunge the first time uliniambia ni fedha Za wauza karanga, mihogo, Dagaa Ndizo Zilizokupa power ya kupiga kampeni hadi Ushindi. Na Kwa maana hiyo ulipoingia bungeni kuna Jamii ambayo si ndogo mpaka Sasa inathanini Na kujua ukifanyacho mjengoji.. Bidii hizi si Za kubeza hata kidogo, matamshi yako ya Juzi si ya kizalendo hata kidogo, Kusema huna mpango Wa kugombea Ubunge Tena 2015 utagombea kuteuliwa kinyanganyiro Cha Urais Na ukaweka wazi kupitia CDM, ingawa umekwenda nje ya utaratibu lakini bado hujavunja sheria yoyote ndani ya KATIBA ya CDM, Na Mtu yeyote asiyejali anaweza Kufanya Kama ulivyofanya lakini mimi sikulaumu Kwa kuropoka hivyo lakini naumia Kwa wewe kwenda mbali zaidi Na Kusema kama CDM haitakuteua Basi utaunga Mkono Mwingine atayechagulia Na kukaa benchi lakini Ubunge No tena, ulichokifanya huwezi Kufanya zaidi ya Hapo.. Which means uwezo wako Wa kiuongozi umeishia hapo, ni sentensi Za Mtu aliye kata tamaa..

Ni kweli Hutaki kuwa Mbunge tena wala Kiongozi tena, Na Inshu kubwa ni Maradhi.. BWANA Mdogo maradhi tumeumbiwa binaadam, usikate tamaa mapema.. Mbona wagonjwa wengi tu lakini wanapeta wanasonga mbele maisha yanaendelea.. Unamuona Leigwanan, Mtu yuko hoi, hata kutembea anavibrate Mwanzo mwisho, bado haitoshi viharusi vinambamiza kila kukicha lakini mzee yupo tu, bado anapiga kelele ntagombea Urais kupitia magambazz, Na masauti yake of which najua hata akipewa hawezi kuzungukia mkoa hata mmoja lakini makelele yake magamba hawalali.. Kidume husifiwa Kazi Na bora yakukute huko mbele Kwa mbele kuliko kukaa bench.. Ukikaa benchi Kwa siasa zetu utasahaulika haraka Kama Moto wa makaratasi..

Wewe mwenyewe unajua 100% CDM hawawezi kukupitisha ugombee Urais, Unafanya fujo tu ili ustaafu uongozi Kama Mtu aliyediriki kufanya Jambo.. Hata Kama CDM wakipuliziwa sana Na ukapita sidhani kama watanzania watampatia uongozi Mtu bachelor asiyejua uongozi hata wa familia ukoje.. Uongozi siku zote huanzia nyumbani babaa.. Sikulaumu kwamba huwezi oa lakini Unafanya viroja sana brother..

Acha makelele, chapa Kazi, ukifika Muda wa kugombea huo URAIS Basi gombea ukishindwa Basi gombea Ubunge tuendelee kupiga Kazi.. Sio kwamba unayo mabaya tu, unayo mazuri mengi pia.. Bado Kigoma Ina mengi ya kufanyiwa.. Serukamba ni mpinzani si Adui, still meza moja mwaweza kaa Kwa maendeleo ya KGM..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom