EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
Nikiri kuwa mimi pia nina maswali ya kumuuliza na hata nikipata nafasi ya kukaa naye face to face tukizungumza tu yaliyo msingi na ndani ya maswali ambayo ninayo inaweza chukua sio chini ya masaa mawili ama zaidi. Naamini ningefanya jitihada zaidi hiyo nafasi ningepata...

Kwa muktadha huo Sijajihami Mkuu... Nimeona ni kheri nitoe tahadhari mapema sababu ni mpitaji mzuri tu hapa JLS, najua ni namna gani watu wanakuwa na sumu kali wakiona jina la Zitto ama lolote lihusulo yeye. Najua kuwa bila tahadhari basi tunaweza kuwa na pages za kejeli na tusipate yaliyo msingi. Nakuhakikishia kuwa maswali yote nitawakilisha na ndiyo maana nikaona nisiwe mchoyo wa hiyo nafasi nihusishe na members pia. Hivo Tukutuku kama una swali uliza na litafikishwa...

Karibu sana.
Poa sister nimekuelewa na naandaa maswali ya kumuuliza na kwa kuwa yeye anatka kuwa kiongozi wetu kwa siku zijazo asiogope kuulizwa maswali hata kama yatakuwa yanauzi lakini atakuwa amepata nafasi hadimu yakujua mawazo ya watu anaotaka kuwatawala!
 
Mkuu mimi nafanya kazi na mwajiri wangu anajua mshahara wangu kwa kuwa yeye ndiye aliyeniajiri na ndiye anayeniandalia huo mshahara.Sisi kama wananchi ni kweli kabisa ni waajiri wa rais,lakini kuna utofauti kidogo kwa sababu there is no direct involvement in the supervision of our employee (Rais).Hata hivyo naamini ukienda ofisi ya rais utumishi unaweza kupata hizi taarifa bila shaka.

Hivi raisi ni nani yeye hata mshahara wake uwe siri?,haya mambo ya kuendesha nchi kwa kufichaficha haya sio mazuri.Kwani raisi ni zaidi ya Mungu?
 
aisee tanzania tuko nyuma sana kimaendeleo na ki uhuru wa maoni..sasa unasema tusimuulize maswali personal hivi unajua ukiamua kuingia kwenye siasa na kugombania cheo kama cha urais basi hamna tena privacy? maisha yako ni public property? lazima tujue kama akiwa Rais je ameoa? ana watoto wa wangapi huwezi ukataka kuingia ikulu alafu unawaambia watu kua hutaki maswala ya kibinafsi yaongelewe well kama hutaki dont run for the presidency..its that simple
 
Hakuna "direct involvement in the supervision of our employee" kivipi? No wonder tupo kwenye hali tuliyonayo!!!!

Na haya mambo ya "naamini ukienda ofisi ya rais utumishi unaweza kupata hizi taarifa bila shaka" ndiyo siyataki mimi. Kwanza unasema "unaamini", halafu unasema "unaweza", halafu katika sentensi hiyo hiyo unasema "bila shaka"!!

Good grief...wewe unajua au hujui?

Mkuu mimi sijui lakini siwezi kulaumu kwa kuwa binafsi sijawahi kufanya jitihada za kutafuta hizi taarifa.Kwa kifupi bila kumumunya maneno mimi nakuhakikishia hizi taarifa zinapatika ofisi ya rais utumishi.
 
Mkuu AshaDii tunashukuru kwa fursa hii adhimu ingawa hujaeleza tunaruhusiwa kuuliza maswali mangapi/mara ngapi. Maswali yangu kwa sasa ni haya;

1. Zitto Zuberi Kabwe umekuwa katika Siasa za Ushindani kwa muda mrefu na sitakosea nikisema una mchango mkubwa katika kuifikisha CDM hapa ilipo sasa kupitia harakati na michango mbalimbali ya hali na mali. Una muono gani kuhusu upinzani nchini na nini nafasi ya upinzani hasa CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ukilinganisha na chama tawala CCM?


2. Umri wako utakuwa miaka 39 mwaka 2015 (kama sijakosea) na kwa mujibu wa Katiba ya sasa hauruhusiwi kugombea nafasi ya urais unless kama Katiba itabadilishwa na ku accomodate umri wako (Ingawa hakuna uhakika maana wenye kuamua hilo ni wananchi). Kwa nini pamoja na wewe kufahamu kuwa hauko eligible umekuwa kila mara ukiibuka na kutangaza kuutaka Urais mwaka 2015? Lengo ni nini hasa? Je tayari una uhakika wa umri huo kushushwa kutoka miaka 40 hadi 35?

Nashukuru tena kwa fursa hii
 
1.Wakati wa Kampeni ya 2010, kwa nini hakuoneka kwenye kampeni za urais za Chadema?, na badala yake alisikika kumsifia JK?.

2.Kwa nini hajaonekana kwenye mikutano ya M4C na badala yake alionekana Ethiopia along side JK?,

3. Kwa vile ameisha aga kuwa 2015 hagombei tena Ubunge bali atagombea urais kupitia Chadema!. Kama Dr. atachange mind na kuamua kugombea, its automatically ZZK atakatwa, jee amejipanga kufanya nini?, au atahama Chama na kugombea kupitia chama kingine chochote?.
 
Ashadii - "maisha binafsi" ndiyo "msingi" wa "maisha ya kiongozi mwadilifu"...! Binadamu awaye yote anapojaribu "kuficha masiha yake binafsi" fahamu fika kuwa huyo binadamu anayo mapungufu makubwa sana "ki-uongozi"...!

Mkuu unaonaje ukianza na wewe kutueleza maisha yako binafsi? Sidhani kama ni busara kwa kiongozi mwenye busara kama ZZK kuanika mambo yake binafsi mitandaono, sasa atakua na utofauti gani na kina Dimond na Wema?
Kwa kukumbusha tu, unakumbuka reaction ya Mwenyekiti wetu wa Chama wakati naibu katibu wa sasa wa mag.amb.a alipoongea mambo yake bungeni?!
 
Zitto kwa nini waislam walio wengi wanadai kuwa chadema ni ya wakristo? Na utafanyaje ili kufuta hii ideology waliyonayo waislam .
 
Nashukuru for the tag,mwaswali yapo lakini sidhani kama yatajibiwa.I'm pessimistic on this one.

Kuna uwezekano mkubwa nikawa msomaji tu.

I would have believed that line if I did not know of your capability on this... I should say I would genuinely be SO dissapointed if you do not present any of your questions. Nadhani in this unakosea... Ilitakiwa utoe maswali; then uangalie if what you think is what will eventually happen hivo kukupa jibu kuwa your pessimism was valid.

Naomba ushirikiano wenu...
 
Mkuu mimi sijui lakini siwezi kulaumu kwa kuwa binafsi sijawahi kufanya jitihada za kutafuta hizi taarifa.Kwa kifupi bila kumumunya maneno mimi nakuhakikishia hizi taarifa zinapatika ofisi ya rais utumishi.

You seem to be a bundle of contradictions!

Unasema wewe hujui halafu hapo hapo "bila kumumunya maneno" unanihakikishia kuwa hizo "taarifa zinapatikana ofisi ya rais utumishi".

Hivi huoni unavyojikanganya?
 
Labda niulize kuwa unapo sema binafsi una maana gani? Kuna maswali binafsi... 'unapenda kula nini', 'siku gani huwezi sahau katika maisha yako?' 'unapenda maisha ya namna gani?' na the like...

Nimetoa hiyo tahadhari sababu watu hawachelewi kuleta maswali kama 'umewahi lala na wanawake wangapi?', 'girlfriend wako ni nani?' 'unafanya mapenzi mara ngapi kwa mwezi?' 'umewahi lala na AshaDii?'

Hivi umenipata maana yangu?

Naamini kabisa kuwa maisha ya Zitto binafsi ni open book, wengi wanamfahamu kwa mbali ama kwa kutokea anako tokea. Sasa kwa mtindo na maswali hayo sioni kuwa tukipata majibu yake kama lina faida yoyote kwa jamii.. Labda kama nakosea; but hivo ndio naamini.

Hayo ni maswali ya Salma kwenye mikasi,hivyo sitegemei kutokea kwa ma GF.!
 
Mwanangu Ashadii umeniudhi leo kwa mara ya kwanza. Inaonekana kama huyo Zitto wako ana matatizo mengi kiasi cha kuogopa baadhi ya mambo yasiguswe.

If indeed he is but a public figure hiyo protectionism ya nini? Hii maana yake ni kwamba unataka aulizwe anachotaka kuulizwa. Kwa mfano, kama ataulizwa ataoa lini au kwanini haoi na umri unakwenda kama kiongozi wa umma kuna ubaya gani? Maana wengi wanashangaa ni vipi ataweza kuongoza taifa iwapo hana hata uwezo wa kuwa na foundational unit yaani familia.

Pili kulikuwa na tetesi kuwa naye ameficha mafweza Uswisi. Hii inaweza kulenga kumchafua ili awagwaye waliofanya hivyo, je huoni kuwa hii ni nafasi adimu ya kuondoa shaka? Pia kama yeye ni mwanasiasa mahiri kwanini akingiwe kifua kama kichanga.


Polee sana mkuu... Pole kwa kukuudhi.

Nimeamini kuwa nimekuudhi kiasi umeona useme 'Zitto wangu'. Umenifanya nisome upya post... But genuinely sioni kuwa I have covered him that much; ila tu ile jitihada zangu za kutaka kuhakikisha kupata comments za msingi. Tena wewe of all people unaelewa fika ni namna gani matusi, kejeli na kashfa juu yake hutolewa hata pasipo stahili.

Nadhani nilikosea kuliwasilisha.. Kwa kijana kama yeye akiwa katika age ambayo anastahili kuoa na hajaoa hata mimi personally inaweza kuwa moja ya swali langu juu yake. Hivo kwa kiasi fulani nakubaliana na hoja yako - ila pia nahitaji na wewe uelewe kuwa nilikuwa na maana gani na isiichukulie literally kama ilivyo. All in all the good thing ni kuwa hicho kipengele nimetoa hivo I believe no more obstacles..

Hio ya kuficha pesa Uswizi hivi inaweza ku qualify as binafsi? How can it be binafsi hali pesa zilizofichw uswizi ni za Watanzania?
 
Mkuu Zitto.
Mimi nimekua nikipendezwa sana na aina ya siasa yako, lakini nina maswali. Je unajisijiaje kutuhumiwa mara kwa mara na wanachama na hata viongozi wenzio wa CDM? Una mpango gani ili kumaliza mambo haya?
Pili, Kama usipopata nafasi ya kuwasilisha chama chako kwenye presidential post una mpango gani kwa mwaka 2015?
 
You seem to be a bundle of contradictions!

Unasema wewe hujui halafu hapo hapo "bila kumumunya maneno" unanihakikishia kuwa hizo "taarifa zinapatikana ofisi ya rais utumishi".

Hivi huoni unavyojikanganya?

Kujua taarifa zinapopatikana na kujua taarifa zenyewe ni vitu viwili tofauti.Sijui kwa nini unashindwa kunielewa.Sijui mshahara wa rais kwa sababu sikuwahi kilipa umuhimu jambo hili,kwa kazi ninayoifanya nafahamu hizi taarifa zilipo ndiyo maana nimekuhakikishia mkuu!
 
Opportunities never come twice: Naomba kuuliza tena kuhusu ushirika wa Zito na Mh. Kafulila. Inasemakana kuwa mna ajenda ya siri na moja ya allegetion ilikuwa kuwa mmeanzisha chama chenu kati ya vyama vilivyosajiliwa hivi karibuni na ndo umejianda kugombea Urais kupitia huko. Je hii ni kweli?
 
Kujua taarifa zinapopatikana na kujua taarifa zenyewe ni vitu viwili tofauti.Sijui kwa nini unashindwa kunielewa.Sijui mshahara wa rais kwa sababu sikuwahi kilipa umuhimu jambo hili,kwa kazi ninayoifanya nafahamu hizi taarifa zilipo ndiyo maana nimekuhakikishia mkuu!

Umejuaje kuwa huko utumishi ndipo zinapopatikana hizo taarifa?
 
Hii inanikumbusha Raisi msatafu Mkapa alivyo kuwa anatembelea shule yetu, Tuliambiwa tuandae mswali yaende kwa Head Master ayachuje, then Head Master Apeleke kwa Mkuu wa Wilaya Achuje, Mkuu wa Wilaya nae ayapeleke kwa wakubwa wake waya chuje,

Alitakiwa Aulizwe kila aina ya Swali na Ni vizuri kama yeye angekuwepo Online mwenyewe, kuulizwa kila aina ya Swali,
 
Maswali yangu kwa mh zzk.

1. Kazi ya utabiri alianza lini? kwani majina karibu yote aliyopendekeza kuwa wajumbe wa kukusanya maoni ya katiba mpya yalichaguluwa na rais.

2.Anatabiri vipi kuhusu umri wa mgombea urais kwenye katiba mpya. Je utapunguzwa ili kumaccomodate au la?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom