EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
Maswali yangu kwako Mh. Zitto:
1. Je, ni kweli CHADEMA ni chama chenye kuendekeza ukabila, ukanda na udini? Kama ni kweli:
(a) Tupe mifano hai katika maeneo hayo.
(b) Wewe kama kiongozi wa chama unafanya nini kuondoa hali hiyo ili kurudisha imani ya walio wengi.

2. Je, ni kweli unataka kugombea urais uchaguzi ujao? Kama ni kweli, kwanini unaanza kutangaza(kama tunayoyasoma ni ya kweli) mapema na nje ya utaratibu wa chama?

3. Ni kwanini hujataja majina ya viongozi walioficha fedha Uswiss kama ulivyoahidi?

4. Unasemaje kuhusu tuhuma kwamba na wewe Zitto ni mmoja wa walioficha fedha Uswiss?

Ngoja nimezee maswali mengine mkuu AshaDii asije akanikodolea macho bure! Kwa kukiuka masharti.
 
Last edited by a moderator:
SWALI LANGU: Je utakuwa tayari kufuatata nyayo za Dr Slaa na kutaja kwenye majukwaa ya siasa majina unayodai kuwa nayo ya wandugu walioficha mabilioni huko Uswiss?
 
Mimi nina maswali kadhaa ambayo ningependa Mheshimiwa Zitto ayajibu kwa ufasaha.

[1] Mheshimiwa Zitto umekuwa mpiga debe mzuri wa kupendekeza umri wa kugombea urais ushushwe hadi miaka 35.Je mapendekezo haya ni kwaajili ya vijana wote Tanzania au umesukubwa na nia ya kutaka wewe binafsi kugombea urais kwakuwa mwaka 2015 bado utakuwa haujafikisha umri wa miaka 40.

[2] Mheshimiwa Zitto kampeni za mwaka 2010 ulisikika ukimsifia Rais Kikwete na kumtosa mgombea wa chama chako Dr W Slaa.Baada ya uchaguzi chama chako kilichukua uamuzi wa kususia hotuba ya rais ya ufunguzi wa bunge wewe ukakaidi na kuamua kutoingia bungeni na mwisho ulizungumza na wanahabari kupinga uamuzi wa chama chako kwania ya kuonysha mapenzi yako binafsi kwa rais Kikwete.Baada ya uchaguzi umekuwa ukiandamana na rais mara kwa mara katika ziara zake za nje South Sudan na Ethiopia.Swali kutokana mlolongo wa matukio yote bado unadhani unastahili kugombea urais kupitia CDM ?.

[3] Mheshimiwa Zitto uchaguzi wa mwaka 2010 gazeti la Mwanahalisi lilichapisha mawasiliano ya simu baina yako na naibu mkuu wa usalama wa taifa Jack Zoka.mpaka leo sijasikia ukikanusha,kwakuwa hakuana kanusho toka kwako unaweza kutueleza mazungumzo yenu yalihusu nini ?.

[4] Mheshimiwa Zitto msimamo wako na kauli zako kuhusu muungano wa EA umekuwa mara zote kutoangalia maslahi ya waTanzania.Mfano wewe unaunga mkono free movement of labour,unaunga mkono access ya ardhi kwa wananchi wa wote wa EA wakati unajua wazi wenzetu hawana ardhi ya kuwagawaiya watanzania.Naomba unieleze nini faida za msimamo wako.

[5] Ni kwanini uonekani kwenye mikutano ya M4C ?.

[6] Mheshimiwa Zitto Viongozi/CDM imekuwa mstari wa mbele kufichua ufisadi.Ninazo taarifa za uhakika kuna mwanachama wenu katafuna fedha za M4C ni kwanini mko kimya ?.
 
ZITTO,ZITTO,ZITO........NANI KAMA ZITTO(Wangapi wanaweza kukubali kujitokeza hapa kuhojiwa maswali ya aina yoyote kama zitto)
Thanx ASHDIII kwa jitihada zako,Lakini pia Zitto wewe ni kiongozi wa mfano na kuigwa kwa hili.
SWALI LANGU LA MSINGI KWAKO RAIS WANGU WA KU-MOYO
>KWENYE SAFARI YAKO YA KUGOMBEA URAIS MWAKA 2015 KAMA UTAPITISHWA NA CHAMA NI MGOMBEA GANI WA CCM AKISIMAMISHWA UNADHANI ANAWEZA KIDOGO AKAWA MSUMBUFU.
otherwise,najivunia kuwa upande wako siku zote za Maisha yangu.
Mungu akupe afya njema,hata hili la kuhojiwa hapa ni ushindi wa heshima​

Duh Mkuu TUNTEMEKE unataka Mh. Zitto awaingize CCM chakani?
 
Last edited by a moderator:
Shukrani sana kwa taarifa,

Maswali yangu kwa mhe Zitto.

1. Hivi dhana ya Bunge kuisimamia na kuishauri Serikali inatekelezeka kwa vitendo? sisi kama wananchi wa kawaida tunaona nguvu hiyo hakuna,Nini kifanyike kurekebisha hali hii kwani serikali ikthibitiwa vizuri na wabunge basi itakuwa makini.

2.Tatizo la Rushwa nchini linaongezeka kwa kasi sana,je taasisi hisika zimeshindwa kazi? nini kifanyike kutoa aibu hii kwa taifa letu?

3.Je mfumo wa kuwapata viongozi katika vyama vyetu uko sahihi? kwa sisi wananchi wa kawaida tumekuwa tukiona viashiria vyenye sura ya uwezo wa fedha na udini katika michakato wa kuwapata viongozi,nini kifanyike kuondoa hali hii ili taifa letu liendelee kuwa na umoja ulioimara?

4.Kutokana na upotevu wa rasilimali mbalimbali za taifa unaofanywa na baadhi ya watendaji,je wanaohusika kuthibiti tatizo hili wameshindwa kazi yao? kwa kuwa wabunge pia wanasehemu ya kuisimamia serikali ili kuthibiti tatizo hili na wabunge wetu pia wameshindwa kuisimamia serikali ili kukomesha tatizo hili? kama vyombo vyote hivi vimeshindwa sisi wananchi tuchukue hatua gani ili kuondoa tatizo hili?
 
1. Anashiriki shughuli za chama na kushiriki katika mikutano kama naibu katibu mkuu?
2. Inasemekana anamiliki HAMMER je? ni kweli na kama sio kweli ana magari mangapi na ni ya aina gani?
3. je kama katiba ijayo aitapunguza umri wa kugombea urais kutoka 45 hadi 35, atagombea ubunge tena kama anavyodai kuwa hatagombea ubunge tena bali atagombea urais?
 
Maswali
1. Naomba utaje mali unazo milki
2. Ni kweli unamiliki HAMMER
3. kweli unataka kugombea urais
 
Zitto,
Unasemaje juu ya ugawaji wa VITI MAALUM kwa ndugu na maswahiba wa VIONGOZI wa chama chenu mfano:
-Zitto na Muhonga Ruhwanya;
-Dr Slaa na Rose Kamili;
-Tundu Lissu na Christina Lissu;
-Ndesamburo na Lucy Owenya;
Haya mambo tulizoea kuyaona kule CCM nanyi mmeyaiga?
Pili, Sababu inayokufanya usimwachie Dr Slaa awe mgombea wenu wa URAIS kwa mara ya pili ni nini?
Tatu, URAIS mzuri ni ule unaoombwa na watu kuliko wewe mwenyewe kuutaka kama vile unachagua mchumba. Hili unalionaje?
 
Mimi nina maswali kadhaa ambayo ningependa Mheshimiwa Zitto ayajibu kwa ufasaha.

[1] Mheshimiwa Zitto umekuwa mpiga debe mzuri wa kupendekeza umri wa kugombea urais ushushwe hadi miaka 35.Je mapendekezo haya ni kwaajili ya vijana wote Tanzania au umesukubwa na nia ya kutaka wewe binafsi kugombea urais kwakuwa mwaka 2015 bado utakuwa haujafikisha umri wa miaka 40.

[2] Mheshimiwa Zitto kampeni za mwaka 2010 ulisikika ukimsifia Rais Kikwete na kumtosa mgombea wa chama chako Dr W Slaa.Baada ya uchaguzi chama chako kilichukua uamuzi wa kususia hotuba ya rais ya ufunguzi wa bunge wewe ukakaidi na kuamua kutoingia bungeni na mwisho ulizungumza na wanahabari kupinga uamuzi wa chama chako kwania ya kuonysha mapenzi yako binafsi kwa rais Kikwete.Baada ya uchaguzi umekuwa ukiandamana na rais mara kwa mara katika ziara zake za nje South Sudan na Ethiopia.Swali kutokana mlolongo wa matukio yote bado unadhani unastahili kugombea urais kupitia CDM ?.

[3] Mheshimiwa Zitto uchaguzi wa mwaka 2010 gazeti la Mwanahalisi lilichapisha mawasiliano ya simu baina yako na naibu mkuu wa usalama wa taifa Jack Zoka.mpaka leo sijasikia ukikanusha,kwakuwa hakuana kanusho toka kwako unaweza kutueleza mazungumzo yenu yalihusu nini ?.

[4] Mheshimiwa Zitto msimamo wako na kauli zako kuhusu muungano wa EA umekuwa mara zote kutoangalia maslahi ya waTanzania.Mfano wewe unaunga mkono free movement of labour,unaunga mkono access ya ardhi kwa wananchi wa wote wa EA wakati unajua wazi wenzetu hawana ardhi ya kuwagawaiya watanzania.Naomba unieleze nini faida za msimamo wako.

[5] Ni kwanini uonekani kwenye mikutano ya M4C ?.

[6] Mheshimiwa Zitto Viongozi/CDM imekuwa mstari wa mbele kufichua ufisadi.Ninazo taarifa za uhakika kuna mwanachama wenu katafuna fedha za M4C ni kwanini mko kimya ?.
Anaweza kujibu swali namba 6. Hayo mengine ni mwiba kwake.
 
Asante mkuu. Narudi palepale kwa baadhi ya wenzangu..kwann asiweke majina ya walioficha mabilioni uswiz hadharani?
 
Maswali
1. Naomba utaje mali unazo milki
2. Ni kweli unamiliki HAMMER
3. kweli unataka kugombea urais

Hapo kwenye Red, Mkuu Hammer mbona ni gari la kawaida kabisa? hebu google bei ya HUMMER na TOYOTA V8 uone kwamba V8 iko mbali sana kwa bei kuliko hummer, Ungesema ana Miliki V8 ningekuelewa
 
Mh ZITTO
inasemekana kuwa uswis wametoa masharti magumu ili waweze kuwataja walio ficha fedha za tanzania nje uswis,je unayaelewa masharti hayo? na kama itashindakana kukidhi masharti hayo nini kifanyike ili kuweza kunusuru pesa zetu?

nakutakia kazi njema
 
Inasemekana kuna siku steven wassira alikuja nyumbani kwako usiku. Naomba ututhibitishie kama ni kweli au uongo. Kama ni kweli, alikuja kufanya nini?
 
thanks mke mwenza kwa jitihada zako mimi ninayomaswali yangu kwa mheshimiwa Zitto nayo ni........
a) anaonaje kazi za kisayansi za watanzania? yeye kama mchumi angeshauri nini kuhusu kazi hizi za kisayansi kwa maendeleo ya nchi yetu kwani kwa muda mrefu sana kazi hizi zimekuwa hazina tija inayotakiwa kwa taifa kwani nyingi zimebaki kama minds alive in shelves. ilihali watafiti hawa wakiwa ni watu wanaotegemea ajira na pesa za wadhamini wa tafiti zao badala ya kuwa kama nguzo za kuwafanya wawe chachu ya uwekezaji kwa taifa hili??
b) je kama mchumi na mwanasiasa anaongeleaje juu ya R&D especially kwa viwanda na wasomi wa taifa hili? ukilinganisha na fursa iliyonazo TIRDO na TEMCO na mashirika mengne yalyoko chini ya wizara ya viwanda na biashara, ambayo hatuyaoni kabisa katika kusapoti tafiti hasa za vijana wasomi wa vyuo vikuu??
c) je anafikiri itumike njia gani ili kuwez kushawishi wawekezaji wa viwandani na mashambani kutumia kazi za watafiti walioko nchini?
d) je kuna sera yeyote tanzania inayompa kijana wa kitanzania nafasi ya kuwa mbunifu?? kama ipo sera hiyo inamshawishi kwa kiasi gani kijana huyo?? je kama mbunge atasaidia vipi kuhakikisha kwamba vijana wanasayansi wa kitanzania wanahamasishwa kutumia muda kufanya applied research zaid kuliko basic research?? je haoni kama wakati muafaka wa kushinikiza viwanda kugharamia tafiti za wanasayansi ili kukwepa importation ya technology??

mke mwenza ninayomengi sana ila kwa hayo naomba niwasilishe.
 
sasa mke mwenza kuna maswali ambayo ni follow up huzaliwa utokana na majibu je haya yatajibiwa ama kuwasilishwa vipi?? nashauri ingekuwepo side thread ya kuchukua comments na maswali mengine halafu moderator aipitie na kumpelekea kwenye jukwaa husika ili ayajibu. mfano kama mm ninayo mengi sana ya kumuuliza hasa kama mchumi na mwanasiasa ambaye anaonekana kupenda kuwatetea vijana.
 
MH.Ngongo nimefurahia sana maswali yako,na nafikiri kama nikuhit the bull amelenga,kwani hayo ndiyo maswali watu wanaitaji sio habari ya Mishahara! Pengine Zto anaihitaji kukujibu maswali hayo kwa kifasaha zaidi
 
Labda niulize kuwa unapo sema binafsi una maana gani? Kuna maswali binafsi... 'unapenda kula nini', 'siku gani huwezi sahau katika maisha yako?' 'unapenda maisha ya namna gani?' na the like...

Nimetoa hiyo tahadhari sababu watu hawachelewi kuleta maswali kama 'umewahi lala na wanawake wangapi?', 'girlfriend wako ni nani?' 'unafanya mapenzi mara ngapi kwa mwezi?' 'umewahi lala na AshaDii?'

Hivi umenipata maana yangu?

Naamini kabisa kuwa maisha ya Zitto binafsi ni open book, wengi wanamfahamu kwa mbali ama kwa kutokea anako tokea. Sasa kwa mtindo na maswali hayo sioni kuwa tukipata majibu yake kama lina faida yoyote kwa jamii.. Labda kama nakosea; but hivo ndio naamini.

Hapo naanza kuona dalili ya uliyoyahofu,kwa mtazamo wangu watu wana wigo mpana wa kmuuliza Mkuu Zitto lakini ona wanaovyoanza kuleta hoja za kwamba Mr Kabwe anajengewa ulinzi ,mi siamini kama Zitto atshindwa kujibu masuali yeyote yatakayo ulizwa kiungwana na yenye mantiki hata kama yatakuwa abit privacy poking,tuombe members wabadilike kimtazamo waache kujilabu na kujinasibu kwa kejeli,inda na hila kwani kukera si uhodari bali ni kujifaharisha kijuha!
 
Maswali kwa Zitto

1. Kwanini hatumuoni kwenye M4C wakati viongozi wote wa chama wanakuwa kwenye hizi harakati Tanzania nzima na wanapangiwa majukumu na kanda za kuhamasisha UMMA.

2. Zitto ametangaza kugombea uraisi 2015 na je chama chake kisipompitisha atachukua hatua gani? je atahamia chama kingine au ataendelea kuwa mwanachama mwaaminifu na kukisaidia chama. Tunataka kujua mapema ili 2015 tuwe na jibu kuwa ukombozi utapatikana bila hata yeye kuwa raisi asijijitaidi kuzuia mabadiliko baada ya kutoteuliwa.

3. Kwenye harakati zake kuna tuhuma kuwa Habibu mchange ni mfuasi wake na amekuwa akimtetea kwa gharama ya kuwachafua viongozi wa chama hususani katibu mkuu, m/kiti taifa na mwasisi wa chama yeye anatoa kauli gani kwa anachofanya Habibu mchange na wengine wengi.

4. Kwanini mara zote Zitto amekuwa anaonekana kuwa mwaminifu sana kwa raisi Kikwete hata wakati mwingine kwenda kinyume na maamuzi ya chama mfano baada ya uchaguzi mkuu 2010. Pia kwenye kauli zake nyingi nimemfuatilia amekuwa anakwepa sana kumtuhumu au kumsema Kikwete vibaya kuna nini nyuma ya Pazia. Maana hata hoja binafsi aliyoitoa bungeni juzi kuhusu fedha zilizofichwa Uswisi huwezi epuka udhaifu wa Kiongozi mkuu wa nchi kutofuatilia rasilimali zilizoibiwa nchini mwake na kukaa kimya tu na Zitto hamkumuhusisha kabisa.

5. Zitto binafsi ana mkakati gani wa kuhakikisha anaizoofisha ccm na kuhakikishia CHADEMA Ushindi 2015.

6. Suala la ndoa ni binafsi lakini la msingi sana kwa kiongozi wa umma na hususani wa chama makini kama CHADEMA, je ana mpango gani kuhusu ndoa?

Kwa sasa wacha niishie hapa ASHADII yapeleke haya yote kwake usimuonee huruma maana yeye ni kiongozi wa watu na itasaidia kuelewa huyu ni kiongozi wa namna gania asije kuwa kama Lowasa juzi BBC anaulizwa maswali anakwepa tu na kudai muda ukifika ndo atatoa maoni na si msimamo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom