I am glad this is cleared…
I am curious… Unaposema kuwa hatasema ukweli una maana umesha ji' tune kuwa lolote atakalo ongea likiwa nje ya lile unalo AMINI tayari juu ya hilo itakuwa sio sawa? Hilo la Uswiz nashauri panga maswali yakiwa directed to him then uone kama hatajibu…
I believe I am prepared. Inawezekana sio kwa ubora kama mtu ambaye tayari mzuri katika anga ya Siasa BUT prepared enough. Hayo mahojiano hayatakuwa maswali na majibu baasi! Kama swali lina utata, ataulizwa swali juu ya hilo swali ili atoe utata huo. Hii ni moja ya sababu kubwa ambayo mimi nilitaka ushirikiano wa members… Kama kawaida kutakuwa na side thread ya members kutoa comments kuhusiana na interview itakayo kuwa inaendelea.
Jmushi1 umezugumza kwa kirefu aina ya maswali… Hivi sijaelewa maybe; ina maana bado kuna maswali unayo na unaona hayataulizwa sababu hayapo valid or hayajibiki? So far naona kuwa that is clear.
In Blue; Jibu ni ndiyo. Ila take note kuwa atanipa time frame yake ya mda gani anaweza kuwepo, maswali mfuatilio ni muhimu ila yataangaliwa kama ni ya msingi na siyo yote hasa penye hoja ambayo atakuwa amejibu na imepwaya.
In Green; labda kama sijaelewa... So far hakuna limitation ya maswali, unaposema dondoo una maana ipi? Kuhusu maswali personal kama mwenyewe ulivyo kiri kuwa nimetolea ufafanuzi. Hajanipa limitation ya the kind of questions za kumuuliza.
The above para naona sasa kuna maswali ya kuwasilisha hapo... Will do so mkuu.
Ninaposema dondoo,nikwasababu unasema maswali yatakayojibiwa ni yale ya msingi.Sasa kila anayeuliza swali huwa anaona kwamba achouliza ni cha msingi(unless stated otherwise by the moderator).
Na ili kuondoa huo utata,ndiyo maana nikasema kuwepo na dondoo,ama kwa maana nyingine,u clarify kwamba atajibu maswali ya aina gani,ili kama yakijibiwa tofauti na vigezo vilivyowekwa,then tunaweza ku conclude kwamba maswali hayo si ya msingi.
Mfano labda mseme ahojiwe kuhusiana na issue za ufisadi,katiba mpya,misimamo ya chama chake,issue za kiuchumi,na pengine pia social issues(just mifano).Kwasababu utapima vipi kwamba swali siyo la kimsingi bila kuiweka hiyo misingi?
Kwa mfano swali kama anaamini chama chake ni cha kidini,linaweza lisionekane kama swali la msingi,lakini kwa wengi ni la msingi kabisa kwasababu alishasema nia yake ya kugombea urais ni ili aondoe hiyo migawanyiko na kwamba yeye ndiye mgombea pekee mwenye kuweza kufanya hivyo,and so therefore ndiyo maana nikauliza uwezekano wa follow up questions kwasababu sasa nitamwuliza atafanyaje kuuondoa huo udini?Je anadhani kama chama chake kimepewa sura ya kidini(kama haamini kuwa ni cha kidini),je nini kifanyike ili kuondokana na hilo?Maana kiukweli hata ccm hutumia hilo popote pale anapopingwa na wanachadema wenzake.Pia hata kushauriwa kwake asigombee uenyekiti last time.
Kama ulivyouliza kwamba nimesema maswali mengine yatakwepwa ama kutojibika,ni mfano wa swali la ni kwanini hakuwataja majina wenye akaunti za uswisi.Hilo nitasubiri jibu kwa hamu kubwa...
Na pia swali kama lile ambalo tumeshauliza mara nyingi,kwamba ni kwanini alimuunga mkono JK kwenye ugombea urais badala ya mgombea wa chadema given that vyama hivyo vinatofautiana sana na pia imani kwamba ccm ni mafisadi na ufisadi ndiyo umetufikisha hapa tulipo?Je alitofautiana kiasi kikubwa hivyo na mgombea wa chama chake hadi kuhamishia sapoti kwa ccm?Sanasana nisikufiche,atakachojibu ni kwamba "Siasa si uadui",sasa hapo kwangu hilo si jibu.Hilo tayari ni sawa na kutosema ukweli.
Wengine wameuliza kuhusiana na kutokuwepo kwake kwenye hizo movement za chadema,kiukweli,kuna watu wameshamjibia,especially wanaomunga mkono ndani na nje ya chama ikiwemo waandishi wa habari.Wao wamekuja na tahmini zao,na watu wanaamini hivyo ndivyo anavyofikiri yeye kwasababu hajawahi kuzungumzia wala kukubali kujibu maswali ya aina hiyo.Na ndiyo maana unakuta waandishi wamebakia kujibizana,wengine wa upande wake na wengine wenye kuona tofauti.
Kiukweli sina mashaka na uwezo wako wa kupick up maswali ama hata uwezo wako wa kujitayarisha.Nina imani kwamba mjadala utakuwa vyema kama ni kweli atajibu maswali yote.Kwasababu uliposema kuhusu maswali ya msingi,nimejiuliza kama unawasiliana naye kumwonyesha maswali uliyoya pick na kuona kama atakubaliana nayo,ama ni kwamba hajui maswali utakayoyachaguwa?Maana hapo kuna utofauti.Siyo kila mwasiasa ni mvumilivu wa kuulizwa maswali asiyoyataka,maana swali lisilo la msingi kwake anayeulizwa linaweza kuwa la msingi kabisa kwa mwulizaji na hata msomaji.