EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
1-muulize Zito! Ametangaza kugombea nafasi ya u-uraisi, je ni kwa kupitia chama gani? Au ni kwa kupitia mgombea binafsi!. Sababu uchaguzi uliopita wa 2010 Dr. Slaa ameweza kuipeperusha vizuri bendera ya chama chake cha Chadema. Na kwa muonekano bado anayo nafasi ya kuipeperusha bendera ya Chadema vizuri kwa mwaka 2015!

2-je tetesi zilizopo anataka pia kugombea na nafasi ya kuwa m/kiti wa chama. Ni za kweli?

3-Zito nafasi zote unazitaka! Je huo si uroho wa madaraka?
 
I would have believed that line if I did not know of your capability on this... I should say I would genuinely be SO dissapointed if you do not present any of your questions. Nadhani in this unakosea... Ilitakiwa utoe maswali; then uangalie if what you think is what will eventually happen hivo kukupa jibu kuwa your pessimism was valid.

Naomba ushirikiano wenu...
Ok mkuu,ushirikiano utaupata tu wala usijali.Ila kwasababu umeshakuja na disclaimer,wengi wana wasiwasi kuhusiana na hayo maswali ya binafsi.Kwakuwa umeshatoa ufafanuzi wa hayo maswali binafsi ambayo hayatakiwi,basi nimekuelewa.Nilidhani kwamba maswali binafsi ni kamavile kuhusu kutajwa kwake kwenye umiliki wa akaunti uswisi(alishapinga hilo na sitegemei jipya),pamoja na umiliki wa magari ya kifahari(nayo alishapinga licha ya wengi kudai kwamba ni kweli),however huko nyuma,alishakubaliana na hilo,na akasema kuwa aliamuwa kuyauza kwasababu ni ya kifahari na kwamba ni gharama sana kuyahudumia.

Kwanza kabla hatujaenda mbele,ebu tuanze na misingi ama nguzo za maswali tunayotakiwa kuyauliza,hapo chini umesema hivi...
Kwa mukatadha huu - hii inakuwa kama 'golden chanc'e kuweza kuitumia kwa wale wote wenye kiu ya kuuliza maswali kwa kutaka kujua juu ya yale ambayo Zitto anajua/fikiria/panga.
Niliposema sitegemei majibu kwenye maswali muhimu ama magumu,ni kwasababu ya msingi/nguzo ulizoziweka kuhusiana na uulizaji ama aina ya maswali hayo.Kwa mfano wengi wetu tunaamini kwamba hatasema ukweli(ndiyo maana ya kuwa pessimistc),kwasababu wengi tunajuwa(upon looking on what he says and believes) yale anayoyajuwa,kwa mfano tunajuwa kwamba anajuwa kuna watu wenye akaunti huko Uswisi,lakini tunajuwa kwamba hataki kuwataja(kama alivyoahidi)

Tunajuwa anayoyajuwa na ndiyo maana sasa ni kama tunafahamu anavyofikiri,pengine anafikiri kuisema hoja hiyo bila kuwataja hao wenye akaunti kutamsadia yeye?Maana sioni hilo lina msaada gani kwa mtanzania yeyote yule.Kwahiyo sijui kama ukimuuliza ni kwanini hawataji kama takuwa na jibu la uhakika.

Je kuhusu anayopanga?Again,wanasiasa ni watu ambao wanajuwa sana kukwepa,na ndiyo maana mambo yasiyo ya wazi ama ya kijanja janja yanahusishwa na siasa.Yani kwenye mawazo yetu,siasa ni jambo linalochukuliwa vyema.Hilo ni kutokana na tabia ya kukwepa kwepa ama hata kuficha ficha ya wanasiasa walio wengi.Ndiyo maana mara nyingi maswali yanakuwepo kwa wanasiasa,lakini wanapolizwa,wakiyajibu inakuwa kama vile majibu yao yameongeza utata zaidi na maswali zaidi.

Hilo linanifanya niamini kwamba maswali hata nikiuliza leo,siyo kwamba ndiyo ukweli wenyewe.Given that wanasiasa pia wana ukigeugeu mara nyingi tu.Kwa mfano Zitto mwenyewe keshazungumza mara nyingi sana kuhusiana na future politics.Lakini majibu yake yamekuwa yakibadilika mara kwa mara.Na hivyo utakuta kuna wananchi wanaodhani wanajuwa mipango yake,ama hata kuwepo na wananchi wenye kumfahamu kwa namna za tofauti kutegemeana na uelewa wa wananchi hao.
Naomba nitadhaharishe kuwa maswali yawe ya msingi, ya kujenga na vilevile kuweza kupata majibu ambayo ni muhimu kwa jamii yetu.
Ni ukweli kuwa tunaweza kutegemea kwamba tutapata majibu ya kujenga,however hilo linategemeana sana na aina ya maswali.Kwasababu mara nyingi wanasiasa wako busy zaidi kujinjenga wao binafsi.Ni muhimu sana tukafahamu tofauti kati ya kujenga vs kujijenga.Yote siyo mbaya.Lakini nina amini kuwa maswali ya kujenga ndiyo yatamjenga mwanasiasa.Whereas majibu ya kujijenga mara nyingi yanaleta migawanyiko zaidi pamoja na ukweli kwamba yanafanya situation kuwa too polarising.

Kwa mfano watu wanaweza kuja na maswali kuhusiana na ugombeaji urais,halafu maybe akaulizwa swali kuwa ni kwanini hashgulikii issue ya kuhusiana na kipengele cha umri kwenye katiba.Sijawahi kuona akijishughulisha kujibu hayo.Badala yake kumekuwa na washabiki wengi wakidai kuwa ni mkwaruzano wake na chama chake kwasababu chama chake ni cha kidini.(polarising).Kwahiyo tunapokuwa hatupati majibu kamili kuhusiana na msimamo wake kuhusu mtizamo wa mashabiki wake kuwa chama chake ni cha kidini,utakuja kuona kwamba uanasiasa ni kitu kibaya na ndiyo maana wengine tunakuwa pessimistic kama nilivyosema hapo awali.

Kwamfano pia,wale wanaomtetea kuhusiana na hatua yake ya kutokuyataja majina ya walio na fedha uswisi,wanasema kuwa ni jitihada zake binafsi za kuyapata majina yale na hivyo asisumbuliwe kuyataja bali ashukuriwe kwa jitihada hizo.Na pia hata yeye mwenyewe alishasema hivyo,kwamba ni jitihada zake na kuwa majina hayo yalikuwa yakiuzwa ghali kwenye cd's,sasa hapo inamanisha kuwa anataka manufaa binafsi?Je ni yapi?Anaziuza na yeye hizo cd zenye majina?Je kuna mtu ambaye hatopenda kuzinunuwa kama yumo kwenye list?

Je kuiepeleka kwake hoja ile kule bungeni kuna utofauti wowote ule vs kuyataja majina hayo?Binafsi ninaamini kuna utofauti mkubwa sana,na pia ninaamini kuwa kuipeleka hoja hiyo bungeni kuna nia ya kutaka kujisafisha kwake kwamba hayuko kwenye listi ile,maana wananchi watasema kuwa kama angekuwepo kwenye listi ile,basi asingepeleka hoja hiyo.Lakini wananchi hao hao hawajui kuwa kuna utofauti mkubwa sana na kwamba kutaja vyeo si sawa na kuyataja majina(vyeo haviwezi kushitakiwa wala kuhojiwa,bali majina).Hoja hiyo itakufa kama ambavyo nyinginezo zilishawahi kujifia.Na mwanasiasa atakuwa amekamilisha nia yake(kupumbaza wananchi kwa kutumia siasa).
Wanachama wengi hupenda kuongea kwa niaba yake kana kwamba wamjua (it may be true or not); na kuwasilisha hoja zao kana kwamba ni za mwisho (final say).
Hapo juu kwa mfano,hayo huwa yanatokea kwasababu ya utata wa wanasiasa.Watu kupendelea kuongea kwa niaba yake kana kwamba wanamjua,ni kwasbabu tu ya kukwepa kujibu maswali na kudharau.Hilo linapelekea watu kuongea kutokana na vile wanavyoona kuwa ni matokeo ya misimamo yake na hata maamuzi yake.Mara nyingi tu huwa anachaguwa kukaa kimya pale ambapo wengi tulidhani angesema jambo.Hilo linapelekea hisia za tofauti.Kuna maswali mengi tu keshaulizwa humu,si kwa utaratibu kama huu wa kwako,lakini kwenye threads mbali mbali ambazo either alianzisha yeye mwenyewe,ama member mwingine alianzisha.Ninakubaliana na wewe kuwa maswali yenye kejeli na matusi hayana nafasi,lakini si yote aliyowahi kuulizwa yana matusi na kejeli.Pengine cha muhimu ni member kujitahidi wajuwe namna ya kuuliza maswali.Kuna maswali ya muhimu sana lakini ni namna ya uulizaji ndiyo inakuwa shida kwa wengi wetu.
naomba tutumie hii fursa kuweza jua what Zitto is all about, what he thinks on certain issues, what he stands for, what he believes in AND why he thinks/ believes/stands for what ever it is that he postulates especially on what defines him... i.e POLITICS.
Hapo juu,ushauri wangu,ni kwamba hicho kipengele ungemtumia ili aandike makala ama essay inayoonyesha ama kusummerize hayo uliyoyasema hapo juu.Hilo litasaidia kwasababu tutakuwa tumeanzia kwenye higher standard given the fact that kunauwezekano mkubwa kukawepo na follow up questions.Na kwasababu style ya maswali na majibu inategemeana na wewe kuyachaguwa maswali,hilo halitaweza kutu guarantee kwamba follow up question zinaweza kuchukuliwa.(Najuwa kwenye "disclaimer",umeshasema kuna wasioridhika).Hivyo sidhani kama follow up questions zina maana ya kutokuridhika peke yake,ama haina maana kwamba kutoridhika basi ni jambo baya.Kwasababu ninakuhakikishia kuwa hatajibu maswali yote,na kuna ambayo atajibu kisiasa zaidi.Hilo ni kutokana na ukweli kwamba wanasiasa wanategemea kusikilizwa na wafuasi wao peke yake.Mara nying hawapendezwi na critics.Hilo huwa linachangiwa na ulevi wa madaraka ambao huwapa kiburi na kutokujali na madharau.

Pengine kwa kumalizia nikuulize,je follow up questions zitakubaliwa?Na je kuna idadi ya maswali ambayo mmepanga kuwa yatachukuliwa/kujibiwa?

Pia je kuna umuhimu wa kuweka dondoo za maswali ambayo atayajibu?Kwa mfano umetolea mifano ya maswali ambayo ni "personal",je umehsamwuliza limitation ya hayo maswali kuwa yepi haswa ni personal na yepi siyo?

Vinginevyo,nadhani angetuwekea misimamo yake kuhusiana na issues zinazoligusa taifa letu kwasasa ie udini,ufisadi,katiba mpya na mengineyo.Je anafikiri ni kweli kuwa chama chake ni cha kidini?Na kama ni kweli,tatizo hilo lishghulikiwe vipi?Je kama anafikiria kugombea urais,atalimalizaje tatizo hilo la udini?Mipango yake je?Ana mpango wa kuyataja majina ya wenye akaunti uswisi?Kama hapana,ni kwanini?Je akifanikiwa kuupata urais endapo atagombea,ana mpango wa kuwashughulikia mafisadi mara baada ya kuwaondoa madarakani?Je hilo litawezekana vipi ukitilia maanani ushirikiano wake na serikali ya ccm na wale wenye kutuhumiwa kuhusiana na ufisadi?

Pia aliposema mikataba iwekwe wazi,alikuwa na maana gani?Je ana maana kwamba ikiwekwa wazi hata sisi wananchi wa kawaida tutaweza kuiona?Ama alimaanisha ni wabunge peke yake?Kama ni wabunge peke yake,hilo litaleta utofauti gani kwenye bunge ambalo wabunge wake wanapiga kura za maamuzi kutokana na chama na si maslahi ya taifa?
Niishie hapa kwasasa.
 
Nafikiri (Sina uhakika haya ni mawazo yangu tu) wanaamini kila mwananchi anajua kupitia mwakilishi (Mbunge),kwa sababu mbunge ana haki ya ku 'access' kila taarifa ya serikali anayofikiri ni muhimu kwake na wananchi wake kuifahamu.

I'm dubious about your reasoning but I'll wait to see if Zitto will answer my questions.
 
mimi napenda kuuliza, ametaja vyeo vya baadhi ya watu walioficha hela Uswis, anazungumziaje kuhusu jina lake naye kuwepo katika list ambayo yeye hajajitaja lakini kulingana na uchunguzi wa Jason Bourne unaonyesha na yeye ni miongoni mwa wale vigogo walioficha fedha Uswis. Na katika list yake kwa nini hajamention JK na Mwanae RZ1 au kwa kuwa ni role model wake hawezi kumtaja
 

Baada ya kukusanywa kwa maswali taarifa itatolewa ya LINI hiyo 'Exclusive Interview'
Ombi langu kwa members wote ambao wapo intersted:
-

Nilikuwa na kiu sana ya kuweza kupata nafasi ya kumhoji Mkuu Zitto kwa niaba ya members wa JF tokana na ukweli kuwa ni mmoja wa wanasiasa vijana ambaye huleta controversies nyingi juu yake na hoja zake. Wanachama wengi hupenda kuongea kwa niaba yake kana kwamba wamjua (it may be true or not); na kuwasilisha hoja zao kana kwamba ni za mwisho (final say).

Naomba ushirikiano wa kuniwasilishia maswali na hoja za msingi, na naomba tutumie hii fursa kuweza jua what Zitto is all about, what he thinks on certain issues, what he stands for, what he believes in AND why he thinks/ believes/stands for what ever it is that he postulates especially on what defines him.

UPDATE:-
Nimetoa kipengele binafsi naona badala ya kuuliza maswali inasababisha kuenda nje ya topic. Bring it on wakuu ulizeni maswali yenu. Karibuni..
Naomba kukuuliza maswali mawili.
1. Kama tayari una msingi wa mahojiano hayo (kwenye nyekundu), je unaonaje ukaorodhesha baadhi ya controversial statements ambazo labda ZIMEKUFANYA UWE NA NIA YA KUMHOJI ONE ON ONE? ili watu waweze kuchangia controversies zaidi wanazoziona?

2. Muda?? Ana muda gani? Ili tuweze kujua maswali mangapi na majibu ya kina kipi yanategemewa?

Mwisho naomba nikuulize hiyo interview itakuwa kama town hall meeting with you as a moderator? au kama interview ya TV/Radio? Gazeti?
Kwa sababu mimi binafsi nina maswali mengi na nataka nijue lipi au yapi yatafaa.
 
AshaDii

Namuuliza Zitto kua ni kweli yeye na J. Kikwete wana urafiki/ukaribu uliopitiliza? Kwamba ndio maana JK hakumnadi mgombea ubunge wa CCM wa jimbo aliloko Zitto uchaguzi wa mpaka 2010, pia ndio maana Zitto hakushiriki kumsusia JK siku ile anafungua Bunge!!
 
Last edited by a moderator:
Hii imetulia sana, naomba swali langu lisiwekwe kapuni, Mimi namuuliza Mh. ZZK, kwa nini hoja nyeti na za msingi anazikumbatia kama zake na si hoja za CDM? Haoni kwamba anaonekana kujitenga ki-dizaini na CDM ambayo inahubiri mshikamano na muungano wakati wote?
 
Mimi nakuuliza wewe mleta thread ni vigezo gani umevitumia kumleta Zitto na kukusanya maswali na ayajibu!!Pia tungependa kuelewa malengo yako ni yepi haswa ili tujue then tumuulize maswali ya msingi.
 
Swali la dogo la nyongeza kwa mh zzk, Je utaratibu wa sasa wa bunge la jmt wa kupiga kura kwa kuuliza wanao sema ndio na wanao sema hapana ni sawa na unakidhi matwaka ya kidemokrasia. Nini maoni yake, uendelee au ubadilishwe na kuboreshwa ili kuongeza imani ya bunge kwa wananchi?
 
Nina maswali mawili tu juu ya CDM kwa mh Zitto Z Kabwe(Naibu katibu mkuu),tena bila uoga wala kung'ata maneno atoe majibu bayana.

1.Mh Zitto, unaizungumziaje demokrasia ndani ya chama chako katika chaguzi,teuzi na kupanga safu za uongozi?

2.Mh Zitto,unaizungumziaje harakati za M4C (uamsho) na impact yake kisiasa na kijamii?

Ni hayo tu...
 
Mweshimiwa Zitto umekuwa mbunge wa Kigoma kaskazi kwa vipindi viwili mfululizo na sasa umetangaza kuwa hautogembea 2015...1. je katika vipindi vyote hivi vya ungozi wako wananchi wa Kigoma kaskazini ungependa wa kukumbuke kwa lipi?...2.je umeandaa mikakati gani kuhakikisha Chadema inatetea vema hicho kiti chake?...3.je endapo wanachadema hawatakupa ridhaa wa kuwawakirisha katika nafasi ya uraisi 2015,umepanga kufanya nini kama Zitto na kukifanyia nini chama ili kizidi kuwatetea wanyonge?...4.nini ulewa wako kuhusu familia?...
 
Napenda jua toka kwa zuberi zito1:anajitofautishaje na shibuda ndan ya cdm ktk mwonekano,matendo na mtazamo?2:kwann ktk uchaguz wa 2010 kikwete under $sm alimshnda Dr Slaa(cdm)hasa ktk jimbo lake ukilinganisha na majimbo mengine ya cdm?3:kwa nn haungan na wabunge wengine ndan ya cdm ktk campain ya M4c?4:kuna tetes kwamba anataka kusepa ndan ya cdm kwan ameahdiwa mambo makubwa na magamba mapema 2015 analizungu mziaje hili?5:zito anapinga ma2miz mabaya ya fedha za umma,je?Magari ya kifakhari anayo badilisha kama nguo ananunua kwa pesa ipi?6:wanzao kenya&uganda wamelidhia walimu kuongezewa mishahara kwa %300, ikiwa ni moja ya mbinu za kuboresha elimu ktk nch hzo.je?maon yake ni yapi kwa mstakabali wa kuboresha elimu Tz.
 
Ok mkuu,ushirikiano utaupata tu wala usijali.Ila kwasababu umeshakuja na disclaimer,wengi wana wasiwasi kuhusiana na hayo maswali ya binafsi.Kwakuwa umeshatoa ufafanuzi wa hayo maswali binafsi ambayo hayatakiwi,basi nimekuelewa.Nilidhani kwamba maswali binafsi ni kamavile kuhusu kutajwa kwake kwenye umiliki wa akaunti uswisi(alishapinga hilo na sitegemei jipya),pamoja na umiliki wa magari ya kifahari(nayo alishapinga licha ya wengi kudai kwamba ni kweli),however huko nyuma,alishakubaliana na hilo,na akasema kuwa aliamuwa kuyauza kwasababu ni ya kifahari na kwamba ni gharama sana kuyahudumia.
I am glad this is cleared…

I am curious… Unaposema kuwa hatasema ukweli una maana umesha ji' tune kuwa lolote atakalo ongea likiwa nje ya lile unalo AMINI tayari juu ya hilo itakuwa sio sawa? Hilo la Uswiz nashauri panga maswali yakiwa directed to him then uone kama hatajibu…

I believe I am prepared. Inawezekana sio kwa ubora kama mtu ambaye tayari mzuri katika anga ya Siasa BUT prepared enough. Hayo mahojiano hayatakuwa maswali na majibu baasi! Kama swali lina utata, ataulizwa swali juu ya hilo swali ili atoe utata huo. Hii ni moja ya sababu kubwa ambayo mimi nilitaka ushirikiano wa members… Kama kawaida kutakuwa na side thread ya members kutoa comments kuhusiana na interview itakayo kuwa inaendelea.

Jmushi1 umezugumza kwa kirefu aina ya maswali… Hivi sijaelewa maybe; ina maana bado kuna maswali unayo na unaona hayataulizwa sababu hayapo valid or hayajibiki? So far naona kuwa that is clear.

Pengine kwa kumalizia nikuulize,je follow up questions zitakubaliwa?Na je kuna idadi ya maswali ambayo mmepanga kuwa yatachukuliwa/kujibiwa?

Pia je kuna umuhimu wa kuweka dondoo za maswali ambayo atayajibu?Kwa mfano umetolea mifano ya maswali ambayo ni "personal",je umehsamwuliza limitation ya hayo maswali kuwa yepi haswa ni personal na yepi siyo?

In Blue; Jibu ni ndiyo. Ila take note kuwa atanipa time frame yake ya mda gani anaweza kuwepo, maswali mfuatilio ni muhimu ila yataangaliwa kama ni ya msingi na siyo yote hasa penye hoja ambayo atakuwa amejibu na imepwaya.

In Green; labda kama sijaelewa... So far hakuna limitation ya maswali, unaposema dondoo una maana ipi? Kuhusu maswali personal kama mwenyewe ulivyo kiri kuwa nimetolea ufafanuzi. Hajanipa limitation ya the kind of questions za kumuuliza.

Vinginevyo,nadhani angetuwekea misimamo yake kuhusiana na issues zinazoligusa taifa letu kwasasa ie udini,ufisadi,katiba mpya na mengineyo.Je anafikiri ni kweli kuwa chama chake ni cha kidini?Na kama ni kweli,tatizo hilo lishghulikiwe vipi?Je kama anafikiria kugombea urais,atalimalizaje tatizo hilo la udini?Mipango yake je?Ana mpango wa kuyataja majina ya wenye akaunti uswisi?Kama hapana,ni kwanini?Je akifanikiwa kuupata urais endapo atagombea,ana mpango wa kuwashughulikia mafisadi mara baada ya kuwaondoa madarakani?Je hilo litawezekana vipi ukitilia maanani ushirikiano wake na serikali ya ccm na wale wenye kutuhumiwa kuhusiana na ufisadi?

Pia aliposema mikataba iwekwe wazi,alikuwa na maana gani?Je ana maana kwamba ikiwekwa wazi hata sisi wananchi wa kawaida tutaweza kuiona?Ama alimaanisha ni wabunge peke yake?Kama ni wabunge peke yake,hilo litaleta utofauti gani kwenye bunge ambalo wabunge wake wanapiga kura za maamuzi kutokana na chama na si maslahi ya taifa?
Niishie hapa kwasasa.

The above para naona sasa kuna maswali ya kuwasilisha hapo... Will do so mkuu.
 
Mh. Zitto ningependa kujua kitu kingine kutoka kwako. Katika Mabadiliko ya Katiba yanayokuja kuna uwezekano mkubwa wa MAWAZIRI wasitokane na nafasi za UBUNGE. Kwa muono mwingine wewe umetangaza kutogombea ubunge jimboni kwako. Hii inaweza kuchukuliwa kuwa unawinda UWAZIRI kwa mlango huu wa nyuma? Ikitokea umebadili msimamo wako wananchi watakuchukulia vipi ndugu yangu?
 
Kuna taarifa kuwa CCM inatumia vyombo vya ulinzi na usalama katika kuudhofisha harakati za vyama vya upinzani, na hasa Chadema. Mheshimwa Zitto, je ni kweli kuwa vyombo vya usalama vinatumika kudhoofisha upinzani?

Na pili, Mh. Zitto amesemekana kuwa na mahusiano na viongozi wa juu wa usalama wa taifa, je mawasiliano yao ni ya kikazi au binafsi? Je kutokana na mahusiano yake ni usalama wa taifa, anahakikisha vipi analinda maslahi ya chama?
 
Mimi na muomba zitto kabwe akachunguze shirika la utangazaji Tanzania TBC hasa radio station zao hazina ubora kabisa hapa nahisi kulifanyika uchakachuaji hapa? Swali kwake je yupo tayar kufatlia ufisadi huu kama upo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom