AshaDii
Platinum Member
- Apr 16, 2011
- 16,189
- 18,114
- Thread starter
- #221
Asha Dii
Tuletee mh. Zitto aingie kwenye mtandao ajibu direct kutoka kwa wahusika
Chama
Gongo la mboto DSM
Mkuu Chama,
Toka nimeanza hili zoezi la kukusanya maswali ni wachache sana ambao wanapitia pages na kuangalia maswali gani yameulizwa na kama hayo maswali ambayo yeye anauliza yanajirudia. Ni sawa pia na hili wazo ulilotoa ambalo kama ingekuwa inawezekana ingekuwa bora zaidi. Kwa bahati mbaya saana haiwezekani kwa sababu zifuatazo:
- Ikitokea kila mmoja akawa na nafasi ya kumuuliza yeye Zitto moja kwa moja LAZIMA maswali yatajirudia tokana na ile tabia ya watu kuona uvivu kuangalia mjadala uliko toka kiasi kwamba hata yeye mwenyewe Zitto atachoka kujirudia; on top of kuna watu wana misuse hiyo nafasi na badala ya hoja watatoa vioja maana sio kila mtu anatii maagizo.
- Nia na malengo yangu katika huu mjadala ni kuhakikisha kuwa by the time tumemaliza hata yule ambaye hatakuwepo kufuatilia siku hio aweze kusoma toka mwanzo hasi mwisho wa mjadala na kuufuatilia bila tatizo lolote.
- Tupo more than 98 thousand members at Jf. Ikitolewa ruhusa ya kila mmoja kuuliza maswali watakuwa active zaidi ya 100 wote wakitaka kuuliza na kujibiwa, hivi mkuu Chama unaweza niambia namna gani itaendeswa? Mpangilio wa thread? Namna na wakati gani itabidi Zitto akae hapo? Week moja haitatosha... Kurahisisha nilifikiria the best way ni kukusanya maswali, kuyapanga vizuri then kumuuliza.
- Take note mkuu hii ni forum inayotegemea kujibishana kwa posts... Ingekuwa ni mdahalo live kama wa TV or Skype kama alivyotaka Mbuzi Mzee labda walau ingewezekana.
Last edited by a moderator: