EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
Zitto athibitishe kuwa yey c mamluk ndan ya cdm akishndwa aseme tumfanye nn kama mbadala wake
 
1. tupo kwenye mchakato wa kupata katiba mpya, katiba ya sasa ina mapungufu mengi katika vipengele vingi vinavyozidiana uzito, swali, ni kipengele gani katika katiba ya sasa kinamapungufu makubwa zaidi kuliko vingine na yeye ana maoni gani?

2. kama leo angechaguliwa kuwa rais wa jamhuri ya Muungano chini ya katiba hii akiwa amekuta maadui wale watatu (ujinga, umaskini na maradhi) wakineemeka hasa wakiwa wamepata mwenzao ufisadi, angetumia jeshi gani/mbinui gani kupambana na maadui hao??
 
Hii inanikumbusha Raisi msatafu Mkapa alivyo kuwa anatembelea shule yetu, Tuliambiwa tuandae mswali yaende kwa Head Master ayachuje, then Head Master Apeleke kwa Mkuu wa Wilaya Achuje, Mkuu wa Wilaya nae ayapeleke kwa wakubwa wake waya chuje,

Alitakiwa Aulizwe kila aina ya Swali na Ni vizuri kama yeye angekuwepo Online mwenyewe, kuulizwa kila aina ya Swali,


Chasha atakuwepo mwenyewe online kujibu maswali... Hapa yanakusanywa maswali kuwakilisha kwake ili ayajibu pamoja. So am kind of curious.. Sababu inakukumbusha Sekondari huna maswali ya kuwakilisha?
 
Zitto Zubeir Kabwe, nini kimekusukuma kutaka kugombea urais na sio ubunge tena?
-Kwa umri wako huoni unafaa zaidi kupambana ukiwa mbunge kuliko ukiwa rais?
-Je, ikiwa chama chako kitakunyima fursa ya kugombea urais ila chama kingine kikaonesha nia ya kukutaka uwe mgombea wake utakisaliti chama chako?
 
Nimejua kupitia kazi ninayoifanya,viongozi wote wa kitaifa wagebill yao ipo ofisi ya rais utumishi!

Kwa hiyo compensations zao ni public information kiasi tu cha raia yeyote kuweza kwenda na kwenye reception desk na kuulizia na kupewa bila tatizo lolote lile?
 
Zitto athibitishe kuwa yey c mamluk ndan ya cdm akishndwa aseme tumfanye nn kama mbadala wake


Kuweza kuwakilisha hili swali lako ningependa kujua kua niliwasilishe namna gani? Unaposema kuwa athibitishe yeye sio mamluki una maana iweje ama afanyeje ili wewe upate uthibitisho? Naomba nisaidie hapo Chater...
 
Mimi binafsi ninashukuru kwa nafasi hii adimu kama tuna uhakika wa kujibiwa

1. Zitto unasimamia kamati nyeti ya mashirika ya Umma, ningependa kuomba mpatiwe perfomance contracts zote za watendaji wakuu na wakuu wa idara tafadhali sana, sambamba na hilo muombe yafuatayo
A. Safari za nje zote walizofanya hata kama ni za mafunzo kwa watendaji wakuu (wakuu wa idara )vs siku wanazokaa ofisini
Kuna taasisi hakika kila mtu anakaimisha nafasi, sehemu ya kuja mtendaji mkuu anakuja ofisa wa chini maaana mnyororo wa safari umezidi

B. Muagize maana kamati inaagiza haiombi, mchanganuo wa utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa kaguzi iliyoisha mpaka hapo mlipo

Naomba sana usisitize perfomance contracts kwa watendaji wote na wakuu wa idara
 
Ashadii mwanangu usihuzunike. Unashangaa ni vipi kuficha pesa ya umma Uswisi inaweka kuwa personal!!! Yes, ni personal kwa kuwa anayefanya hivyo hata kama anaficha pesa ya umma, anaamini ni yake kutokana na ujanja wake. Kwake neno public does not exist. Hivyo, it becomes difficult--very difficult-- to draw the line between public and personal. Again, kuhusiana na "Zitto wako" my apology. I remorsely wish to say that if it had caused any heck forgive me. Hata hivyo umejifunza jinsi ya kuwasilisha. Zitto has to defed himself and freedom of speach has to be respected to letters. Kwa leo acha niishie hapa.
 
Samahani naona nimetoa kama maoni, ila naomba mh Zito aulizwe kama hiyo yawezekana ?
 
Q: The people of Kigoma constituency have benefited a lot from the Government because of your good relations with President Kikwete; is it genuine friendship or just a ploy to isolate you from the force of M4C?

Q: You are a leader who has displayed integrity and done a remarkable job in your constituency and the whole country; do you plan to enter the race for State House in 2015? Under which party?
 
kwa hiyo compensations zao ni public information kiasi tu cha raia yeyote kuweza kwenda na kwenye reception desk na kuulizia na kupewa bila tatizo lolote lile?
sawa kabisa,hizi taarifa ni za umma kila mtu ana haki ya kuzipata.ingawa wakati mwingine huwa kunakuwa na uzembe,kwa mfano, vitabu vya bajeti ya taifa ni haki ya kila mtanzania kujua kilichoandikwa na kupata nakala,lakini ukienda kuomba nakala wizara ya fedha watakwambia tunaupungufu wa nakala,haya ndiyo matatizo yetu sisi watanzania!
 
sawa kabisa,hizi taarifa ni za umma kila mtu ana haki ya kuzipata.ingawa wakati mwingine huwa kunakuwa na uzembe,kwa mfano, vitabu vya bajeti ya taifa ni haki ya kila mtanzania kujua kilichoandikwa na kupata nakala,lakini ukienda kuomba nakala wizara ya fedha watakwambia tunaupungufu wa nakala,haya ndiyo matatizo yetu sisi watanzania!

Kama ni taarifa za umma kwa nini huwa hazitangazwi walau mara moja kwa mwaka?
 
Nashukuru kwa nafasi hii.Maswali yangu ni:-
1.Kwanini wabunge, hasa wa upinzani, hamdai kanuni za kuendesha bunge zibadilishwe?Hamuoni spika amepewa madaraka makubwa mno?
2.Kwanini zito umeshindwa kutaja majina ya walioficha mabilioni uswiswi kama ulivyoahidi kufanya na badala yake ukatoa taarifa tu kuhusu ufisadi huo bungeni.?
 
Hatakuwa na Jipya zaid ya tunayoyajua tayar.
Sana sana tutmie nafasi hii kutokummuliza tu maswali bali kumpa kwenda mbele zaid na kumshaur kama ifuatavyo

1. Ni kwa nini haonekani kwenye harakati za Kukijenga chama thru M4C
2. Ni kwanini anafanya urafiki na watu ambao wanawaza kila siku Njia za Kuingamiza CDM eg Mkwe.re
3. Kwanini anatoa kauli ambazo effects zake ni kuwagawa wana CDM eg Kutaka kugomea Urais,
4. Reffer Before 2010 alitangazaga kuwa hatagombea Ubunge tena 2010, lakini cha ajabu 2010 akagombea tena, nini kilimfanya kusaliti msimamo wake ule?
5 na mwisho ni lini hasa ataacha kutumiwa na CCM kukivuruga CDM??
 
Ashadii mwanangu usihuzunike. Unashangaa ni vipi kuficha pesa ya umma Uswisi inaweka kuwa personal!!! Yes, ni personal kwa kuwa anayefanya hivyo hata kama anaficha pesa ya umma, anaamini ni yake kutokana na ujanja wake. Kwake neno public does not exist. Hivyo, it becomes difficult--very difficult-- to draw the line between public and personal. Again, kuhusiana na "Zitto wako" my apology. I remorsely wish to say that if it had caused any heck forgive me. Hata hivyo umejifunza jinsi ya kuwasilisha. Zitto has to defed himself and freedom of speach has to be respected to letters. Kwa leo acha niishie hapa.


Tupo pamoja mkuu... Nimekusikia na kukupata kabisa maneno ya post yoote - usitie shaka. I accept the apology and humbly appreciate it. Ila hata hivo sitakuelewa hadi uwasilishe maswali yako... Nakubali kuwa kwa leo uishie hapo; ila God willing you have time tomorrow hivo am looking forward to your questions. Pamoja saana.
 
Ashadii - "maisha binafsi" ndiyo "msingi" wa "maisha ya kiongozi mwadilifu"...! Binadamu awaye yote anapojaribu "kuficha masiha yake binafsi" fahamu fika kuwa huyo binadamu anayo mapungufu makubwa sana "ki-uongozi"...!

Mhe Zitto unategemea kuoa lini? Apatae mke apata kibali toka kwa Bwana.
Queen Esther
 
Samahani naona nimetoa kama maoni, ila naomba mh Zito aulizwe kama hiyo yawezekana ?


Kwa sababu nitakusanya maswali yoote pamoja... There will be a need of re-arranging hivo usitie shaka Nsiande. It will be done.
 
Kama ni taarifa za umma kwa nini huwa hazitangazwi walau mara moja kwa mwaka?
Nafikiri (Sina uhakika haya ni mawazo yangu tu) wanaamini kila mwananchi anajua kupitia mwakilishi (Mbunge),kwa sababu mbunge ana haki ya ku 'access' kila taarifa ya serikali anayofikiri ni muhimu kwake na wananchi wake kuifahamu.
 
Hatakuwa na Jipya zaid ya tunayoyajua tayar.
Sana sana tutmie nafasi hii kutokummuliza tu maswali bali kumpa kwenda mbele zaid na kumshaur kama ifuatavyo

1. Ni kwa nini haonekani kwenye harakati za Kukijenga chama thru M4C
2. Ni kwanini anafanya urafiki na watu ambao wanawaza kila siku Njia za Kuingamiza CDM eg Mkwe.re
3. Kwanini anatoa kauli ambazo effects zake ni kuwagawa wana CDM eg Kutaka kugomea Urais,
4. Reffer Before 2010 alitangazaga kuwa hatagombea Ubunge tena 2010, lakini cha ajabu 2010 akagombea tena, nini kilimfanya kusaliti msimamo wake ule?
5 na mwisho ni lini hasa ataacha kutumiwa na CCM kukivuruga CDM??


Bramo umeniacha njia panda kidogo... Tokana na maelezo yako hayo niliyo bold na ku color yanaenda tofauti na number-pointed points zako. Niwasilishe? Maana hayo yoote ni maswali na sio ushauri kama unavyodai... Ila itapendeza tuyawasilishe hivo hivo kama hutajali kama maswali.
 
1. Unafikiri mpaka sasa hivi CHADEMA ipo kwenye mkondo sahhihi kisiasa na kama sivyo ni maeneo gani penye udhaifu?
2. Unafikiri msimamo wako wa kukataa kupokea posho umepokelewa vizuri na wabunge wa chama chako
3. Unafikiri uongozi wa sasa wa CHADEMA ukiacha wewe una uwezo wa kuikifikisha chama kushika dola?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom