European Parliament resolution on Tanzania

European Parliament resolution on Tanzania

Nawewe unataka kuwa mjinga.Hata kama Rais kasema, mihimili mingine inaweza kulisimamia hili swala kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.Au sheria inasemaje?
Bwana Huyu baada ya kulalamika kwamba biashara zake zinamwendea kombo ,kupunguza wafanyakazi na kuhamia kwenye ofisi ya bei rahisi,sasa naona anajikomba kwa watawala angalau wamkumbuke uDC!
 
Dunia haipaswi kuwa kimya kuona watu wanauawa na kudhulumiwa haki zao.

Kama hawakusema kitu kwa Trump (japo sikioni), hai justfy kukaa kimya dhidi ya uvundo unaoendelea Africa
 
Uhuru wetu umehodhiwa na mtu mmoja ambaye anajifanyia kila atakacho mwenyewe,na ndicho wazungu wanakipinga wanataka kila mtu afaidi matunda ya uhuru wake.
 
Ukosefu wa akili na busara ni jambo baya sana.

Wewe huoni mnazidi kuwarahisishia kazi yao hao mabeberu kwa juhudi zenu za kuwatengeneza unaowaita "vibaraka?"

Mtu kama unayo akili nzuri na unajua tabia za hao wanaokuzonga, utafanya kila juhudi za kuwanyima fursa hiyo. Unafanya mambo yako bila kuzalisha vibaraka.

Sasa, kwa mifano uliyotoa hapo juu, matokeo yake tunayajua. Kama mtaendelea kuzalisha 'vibaraka' na nyinyi mtakumbwa na kimbunga kile kile kilichowakumba Ghadafi na Saddam.
Mkuu, huyo unaejaribu kumpa uelewa hawezi kukuelewa ng'oo, hapo ndipo iq yake ilipoishia, usimjaze zaidi atapata kifafa cha ubongo, hebu soma comments zake itajua nini nakwambia
 
Mimi Nina uhakika watanzania wengi sana wakiwemo hao wa chama tawala wanafurahia kimoyomoyo kuona Jiwe katikiswa.
 
CCM wanaona aibu wanaogopa hata kuitisha maandamano ya vijana wake kupinga maazimio ya EU. Eti "JINGA LAO" anawaomba CHADEMA watoe tamko.
 
Historia huwa haipotei na kamwe haidanganyi. Wananchi wa Libya waliambiwa na Mabeberu kwamba Ghadafi ni tatizo na iwapo akiondoka madarakani wananchi wa Libya wataishi maisha mazuri sana. Hebu tujiulize: Wamarekani waliongoza mapambano ya kumuua na kumuondo madarakani Rais Muamar Ghadafi, JE, Libya wana maisha gani mazuri leo hii zaidi ya mateso makali?

Walibya waliahidiwa kwamba Ghadafi akiondoka madarakani nchi ya Libya itakuwa na Demokrasia safi na ya kweli. Hebu tujiulize: Iko wapi hiyo Demokrasia nchini Libya baada ya Mabeberu kumuua Ghadafi? Hakuna Demokrasia zaidi ya mateso nchini Libya na maisha magumu.

Tusisahau yanayowakuta Iraki na Siria kwa Bashar Asad ambapo mabeberu wanataka kupandikiza vibaraka wao ili wachote rasilimali ya mafuta kwa manufaa yao. Kote huko ni mateso makali. Walimuua Rais Saddam Hussein na kuwahakikishia wana dunia hii kwamba Iraki itakuwa na Demokrasia na maisha mazuri. Tujiulize yako wapi maisha mazuri Iraki zaidi ya machafuko yasiyoisha tangu Mwaka 2003 hadi leo hii?

Watanzania tunapaswa kutumia yanayowapata Walibya na wairaki kujifunza kwamba kamwe Mabeberu wa Ulaya na kwingineko duniani hawawezi kusimama na serikali yetu pale wanapoona tunajenga uchumi wetu ili tujitegemee. Lazima tufahamu kwamba watatuchonganisha na kupandikiza vibaraka wao nchini wakiwemo waafrika wenzetu ambao leo hii tunawaona wakidiriki kupigia upatu Mashinikizo yao ya kijinga yakiwemo ushoga, Mara wanatetea demokrasia yetu nk.

Wameshindwa kuisadia Libya na Iraki kama walivyoahidi na kuaminisha ulimwengu kwamba kuna matatizo makubwa ya kidemokrasia katika nchi hizo nk, hakuna amani huko zaidi wamesababisha machafuko makubwa katika nchi hizo; watawezaje kutusaidia sisi watanzania tena Taifa letu ambalo tuko salama sana, hatuna matatizo kama wanavyoeleza mabeberu na vibaraka wao?

Mabeberu hao wasiofaa hata kidogo wamekaa kimya kuhusu yanayoendelea nchini Ufaransa kana kwamba hawaoni kitu. Watu wanaandamana mwezi mzima kumshinikiza Rais Emmanuel Macron aondoke madarakani lakini tujiulize ni lini Mabeberu wa EU na vibaraka wao walitoa tamko lolote kumshinikiza beberu mwenzao aondoke madarakani? Watanzania sharti kustukia maigizo ya mabeberu na uonevu dhidi ya mataifa ya kiafrika.

Kudhibiti Makinikia na biashara harama za kutupora madini yetu haijawapendeza wazungu hata kidogo na kwa hiyo basi wameamua kupambana na sisi kwa namna mbalimbali ikibidi hata watufarakanishe ili nchi yetu ipoteze mwelekeo na isitawalike. Mabeberu wanatueleza wanapigania demokrasia ndani ya nchi yetu wakati wanajua fika walitoa ahadi ya aina hiyo kwa Libya na kwingineko duniani lakini hadi leo hii Libya hakuna demokrasia wala amani bali machafuko.

Walibya wanajuka kukubali kuhadaiwa na mabeberu, wanamkumbuka ghadafi na kujuta sana kuuawa kwa Rais Muamar Ghadafi. Wanakumbuka fadhila za Ghadafi aliyekuwa akiwapatia malipo ya chakula kila mwezi wananchi masikini, leo hakuna malipo hayo. Wanamkumbuka ghadafi aliyekuwa akiwalipia mahali za kuoa walibya masikini lakini leo hakuna fadhila hizo. Wanamkumbuka ghadafi aliyeapa kupambana na ubeberu ili usiitawale afrika. Ghadafi alijipambanua kama kiongozi asiyetaka kuona Afrika inaonewa na kushikizwa kufanya mambo ya kijinga kwa maslahi ya mabeberu.

Watanzania tupeuke mtego uliowamaliza walibya ili tusije kujuta kama walibya leo hii. Hawa vibaraka na vijakazi wa mabeberu wanaopiga kelele kwamba Tanzania tunaenda vibaya hawana mana kabisa bali wanatumikia mabeberu wanaotaka kututawala ili wapole rasilimali zetu. Hawa vibaraka na mabeberu wao tuwaogope kama Ukoma.

Pinga UBEBERU NA VIBARAKA wao wote kwa maslahi ya Taifa hili.
Mnaandika propaganda nyiiingi hata zisizo na maana badala ya kutuambia ni vipi tutajaza nakisi iliyopo kwenye bajeti yetu bila kuwategemea hao, mnaowaita "Mabeberu". Hayo ndiyo tunataka kufahamu sio mambo ya umbeya umbeya haya uliyoandika. This is utter rubbish, we want solution not propaganda or rhetorics.
 
Taifa hili si la mtu, ni la wananchi wote. hivyo basi kila mtu atambue anahaki na taifa hili bila kupangiwa na fulani nje ya sheria ambazo wananchi tunazitaka zituongoze.

Mambo kadhaa mawakili wanatukumbusha ambayo hata kisheria hayajawahi kupatiwa majibu huenda kutokana na wanaotenda ni:-

▶Kupigwa risasi watu na kukosekana kwa uchunguzi hadi leo!, Uhai wa watu ni muhimu kuliko vitu.

▶Dola kutafutiza makosa ili kuwafunguliwa kesi za kisiasa wapinzani.

▶Kutekwa watu na wengine kurudi pasipo kuwekwa wazi au chunguzi au maelezo hata kwa waliotekwa ili kuelezea kinagaubagwa au kuhojiwa na wanahabari.

▶Watu kupotea na kukutwa kwenye viroba katika maeneo ya fukwe za bahari, hakuna majibu hadi leo!.

▶Kutungwa kwa sheria ngumu ya mitandao, kuzuia haki ya kujieleza kinyume na misingi ya haki za kikatiba na haki za binadamu.

▶Kudorora kwa haki za binadamu eg. wanafunzi waliopata ujauzito kutopata haki ya kuendelea kusoma.

▶Kubadili kwa Sheria na Kanuni za Chaguzi za kupata viongozi wa Kiserikali ili kuwazuia wapinzani wasipate ushindi, hiyo ni nje ya matumizi mabaya ya Vyombo vya Usalama. eg. PolisiDola/...

▶Kukosekana kwa utawala bora hata katika hali tu iliyozoeleka katika kutofuata sheria za nchi.

Mawakili hawajawahi kuwa wajinga, wanatambua yanayoendelea, kutofuatwa kwa Sheria na kukiukwa kwa Haki za binadamu nchini.

Mungu awaongoze wananchi wote kuendelea kuungana na kushikamana katika kusimamia haki na sheria. "Sema inatosha sasa"!.
 
sikiliza we mjinga.kujua kuandika sio ndo ulete upopoma humu.Unadhan walioandika ni wajinga kama wewe.mambo mengine walioeleza umeona ni ya kijinga?Au umeshiba kifaduro.
 
Huo ndio ukweli ...muungano wa vyama vidogo vidogo vya kutetea mashoga vimetumia mwamvuli wa EU kuandaa Resolutions zenye ajenda ya kutulazimishia Ushoga.
 
Maazimio ya EU yanapaswa kutafsiriwa kuwa ni uingiliwaji wa masuala ya Taifa Huru. Kwa nini hawakutoa azimio dhidi ya Donald Trump kwa kauli yake ya kupinga ndoa za jinsia moja? Wana njama dhidi ya Waafrika na wanashtushwa na utekelezaji wa Rais Magufuli
Unamjua aliyekupa uhuru?
 
Huo ndio ukweli ...muungano wa vyama vidogo vidogo vya kutetea mashoga vimetumia mwamvuli wa EU kuandaa Resolutions zenye ajenda ya kutulazimishia Ushoga.
Wakifi.wa wao mnaumiaje nyie?
 
Back
Top Bottom