Erick Kabendera: Rais Samia “Thucydides Trap” haitakuacha salama

Retired

JF-Expert Member
Jul 22, 2016
40,402
74,005
Kwenye historia ya vita na mahusiano ya kimataifa, kuna nadharia inaitwa “Thucydides Trap” ambayo utumika kuelezea ulazima wa kutokea mgogoro au vita endapo taifa linalochipukia linapotishia kulizidi nguvu na ushawishi taifa lenye nguvu.

Kama wewe ni msomaji wa siasa za Nicollo Machiavelli, utakumbuka kuwa msingi wa nadharia zake ni kuwa kiongozi akihodhi madaraka na mamlaka, hawezi kutengeneza muhimili mwingine wa kisiasa wenye nguvu na ushawishi kama wake. Ndiyo maana marais ushauriwa wasiwateue wagombea wenza au mawaziri wakuu wenye nguvu au ushawishi wa kisiasa kuliko wao.



Bado hatujui sababu za Rais Samia kumteua Makonda lakini tunajua kuwa Makonda alimhadaa Magufuli kiasi kwamba “aliogopa” kumuondoa kwenye nafasi ya mkuu wa mkoa licha ya kukabiliwa na tuhuma nzito. Tulichokiona wiki iliyopita wakati wa ziara za Makonda kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa ni kutumia mbinu zile zile alizozitumia kwa Magufuli kumhadaa Rais Samia; anaonekana kama vile anampigia kampeni Rais Samia wakati huohuo anasafisha jina lake na kuandaa mtaji wake wa kisiasa wa huko mbeleni.



Mwanasiasa yoyote mkongwe hawezi kuamini maneno ya Makonda kutokana na historia yake na ukweli kwamba anachokiwaza kichwani mwake ni tofauti na matendo yake.

Kufanikiwa kwake kisiasa kumetokana na kuwahadaa watu, kuwadhalilisha wana CCM, wapinzani na viongozi washaafu. Hawezi kushidwa kumfanyia vitendo kama hivyo Raisa Samia hata kama amekula kiapo cha utii kwake. Kwahiyo ni wazi kuwa Makonda anazitumia ziara hizi kujenga taswira kuwa serikali ipo chini yake kwa kutoa maelekezo kwa mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali.

Kumruhusu aendelee kufanya hivyo ni kurudia makosa aliyoyafanya Rais Mkapa kwa kumjenga Magufuli kisiasa. Natumaini Rais Samia amewaza kwa undani na kupokea ushauri wa watu wake wa karibu kabla ya kufikia uamuzi huu.

Kama hakufanya hivyo, atajikuta anamuandaa mshindani wake kwenye uchaguzi ujao au anamtengeneza mwanasiasa atayeiingiza nchi kwenye matatizo baada ya kuondoka kwake madarakani. Hapo ndipo dhana ya “Thucydides Trap” itakapodhibitika.

c&p
Thucydides's Trap refers to the natural, inevitable discombobulation that occurs when a rising power threatens to displace a ruling power...[and] when a rising power threatens to displace a ruling power, the resulting structural stress makes a violent clash the rule, not the exception

Tunao memo huu: Mgema akisifiwa, tembo hulitia maji
 
Nani asiye kufahamu Kabendera kwa namna unavyotumika na wanasiasa wasio mpenda yeyote awaye ahatarishaye chakula cha mafisadi?!

Hata sasa, ni wazi wale waliokutumia kipindi cha Magufuli ndiwo hao hao wameanza kukutumia kipindi hiki Makonda anapoanza kuhatarisha chakula cha vipenzi wako mafisadi.

Wape salamu wapendwa wako;-

Zitto
January
Nape
Kinana.
 
Kwenye historia ya vita na mahusiano ya kimataifa, kuna nadharia inaitwa “Thucydides Trap” ambayo utumika kuelezea ulazima wa kutokea mgogoro au vita endapo taifa linalochipukia linapotishia kulizidi nguvu na ushawishi taifa lenye nguvu.

Kama wewe ni msomaji wa siasa za Nicollo Machiavelli, utakumbuka kuwa msingi wa nadharia zake ni kuwa kiongozi akihodhi madaraka na mamlaka, hawezi kutengeneza muhimili mwingine wa kisiasa wenye nguvu na ushawishi kama wake. Ndiyo maana marais ushauriwa wasiwateue wagombea wenza au mawaziri wakuu wenye nguvu au ushawishi wa kisiasa kuliko wao.



Bado hatujui sababu za Rais Samia kumteua Makonda lakini tunajua kuwa Makonda alimhadaa Magufuli kiasi kwamba “aliogopa” kumuondoa kwenye nafasi ya mkuu wa mkoa licha ya kukabiliwa na tuhuma nzito. Tulichokiona wiki iliyopita wakati wa ziara za Makonda kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa ni kutumia mbinu zile zile alizozitumia kwa Magufuli kumhadaa Rais Samia; anaonekana kama vile anampigia kampeni Rais Samia wakati huohuo anasafisha jina lake na kuandaa mtaji wake wa kisiasa wa huko mbeleni.



Mwanasiasa yoyote mkongwe hawezi kuamini maneno ya Makonda kutokana na historia yake na ukweli kwamba anachokiwaza kichwani mwake ni tofauti na matendo yake.

Kufanikiwa kwake kisiasa kumetokana na kuwahadaa watu, kuwadhalilisha wana CCM, wapinzani na viongozi washaafu. Hawezi kushidwa kumfanyia vitendo kama hivyo Raisa Samia hata kama amekula kiapo cha utii kwake. Kwahiyo ni wazi kuwa Makonda anazitumia ziara hizi kujenga taswira kuwa serikali ipo chini yake kwa kutoa maelekezo kwa mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali.

Kumruhusu aendelee kufanya hivyo ni kurudia makosa aliyoyafanya Rais Mkapa kwa kumjenga Magufuli kisiasa. Natumaini Rais Samia amewaza kwa undani na kupokea ushauri wa watu wake wa karibu kabla ya kufikia uamuzi huu.

Kama hakufanya hivyo, atajikuta anamuandaa mshindani wake kwenye uchaguzi ujao au anamtengeneza mwanasiasa atayeiingiza nchi kwenye matatizo baada ya kuondoka kwake madarakani. Hapo ndipo dhana ya “Thucydides Trap” itakapodhibitika.

c&p
Thucydides's Trap refers to the natural, inevitable discombobulation that occurs when a rising power threatens to displace a ruling power...[and] when a rising power threatens to displace a ruling power, the resulting structural stress makes a violent clash the rule, not the exception

Tunao memo huu: Mgema akisifiwa, tembo hulitia maji
Wewe unaongea kama nani? Wewe ni kibaraka wa mabeberu! Magu alikuweka korokoroni kwasababu moja kuu ya kushindwa kuthibitisha mihamala ya hela uliyokuwa unatumiwa kwenye account yako alafu unakusanya watu unaanza kuwagawia! Kuna viongozi wanaozaliwa wakiwa viongozi lakini kuna viongozi wanaotengenezwa! Magufuli kutengenezwa na Mkapa kama ulivyosema na akaja kuwa kiongozi mzuri (kwa mukutadha wa wananchi waliowengi) na wachache mafisadi, wala rushwa, makuwadi wa mabeberu kama wewe walimchukia.
Suala la Makonda halina shida ili mradi yuko ndani ya CCM na wanautaratibu wao wa kuwekana sawa! Edward Lowasa ilikuwaje? Kwahiyo, ondoa shaka Makonda ni kiongozi mzuri na nilazima tuwe na watu vinginevyo ukitaka kiongozi afanye jinsi Wewe unavyotaka basi hii nchi yakwako peke yako? Tutakuwa na viongozi wenye mtizamo kinzani wote katika kujenga! Ongera makonda
 
Wewe unaongea kama nani? Wewe ni kibaraka wa mabeberu! Magu alikuweka korokoroni kwasababu moja kuu ya kushindwa kuthibitisha mihamala ya hela uliyokuwa unatumiwa kwenye account yako alafu unakusanya watu unaanza kuwagawia! Kuna viongozi wanaozaliwa wakiwa viongozi lakini kuna viongozi wanaotengenezwa! Magufuli kutengenezwa na Mkapa kama ulivyosema na akaja kuwa kiongozi mzuri (kwa mukutadha wa wananchi waliowengi) na wachache mafisadi, wala rushwa, makuwadi wa mabeberu kama wewe walimchukia.
Suala la Makonda halina shida ili mradi yuko ndani ya CCM na wanautaratibu wao wa kuwekana sawa! Edward Lowasa ilikuwaje? Kwahiyo, ondoa shaka Makonda ni kiongozi mzuri na nilazima tuwe na watu vinginevyo ukitaka kiongozi afanye jinsi Wewe unavyotaka basi hii nchi yakwako peke yako? Tutakuwa na viongozi wenye mtizamo kinzani wote katika kujenga! Ongera makonda
Jadili hoja ya "Thucydides Trap", disapprove it or approve it!
 
Kama kuna ukweli juu ya tetesi zimuhusuzo Makamu wa Mwenyekiti Taifa wa chama, basi teuzi ya mwenezi mpya inaweza kuwa ni mojawapo ya mambo yanayopelekea hali ya mtafaruku unaofukuta chini kwa chini. Utendaji wa muenezi mpya wa kutoa maagizo ya moja kwa moja na kuyaelekeza kwa mawaziri, ambao mamlaka yao ya uteuzi ni Rais mwenyewe, ni kitu ambacho hakitarajiwi kutoka kwa mtu wa nafasi ya katibu muenezi wa chama.

Hii ni aina ya nguvu mpya ya mamlaka inayojijenga ndani ya chama dola, pengine isingalionekana ni jambo geni endapo maagizo kama hayo yangalitoka katika kinywa cha PM ama kidogo hata kwa KM wa chama. "It is plain reality that an hegemony is threatened by this new emerging power, there will be likelihood of war between the two powers in the near future".

Kupanga ni kuchagua. "SSH must be real smart in this time, otherwise things will fall apart".
 
Back
Top Bottom