Baraka Mina
JF-Expert Member
- Sep 3, 2020
- 581
- 574
Mwimbaji mkongwe wa nyimbo za injili na Askofu wa Hossana Assemblies of God Ephraim R. Mwansasu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo (29/08/2021). Mwasasu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu, kwa sasa msiba upo Kimara Mwisho.
Mwansasu atakumbukwa kwa nyimbo zake nyingi alizoziimba kwa mvuto wa aina yake na kutoa ujumbe mzuri kwa kila aliyesikiliza na kuona video za nyimbo hizo zilizopendwa na kupata umaarufu Tanzania na nje ya Tanzania.
Baadhi ya nyimbo za Mwasasu ni:
Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe, Pumzika kwa amani nguli wa nyimbo za injili Askofu Ephraim R. Mwansasu.
Mwansasu atakumbukwa kwa nyimbo zake nyingi alizoziimba kwa mvuto wa aina yake na kutoa ujumbe mzuri kwa kila aliyesikiliza na kuona video za nyimbo hizo zilizopendwa na kupata umaarufu Tanzania na nje ya Tanzania.
Baadhi ya nyimbo za Mwasasu ni:
- Siku nikilala mauti.
- Nangojea wakati.
- Kutesa kwa zamu.
- Dunia inapita.
- Tukimaliza kazi.
- Kiama.
- Heri wenye moyo safi.
- Tutatesa milele.
- Wosia wa baba.
- Watoto wachanga.
- Wanawake.
- Maumivu ya Yesu.
Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe, Pumzika kwa amani nguli wa nyimbo za injili Askofu Ephraim R. Mwansasu.