Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Sijui una maana gani unaposema bado naamini Trump atakwama, nilichosema ni kwamba Trump atapata wakti mgumu kuliko aliowahi kupata hata huyo Obama aliyemtangulia.

Tatizo ni kwamba wengi wenu mna-underestimate feeling iliyopo mtaani following Donald Trump win. Wengine wenu yawezekana mnaishi hata Marekani lakini nina wasi wasi kama kweli mnajua hisia za walio wengi na wanavyojuta kumpa mwanya huyo bwana.

Tofauti ni kwamba huko Marekani, watu wanapokuwa disappointed hawakai kimya, watapaza sauti zao na wataonesha hisia zao kwa matendo.

Nafikiri mnasahau Tea Party ya Republicans baada ya ushindi wa Obama lakini nawahakikishia safari hii mambo ni tofauti kidogo. Jamaa wanasubiri Trump aapishwe halafu naomba turudi hapa jamvini tupashane yanayojiri.

Keep betting against the Trumpster!
 
Sijui una maana gani unaposema bado naamini Trump atakwama, nilichosema ni kwamba Trump atapata wakti mgumu kuliko aliowahi kupata hata huyo Obama aliyemtangulia.
Huo wakati mgumu aliopata Rais Obama ni baada ya kupoteza control ya House 2010 na haikurudi tena Democrat hadi leo (miaka 6). Na balaa lingine kupoteza control ya Senate 2014 hadi leo Senate control ipo chini ya Republicans.

Lakini ukweli ambao hutaki kuzungumzia ni kuwa Rais Obama ni responsible kwa kiasi kikubwa kwa huo 'wakati mgumu' unaouzungumzia.

Senate Majority na House Majority ni Republican, na performance ya Trump kwa miaka miwili hii na ijayo ndio moja ya sababu kubwa itakayo-determine sura ya Congress. Sasa sijui utasemaje elections za Class I Senators na MoHR 2018 zikija kuongeza Seats kwa Republicans?

Usikae ukaamini kuwa Republicans wataenda kumuangusha Rais wa chama chao na kuwapa ahueni Democrats ambao wamekuwa na WH kwa miaka minane. Party politics kwenye Congress ni strong kuliko unavyodhani.

Lakini ugumu anaoupata POTUS ni kutokana na suala na suala. Lindsey Graham na John McCain wanaweza kuwa na mawazo tofauti kuhusu Putin na Russia lakini wote wanasupport sera nyingi za Trump.

Tatizo ni kwamba wengi wenu mna-underestimate feeling iliyopo mtaani following Donald Trump win. Wengine wenu yawezekana mnaishi hata Marekani lakini nina wasi wasi kama kweli mnajua hisia za walio wengi na wanavyojuta kumpa mwanya huyo bwana.

Hizo hisia za walio wengi umezipimaje?

Tofauti ni kwamba huko Marekani, watu wanapokuwa disappointed hawakai kimya, watapaza sauti zao na wataonesha hisia zao kwa matendo.

Kweli, lakini pia kuna unafiki mwingi tu kwenye hayo mambo. Nadhani ulisikia kuwa waandamaji wengi tu walilipwa kuandamana kumpinga Trump na kuwashawishi Electors wa Rep wasimpigie kura Trump. Hadi Eectors walitishiwa kuuawa.

Kuna waandamanaji walikuwa wakiandamana huku wakiwa hawajui wanachoandamania. Namaanisha kuna watu wengi tu walikuwa wakimpinga Trump kwa sababu waliambiwa ni racist, mysogynist, bigot, dictator, xenophobic n.k lakini wameanza kuona kuwa kumbe vyote vilikuwa uongo tu na wanajuta kutokumpigia kura.

Nafikiri mnasahau Tea Party ya Republicans baada ya ushindi wa Obama lakini nawahakikishia safari hii mambo ni tofauti kidogo. Jamaa wanasubiri Trump aapishwe halafu naomba turudi hapa jamvini tupashane yanayojiri.

Inaeleweka kuwa Democrats wanapanga kumkwamisha Trump. Hivi baada ya Trump kuwaaibisha hao Team Hilary wakiongozwa na Marais wawili wa US unategemea watampa ushirikiano 100%?.

Usije ukashangaa huo msimamo wa Democrats ukawacost kwenye uchaguzi wa 2018 na wakaendelea kupoteza seats.

Je, unajua kuwa katika kipindi cha Rais Obama ndipo Democrats wamepoteza zaidi kuliko kipindi chochote katika historia ya US?
 
Huo wakati mgumu aliopata Rais Obama ni baada ya kupoteza control ya House 2010 na haikurudi tena Democrat hadi leo (miaka 6). Na balaa lingine kupoteza control ya Senate 2014 hadi leo Senate control ipo chini ya Republicans.
El Jefe, either you are being disingeneuous or just acting plain dumb. Republicans waliapa kumkwamisha Obama toka siku ile anaapishwa na kuhakikisha hatapata awamu ya pili na ushahidi upo. Kilichotokea ni kwamba kwa miaka miwili toka 2008, Obama kwa kutojua (ni kweli alijidanganya) went out of his way to reach out akifukuza mirage, non-partisan support!

Ajabu ni kwamba hata pale Obama alipounga mkono mambo yaliyopendekezwa na Republicans wenyewe, waliamua kumruka. Affordable Care Act ilikuwa ni blue print ya care act ya Republicans na si walichotaka Democrats hivyo wengi waliamua kukaa kando na kumwachia jukumu la kuinadi peke yake. Republicans walipoona hivyo nao wakaamua kuipinga na hicho ndicho kilichowafanya Democrats kuzinduka na kuipitisha bila Republican hata moja kuwaunga mkono.

Republicans baada ya ACA kupitishwa na kuona inaanza kupendwa waliamua kufanya jitihada za kuihujumu kwa lengo la kuikwamisha. Mbinu moja waliyoitumia na ikafanikiwa miongoni mwa watu wenye uelewa mdogo ni kuibatiza jina la Obama Care Act na kujaribu kuonesha kuwa ni tofauti na Affordable Care Act. Kwa kitendo hiki Republicans wakafanikiwa kuwachanganya wengi wakiamini hivi ni vitu viwili tofauti...wako waliopenda ACA na si Obama Care.
Lakini ukweli ambao hutaki kuzungumzia ni kuwa Rais Obama ni responsible kwa kiasi kikubwa kwa huo 'wakati mgumu' unaouzungumzia.
Ndiyo hiyo ni kweli, Obama alisababisha hali hiyo kwani alijikita katika kutafuta muafaka ambao hangeupata kwa watu walioapa toka awali kumkwamisha. Kwa kufanya hivyo ili kutimiza ndoto yake kama unifier akawasahau Democrats ambao nao kwa upande wao wakaamua kuwa kama watazamaji tu!
Senate Majority na House Majority ni Republican, na performance ya Trump kwa miaka miwili hii na ijayo ndio moja ya sababu kubwa itakayo-determine sura ya Congress. Sasa sijui utasemaje elections za Class I Senators na MoHR 2018 zikija kuongeza Seats kwa Republicans?
Ni kweli Trump ana Senate na House majority lakini sidhani kama anamfikia Obama mwaka 2008. Njia pekee aliyo nayo tofauti na alichofanya Obama ni kuvitumia hivyo vyombo viwili kusukuma ajenda zake, partisan politics, bila kujali wapinzani wake wanasemaje. Tatizo alilo nalo ni kwamba kwanza, anaingia White House na idadi ndogo ya Wamarekani. La pili ni kwamba hana total support ndani ya chama chake na positively zero support nje ya chama chake.
Usikae ukaamini kuwa Republicans wataenda kumuangusha Rais wa chama chao na kuwapa ahueni Democrats ambao wamekuwa na WH kwa miaka minane. Party politics kwenye Congress ni strong kuliko unavyodhani.

Lakini ugumu anaoupata POTUS ni kutokana na suala na suala. Lindsey Graham na John McCain wanaweza kuwa na mawazo tofauti kuhusu Putin na Russia lakini wote wanasupport sera nyingi za Trump.
Nadhani kwa hiyo sentensi ya pili umejijibu na juzi tu tumeshuhudia Republicans wakianza kwa kujikwaa.
Hizo hisia za walio wengi umezipimaje?
Nazipima kwa kura karibu milioni tatu za Democrats dhidi ya Republicans.
Kweli, lakini pia kuna unafiki mwingi tu kwenye hayo mambo. Nadhani ulisikia kuwa waandamaji wengi tu walilipwa kuandamana kumpinga Trump na kuwashawishi Electors wa Rep wasimpigie kura Trump. Hadi Eectors walitishiwa kuuawa.

Kuna waandamanaji walikuwa wakiandamana huku wakiwa hawajui wanachoandamania. Namaanisha kuna watu wengi tu walikuwa wakimpinga Trump kwa sababu waliambiwa ni racist, mysogynist, bigot, dictator, xenophobic n.k lakini wameanza kuona kuwa kumbe vyote vilikuwa uongo tu na wanajuta kutokumpigia kura.
Nitajie uongo moja tu aliopandikiziwa Donald Trump. Ninavyojua watu wengi wanajuta si kwa kutompigia kura Trump bali kwa kumpuuzia na hivyo kutokujitokeza kupiga kura dhidi yake!
Inaeleweka kuwa Democrats wanapanga kumkwamisha Trump. Hivi baada ya Trump kuwaaibisha hao Team Hilary wakiongozwa na Marais wawili wa US unategemea watampa ushirikiano 100%?.
Huo mpango uliusikia wapi? Na hata kama ingekuwa kweli...au ni yale yale ya mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu uchungu.
Usije ukashangaa huo msimamo wa Democrats ukawacost kwenye uchaguzi wa 2018 na wakaendelea kupoteza seats.
Kama msimamo kama huo wa Republicans kumkwamisha Obama uliwanufaisha kwenye uchaguzi wa 2010 kwa nini iwe tofauti kwa Democrats? Unaona unavyoongozwa na mihemuko!
Je, unajua kuwa katika kipindi cha Rais Obama ndipo Democrats wamepoteza zaidi kuliko kipindi chochote katika historia ya US?
Lakini bado wakampa Obama kipindi cha pili mwaka 2012 na sasa anauacha Urais akiwa anapendwa kwa zaidi ya asilia 50% ya Wamarekani. Subiri shujaa wako Trump aapishwe baadaye mwezi huu...weka tu akiba ya maneno.
 
"Mag3, post: 19193443, member: 10873"]El Jefe, either you are being disingeneuous or just acting plain dumb.

Republicans waliapa kumkwamisha Obama toka siku ile anaapishwa na kuhakikisha hatapata awamu ya pili na ushahidi upo.
Mitch McConnell alisema. Kwamba, Obama awe one term president
Ajabu ni kwamba hata pale Obama alipounga mkono yaliyopendekezwa na Republicans , waliamruka. Affordable Care Act ilikuwa ni blue print ya care act ya Republicans na si walichotaka. Republicans walipoona hivyo nao wakaamua kuipinga na hicho ndicho kilichowafanya Democrats kuzinduka na kuipitisha bila Republican hata moja kuwaunga mkono.
Na hapa ndipo wengi hawana ufahamu.

GOP hawana affordable care. Wanachokifanya ni kutengeneza mbadala wa Obamacare.
Hawakuwa na sera bali kushambulia Obama care bila kitu mbadala.

Repubican hawakuwa na detailed act kwasababu Obamacare originally ni yao

Hili lina maana, Watu walipiga kura dhidi ya Obamacare bila kujua ACA ya Republican

Kitakachotokea sasa hivi baada ya watu kujiunga zaidi
1. Kufuta Obamacare na kuleta tatizo katika uchumi kama wanvyoonyesha wasomi
2. Kubakiza Obamacare katika baadhi ya vifungu na hiyo itabaki kuwa Obamacare

Nimesoma WSJ kwamba inawezekana siku 100 za kwanza hiyo act isiwe tayari
Na kwamba tayari kuna mgawanyiko Republican

Mgawanyiko unatokana na ukweli wengi waliona nafuu ya Obamacare hata kama kuna premiums zimeongezeka.Dem wanakiri , wanachosema suluhu si kubomoa ni kukarabati

Affordable care inaonekana katika mtazamo wa 'build the wall''.

Jana Trump kasema ataomba congress wasaidie kujenga ukuta tofauti na kauli yake ukuta utajengwa na Mexico. Ugumu wa ukuta ni kutokana na mandate aliyo nayo.

Kama ilivyo ACA , ukuta utasababisha matatizo yale yale kuwa sehemu ya jamii itakuwa na nguvu za kumpinga. Kupeleka ukuta congress ni kuwataka walipa kodi walipie.

Unaweza kuona jinsi mambo alivyoanza kuwa tofauti na ilivyotarajiwa.
Kwa maneno mengine ACA na ukuta anaikabidhi kwa house na senate

Yote mawili yatahitaji pesa zisizoainishwa zitapatikana wapi.

Tatizo hapa ni kuongezeka kwa deni kinyume na msingi wa GOP wa fiscal discipline

Kampeni yote national debt haikuwa 'agenda' ya Trump.

Swali , kwa gharama zinazoonekana ataweza kushawishi Republican 'spending spree'?

Hili litawagawa Republican, kuna program ya infrastructure na tax cut kama walivyoahidi

Kufanyia ACA marekebisho ni kudumisha Obamacare kitu Republican wasichokitaka
 
TAARIFA YA 'INTEL COMMUNITY'

Rais mteule Trump amekutana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama 'intelligence community'
Ni baada ya wiki takribani moja ya 'kuvisema' hadharani vyombo hivyo kwa tweets

HIilo limeumiza IC na kusema ni haki kwa Trump kukosoa,si vema kudharau(disparage)

Kauli imekuja baada ya Trump kusema ana taarifa wengi wasio nazo angezito J5 au Alhm

Trump aliyasema kwa jitihada za kitisha IC kama pre-preemptive strategy
IC ilishikilia msimamo hakukuwa na kuahirishwa kwa mkutano bali ulipangwa Ijumaa

Wiki nzima habari ikawa Russia, Trump akatumia mbinu kuondoa watu katika hoja
Kwanza, alitoa taarifa ya kupunguza mamlaka ya NSA akitaraji ingechukua uzito

Pili, zikaja 'tetesi' atabadili mabalozi waliochaguliwa na Obama, halikubadili majadiliano

Tatu, akaja na tweets akimlaumu Shwatzniger kwa rating ndogo ya apprentice
Yote aliyafanya kupunguza mjadala unaomhusu yeye na IC na jinsi alivyowadharau

Dharau kubwa ni kusema J. Assenge amesema Russia haikuhusika.
Wengi walihoji Rais wa US kusimama na Assenge na Russia dhidi ya IC yake

Hatimaye IC imekutana naye na kutoa taarifa ambayo baadhi ya maeneo ni 'classified'
Habari classified ni wanazohisi ni muhimu kuendelea kufanyia kazi na si kwa umma

Taarifa ime eleza mengi, kwamba, Russia na Putin wamehusika.
Vyama vyote vilifanyiwa hacking, kulikuwa na lengo la kumdhuru Clinton(unfair)

IC inasema wana uhakika. IC ikasema Russia walihusika ingawa impact yake kisiasa hawakufanya kwasababu si kazi yao kufuatilia mienendo ya siasa

IC imesema wazi hakukuwa na kuingiliwa kwa mfumo wa upigaji kura kwa namna yoyote

Trump ametoa taarifa Russia haikuathiri matokeo yaliyopo kwa namna nyingine yoyote

Taarifa ya mteule haikuvisema vyombo vya ulinzi ikiwa ni dalili ya kukubaliana na taarifa
Trump anasema, ataunda tume kwa ajili ya kuangalia cyber security

Kwa mnaofuatilia mjadala, kuna mambo tuliyasema ambayo sasa yanazidi kujitokeza
Tweets za Trump ni za ku divert attention, na inaonekana media imelitambua hilo

Pili, hakuna namna uchaguzi wa US ambao ni local unaweza kuwa hacked kwa ujumla
Na kwamba, tatizo linaloonekana si ushindi, bali namna uchaguzi ulivyoingiliwa

Mwisho tukasema tweets na ugomvi na IC za US hautakuwa na mwisho mzuri kwa DT

IC, inaonekana transition team imekubaliana na suala moja, Russia walihusika

Walihusika kiasi gani na impact yake ni ipi, ni suala jingine

Tusemezane
 
Mwisho tukasema tweets na ugomvi na IC za US hautakuwa na mwisho mzuri kwa DT

IC, inaonekana transition team imekubaliana na suala moja, Russia walihusika

Walihusika kiasi gani na impact yake ni ipi, ni suala jingine

Tusemezane
Uzuri wa Marekani ni kwamba hakuna mwenye uwezo wa kuzima uchunguzi unaotarajiwa kufanyika hata akiwa Rais na haijalishi huo uchunguzi unachukua muda gani. Kuhusika kwa Russia si swali tena bali impact yake katika zoezi zima la uchaguzi na bahati nzuri ushahidi wa maneno na video upo.

Transition team ya Trump inajitahidi kweli kweli kujaribu kupunguza makali ya ripoti ya IC ingawa wengi wao hawajui kwa undani kilichopo kwenye Classified Report. Kwanza Trump mwenyewe hawezi kuwapa hizo taarifa alizopewa, hivyo kwa kiwango fulani ni kwamba wanajitahidi kutetea wasichokijua.

Hata hivyo muhtasari wa Declassified report yenye kurasa 6 ambayo sasa iko mtandaoni imeweka wazi wikileaks walikuwa wanapata ripoti zao kutoka wapi. Hii ndiyo sababu hata pale ilipozimiwa mtandao bado ripoti ziliendelea kutoka na swali litakalohitaji majibu ni uhusiano wa Trump team na wikileaks.

Kwa nini Donald Trump alikuwa anakataa uhusika na Russia lakini alikuwa mwepesi sana kukiri uhusika wa wikileaks huku akiidondoa na kuisifu kwa kazi nzuri. Pamoja na kukataa uhusika wa Russia yuko kwenye rekodi akiiomba Russia ku hack na kuweka wazi Email za mpinzani wake Hillary Clinton.
 
Mimi sikubali kwamba hiyo inayodaiwa kuwa ndo hacking ya Russia imemsaidia Trump.

Kwa nini nasema hivyo?

Nasema hivyo kwa sababu ukilinganisha hizo emails ambazo inadaiwa zilipatikana kutokana na hiyo hacking halafu ukazilinganisha na mambo alokuwa anayasema na kuyafanya Trump kwenye campaign trail, hizo email zina pale in comparison.

Hizo emails ukizilinganisha na ile tape ya Trump ya ku grab them by the pussy, utaona kuwa haziko damning kabisa kama hiyo tape.

Ile tape ilipovuja ni nani ambaye hakudhani kuwa huo ndo ulikuwa msumari wa mwisho kwenye jeneza la Trump?

Trump alisema na kufanya mengi mno ambayo yako damning dhidi yake kuliko hizo emails zilizodukuliwa.

Ni kitu gani au jambo gani kwenye hizo emails ambalo hata linaweza hata kukaribiana na hiyo tape ya Trump au kile kitendo chake cha kumkejeli yule mwandishi mlemavu?

Sasa iweje emails ambazo hazikuwa damning kabisa ukizilinganisha na matendo na kauli za Trump ndo ziwe sababu ya Hillary kushindwa?

Haiwezekani hata kidogo. Hillary kashindwa kihalali kabisa na kuilaumu Urusi ni jaribio tu la kuhamisha lawama.

Hillary hakuwa mgombea mzuri. Hata mwaka 2008 yeye ndo alikuwa favorite wa kupata nomination lakini akashindwa na Obama.

Mwaka huu nao kama isingekuwa figisu za vigogo wa chama chake basi mzee Bernie Sanders alikuwa anaibuka kidedea.

Lakini kwa vile vigogo wa Democrats walikuwa wanamtaka Hillary basi ikabidi wafanye figisu ili aipate hiyo nomination.

Licha ya figisu zote dhidi ya Bernie, mzee alimchachafya kweli huyo bibi.

Kwa hiyo naamini kabisa kuwa hiyo hacking inayodaiwa, kama ni kweli ilitokea, haikuwa na athari zozote zile katika kushinda kwa Trump na kushindwa kwa Hillary.
 
Kwa nini Donald Trump alikuwa anakataa uhusika na Russia lakini alikuwa mwepesi sana kukiri uhusika wa wikileaks huku akiidondoa na kuisifu kwa kazi nzuri. Pamoja na kukataa uhusika wa Russia yuko kwenye rekodi akiiomba Russia ku hack na kuweka wazi Email za mpinzani wake Hillary Clinton.
Juzi ali tweet,wasiotaka uhusiano mzuri wa US na Russia ni 'stupid'. Hili litamsumbua sana katika uongozi

Kwanza, Republican kama akina McCain na Graham kama viongozi wanazidi kukereka
Nao wataonyesha misuli yao wakati wakiwa na 'kisu' hasa kupitisha sera

Pili, kuendeleza malumbano na IC ambao wamempa ushahidi ni kutafuta mengine

Uhusiano wake na Russia utakuwa kisiasa tu. Kiulinzi , usalama na kiuchumi vitakavyohitaji mkono wa congress vitakutana na vikwazo kwasababu tayari kuna shaka juu yake na Russia

Uhusiano mbaya kati yake na IC utafungua matatizo mengine.
IC, obvious wanachukizwa na Trump kumuamini Putin na Assange watataka ku prove him wrong.

Itachukua muda lakini lazima interest za Trump Russia zitawekwa wazi.
IC wana uwezo huo, hawataweka kama wao bali wataziacha tu zizagae au wanaweza ku leak

By the way alisema anajua mengi atayaweka wazi Jumatano au alhamisi, hakuyaweka

MKUTANO

Jumatano Trump atakuwa na mkutano na waandishi.

Kwa kumbu kumbu, utakuwa mkutano wake rasmi kwa zaidi ya siku 160, mara ya mwisho ikiwa ni July

Trump amepanga mkutano huo Jumatano, wakati Obama ana farewell speech Jumanne jioni

Hapa kuna mambo mawili
1. Kwanza, ili apate nafasi ya kujibu hoja za Obama kama itabidi.

Kwa weledi wa Obama haitarajiwi ataeleza lolote lenye utata zaidi ya kuweka rekodi yake sawa.

Hili litaleta ugumu katika kumjibu au kumshambulia.

2. Trump anataka habari za farewell speech zisivume katika media.
Njia rahisi ni kufanya mkutano baada ya hapo ili habari zake zifunike

Trump anaweza kufanikiwa kufunika habari za Obama
Tatizo ni kuwa atakutana na waandishi akiwa president elect, the stake is too high.

Maswali atakayokutana nayo hayata reflect hotuba ya Obama bali tweets zake

Ataulizwa kuhusu mambo ya dunia kwa ujumla, na mwelekeo wa serikali yake
 
"Nyani Ngabu, post: 19221375, member: 188"]Mimi sikubali kwamba hiyo inayodaiwa kuwa ndo hacking ya Russia imemsaidia Trump.
Hii ni sehemu moja ya suala zima. Sehemu ya hacking inahusu Russia kuingilia uchaguzi wa Marekani.

IC na zile za Poland na Ujerumani zimeeleza hali kama hiyo. Hivyo, hoja si kama ameshinda au la, ni involvement ya Russia na kwamba kuna interest gani.
Nasema hivyo kwa sababu ukilinganisha hizo emails ambazo inadaiwa zilipatikana kutokana na hiyo hacking ukazilinganisha na mambo alosema na kuyafanya Trump kwenye campaig trail,email zina pale in comparison.

Tape ya Trump ya ku grab them by the pussy, utaona kuwa haziko damning kabisa kama hiyo tape.Ile tape ilipovuja ni nani ambaye hakudhani kuwa huo ndo ulikuwa msumari wa mwisho kwenye jeneza la Trump?
Tape ilikuwa na mtazamo wa jamii ambao sehemu kubwa walikuwa wanawake.

Emails zilikuwa kwa mtazamo wa Democrats ambao ziliumiza Dem 'within'

Kama utakumbuka uzi wa primaries tulijadili,Trump atashinda hata GOP wakiungana

Trump alikuwa anashinda katika wastani wa 30% wengine wakigawana.

Hii maana yake alikuwa na base ya 30% isiyojali nini kinatokea bali Trump

Katikati kulikuwa na independents ambao ni 'tie breaker' ilivyo wa US

Ndani ya Democrats kuliwa na timbwili la Bernie Sanders na Clinton.

Bernie alikuwa millennial wengi waliomuunga mkono. Ilifikia mahali na kama ulivyosema ilionekana DNC walikuwa wana favour Clinton

Hiyo ilibaki 'speculation' ikiwa ina doubts miongoni mwa Millennials.

Kuvuja kwa emails kuliamsha hisia na kuonyesha mengine ambayo hayakupaswa kuwa wazi kwa public

Hapo ndipo effects ya leaking emails inapoonkena. Ddamning effects ilikuwa ndani ya Democrats na si nje. Hivyo millennial walioegemea Dem hawakupiga kura kwasababu hawakumpenda Trump, na hakupiga kura kwasababu ya hasira zao dhidi ya Clinton iliyotokana na uchaguzi ndani ya Democrats

Kwa msingi huo, Trump haku gain chochote kutoka kwa millenial wa Dem, lakini Clinton ali loose kwa millennial waliotegemea kumpa boost kama ilivyokuwa kwa Obama.

Kama utakumbuka Obama aliombwa sana kusaidia kuamsha hamasa ya Millennial kutokana na hilo

Uchaguzi ukahamia kwa independents ambapo tayari mmoja alisha lose camp mwingine hakuathirika

Kwa hesabu mmoja alipoteza na mwingine hakupata lakini hakupoteza
Trump alisema na kufanya mengi mno ambayo yako damning dhidi yake kuliko hizo emails zilizodukuliwa.
Athari si kwa Trump kwasababu katika makundi, alikuwa na kundi lisilojali amefanya nini. Walioathirika na aliyofanya ni Republican ambao siyo necessary kuwa walipigia Dem
Independents walikuwa na uwezo wa kupima athari za wote, kauli, matendo na emails
Democrats wali 'suppress' wapiga kura wao waliokuwa na shaka kuhusu process, emails zika confirm na hivyo hawakupiga kura kwa GOP na Dem, lakini aliyeathirika ni Dem
Haiwezekani hata kidogo. Hillary kashindwa kihalali kabisa na kuilaumu Urusi ni jaribio tu la kuhamisha lawama.
Kashindwa perfect and square, lakini si hoja ya hacking
IC imesema hakuna ballot box yoyote iliyoathirika na hacking.

Kuna hoja labda tujiulize. Kwanza, tusahau na to assume hakuna impact yoyote katika uchaguzi
1. Je, Russia wali hack uchaguzi?
2. Je, wali hack vyama vyote?
3. Kwanini walitoa emails za Dem peke yake?
5. Je, Russia walifanya hivyo kujifurahisha au walikuwa na sababu?
6. Malalamiko ya Ujerumani na Poland kama ya US ni ya kweli au ni uzushi?
7. Kwanini Trump hatoi evidence nyingine ku refute taarifa ya IC
8. Kwanini Trump anaamini Assenge na Russia kuliko vyombo vyake tarehe 20?
 
Hii ni sehemu moja ya suala zima. Sehemu ya hacking inahusu Russia kuingilia uchaguzi wa Marekani.

IC na zile za Poland na Ujerumani zimeeleza hali kama hiyo. Hivyo, hoja si kama ameshinda au la, ni involvement ya Russia na kwamba kuna interest gani. Tape ilikuwa na mtazamo wa jamii ambao sehemu kubwa walikuwa wanawake.

Emails zilikuwa kwa mtazamo wa Democrats ambao ziliumiza Dem 'within'

Kama utakumbuka uzi wa primaries tulijadili,Trump atashinda hata GOP wakiungana

Trump alikuwa anashinda katika wastani wa 30% wengine wakigawana.

Hii maana yake alikuwa na base ya 30% isiyojali nini kinatokea bali Trump

Katikati kulikuwa na independents ambao ni 'tie breaker' ilivyo wa US

Ndani ya Democrats kuliwa na timbwili la Bernie Sanders na Clinton.

Bernie alikuwa millennial wengi waliomuunga mkono. Ilifikia mahali na kama ulivyosema ilionekana DNC walikuwa wana favour Clinton

Hiyo ilibaki 'speculation' ikiwa ina doubts miongoni mwa Millennials.

Kuvuja kwa emails kuliamsha hisia na kuonyesha mengine ambayo hayakupaswa kuwa wazi kwa public

Hapo ndipo effects ya leaking emails inapoonkena. Ddamning effects ilikuwa ndani ya Democrats na si nje. Hivyo millennial walioegemea Dem hawakupiga kura kwasababu hawakumpenda Trump, na hakupiga kura kwasababu ya hasira zao dhidi ya Clinton iliyotokana na uchaguzi ndani ya Democrats

Kwa msingi huo, Trump haku gain chochote kutoka kwa millenial wa Dem, lakini Clinton ali loose kwa millennial waliotegemea kumpa boost kama ilivyokuwa kwa Obama.

Kama utakumbuka Obama aliombwa sana kusaidia kuamsha hamasa ya Millennial kutokana na hilo

Uchaguzi ukahamia kwa independents ambapo tayari mmoja alisha lose camp mwingine hakuathirika

Kwa hesabu mmoja alipoteza na mwingine hakupata lakini hakupoteza
Athari si kwa Trump kwasababu katika makundi, alikuwa na kundi lisilojali amefanya nini. Walioathirika na aliyofanya ni Republican ambao siyo necessary kuwa walipigia Dem
Independents walikuwa na uwezo wa kupima athari za wote, kauli, matendo na emails
Democrats wali 'suppress' wapiga kura wao waliokuwa na shaka kuhusu process, emails zika confirm na hivyo hawakupiga kura kwa GOP na Dem, lakini aliyeathirika ni DemKashindwa perfect and square, lakini si hoja ya hacking
IC imesema hakuna ballot box yoyote iliyoathirika na hacking.

Kuna hoja labda tujiulize. Kwanza, tusahau na to assume hakuna impact yoyote katika uchaguzi
1. Je, Russia wali hack uchaguzi?
2. Je, wali hack vyama vyote?
3. Kwanini walitoa emails za Dem peke yake?
5. Je, Russia walifanya hivyo kujifurahisha au walikuwa na sababu?
6. Malalamiko ya Ujerumani na Poland kama ya US ni ya kweli au ni uzushi?
7. Kwanini Trump hatoi evidence nyingine ku refute taarifa ya IC
8. Kwanini Trump anaamini Assenge na Russia kuliko vyombo vyake tarehe 20?

Yatasemwa mengi sana lakini ukweli ni kwamba:

[1] Hillary alikuwa ni mgombea mbovu. Zaidi ya jinsia yake hakuwa na jingine lolote lile la kutia hamasa. Shabaha yake kubwa ilikuwa ni kuvunja lile 'dari la kioo' na kuwa mwanamke wa kwanza kuwa rais wa Marekani. Hakuwa na jingine zaidi ya hapo.

[2] Huu ulikuwa ni uchaguzi wa mabadiliko [change election]. Mara nyingi Wamarekani huwa hawatoi mihula mitatu kwa chama kimoja. Ni jambo gumu sana. Hata Al Gore alishindwa licha ya uchumi kuwa katika hali nzuri ile mwaka 2000. Aliweza George H.W. Bush lakini matokeo yake akaja kuja kuwa rais wa muhula mmoja tu. Bush alibahatika tu kusafiria nyota ya Ronald Reagan. Hillary nafasi yake nzuri ya kushinda ilikuwa mwaka 2008. Lakini watu wa chama chake wakamkataa na kumpa uteuzi Obama ambaye hata hakuwa na tajiriba kama ya Hillary. 2016 haukuwa mwaka wa Democrats.

[3] Kwa hiyo haya mambo ya sijui udukuzi na blah blah nyingine kama hizo yamejawa na siasa mno. Dems wanayatumia kwa manufaa yao ya kisiasa katika kuyaunganisha na ushindi wa Trump na yeye anajibu mapigo. Halafu utadhani wao hawana hiyo dhambi ya kujiingiza katika mambo ya nchi zingine....Haiti, Congo, Honduras, Vietnam, na kwingineko.
 
1. Je, Russia wali hack uchaguzi?
2. Je, wali hack vyama vyote?
3. Kwanini walitoa emails za Dem peke yake?
5. Je, Russia walifanya hivyo kujifurahisha au walikuwa na sababu?
6. Malalamiko ya Ujerumani na Poland kama ya US ni ya kweli au ni uzushi?
7. Kwanini Trump hatoi evidence nyingine ku refute taarifa ya IC
8. Kwanini Trump anaamini Assenge na Russia kuliko vyombo vyake tarehe 20?

Nafikiri huu ndio unapaswa kuwa ndio msingi wa mjadala bila kujali nia halisi ya waliohusika na udukuzi ilikuwa ni kumnufaisha nani. Trump kwa nafasi yake hawezi kukubali 100% kinachosemwa na intelligence agencies wake sababu atakuwa anajikaanga mwenyewe pia.

Nilishasema kabla kwamba unless mheshimiwa Trump aje na uchunguzi mbadala utakaobaini wahusika udukuzi kuwa sio warusi basi tuhuma zilizotolewa na CIA & FBI zitaendelea kusimama. Suala la kukubaliana/kutokubaliana nao ni juu yake, pia ikiwa atachukua hatua zozote au atapotezea pia ni juu yake... lakini mwisho wa siku suala hili litaendelea kumuandama kisiasa asipochukua hatua zozote na akiendelea kupingana na intelligence agencies.

Obama ameitwa majina mengi kwamba anaunga mkono magaidi wa kiislamu, mjamaa etc kutokana na sera zake juu ya Iran, Cuba n.k. Hivyo tusishangae sana Trump naye akiandamwa na tuhuma kwamba ni puppet wa Urusi... Ndio siasa hizo!
 
Mwalimu, post: 19224548, member: 11689"]Trump kwa nafasi yake hawezi kukubali 100% kinachosemwa na intelligence agencies wake sababu atakuwa anajikaanga mwenyewe pia.
Mkuu, Trump ame miss opportunity. Tulisema hapa kuwa alichopaswa kufanya ni kukaa kimya au kuungana na wenzake kuwa kulikuwa na cyber attack na hilo ataliangalia
Jana baada ya kupata briefing za Intel community, akasema ataunda tume ya cyber security

Yaani alimalizia pale alipopaswa kuanzia. Tulijadili hili na NN.

Kinyume chake Trump akaanza malumbano na Intel community akiwa hana evidence yoyote ya ku back up madai yake.

Alichokifanya ni spinning kwamba hacking haikubadili matokeo

Hoja hiyo ilipoteza mashiko pale ambao Dem, Rep, media na Intel comm zote ziliposema ameshinda kwa kura na hakuna wizi katika upigaji.

Akabadili na kusema wanataka ku delgitimize urais wake

Hoja ikafa kwamba, ameshinda ndiye pres elect na hakuna wizi ni legit pres elect

Mwisho akaanza tweets za ku denigrate intel community.

Hapo ndipo walipokaa sawa kwani walijua kosa moja tu atalitumia vema.

Wamempa hadi go between wa Russia na Assenge anaowaamini

Bado ana tweet wanaotaka mahusiano mabaya ni stupid hata baada ya evidence zote

Sasa hivi ana 'vita' na intel community, Republican achilia mbali adversary wake Dem

Unaweza kuona alivyo drag na poor handling itakavyo mgharimu siku zijazo
Trump aje na uchunguzi mbadala utakaobaini wahusika udukuzi kuwa sio warusi basi tuhuma zilizotolewa na CIA & FBI zitaendelea kusimama
Uchunguzi mbadala alisema Jumatano au Alhamisi. Kumbe alisubiri mahojiano ya Assenge na Fox akidhani atapata mahali.
Hana evidence ya kukabiliana na hoja za 16 security agencies ambazo unanimously zimeafiki kuwa ipo hacking na ilitoka Russia na imefanyika sehemu nyingine pia.
Obama ameitwa majina mengi kwamba anaunga mkono magaidi wa kiislamu, mjamaa etc kutokana na sera zake juu ya Iran, Cuba n.k. Hivyo tusishangae sana Trump naye akiandamwa na tuhuma kwamba ni puppet wa Urusi... Ndio siasa hizo!
Obama ni smart sana.

Kila alichofanya alikuwa na majibu tayari

Iran, aliuliza wenye mbadala wauweke hadharani.

Hakuna aliyekuwa nao na in fact wengine wanakubaliana naye.

Kilichotokea na hasa Trump alisema deal ya Iran Obama alitoa pesa cash

Ukweli ni kuwa pesa za Iran zilikuwa zimezuiliwa na suala hilo lilifika mahakama za dunia

Kuendelea kukaa nazo ni kuongeza interest kwasababu mwisho wa siku watalipa

Akatumia nafasi kuibana Iran, kwa kamba waliyokuwa nao Iran na kuwatia kitanzi

Cuba: Obama ameeleza sanction zipo miaka 50 na ushee, nini kipya kimetokea?

Uhusiano wake na Cuba ni approach mpya ya kuingia Cuba na kufanya instigation
Ndivyo US walivyofanya mataifa mengi.

Obama hatakuwepo lakini 20 yrs to come outcome itaonekana. USSR haikuanguka na Reagan,ilianza mika mingi Ronald akamalizia tu

Ujamaa: Walimtuhumu sana, akuliza ni nchi gani ya kibepari iliyofanya tofauti na yeye

Obamacare: Hadi jana aliuliza, kama Obamacare ni mbaya mbadala upo wapi?
Sote tunajua Trump hana na Republican wanahangaika kutengeneza sasa hivi

Kwahiyo kuna tofauti ya u-smart kati ya wawili hao katika hatua za mwanzo tu.

Tofauti zitaendelea kujadiliwa kutokana na maamuzi ya Trump , anaweza kufanya vizuri au vibaya hilo ni suala lisiloweza kujadilika akiwa hana power.

So far bado anajifunza. Vita na intel community itamweka pagumu

Maamuzi yote yataangaliwa kwa jicho la shaka sana na hilo litakuwa tatizo
Wiki hii wanaanza confirmation ya cabinet.
 
Trump Akubali Urusi Ilifanya Udukuzi.

Rais Mteule wa marekani Donald Trump ameikubali ripoti ya ujasusi kwamba Urusi ilihusika katika mashambulizi ya mitandao yaliyolenga kuvuruga uchaguzi wa Marekani.

Mkuu mtarajiwa wa shughuli za ikulu katika serikali ya Trump Reince Priebus amesema na kuongeza huenda hatua zikachukuliwa.

Akizungumza na shirika la habari la FOX siku ya Jumapili, Priebus amesema Trump anakubali kuwa kuhusu hoja hii, ni taasisi za Urusi ambazo zilihusika na uingiliaji huo wa mpangilio na shughuli katika chama cha Democratic.

Priebus amesema Trump anapanga kuziagiza taasisi za ujasusi kutoa mapendekezo ya kuhusu kile kinachostahili kufanywa. Kwa kutegemea mapendekezo hayo, hatua zinaweza kuchukuliwa.

Lakini timu ya mpito ya Donald Trump imekilaumu chama cha Democratic kwa kuruhusu anwani za barua pepe zao zao kudukuliwa. Timu hiyo imepuuzilia mbali ripoti za mashirika ya ujasusi kwamba Urusi iliingilia mchakato wa uchaguzi.

Naye Rais Barrack Obama amekiri kuwa hakutiilia uzito athari ambazo habari potofu za udukuzi zinaweza kuhujumu demokrasia ya nchi, kauli inayojiri baada ya ripoti ya ujasusi kuhusu hatua ya Urusi kuingilia kati uchaguzi wa Marekani.

Akihojiwa na shirika la habari la ABC, Obama amemtahadharisha mrithi wake anayechukua hatamu za uongozi katika muda wa wiki mbili zijazo Donald Trump kuhusu tofauti kati ya kampeni na utawala, huku akisema rais mteule hataendesha urais kama anavyoendesha biashara ya kinyumbani.

Mahojiano hayo ya Obama yalirekodiwa Ijumaa. Siku ambayo pia shirika la ujasusi lilitoa ripoti mpya iliyosema kuwa Rais wa Urusi Vladimir Putin aliagiza kampeni ya udukuzi kufanywa na kuzifichua taarifa za siri na porojo kupitia vyombo vya habari kwa lengo la kumhujumu aliyekuwa mgombea wa urais wa chama cha Democratic Hillary Clinton.

Trump akubali Urusi ilifanya udukuzi | Matukio ya Kisiasa | DW.COM | 08.01.2017
 
Trump Akubali Urusi Ilifanya Udukuzi.

Rais Mteule wa marekani Donald Trump ameikubali ripoti ya ujasusi kwamba Urusi ilihusika katika mashambulizi ya mitandao yaliyolenga kuvuruga uchaguzi wa Marekani.

Akizungumza na shirika la habari la FOX siku ya Jumapili, Priebus amesema Trump anakubali hoja hii, ni taasisi za Urusi ambazo zilihusika na uingiliaji huo wa mpangilio

Timu hiyo imepuuzilia mbali ripoti za mashirika ya ujasusi kwamba Urusi iliingilia mchakato wa uchaguzi.
Mkuu hii taarifa umeona inavyojichanganya?
 
Mkuu hii taarifa umeona inavyojichanganya?
Hata mimi nilipata walakini, kwamba Trump amekubali ripoti ya IC lakini timu ya mpiti inapinga taarifa za Urusi kuingilia uchaguzi.
May be Mwandishi anamaanisha timu ya Trump ilipinga kabla Trump hajakutana na IC
 
Hata mimi nilipata walakini, kwamba Trump amekubali ripoti ya IC lakini timu ya mpiti inapinga taarifa za Urusi kuingilia uchaguzi.
May be Mwandishi anamaanisha timu ya Trump ilipinga kabla Trump hajakutana na IC
Mkuu ukimfahamu Trump, utaelewa kwanini anafanya hivyo

Alisema ana ushahidi atautoa kwasababu wengi hawajui.

Ushahidi hakuwa nao alichokuwa anasubiri ni Assenge aseme ili naye adakie
Hapa alikwenda chini sana, kwamba, Assenge anajua zaidi ya intel comm zake!

Hoja yake ni kuwa urusi haikuingilia wala kubadili matokeo.
Anachotaka ni hoja ibaki hapo

IC imemueleza wazi kuwa hakuna kura iliyobadilishwa au kuibiwa.
Wakasema hawafanyi tathmini ya mwenendo wa siasa za Marekani

Walichokifanya ni kutafuta ukweli ikiwa Urusi iliingilia.

Wakampa Trump kila aina ya ushahidi alioutaka
Huko nyuma Trump alisema mbona hawaweki ushahidi

Baada ya briefing Trump akasema ataunda cyber security team.
Kwa maana ya kuwa amekubaliana na Intel community.

Transition team ikasema uchaguzi haukuvurugwa,kuondoa watu ktk hoja ya Russia

Hapa anacheza na akili za watu na kwakweli ni mtaalam

Ni mtaalam, jana ametangaza Kushner kuwa mshauri wa WH na Ivanka ku resign Trump org.

Matangazo hakuyatoa kwa bahati mbaya , yalikuwa ni timing kama ambavyo tweet zimekuwa

Alichotaka ni kuondoa media katika ''confirmation hearing'' watu wake wanatiliwa mashaka

Yupo Secession aliyeahi kunyimwa ujaji. Yupo Tillerson ambaye uhusiano wake na Russia una utata n.k

Hivyo alitaka kuondoa media katika hilo na alifanikiwa.Habari za jana zilikuwa juu ya Kushner na Ivanka.
 
Mkuu ukimfahamu Trump, utaelewa kwanini anafanya hivyo

Alisema ana ushahidi atautoa kwasababu wengi hawajui.

Ushahidi hakuwa nao alichokuwa anasubiri ni Assenge aseme ili naye adakie
Hapa alikwenda chini sana, kwamba, Assenge anajua zaidi ya intel comm zake!

Hoja yake ni kuwa urusi haikuingilia wala kubadili matokeo.
Anachotaka ni hoja ibaki hapo

IC imemueleza wazi kuwa hakuna kura iliyobadilishwa au kuibiwa.
Wakasema hawafanyi tathmini ya mwenendo wa siasa za Marekani

Walichokifanya ni kutafuta ukweli ikiwa Urusi iliingilia.

Wakampa Trump kila aina ya ushahidi alioutaka
Huko nyuma Trump alisema mbona hawaweki ushahidi

Baada ya briefing Trump akasema ataunda cyber security team.
Kwa maana ya kuwa amekubaliana na Intel community.

Transition team ikasema uchaguzi haukuvurugwa,kuondoa watu ktk hoja ya Russia

Hapa anacheza na akili za watu na kwakweli ni mtaalam

Ni mtaalam, jana ametangaza Kushner kuwa mshauri wa WH na Ivanka ku resign Trump org.

Matangazo hakuyatoa kwa bahati mbaya , yalikuwa ni timing kama ambavyo tweet zimekuwa

Alichotaka ni kuondoa media katika ''confirmation hearing'' watu wake wanatiliwa mashaka

Yupo Secession aliyeahi kunyimwa ujaji. Yupo Tillerson ambaye uhusiano wake na Russia una utata n.k

Hivyo alitaka kuondoa media katika hilo na alifanikiwa.Habari za jana zilikuwa juu ya Kushner na Ivanka.
Nguruvi3, leo vyombo vingi vya habari vimejikita katika mahojiano ya mteuliwa wa Trump kwa nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jeff Sessions na Senate Judiciary Committee. Hata hivyo yaliyokuwa yakiendelea kwenye mkutano wa Senate Intelligence Committee na IC, yamezua maswali yanayoweza kuleta sintofahamu kubwa mbele ya safari. Donald Trump akae chonjo!
 
Nguruvi3, leo vyombo vingi vya habari vimejikita katika mahojiano ya mteuliwa wa Trump kwa nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jeff Sessions na Senate Judiciary Committee. Hata hivyo yaliyokuwa yakiendelea kwenye mkutano wa Senate Intelligence Committee na IC, yamezua maswali yanayoweza kuleta sintofahamu kubwa mbele ya safari. Donald Trump akae chonjo!
Ndiyo habari hiyo niliifuatilia kwa muda kupata undani wake ili tujadiliane jamvini

''TIMU YA TRUMP ILISHIRIKIANA NA RUSSIA''
Kwanza,Trump ame tweet ' hakuna lolote ni kutafuta mchawi kisiasa' kwa tafasiri isiyo rasmi

Ni kufuatia inafuatia habari zinazovuma katika media kuwa Russia na surrogates (wa kampeni yake) walikuwa na mawasiliano

Majuzi tuliwaeleza IC ilikuwa ina andaa taarifa mbili, declassified na classified
Classified ilifikishwa kwa Obama na Trump. Declassified ikawa public

Mtakumbuka tulisema ugomvi wa Trump na IC si mzuri kwani watata kum- prove wrong
Trump aliwakejel hawana ushahidi, kisha akasema wanatengeneza kesi

IC iliandaa taarifa ikiwa na ushahidi wa 'Russia'wakishangilia ushindi wa Trump

Katika taarifa, waliambatanisha kurasa za ushahidi wa timuTrump 'walivyoshirikiana'

IC wanasema kurasa kwa mujibu zimewasilishwa kwa wote wawili

IC inafuatilia kwa undani habari hizo zinazoshabihiana sana na walizo nazo

Ni sehemu ya classified info zilizo leak katika media.Wanasema hakuna siri Washington'

MKASA ULIVYO

Shirika moja la Russia lilikuwa linafanya uchunguzi wa biashara za Trump Russia

Mmoja wa wachunguzi akakutana na habari ya uhusiano wa timu ya Trump na Russia

Habari akazifikisha kwa mtaalam mzoefu wa M16 ya Uingereza aliyezifuatilia kwa ukaribu

Baada ya kupata ushahidi aliwasiliana na balozi wa zamani wa Uingereza nchini Urusi

Balozi naye akawasiliana na John McCain.
Senta McCain aktuma mtu kuona na huyo wa M16 na taarifa za uchunguzi akaletewa.

McCain akakutana na FBI Director Comey kwa dakika 5 na kumkabidhi

Hii ilikuwa kabla ya uchaguzi, Comey akasema hilo litaingilia uchaguzi liachwe kwanza

Mtakumbuka tulisema kwanini Comey alitoa taarifa za email za Clinton na kama hilo halitaingilia uchaguzi? Hapa unaweza kuona 'double standard'

Huo ndio ukawa mwanzo wa taarifa hizo kufika IC na katika seneti na Bunge

Wakuu wa (IC), DNI,CIA, FBIA, NSA kwa pamoja walikutana na Obama na Trump na kuwapa taarifa ya hacking ya Russia na pages

Tuwarudishe nyuma kidogo, tuliwahi kusema McCain na Senta Graham walikuwa wanajiamini sana. Sasa tunajua, kujiamini kulikuwa na sababu za 'data' za kutosha

Ndiyo maana Spika Ryan na VP Pence walikubali Russia walikuwa wanaingilia uchaguzi

Majina ya wahusika wa uchunguzi yapo ingawa media zimekataa kutoa kwa usalama

Tweet ya mstari wa kwanza ya Trump inaeleza hali ilivyo kwa upande wake.

Katika mazingira ya kawaida Trump angeandika ya kutosha.

Sasa anasema anatafutwa mchawi wapiga debe wakishindwa kukanusha au kutihibitisha

Picha inaanza kujionyesha kwanini Trump hakupenda uchunguzi akisema wanataka ku delegitimize Urais wake.

Kwa hili la timu yake kuhusika, kama litathibitishwa atakuwa ame ji legitimize mwenyewe

Tusemezane
 
Ndiyo habari hiyo niliifuatilia kwa muda kupata undani wake ili tujadiliane jamvini

Picha inaanza kujionyesha kwanini Trump hakupenda uchunguzi akisema wanataka ku delegitimize Urais wake. Kwa hili la timu yake kuhusika, kama litathibitishwa atakuwa ame ji legitimize mwenyewe
Mkuu Nguruvi3, hizi habari hata Seneta Reed alikuwa amezidaka na ndio maana kuna wakati aliongea kwa uchungu sana dhidi ya Trump. Katika post yangu # 427 nilidokeza tu kwamba Team Trump wengi hawajui hata kile wanachotetea lakini hii habari ni nzito kweli kweli. Kesho ni kesho labda Trump aahirishe conference yake na waandishi.
 
Ndiyo habari hiyo niliifuatilia kwa muda kupata undani wake ili tujadiliane jamvini

''TIMU YA TRUMP ILISHIRIKIANA NA RUSSIA''
Kwanza,Trump ame tweet ' hakuna lolote ni kutafuta mchawi kisiasa' kwa tafasiri isiyo rasmi

Ni kufuatia inafuatia habari zinazovuma katika media kuwa Russia na surrogates (wa kampeni yake) walikuwa na mawasiliano

Majuzi tuliwaeleza IC ilikuwa ina andaa taarifa mbili, declassified na classified
Classified ilifikishwa kwa Obama na Trump. Declassified ikawa public

Mtakumbuka tulisema ugomvi wa Trump na IC si mzuri kwani watata kum- prove wrong
Trump aliwakejel hawana ushahidi, kisha akasema wanatengeneza kesi

IC iliandaa taarifa ikiwa na ushahidi wa 'Russia'wakishangilia ushindi wa Trump

Katika taarifa, waliambatanisha kurasa 35 za ushahidi wa timuTrump 'walivyoshirikiana'

IC wanasema kurasa 35 kwa mujibu zimewasilishwa kwa wote wawili

IC inafuatilia kwa undani habari hizo zinazoshabihiana sana na walizo nazo

Ni sehemu ya classified info zilizo leak katika media.Wanasema hakuna siri Washington'

MKASA ULIVYO

Shirika moja la Russia lilikuwa linafanya uchunguzi wa biashara za Trump Russia

Mmoja wa wachunguzi akakutana na habari ya uhusiano wa timu ya Trump na Russia

Habari akazifikisha kwa mtaalam mzoefu wa M16 ya Uingereza aliyezifuatilia kwa ukaribu

Baada ya kupata ushahidi aliwasiliana na balozi wa zamani wa Uingereza nchini Urusi

Balozi naye akawasiliana na John McCain.
Senta McCain aktuma mtu kuona na huyo wa M16 na taarifa za uchunguzi akaletewa.

McCain akakutana na FBI Director Comey kwa dakika 5 na kumkabidhi

Hii ilikuwa kabla ya uchaguzi, Comey akasema hilo litaingilia uchaguzi liachwe kwanza

Mtakumbuka tulisema kwanini Comey alitoa taarifa za email za Clinton na kama hilo halitaingilia uchaguzi? Hapa unaweza kuona 'double standard'

Huo ndio ukawa mwanzo wa taarifa hizo kufika IC na katika seneti na Bunge

Wakuu wa (IC), DNI,CIA, FBIA, NSA kwa pamoja walikutana na Obama na Trump na kuwapa taarifa ya hacking ya Russia na hizo 35 pages

Tuwarudishe nyuma kidogo, tuliwahi kusema McCain na Senta Graham walikuwa wanajiamini sana. Sasa tunajua, kujiamini kulikuwa na sababu za 'data' za kutosha

Ndiyo maana Spika Ryan na VP Pence walikubali Russia walikuwa wanaingilia uchaguzi

Majina ya wahusika wa uchunguzi yapo ingawa media zimekataa kutoa kwa usalama

Tweet ya mstari wa kwanza ya Trump inaeleza hali ilivyo kwa upande wake.

Katika mazingira ya kawaida Trump angeandika ya kutosha.

Sasa anasema anatafutwa mchawi wapiga debe wakishindwa kukanusha au kutihibitisha

Picha inaanza kujionyesha kwanini Trump hakupenda uchunguzi akisema wanataka ku delegitimize Urais wake.

Kwa hili la timu yake kuhusika, kama litathibitishwa atakuwa ame ji legitimize mwenyewe

Tusemezane

The whole thing has been shot down.

It was fake news.

How BuzzFeed crossed the line in publishing salacious ‘dossier’ on Trump
 
Back
Top Bottom