a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,397
- 1,358
Nilishawahi kusema humu kuwa, Huu si Wakati wa Mivutano isiyokuwa ya lazima, aina ya serikali iliyopo ni Mtaji bora kuwahi kupata, ila tu Akili kubwa inahitajika.Mkuu Nguruvi3 na wengineo
Tatizo kubwa linalotukabili Tanzania sasa hivi ni kuangalia kila jambo kwa mizani ya kisiasa ya SISI vs WAO, CCM vs UKAWA n.k.
Inawezekana kabisa Mheshimiwa Rais anaona kwamba Makonda amevurunda lakini akiangalia wapiga filimbi wakubwa ni kina Gwajima, Tundu Lissu na Mange Kimambi! Hapo ndipo kigugumizi kinapoanza kwamba akimtumbua Makonda itaonekana amefanya kwa shinikizo la wapinzani wake... kitu ambacho hayuko tayari kukubali! Shida kubwa iko hapo... EGO!
Moja ya madhaifu makubwa ya mheshimiwa ni kujawa na roho ya kiburi, pride, ego na kumchukulia kila anayempinga ama kumkosoa kuwa ni adui na anamkwamisha kutekeleza kazi yake. Kila mwenye mawazo tofauti na yeye moja kwa moja anachukuliwa kwamba ni adui. Ndio maana kwa mfano aliwatamkia wanasheria wanaotetea watuhumiwa kuwa nao watashughulikiwa!
Ndio maana jana amesema kwamba hafanyi kazi kwa kushinikizwa na "mitandao"... sio kwamba hajui kwamba kuna tatizo la hasha! Bali ni "pride" na "ego" iliyopo kuona kwamba atakuwa anajishusha kwa kusikiza ushauri kutoka kwa malofa wa mitandaoni. Ingawa kwa upande mwingine yeye mwenyewe ameonesha kuwa ni mshabiki wa mambo hayo hayo ya udaku (shilawadu)!