Duru za Siasa: Awamu ya 5 - Uongozi na Yanayojiri

TUANGALIE MAELEZO YA Mh WAZIRI KUHUSU MFUMO

Kwa hisani ya gazeti la Mwananchi
Serikali yafuta GPA katika elimu, yarejesha divisheni

Waziri wa elimu anaeleza NECTA ilivyoshindwa kuja na majibu ya GPA.
Anasema baadhi ya watahiniwa wa GPA wanaonyesha kiwango kidogo kuliko GPA zinavyoonyesha.

Hoja hii inathibitisha kauli yetu kuwa, GPA iliwekwa kufunika uchafu kwa kutumika kisiasa

Waziri anaendelea , NECTA walimweleza kuingia katika mfumo huo kunatokana na hoja za wadau.
NECTA ikashindwa kuthibitisha ni wadau wapi na katika mikutano au mikusanyiko gani

Hapa inaonyesha NECTA inadanganya. Hiki ni chombo kinachosimamia elimu, moyo wa Taifa lolote

Chombo hiki kinapokuwa cha kibabaishaji inatia hofu na ni hatari kama waziri alivyosema pia.

Waziri ameendele kusema, mfumo huo haukupitia kwa kamishna wa elimu kupata kibali.
Maagizo ya serikali yanasema kila kitu kianze kutumika JUNI 2016

Tunaona ushiriki wa serikali kwa kutoa siku ya kuanza kutumika mfumo.
Wakati kamishna hakutoa kibali, haieleweki serikali ilitoa vipi agizo

Waziri anasema kanuni za mitihani zilipitishwa miaka 2 baada ya kuanza kutumika utaratibu wa GPA

Kanuni zilipitishwa na waziri Oktoba 28,2015 (kipindi cha uchaguzi) na kuingizwa katika gazeti la serikali November 6, siku ambayo Rais Mpya alikuwa na siku 1 tu ofisini

Tunachokiona ni mfumo mbaya, si wa elimu ni wa ujumla. Baraza la mawaziri linapaswa kuvunjwa isipokuwa kwa dharura tu. Waziri anapopitisha kanuni Oktoba 28,2015 kura zikihesabiwa kuna tatizo.
Yaani waziri alikuwa kazini hadi uchaguzi ulipomalizika

Kwa maneno mengine, kuna uwezekanO alifanya hivyo kwa shinikizo la watu.
Elimu na mitaala au mitihani si suala la dharura, kwanini waziri afanye yote akijua huenda asingerudi?

Kitu tunachopaswa kuelewa ni jinsi ambavyo maelezo ya waziri yanavyochanganya.

Kuna maeneo anaitetea serikali, na maeneo mengine serikali ikionekana kushiriki.

Hivyo, tunaweza kusema NECTA walifanya kazi na serikali ina a way, ingawa wadau wakuu kama kamishna wa elimu hawakushirikishwa

Haya yanatokea kwa sababu hatuna mfumo mzuri wa utawala,inaonekana wazi katika sakata la elimu

Mambo yanafanyika gizani kiasi cha waziri kutoweza kuelewa Ilikuwaje, hawezi ku trace nini kilifanyika

Lakini pia waziri aliambatana na Mkurugenzi wa NECTA. Akiwa naye, mh alisema maelezo aliyopewa NECTA kuhusu GPA yalikuwa ya bla bla.

Maana yake maeelezo ya mkurugenzi hayakumridhisha bali ubabaishaji
Laiti waziri angekuwa na nguvu juu wa mkurugenzi, pengine asingetokea naye kwenye mkutano

Mkurugenzi anateuliwa na chombo kingine hivyo waziri hana la kufanya isipOkuwa kushauri tu

Mfumo unakwaza viongozi kiutendaji. Ni kama ule wa Bandari tulioona watu Zaidi ya 4 wanateuliwa na mamlaka moja wakiwajibika kwa mamlaka hiyo na kila mmoja kuwa 'bosi' kivyake

Hili la elimu linaeleza wazi kuhusu mfumo. Tunarudia, kama waziri ambaye alikuwa Mkurugenzi wa NECTA miaka miwili iliyopita haelewi nini kimetokea, nani nje ya system anayeweza?

Je, Watanzania hatuoni tatizo letu kama mfumo na si mtu au watu?

Taasisi zinafanya kazi bila kujua moja infanya nini. Maamuzi yanapitishwa kisiasa, wengine kutoshirikishwa pengine kwa hofu ya 'ukaidi'.

Serikali iliridhia vinginevyo kwanini itangaze jambo isilokubaliana nalo?

Tutaendelea...
Bandiko hili #69 na #52 tumeongeelea tatizo la mfumo wa elimu analokumbana nalo Waziri wa elimu Mh Ndalichako

Jambo moja tunalikubaliana kama taifa ni kuwa mfumo wetu wa elimu una matatizo
Ukubwa wa tatizo umeongezeka awamu ya nne ambapo mambo mengi yamefanyika kienyeji

Bila shaka kazi aliyo nayo waziri wa elimu ni kubwa na ngumu na huenda inapelea yeye kuwa kiongozi wa hoja zenye utata 'controversy' kila mara

Waziri Ndalichako'anashambuliwa' bila kuonyeshwa mbadala au mapungufu ya hoja zake

Sehemu ya tatizo analitengeneza mwenyewe hasa kwa matamko yake kama amri

Akiwa waziri ana nafasi ya kutoa amri, lakini asisahau nafasi yake ya kiongozi wa umma

Sifa ya kiongozi wa umma ni kusikiliza, kujadiliana, kutoa hoja kwa facts na si matamko

Tatizo la pili linalomkumba Mh waziri ni kuvutika katika migogoro ya kisiasa

Ni mwanataaluma akiwa na nafasi ya siasa. Zipo sehemu siasa haichukui nafasi ya taaluma

Tunasema haya kwasababu kuu mbili.

Kazi ya kujenga mfumo mbovu ni ngumu na hatutegemewi awe malaika kwa usahihi.

Lakini pia yapo anayosimamia ambayo kwa mtazamo ni sahihi na anayopotoka

Ni kwa msingi huo, tutapitia hoja na matamko yake kwa ukaribu

MITIHANI YA BAADHI YA TAASISI BINAFSI NA UMMA KURATIBIWA NA NECTA

Moja ya hatua nzuri za Mh Waziri ni kuahakikisha mitihani kwa baadhi ya taasisi inaratibiwa na chombo kimoja.

Kwamba NECT itapima watahaminiwa wa taasisi binafasi na zile za umma

Tukumbuke, soko huria lilifungua milango na elimu ni sehemu mojawapo.

Kwa muda mfupi kulizuka vyuo na taasisi zinazotahini wanafunzi kisha kutunuku vyeti

Taasisi binafsi zinatoa elimu kwa utaratibu wa biashara.

Ubora ambalo ni la kwanza, hupewa umuhimu wa pili baada ya biashara kufanyika.

Tumekuwa na matatizo ya watahiniwa waliopata vyeti katika mazingira ya kusikitisha

Kitendo cha kuamua watahaniwa wapimwe kwa chombo kimoja kama NECT ni kizuri sana

Hili linapima ubora na kupora nguvu za ''biashara'' kwa wafanyabishara ya elimu

Ingawa baadhi ya watu hawakufurahia, jambo hili ni la kuungwa mkono na kupongezwa.

Tunahitaji ubora katika elimu si mchezo wa biashara katika suala nyeti na muhimu kama elimu kwa Taifa

Inaendelea...
 
''KUSHAMIRI'' KWA VYUO VIKUU

Katika kipindi cha miaka 10 Taifa limekuwa na vyuo kuliko awamu tatu kwa mfululizo

Katika kipindi hicho idadi ilifikia 50 kwa vile vya umma na binafsi

Kama tulivyoeleza awali, mfumo wa soko huria ulichukuliwa huria katika maeneo nyeti

Awamu ya pili iliyofungua soko huria ilikuwa makini, kama ilivyokuwa awamu ya tatu

Vyuo holela vilishamiri awamu ya 4, na kushindwa kutofauti high school na University

Ubora wa baadhi ya vyuo hasa binafsi ni wa kutilia shaka kila eneo

Tatizo lilianzia wapi?

1. Serikali:
Haikuwa na mipango madhubuti ya elimu kuanzia ngazi za chini.
Kukawa na ongezeko la wanafunzi wanaohitaji elimu ya juu kwavile hakukuwa na maandalizi ya muda mfupi na mrefu. Kilichotokea ni mambo ya zimamoto

Tatizo hii lilitengenezwa na siasa kutawala utaalam.
Kwamba, wanasiasa walichotaka ni idadi ya vyuo na wanafunzi ili kujenga hoja ya maendeleo bila kujali ubora wa elimu na wahitimu wake

2. TCU:
Tume ya vyuo yenye jukumu la kutathmini/kusimamia ubora wa elimu ikawa njia panda

Kwanza, inaongozwa na maamuzi ya wanasiasa, utaalam haukuwa sifa au muhimu tena

Pili, wahadhari wa vyuo vikongwe wakaona huo ni mradi wa kupata part time
Wakasimama kidete dhidi ya tume na serikali ili mradi wao wa 'pembeni' uwe endelevu

Kwa pamoja, wanasiasa na wahadhiri wakapoka nguvu za TCU kusimamia uanzishwaji na ubora wa elimu inayotolewa.

Tukafika mahali ambapo mwanafunzi aliyemaliza chuko kikuu ni mhadhiri katika majengo yaliyopakwa rangi na maua na mti wa bendera nje. Ni chuo kikuu!

3. Mashirika na wafanya biashara wakatumia udhaifu wa serikali na wanataaluma kuanzisha vyuo hata kupanga namna gani wanataka wanafunzi wafaulu biashara iwe endelevu

Hatua za Mh Waziri kufunga vyuo visivyo na sifa ni ya kuungwa mkono
Hatuhitaji lundo la wenye degree zisizo na ubora.

Tunahitaji wahitimu watakaoshindina katika soko la dunia katika mazingira yetu kwa ubora ule ule unaopatikana kwingine.

Tunahitaji vyuo kama centre for excellence na si mkusanyiko wa wanafunzi

Zoezi halifurahiwi na baadhi yakiwemo mashirika , wafanyabiashara na wahadhiri

Ni zoezi la maana kwa muskabali wa taifa letu, inasikitisha waziri akipingwa kwa hili

Je wapi waziri amekosea?

Na nini mbadala wake kwa haya tunayoona ambapo chuo kikuu cha afya hakiwezi kutunza afya za wananchi kwa kutupa 'vitu nyeti' hovyo kama tulivyoona kule Mbezi?

Kwanini chuo kama hicho kiendelee kuwepo? Chuo hicho kinatoa elimu gani?

Inaendelea
 
'UTATA' WA WAZIRI WA ELIMU

Pamoja na mazuri mengi na ugumu anaokutana nao, waziri wa elimu amekuwa na mambo tata

ADA ELEKEZI
Waziri amekuwa katikati ya mgogoro wa shule moja binafsi kuhusu madai ya wazazi ya ada kubwa
Hilo nalo limekuwa na utata kwingine, shule binafsi zikiwa na ada 'elekezi'

Kama tulivyoeleza, soko huria lilifungua elimu katika huria kama masoko ya huduma na bidhaa nyingine
Elimu ikawa huduma inayolipiwa kama huduma za afya, bima , benki n.k.

Wajibu wa serikali ni kuweka mitaala, kusimamia utoaji wa elimu pamoja na kutathmini

Kwanini mzazi anapeleka mtoto shule ya kulipia, hilo linabaki kuwa tatizo la mzazi na si serikali

Mzazi asiymudu gharama za elimu ana wajibu wa kutafuta eneo jingine litakalokidhi haja yake

Kulalamika ada ni ya juu ni sawa na kulalamika bima ya magari au huduma za afya ni za juu

Kwa upande wa waziri, suala si kutoa ada elekezi bali kujiuliza kwanini shule binafsi zinakithiri.

Jibu jepesi ni kuwa elimu katika shule za sekondari imeshuka.

Idadi ya wanafunzi, vitendea kazi duni, walimu hakuna au waliopo ni duni n.k.

Kuimarisha shule za umma kutaleta ushindani kwa shule binafsi
Ushindani utakwenda sambamba na utoaji wa huduma zinazolingana na ubora na gharama halisi

Njia ya pili ni kuacha bei ya soko iamue.
Ushindani utatokea miongoni mwa wamiliki wa shule binafsi na hiyo iTasaidia kupunguza gharama

Fikiria wakati wa Mobitel inaanza, simu ya mkononi ilikuwa kitu cha watu wenye uwezo.
Serikali haikupanga bei elekezi, iliacha other players kuingia.

Kwa muda gharama zikapungua kiasi cha watu wengi kumudu.
Hata hivyo, kama mashirika zaidi yatarhusiwa, gharama zitakwenda chini zaidi ya sasa

Waziri hapaswi kuwa katikati ya mgogoro wa wazazi na wamiliki.
Anachotakiwa kufanya ni kutengeneza mazingira mazuri ya ushindani.

Kwanza, kuimarisha shule za umma katika ubora na unafuu
Pili, kujenga mazingira ya washindani wengine kuingia katika sekta ya elimu
Tatu, kusimamia sera ya taifa ya elimu kuanzia ufundishaji hadi kutahini

Kuingia katika mgogoro ni kutafuta utata usio na ulazima.

Inaendelea...
 
UTATA WA WAZIRI

VYUO VYA CHINI, KATI NA VYUO VIKUU

Waziri alinukuliwa akisema wanaosoma kada za chini na kati hawawezi kwenda kusoma University
Kauli ilileta utata ingawa ilifafanuliwa waziri alinukuliwa vibaya

Kwa vyovyote itakavyokuwa kuna umuhimu wa kueleza kwanini suala hili lina utata

1.Uwepo wa kada za kitaaluma

Kuna sababu za msingi za kada mbali mbali kuwa na viwango vya wataalam kwa ngazi tofauti

Hili ni suala lililopo duniani kote kuanzia nchi zilizoendelea hadi nchi masikini. Kuna sababu

a)Mgawanyo wa kazi kulingana na kada husika

Katika serikali, taasisi, mashirika, NGO au makampuni kuna viongozi wa juu mfano wa CEO

Wawe ni wataalam wa fani husika au la, kazi yao ni kutengeneza mazingira ya kazi pamoja

Kutoa maamuzi mazito yanayohusu kazi, na kuwa viungo kati ya maeneo yao na mengine

Hapa tutoe mfano rahisi kueleweka. Kazi ya CEO wa kampuni ya ujenzi ni kutafuta fursa au kupokea fursa na kuzifanyia tathmini. Kazi hii husaidiana na wenzake katika ngazi za juu 'management'

Hivyo kazi yaCEO ni kuhakikisha fursa iliyopo inatengenezewa mazingira mazuri na management.
Kazi ya kuiweka management pamoja ni yake.

kuanzia hapo management inatumia wataalam kutathmini, kupanga mikakati kwa kuwatumia wataalam

Kwa wataalam hapo utakuta Architect, Civil Engineer, structural engineer, Energy, communication, transportation, watu wa drainage, buiding materials, accountants n.k. orodha inaendelea

Kundi hili lina wataalam wanaoweza kutoa tathmini, kutafsiri na kutafuta njia mbadala kufikia malengo
Wana uwezo wa kueleza na kujenga hoja za kitaalam

Itafuta kada nyingine kama ya Technicians wenye majukumu yao wakisimamiwa na kada ya juu

Mwisho itakuja kada ya chini ya wenye certificate nao wanawajibika kwa ngazi inayofuata

Mpangilio huo hautokei kwa bahati mbaya, unatokea kutokana na mafunzo kutoka katika mitaala

Kwa mfano huo tunapata vyuo vya kada mbalimbali, kama certificate, Diploma, Degree n.k.

Utaratibu huo huonekana kila mahali, kwa mfano kuanzia karani hadi katibu mkuu, waziri na kuendelea

Uwepo wa kada mbali mbali ni suala la ulazima na universal, si la Tanzania tu.

Tutajadili kwa undani utata uliozuka kuhusu suala hili.

Tuangalie sababu ya pili ya uwepo wa kada hizo

Inaendelea
 
Inaendele

VYUO VYA CHINI, KATI NA JUU

Sababu ya pili ya kuwa na kada hizo ni kupata wataalam katika viwango na mahitaji tofauti
Huwezi kumpeleka mtu wa ngazi fulani katika kijiji lakini unaweza kupata watu wa kada eneo hilo

Hapa ina maana kuwa kazi ndogo zinazohitaji utaalam wa kiwango hicho hufanywa katika maeneo kama vijijini na watalaam wa kada za chini , na linapokuwa jambo zito wataalam hao watashauri

Kwa mfano Clinical officer atatibu kwa kiwango alichoelekezwa.
Ikitokea haja atafanya rufaa katika ngazi ya juu na hilo litaendelea hadi ya juu kabisa.

Ndivyo ilivyo dunia kote na si suala la Tanzania tu

ii) Katika nchi changa kama yetu, baada ya uhuru tulikuwa hatuna wataalam.
Kilichofanyika ni program za kupata wataalam wa kada za chini kusaidia kwanza tukijenga uwezo

Kwa walioishi miaka ya 60, 70 na hata 80 watakubaliana na hoja hii.
Ndio maana tulikuwa na vyuo vingi vya kati na chini kuliko ilivyo sasa.

Hili lilisaidia sana kupunguza tatizo la wataalam ingawa halikuwa suluhisho kamili.

iii)Miaka 10 tu iliyopita tulikuwa na vyuo vikuu si zaidi ya vitano.
Idadi ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita ilikuwa kubwa kuliko uwezo wa vyuo hivyo

Kuwapa elimu katika vyuo vya kati ilikuwa suluhisho la tatizo

Kutokana na sababu hizo zote zilizojadili, ni makosa kudhani kuwa waliopitia vyuo vya kati na chini wana uwezo duni na hawana haki ya kujiendeleza. Hapa ndipo mh Waziri alipopotoka

Kwanini tunasema Mh Waziri alipotoka? Hili tunalijadili kwa kuangalia historia fupi tu ya vyuo kama Marangu(elimu), Butimba(elimu), Mlingano(Kilimo). Olmotoni( Nyuki na misitu),Mpwapwa(elimu),Kigurunyembe(elimu),Ifunda (elimu/ufundi), Bugando(Clinical officer), Machame(Clinical officer), KCMC(Clinical officer) Ifakara (Clinical officer) Dar tech(Ufundi) Arusha tech(ufundi) n.k.

Inaendelea
 
VYUO

Vyuo tuloivyotaja bandiko la awali vilikuwa na hadhi na vimetoa wataalam katika fani mbali mbali
Kwa mfano, chuo cha elimu Marangu kilijulikana kwa kutoa wahitimu wazuri sana katika elimu

Chuo cha Mlingano Tanga kilifikia hatua ya kuwa taasisi ya utafiti kikiwa affiliated na SUA
Chauo cha Olomotoni, hadi leo ni sehemu ya chuo kikuu cha SUA

Arusha na Dar tech navyo kama vile vya afya tulivyotaja vilitoa wataalam katika viwango vizuri sana
Wahatimu wa vyuo hivyo waliweza kujiendeleza hadi ngazi za udkatari na uprofesa

Swali kwa mh waziri,ni kwanini iwe ni lazima kupitia kidato cha sita kuingia chuo kikuu?
Wanafunzi wa kidato cha sita na wanaomaliza vyuo na kujiung hutahiniwa sawa

Waziri angejiuliza, ikiwa wametahaniwa na kufaulu au kufeli kwanini liwe tatizo kwa upande wa wanaopitia vyuoni? Je, ana takwimu za kuthibitisha madai kisayansi?

Waziri angetafakari,wanafunzi wanaomaliza vyuo wana msingi mzuri katika fani husika na uwezo wa vitendo 'practical'

Hii haimfanyi wa kidato cha sita kuwa hafifu, ni ukweli, kidato cha sita kinamjenga mwanafunzi uelewa wa haraka na kupambanua mambo kwa wepesi. Ni ukweli

Hoja ya Mh Waziri waliomaliza vyuo hawapaswi kujiunga na chuo kikuu haina mantiki

Hoja ingekuwa na mantiki kama Waziri angefuata mfumo unaotumika kwingine duniani

Taasisi za elimu ya juu zinatoa 'accreditation' kwabaadhi ya vyuo vya kati

Mfano, vyuo vikuu vingefanya tathmini ya mitaala ya vyuo ili kuvipa 'accreditation'

Kama SUA watatambua Mlingano au Olmotoni hakuna sababu ya kuzuia mwanafunzi

UDSM wakitambua mitaala ya vyuo kama Marangu, Mpwapwa, Butimba n.k.hakuna sababu ya kumzuia mwanafunzi

Muhimbili wanatambua Diploma zinazotolewa na baadhi ya vyuo vya afya,kwanini basi vyuo vingine visitazame utaratibu huo?

Kwa wenzetu, kabla mwanafunzi hajajiunga na chuo au taasisi ya elimu ya kati,kuna taarifa za wazi chuo husika hakitoi 'credit' ya kujiunga na elimu ya juu, au kinatoa

Badala ya kupiga marufuku, Mh waziri angekaa na wataalam waangalie jinsi ya ku streamline utaratibu

Nia ya Mh waziri ni njema kwa mengi tu, lakini pia kuna maeneo anapotoka. Tumsaidie

Utitiri wa vyuo vikuu na athari zake... Inafuata
 
VYUO VIKUU NA VIWANGO 'DUNI'

Katika mambo yalitikisa awamu ya tano ilipoingia madarakani ni la wanafunzi wa UDOM

Wanafunzi walitimuliwa baada ya kubainika walikuwa na viwango duni

Hili ni jambo jema katika jitihada za kupata watalaam walio bora na katika viwango

Hata hivyo kuna kitu kimejitokeza, badala ya kutafuta chanzo hisia na jazba zilitawala

Miongoni mwa waliofukuzu kwa uduni wa viwango wapo wa mwaka wa pili, tatu

Swali, kama wanaviwango duni waliwezaje kuvuka mwaka wa kwanza au wa pili?

Badala ya kuwafukuza viwango duni waliovuka miaka, Mh Waziri angejiuliza walivukaje?

Pili,tume ya vyuo vikuu inayohakiki viwango ilikuwa wapi bila kubaini viwango duni?

Tatu, Mh Waziri aliongea na wahadhiri kujua kwanini viango hafifu vilifanya vema?

Laiti Mhe angejiuliza uchache wa maswali, kutimua kungekuwa jambo la mwisho.

Maana yake waziri angekuwa na majibu ya kwanini anawatimu na hapo ndipo pa kuanzia

Kuwatimua tu ilikuwa kuwaadhibu bila sababu za msingi.

Waliomba, wakachaujwa ,wakaingia, wakatahiniwa, wakavuka mwaka. kosa lao li wapi.

Hatua ya Mh waziri ilikuwa na lengo zuri, kwa bahati mbaya iliongozwa na jazba na siasa badala ya sayansi ya utafiti wa tatizo, chanzo na suluhisho.

Je, kuwatimua wanafunzi wa UDOM kume solve matatizo kama hayo katika vyuo vingine na nchi kwa ujumla wake?

Tusemezane
 
WASOMI NA WATAALAM MPO WAPI?

HAYA YA UTATA WA KATIBA HAYAWAHUSU?

Tumejadili kwa uchache kuhusu tatizo la elimu na maamuzi yatokanayo hapo nyuma

Umuhimu wa elimu hauelezeki kwa maneno machache.
Kwa ujumla ndiyo silaha kubwa aliyo nayo mwanadamu au anayopaswa kuwa nayo

Kuna kutokuelewa maana nzima ya elimu hasa kwa walioelemika.
Wengi wanadhani elimu ni ''nyenzo'' kufanya kazi, kuendelea na maisha hata kupata ajira

Dhana ya elimu ni kumwezesha mwanadamu kujitambua, kutambua mazingira, kupambana na changamoto zinazotokanazo kubwa na madogo

Sifa ya usomi ni nguvu ya kuelewa, kupambanu, kufikiri kwa mantiki na kutoa majibu

Hayo ndiyo yanayomtofautisha msomi na mtu mwingine.

Mwanafunzi hufundishwa mengi, kuna nyakati hayatumia katika maisha hata siku moja.

Lengo ni kujenga uwezo wa kuelewa, kupambanu, kutafakari na kupata suluhu

Tumeyasema haya kutokana na hali ya wasomi wetu na usomi kitaaluma tu

Hakuna sababu za kuamini Engineer , daktari, wanasheria n.k. hawawezi kufikiri nje ya taaluma zao.

In fact mambo nje ya taaluma zao yanawagusa kuliko yaliyomo ndani

Ni uelewa finyu kama msomi atadhani masuala kama KATIBA hayamhusu , ni ya kisiasa

Kinyume chake katiba inamhusu msomi inaamua maisha yake nje na ndani ya taaluma

Na kwa vile anaishi na usomi, uwezo wa kuelewa masuala kama ya katiba bila kujali taaluma ni mkubwa kuliko mwanachi wa kawaida aliyekosa fursa hiyo.

Wajibu wa msomi hauishii katika eneo au familia yake, ni pamoja na jamii inayomzunguka

Tuna tatizo la wasomi, na haionekani hali kuimirika.

Mjadala ulioanzishwa na waziri wa zamani kuhusu uteuzi wa wabunge unatueleza hali ya wasomi wetu

Inaendelea......
 
WASOMI NA HILI LA KATIBA

Inaendelea

Waziri huyo wa zamani amehoji kuhusu nafasi za utezi 10 alizopewa Rais kuwa hazikuzingatia katiba
Kwamba Rais atakuwa amevunja katiba kwa kuteua wabunge wa kiume wengi kuliko wanawake

Hoja iliwarudisha watu katika ya Tanzania ya mwaka 1977 yenye marekebisho kwa nyakati tofauti

Kilichotokea ni tafsiri mbili za kiswahili na Kiingereza zikiwa na maneno yaliyonyofolewa kwa moja

Kutokana na tafsiri mbili zenye utata, mjadala umekuwa mkubwa kuliko isivyotarajiwa

Tuliegemea katiba iwe na majibu, inaonekana katiba imezidisha tatizo. Kila mmoja anatumia tafsiri inayokidhi hoja zake na si tafsiri iliyopo katika katiba

Tatizo la kwanza: Si uteuzi, bali mwongozo wa uteuzi ulioacha mwanya na sasa kila mmoja anajazia tu

1. Ikuwaje kukawa na katiba moja yenye tafsiri tofauti? Wasomi wetu wa sheria walikuwa wapi kuliona tatizo hilo ikiwa tunao wasomi katika fani ya sheria wakibobea katika katiba?

2. Wasomi wetu walikuwa wapi bila kuona utata huo?
Hata kama hauna maana midhali umeleta sintofahamu hauwezi kupuuzwa.

Wasomi wapo katika idara na wizara za umma, bungeni katika mashirika n.k. kwanini hakuna aliyeona!

Baya zaidi, baada ya kutokea utata, uwe ni mdogo sana au mkubwa, kwavile kuna sintofahamu katika sehemu jamii, wako wapi wasomi wetu kwa ujumla wao kusimama na kuisaidia jamii kuelewa?

Hili laweza kuwa jambo dogo la kipuuzi na lisilo na maana.
Hata hivyo, linapoleta sintofahamu tayari lina maana kubwa kuliko inavyodhaniwa

Wasomi wetu wa fani na kada zote tunaojua wanaweza kupambanua, kuelewa n.k wapo wapi?
Nani ataisaidia jamii kama si wao?

Nini kinawafunga mikono? Ni njaa, uwezo mdogo, au kutoelewa wajibu wao kwa jamii?

Hivi tunahitaji kuagiza wataalam wa kutafsiri katiba yetu na kutueleza kwanini Rais yupo sahihi au kakosea na kwa sababu gani? Kwanini katiba moja ina tafsiri mbili zinazotofautiana?

Ilikuwaje na itazuilika vipi? Nini kifanyike kuondoa utata na wananchi wanapaswa kuelewa nini?

Wako wapi?

Tusemezane
 
With respect to uniforms, my recollection is once you are an officers in the army, police force or prison service, you buy your own uniforms. This provision has been in place since Kambarage was at the helm.

However, if you are not an office, you receive your uniforms from the quartermaster. In case you die, retire, or dismissed from the service, you are required to return the uniforms to its respective owner, the government.

Officers don't returns their uniforms when they retire. And when they while in service or not, their beneficieries are entitled to use the uniforms as the feel fit.
 
WIKI YA MATUKIO NCHINI

Tunaelekea wapi ndilo swali

Wiki imegubikwa na habari nyingi mchanganyiko.

1. Kukamatwa kwa Wabunge

Mbunge wa Upinzani amekamatwa kutoka Dodoma alipokuwa anahudhuria kikao

Si maudhui ya bandiko kujali hoja ya kukamatwa kwake, bali yatokanayo

Timbwili limemlazima Mbunge Zitto kufikisha malalamiko ya kukiukwa taratibu za Bunge

Katika hoja, Zitto alionyesha utaratibu unaotumika mbunge akifungwa au kukamatwa
Alifanya rejea za Bunge letu na mabunge ya commonwealth

Katika hali isiyo ya kawaida na isiyojibu hoja za Zitto, Naibu Spika alikataa kutolewa kwa hoja akisema sheria inazungumzia makosa aliyosema hayahusishi utaratibu wa Bunge

Kuna hoja hapa

1. N.Spika hakujibu hoja kuhusu mbunge aliyefungwa na kama bunge lina taarifa

2. Wabunge hukamatwa kwa mahojiano na Polisi, yeye alijuaje aina ya makosa?

3. Utaratibu ni Uongozi ni kufahamishwa kukamatwa siyo kwanini amekamatwa

Ilikuwaje Naibu Spika akaelewa ni makosa nje ya utaratibu wa bunge ikiwa Polisi hawakusema kwanini wamemkamata mhusika!

Kutokana na hali hiyo historia ya kumsusia ikajirudia na kuzidi kuweka wingu nene juu ya umakini, hekima , weledi na busara za Naibu Spika katika kushughulikia Bunge

Hata kama yupo sahihi kwa namna yoyote, bado kuna mapungufu ya hekima na busara

Naibu Spika angeliacha bunge lijadili kwanza akiongoza mjadala
Bado alikuwa na fursa ya kukataa hoja baada ya wenzake kujadili

Naibu Spika ni sehemu ya Bunge na wala si bunge zima kama inavyodhaniwa

Kitendo cha kuzima hoja tu kama ilivyozoeleka kinatafsiriwa kwa upana kabisa ni kukosa busara, hekima na mapungufu ya kuongoza. Hilo linatia doa Bunge

Hilo limezidi kupeleka Bunge kudharauliwa kama mhimili unaojitegemea na baadhi ya viongozi wa mihimili mingine. Dharau hiyo sasa inatafuna heshima na hadhi ya bunge

Tutajadili hili kwa upana

Inaendelea
 
Mimi naweka nafasi, ili niweze kufuatilia kwa karibu maelezo yako ya kina juu vita dhidi ya dawa (sumu) za kulevya vinavyopiganwa kwa staili mpya inayoratibiwa na RC Makonda.
====
Naunga mkono vita hiyo ili kunusuru kizazi hiki na vijavyo!
 
HESHIMA YA BUNGE

Kiongozi mmoja amesikika akitoa kauli zinazoashiria kulidharau bunge
Bunge limechachamaa kwa kile kinachosemwa limevunjiwa hishma na kudharauliwa

Bunge limeazimia kuwaita baadhi ya viongozi katika kamati zake kwa 'mahojiano'

Hoja: Hatua ya bunge imechelewa na hakika kudharaulika ni zao la ubutu wa Bunge
Kwanza, mengi yamefanyika katika kujidhalilisha lenyewe ikiwemo kutoelewana

Pili, wakati wabunge wananyakuliwa na Polisi katika maeneo yao hakukuwepo malalamiko
Hayo ni kutokana na ukweli kuwa wabunge husika walikuwa wa upinzani

Kitendo hicho tu kilifungua milango ya Bunge kupoteza heshma

Kauli ya viongozi kuhusu madawa na tuhuma kwa baadhi ya watunga sheria ni mwendelezo wa Bunge lenyewe kutojisamamia, kuacha uvyama na kuwa taasisi

Tatu, uongozi wa Bunge unaonekana kupwaya na kuudhofisha mhimili huo
Maamuzi mengine hayawezi kutofautishwa kati ya bunge na serikali

Bunge linaendeshwa kibabe na si hoja. Kwamba,baadhi ya mijadala ima huwekwa kapuni au wahusika kukalishwa chini. Kwa ufupi hoja zinajifia tu

Hatudhani bunge lina sababu za kualalamika.
Bunge liliruhusu kuingiliwa taratibu , kuvunjiwa heshima, ukimya unaligharimu

Ukimya huo unagusa mhimili mwingine taratibu kama ilivyoanza kwa Bunge

Hakuna kuheshimiana miongoni mwa wadau wa mihimili

Sakata la madawa ya kamata kamata ya wabunge na madawa ya kulevya vimesaidia sana kuonyesha Bunge na nafasi yake kwa jamii.

Wabunge wajitambue kwanza kwamba tofauti zao za kiitikadi, kidini, kijamii au kijinsia zipo chini ya mwamvuli wa taasisi ya Bunge.

Hadi watakapojitambua na kuwa kitu kimoja kama taasisi, heshima ya Bunge itamegwa na awaye atakuwa mwathirika tu. Wabunge wasilalamike, wajitazame wameangukia wapi?

Sakata la madawa... inafuata
 
Bado nasubiri tathmini yako Mwalimu Mkuu wangu (Nguruvi3)! Leo tumeambiwa awamu ya tatu ya wale wanaojihusisha na sumu za kulevya wapo toka enzi ya Ruksa! Timesikia na namna kamishna na wenzake watavyo dhibiti sumu hizi za kulevya!
Nadhani tumepata mtu sahihi kwenye nafasi ile!
 
Bado nasubiri tathmini yako Leo tumeambiwa awamu ya tatu ya wale wanaojihusisha na sumu za kulevya wapo toka enzi ya Ruksa!

Timesikia na namna kamishna na wenzake watavyo dhibiti sumu hizi za kulevya!
Nadhani tumepata mtu sahihi kwenye nafasi ile!
Mkuu hili la madawa ya kulevya lipo katika sura mbili.

Madawa yapo yametumika kwa miaka dahari kama bangi, mirungi n.k.

Madawa yenye uraibu wa dhahiri kama Cocaine, Heroine n.k.

Changamoto ni kupambana na kundi la pili, lakini huwezi ku ignore kundi la 1

Madawa ya kundi la pili yamekuwepo miaka nenda rudi si toka wakati wa Mwinyi

Tofauti na sasa, zamani yalipatikana kwa uchache , watu wa kawaida hawakumudu

Biashara ya madawa ni kubwa kama inavyojulikana.
Hilo limechagiza ongezeko la uzalishaji , usambazaji na soko.

Ongezeko la uzalishaji kimesababisha supply kubwa zaidi ya demand
Supply imeongeza upana wa soko na hapa ndipo vijana walipoingia mtegoni

Ni tatizo kubwa duniani na wala si nchini kutokana na ukubwa wa biashara

Ni ukweli, upatikanaji rahisi wa madawa umeongeza matumizi kwa kizazi cha leo
Hilo limeathiri jamii na lazima tukubaliane ni tatizo kubwa duniani na ktk jamii yetu

Tumetambua ni tatizo,kupambana na tatizo si option bali ni lazima
Tunapambanaje na tatizo, hapo ndipo kuna tatizo la pili

Mapambano yanahitaji akili zaidi ya nguvu.
Marekani walijaribu hadi kumkamata viongozi wa nchi na kila mbinu.

Tatizo lipo na linaendelea licha ya resources walizo nazo
Approach yao si kutumia chopper bali kuangalia source na kutokomeza

Ni biashara kubwa ikiwa na mtandao mpana na hatari
Kamisha ameeleza vizuri sana approach yake.

Kwa kuongezea, kuna source, supply chain, logistics , distributors hadi consumer
Kuna umuhimu wa mkakati wa kisayansi na kitaalam

Hili la RC na madawa ni jambo jema, at least ameonyesha kujaribu eneo lake

Tatizo ni kuwa RC hakuwa na mkakati kabla ya kuanza.
Alikuwa na idea lakini anaitekelezaje ndipo penye walakini

Kama ulisikia, bunge lililalamika hakuna kamishna wa kamisheni ya madawa
Rais kamteua juzi na leo ndio siku yake ya kwanza kazini

Umemsikia Mh Rais akisema kuna uwezekano PM hakujua na wala mawaziri hawakujua

Na unaweza kuona huwezi kudhibiti madawa Dar es Slaam ukasema umemaliza tatizo

Katika mazingira hayo, unaweza kuona RC alianzisha kitu bila kuwa na ''background''
Kwamba hakujua nani mwenye zoezi kisheria, na wapi atapata resources

Hapa kutahitajika ufafanuzi

Inaendelea.....
 
Kwenye vita dhidi ya madaya ya kulevya,

Bila kujenga, kuwezesha na kuimarisha taasisi za ulinzi na usalama kufanya kazi zake kwa weledi na uhuru itakuwa ngumu sana kushinda vita hii. Vyombo vya ulinzi na usalama visimame katika nafasi yao kwenye kuchunguza, kupeleleza ili kupata ushahidi wa kuwatia hatiani watuhumiwa. Tuachane na hizi approach za kisiasa za kutajana majina hadharani halafu tukategemea kudhibiti au kukomesha biashara hii hatutafanikiwa zaidi ya kuangukia pua mahakamani.
 
Inaendelea kutoka bandiko 275

Katika mazingira yanayoonekana RC alichukua hatua bila kuwa na background
1. Suala la madawa ni pana, kupigana nayo Dar pekee hakutoi jibu
2. RC wa Dar siyo mkuu wa RCs wa mikoa yote.
Tamko lilikuwa localized likihitaji (national consensus) muafaka wa kitaifa
3. Alianza bila kushirikisha viongozi na hivyo kuwa na mapungufu ya kisheria na rasilimali
4. Hakuzingatia sheria tulizojiwekea ikiwemo uanzishwaji wa kamisheni ya madawa
5. Ameongozwa na hamasa zaidi kuliko mantiki

Hayo tunaweza kuyaona kama ifuatavyo

Namba 1 hapo juu.
Mkuu wa kamisheni bw Sianga kasema vita ya madawa ikibidi itaenda Zanzibar. Hapa alikuwa anaeleza kuwa vita haiwezi kuwa ya Dar pekee.
Akasema Tanzania inaonekana kuwa ''corridor'' kwa maana ya ujumla

Namba 2:Rais alipoongea Ikulu akasema hili si la RC wa Dar pekee ni la kitaifa. Alichofanya ni kuelekeza RCs kuchukua hatua kwa kuelewa kauli ya RC Dar si ya kitaifa

Namba 3: Mh Rais kasema wapo wenye dhamana ambao hawajui kama wanadhamana. Hii maana yake hakukuwa na coordination na uteuzi Sianga haraka unashadidia hoja
Uteuzi wa Sianga upo kisheria na Rais alifanya hivyo haraka ili kutoa mwelekeo wa kisheria

Namba 4: Bunge lililamika kutokuwa na uongozi wa kamisheni ya madawa
Kilichoonekana ni utendaji mwongozo wa kisheria
Hili lilitoa nafasi ya watu kutuhumu na kulifanya suala hilo kwa mtazamo mwingine

Namba 5:Kitendo cha kuanza kutaja watu kwa habari, hakikufuata taratibu.
Watu waliitwa Polisi kwa vyombo vya habari, wakihojiwa na kukamatwa hapo hapo.

Ukimsikiliza Sianga, amesisitiza sana suala la kufuata sheria na taratibu

Hayo ni sehemu tu ya mapungufu mengi yanayotoa mwanya zaidi na si matokeo

Tumemsikiliza Kamishna Sianga akizungumza siku ya kwanza.

Kwa namna yoyote tukiri anaelewa tatizo, anaelewa anataka kufanya nini na kwa utaratibu gani. Kwa ufupi ana weledi mkubwa sana wa suala zima hili tukubaliane na hilo

Alichosema Sianga na mantiki zake kitaalamu na kijamii

Inaendelea...
 
ALICHOSEMA KAMISHNA SIANGA NA MANTIKI ZAKE

Katika hotuba, kamishna Sianga alisema mambo kadhaa kuonyesha uelekeo.
Kwa maana alipanga safu yake, akatoa dira ya mapambano

1. Kamisha aliwatambulisha wakuu wawili, Intelejensia na Oparesheni
Hii ni kuwa na habari za uhakika ili kuwezesha operesheni kufanyika

2. Bw. Sianga akazungumzia matumizi ya sheria katika mapambano
Alimaanisha kuepuka ukiukwaji wa haki za watu(intelejensia na oparesheni)

3. Sianga akagusia hatua kwa maafisa wa serikali wanaozembea madawa kuingia nchini.
Sianga ana maanisha kama dawa hazitaingia, hakutakuwa na wateja

Na kwamba, dawa inawezaje kufika Morogoro, Manzese au Mbagala bila kuingizwa?

Hoja ya Sianga ni kuwa tatizo si watumiaji, bali watumiaji wanapata kutoka wap?
Kitaalam Sianga anajaribu kuziba mianya ya kuingiza madawa (conduit)

4. Akazungumzia mahakimu na mawakili wa serikali wanaovuruga kesi
Alilimaaminisha pesa inatumika, hivyo mapapa yanaendelea kuwepo

5. Kamishna akasema mapambao ikibidi yatafika Zanzibar
Hoja, huwezi kupambana na madawa kwa mkoa ni vita ya kila kona ya nchi

6. Akasema, walioathirika watapata msaada wa matatibu.
Ni katika kuonyesha kuwa waathirika ni 'victims' na siyo criminals

Criminals ni 'supply chain' mzigo unapotoka hadi unapomfikia mtumiaji (conspiracy)

Kwa hoja hizo tunaona mkakati unavyotofautiana na harakati

Vita ya madawa ni watu wenye uwezo, hatutegemei matokeo ya haraka, lakini kuna jambo moja tukubaliane, kwamba, ni vita ya fikra na si maguvu

Vyovyote iwavyo tunarudia kusema kwa dhati, Kamishna Sianga anajua anachofanya

Changamoto inayomkabili ni kupewa ushirikiano bila kuingiliwa kisiasa

Changamoto ya pili ni mfumo unaoweza kum 'frustrate' kutimiza majukumu

Tusemezane
 
WAZIRI WA SHERIA NA HOJA ZA TLS

Waziri wa sheria ametoa kauli ya nia ya kukifuta chama cha kitaaluma cha wanasheria

Hoja yake ya msingi ni kuwa chama hicho 'kina mwelekeo wa kisiasa' badala ya kitaaluma

Kauli ya waziri imekuja wakati TLS wakijiandaa kufanya mkutano wa uchaguzi

Kauli imechagizwa wanasiasa/wanasheria kuonyesha dhamira uongozi wa chama

TLS ni chama cha kitaaluma na kinaongozwa kwa misingi waliyojiwekea wanasheria

Misingi imekubaliwa na serikali kwa nusu karne ya uwepo wa chama

Zipo sheria za nchi zinazowabana wanasiasa katika utumishi hasa wa umma

Haijathibitika kama kuna sheria inayobana wanasiasa kushirikia shughuli za taaluma yao

Wanasiasa wanawajibika kimaadili kutoshiriki uongozi na siyo kutoshiriki shughuli za kitaaluma ili kukwepa conflict of interest. Kisheria hawalazimiki kutogombea uongozi

Ni vema waziri akatambua,wenye chama ni wanataaluma na si serikali
Kazi ya serikali ni kusajili vyama ili vipate 'uhalali' wa kisheria na uwepo wake

Wanaopaswa kuona mwelekeo wa TLS ni wanachama si waziri au serikali

Kama waziri ana ushahidi wa TLS kuondoka katika misingi yake, ana kila sababu za kuweka wazi au mbele ya sheria au kutumia sheria kujenga hoja

Si suala la dhana tu kwavile kunahisia za wanasiasa kugombea uongozi

Kubwa zaidi, ni kwanini serikali imekuwa na 'interest' na TLS, na si vyama vingine?

Kuna kila sababu za baadhi ya wanoamini kauli ya Waziri ni kutishia uwepo wa TLS

Tishio linaambatana na kushawishi 'influence' wapiga kura kuhusu hatma ya chama

Inaendelea
 
WAZIRI WA SHERIA NA HOJA ZA TLS (II)
Inaendelea...

TLS imekuwepo miaka zaidi ya 50, na uongozi uliopo utamaliza muda March 2017

Katika kipindi cha miaka 3 au 5, ni lini chama hicho kimeonyesha mkondo wa kisiasa?

Kuelekea uchaguzi, waziri ameona wagombea, bila uthibitisho kaweka hisia zake kuhusu mwelekeo wa TLS. Hisia ambazo wanachama wa TLS hawajazionyesha

Hata kama zitakuwepo jukumu na dhima ya TLS ipo mikononi mwa wanasheria hao

Kwanini basi waziri afanyie kazi hisia zake kwa kuambatanisha na sheria za nchi?

Kwamba anahisi TLS itakuwa ya siasa,atatumia sheria kukifuta kukamilisha hisia zake.

Hili si sahihi. Waziri angesubiri kuwa na ushahidi kwanza, na si hisia tu

Kwa upande mwingine, kauli ya Mh Waziri ichukuliwe na TLS kama 'wake up call'

TLS ni chama kilichopteza malengo kwa uchache wa kusema

Pale taaluma inapoingiliwa, dhihakiwa au dharaulika, TLS wametelekeza wajibu wao.
Si kwa taaluma bali kwa jamii wakiwa wana taaluma

Udhaifu wa TLS unatokana na ukweli, wanachama wake ni 'beneficiary' siasa.
Tumesikia wakiambiwa, 'endapo watakuwa na mtu wa upinzani' hatateuliwa

Mtiririko huo unaonekana katika teuzi za kisiasa
Wanachama wanakuwa ''loyal'' wakitegemea mbele ya safari lipo jema litatokea

TLS wameambiwa 'mawakili' watachukuliwa hatua wakitekeleza kazi, TLS wapo kimya

Orodha inayoonyesha udhaifu wa TLS ni kubwa, inatosha kusema ni chama ''mfu''

Taaluma yao inaingilika kirahisi tu kwasababu ya udhaifu wao

Wanaelekezwa nani wa kuongoza mchana kweupe, dharau ya kiwango kizuri tu

Hili lazima wajitathmini kama malengo ya chama yapo au kimegeuka kuwa 'spring board' au launching pad mtu anapofikiria masilahi yake mbeleni

Nguvu ya TLS ibaki kwa wanachama wenye dhati na malengo ya uanzishwaji wake
TLS watafanya kosa kuchagua wanyenyekevu, au kukaa kimya wakitumai bahati

Watatenda kosa kubwa kutishiwa na kukubali. Hilo litaendeleza kile kinachosema 'maagizo kutoka juu'.

Ni udhaifu huo ndio umewafikisha mahali wanatishiwa tu kuliko chama kingine

Wanachama takribani 6,000 wasitegemee kuwa wanufaika siku za mbeleni.

Wajitathmini wananufaikaje na TLS,si kufikiria wanachama 50 watakaonufaika binafsi

Tusemezane
 
Back
Top Bottom