Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,399
- 31,352
- Thread starter
- #261
Bandiko hili #69 na #52 tumeongeelea tatizo la mfumo wa elimu analokumbana nalo Waziri wa elimu Mh NdalichakoTUANGALIE MAELEZO YA Mh WAZIRI KUHUSU MFUMO
Kwa hisani ya gazeti la Mwananchi
Serikali yafuta GPA katika elimu, yarejesha divisheni
Waziri wa elimu anaeleza NECTA ilivyoshindwa kuja na majibu ya GPA.
Anasema baadhi ya watahiniwa wa GPA wanaonyesha kiwango kidogo kuliko GPA zinavyoonyesha.
Hoja hii inathibitisha kauli yetu kuwa, GPA iliwekwa kufunika uchafu kwa kutumika kisiasa
Waziri anaendelea , NECTA walimweleza kuingia katika mfumo huo kunatokana na hoja za wadau.
NECTA ikashindwa kuthibitisha ni wadau wapi na katika mikutano au mikusanyiko gani
Hapa inaonyesha NECTA inadanganya. Hiki ni chombo kinachosimamia elimu, moyo wa Taifa lolote
Chombo hiki kinapokuwa cha kibabaishaji inatia hofu na ni hatari kama waziri alivyosema pia.
Waziri ameendele kusema, mfumo huo haukupitia kwa kamishna wa elimu kupata kibali.
Maagizo ya serikali yanasema kila kitu kianze kutumika JUNI 2016
Tunaona ushiriki wa serikali kwa kutoa siku ya kuanza kutumika mfumo.
Wakati kamishna hakutoa kibali, haieleweki serikali ilitoa vipi agizo
Waziri anasema kanuni za mitihani zilipitishwa miaka 2 baada ya kuanza kutumika utaratibu wa GPA
Kanuni zilipitishwa na waziri Oktoba 28,2015 (kipindi cha uchaguzi) na kuingizwa katika gazeti la serikali November 6, siku ambayo Rais Mpya alikuwa na siku 1 tu ofisini
Tunachokiona ni mfumo mbaya, si wa elimu ni wa ujumla. Baraza la mawaziri linapaswa kuvunjwa isipokuwa kwa dharura tu. Waziri anapopitisha kanuni Oktoba 28,2015 kura zikihesabiwa kuna tatizo.
Yaani waziri alikuwa kazini hadi uchaguzi ulipomalizika
Kwa maneno mengine, kuna uwezekanO alifanya hivyo kwa shinikizo la watu.
Elimu na mitaala au mitihani si suala la dharura, kwanini waziri afanye yote akijua huenda asingerudi?
Kitu tunachopaswa kuelewa ni jinsi ambavyo maelezo ya waziri yanavyochanganya.
Kuna maeneo anaitetea serikali, na maeneo mengine serikali ikionekana kushiriki.
Hivyo, tunaweza kusema NECTA walifanya kazi na serikali ina a way, ingawa wadau wakuu kama kamishna wa elimu hawakushirikishwa
Haya yanatokea kwa sababu hatuna mfumo mzuri wa utawala,inaonekana wazi katika sakata la elimu
Mambo yanafanyika gizani kiasi cha waziri kutoweza kuelewa Ilikuwaje, hawezi ku trace nini kilifanyika
Lakini pia waziri aliambatana na Mkurugenzi wa NECTA. Akiwa naye, mh alisema maelezo aliyopewa NECTA kuhusu GPA yalikuwa ya bla bla.
Maana yake maeelezo ya mkurugenzi hayakumridhisha bali ubabaishaji
Laiti waziri angekuwa na nguvu juu wa mkurugenzi, pengine asingetokea naye kwenye mkutano
Mkurugenzi anateuliwa na chombo kingine hivyo waziri hana la kufanya isipOkuwa kushauri tu
Mfumo unakwaza viongozi kiutendaji. Ni kama ule wa Bandari tulioona watu Zaidi ya 4 wanateuliwa na mamlaka moja wakiwajibika kwa mamlaka hiyo na kila mmoja kuwa 'bosi' kivyake
Hili la elimu linaeleza wazi kuhusu mfumo. Tunarudia, kama waziri ambaye alikuwa Mkurugenzi wa NECTA miaka miwili iliyopita haelewi nini kimetokea, nani nje ya system anayeweza?
Je, Watanzania hatuoni tatizo letu kama mfumo na si mtu au watu?
Taasisi zinafanya kazi bila kujua moja infanya nini. Maamuzi yanapitishwa kisiasa, wengine kutoshirikishwa pengine kwa hofu ya 'ukaidi'.
Serikali iliridhia vinginevyo kwanini itangaze jambo isilokubaliana nalo?
Tutaendelea...
Jambo moja tunalikubaliana kama taifa ni kuwa mfumo wetu wa elimu una matatizo
Ukubwa wa tatizo umeongezeka awamu ya nne ambapo mambo mengi yamefanyika kienyeji
Bila shaka kazi aliyo nayo waziri wa elimu ni kubwa na ngumu na huenda inapelea yeye kuwa kiongozi wa hoja zenye utata 'controversy' kila mara
Waziri Ndalichako'anashambuliwa' bila kuonyeshwa mbadala au mapungufu ya hoja zake
Sehemu ya tatizo analitengeneza mwenyewe hasa kwa matamko yake kama amri
Akiwa waziri ana nafasi ya kutoa amri, lakini asisahau nafasi yake ya kiongozi wa umma
Sifa ya kiongozi wa umma ni kusikiliza, kujadiliana, kutoa hoja kwa facts na si matamko
Tatizo la pili linalomkumba Mh waziri ni kuvutika katika migogoro ya kisiasa
Ni mwanataaluma akiwa na nafasi ya siasa. Zipo sehemu siasa haichukui nafasi ya taaluma
Tunasema haya kwasababu kuu mbili.
Kazi ya kujenga mfumo mbovu ni ngumu na hatutegemewi awe malaika kwa usahihi.
Lakini pia yapo anayosimamia ambayo kwa mtazamo ni sahihi na anayopotoka
Ni kwa msingi huo, tutapitia hoja na matamko yake kwa ukaribu
MITIHANI YA BAADHI YA TAASISI BINAFSI NA UMMA KURATIBIWA NA NECTA
Moja ya hatua nzuri za Mh Waziri ni kuahakikisha mitihani kwa baadhi ya taasisi inaratibiwa na chombo kimoja.
Kwamba NECT itapima watahaminiwa wa taasisi binafasi na zile za umma
Tukumbuke, soko huria lilifungua milango na elimu ni sehemu mojawapo.
Kwa muda mfupi kulizuka vyuo na taasisi zinazotahini wanafunzi kisha kutunuku vyeti
Taasisi binafsi zinatoa elimu kwa utaratibu wa biashara.
Ubora ambalo ni la kwanza, hupewa umuhimu wa pili baada ya biashara kufanyika.
Tumekuwa na matatizo ya watahiniwa waliopata vyeti katika mazingira ya kusikitisha
Kitendo cha kuamua watahaniwa wapimwe kwa chombo kimoja kama NECT ni kizuri sana
Hili linapima ubora na kupora nguvu za ''biashara'' kwa wafanyabishara ya elimu
Ingawa baadhi ya watu hawakufurahia, jambo hili ni la kuungwa mkono na kupongezwa.
Tunahitaji ubora katika elimu si mchezo wa biashara katika suala nyeti na muhimu kama elimu kwa Taifa
Inaendelea...