Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,399
- 31,352
- Thread starter
- #441
TUNARUDI KULE KULE, AJIRA ZA MUUNGANO!
AJIRA NI GHARAMA, MCHANGO WA ZNZ UPO WAPI?
Habari hii ni kwa hisani ya gazeti la Mwananchi katika makala hii
Mwandishi anajitambulisha kama Salim Said Salim.
Bw Salim ''amekusanya' maoni ya Wazanzibar kuhusu ajira za muungano
Ni vigumu kutofautisha kama ni maoni yake kwa kutumia neno wznz au ni maoni ya kutoka katika vyanzo alivyosema. Jambo moja linaloonekana wazi ni weledi na upotoshaji
Kwanza, mwandishi ameeleza Wazanzibar kunyimwa ajira katika serikali ya muungano
Hakueleza ni eneo au taasisi gani wala kufafanua ajira za muungano ni zipi anazoongelea
Inaeleweka, asilimia '21' ya ajira za muungano kwa Zanzibar katika taasisi za muungano
Kwa makusudi na nia ya kupotosha umma wa wznz, Bw Salim hakueleza ukweli huo
Mwandishi aelewe ajira za taasisi nje ya zile za muungano si haki ni fadhila na hisani
Kuna idadi ya Wazanzibar wameajiriwa halmashauri za miji za Bara na taasisi zisizo za muungano. Ndiyo maana soko kubwa la ajira kwa Wazanzibar ni Tanzania bara,ni ukweli
Katika kuchanganya umma au weledi hafifu ameongelea ajira za muungano kwa ujumla
Ameongelea taasisi bila kutofautisha akidhani kila taasisi zote za bara ni ya muungano
Pili, Salim anasema kuna taasisi za muungano ambazo hazijaongozwa na Mzanzibar tangu muungano uasisiwe. Bw Said atambue ajira haziangalii eneo au sura bali uwezo na weledi
Tatu, anasema tume ya kuangalia ajira inapaswa kuwa na uwiano sawa wa wajumbe
Salim anapaswa kutambua usawa anaousema hauji tu kama mvua bali kuna wajibu
Kwamba, gharama za muungano ni za Tanganyika na hilo halijawahi kupingwa.
Hakuna mzanzibar anayeeleza kwa miaka 10 au 20 Zanzibar imechangia nini katika muungano unaotoa ajira wanazodai
Mawazo ya Salim ndiyo waliyo nayo viongozi wengi kutoka Zanzibar
Ajira ni gharama ni wajibu kueleza mchango wa Zanzibar kabla ya kudai 'haki'
Salim anapotosha kwa kusema uwepo wa serikali 3 utasaidia ZNZ katika ajira
Ni muhimu atambue ajira za taasisi za muungano na zile zisizo za muungano zinazotoka Tanganyika au Tanzania bara zinatoa ni nyingi kuliko ajira za SMZ kwa ujumla wake
Lakini pia Salim atambue ''taasisi muungano'' kama tulivyoeleza nyuma zina mbadala znz
Hakuna sababu ya Mzanzibar kuajiriwa TFDA , HESLB, TBS, SUMATRA, MARITIME, TANESCO n.k. akidhani ni taasisi za muungano.Ikitokea ni hisani na fadhila si haki
Kwa taasisi ambazo Zanzibar imeanzisha mbadala, zile za Bara ni za watu wa bara tu
Ikitokea Mzanzibar kuajiriwa ni fadhila si haki kama Bwana Said pengine asivyoelewa
Ni wakati Wazanzibar waeleze mchango katika kuendesha muungano kabla ya madai. Tunasema hivi kwasababu 'ukiona vyaelea ujue vimeundwa'
Viongozi na waandishi kama Salim waeleze ukweli wa gharama za muungano na si kuorodhesha madai na waweze kutofautisha kati ya hisani na haki, wajibu na madai
Hakuna madai ya ZNZ yatakayobeba uzito ikiwa hayatasimama katika kuonyesha mchango wa Zanzibar katika kuendesha muungano ni upi au kiasi gani
Hiki ni chombo chenye gharama kubwa na madai yao yajengwe katika mchango
Tusemezane
AJIRA NI GHARAMA, MCHANGO WA ZNZ UPO WAPI?
Habari hii ni kwa hisani ya gazeti la Mwananchi katika makala hii
Mwandishi anajitambulisha kama Salim Said Salim.
Bw Salim ''amekusanya' maoni ya Wazanzibar kuhusu ajira za muungano
Ni vigumu kutofautisha kama ni maoni yake kwa kutumia neno wznz au ni maoni ya kutoka katika vyanzo alivyosema. Jambo moja linaloonekana wazi ni weledi na upotoshaji
Kwanza, mwandishi ameeleza Wazanzibar kunyimwa ajira katika serikali ya muungano
Hakueleza ni eneo au taasisi gani wala kufafanua ajira za muungano ni zipi anazoongelea
Inaeleweka, asilimia '21' ya ajira za muungano kwa Zanzibar katika taasisi za muungano
Kwa makusudi na nia ya kupotosha umma wa wznz, Bw Salim hakueleza ukweli huo
Mwandishi aelewe ajira za taasisi nje ya zile za muungano si haki ni fadhila na hisani
Kuna idadi ya Wazanzibar wameajiriwa halmashauri za miji za Bara na taasisi zisizo za muungano. Ndiyo maana soko kubwa la ajira kwa Wazanzibar ni Tanzania bara,ni ukweli
Katika kuchanganya umma au weledi hafifu ameongelea ajira za muungano kwa ujumla
Ameongelea taasisi bila kutofautisha akidhani kila taasisi zote za bara ni ya muungano
Pili, Salim anasema kuna taasisi za muungano ambazo hazijaongozwa na Mzanzibar tangu muungano uasisiwe. Bw Said atambue ajira haziangalii eneo au sura bali uwezo na weledi
Tatu, anasema tume ya kuangalia ajira inapaswa kuwa na uwiano sawa wa wajumbe
Salim anapaswa kutambua usawa anaousema hauji tu kama mvua bali kuna wajibu
Kwamba, gharama za muungano ni za Tanganyika na hilo halijawahi kupingwa.
Hakuna mzanzibar anayeeleza kwa miaka 10 au 20 Zanzibar imechangia nini katika muungano unaotoa ajira wanazodai
Mawazo ya Salim ndiyo waliyo nayo viongozi wengi kutoka Zanzibar
Ajira ni gharama ni wajibu kueleza mchango wa Zanzibar kabla ya kudai 'haki'
Salim anapotosha kwa kusema uwepo wa serikali 3 utasaidia ZNZ katika ajira
Ni muhimu atambue ajira za taasisi za muungano na zile zisizo za muungano zinazotoka Tanganyika au Tanzania bara zinatoa ni nyingi kuliko ajira za SMZ kwa ujumla wake
Lakini pia Salim atambue ''taasisi muungano'' kama tulivyoeleza nyuma zina mbadala znz
Hakuna sababu ya Mzanzibar kuajiriwa TFDA , HESLB, TBS, SUMATRA, MARITIME, TANESCO n.k. akidhani ni taasisi za muungano.Ikitokea ni hisani na fadhila si haki
Kwa taasisi ambazo Zanzibar imeanzisha mbadala, zile za Bara ni za watu wa bara tu
Ikitokea Mzanzibar kuajiriwa ni fadhila si haki kama Bwana Said pengine asivyoelewa
Ni wakati Wazanzibar waeleze mchango katika kuendesha muungano kabla ya madai. Tunasema hivi kwasababu 'ukiona vyaelea ujue vimeundwa'
Viongozi na waandishi kama Salim waeleze ukweli wa gharama za muungano na si kuorodhesha madai na waweze kutofautisha kati ya hisani na haki, wajibu na madai
Hakuna madai ya ZNZ yatakayobeba uzito ikiwa hayatasimama katika kuonyesha mchango wa Zanzibar katika kuendesha muungano ni upi au kiasi gani
Hiki ni chombo chenye gharama kubwa na madai yao yajengwe katika mchango
Tusemezane