Haya mambo yako wazi sana,ndio maana nakuuliza marejeo yako yapo wapi ?
Sasa hilo hulioni wewe,ila wakubwa zetu katika elimu ambao ni warithi wa mitume wamefafanua hivyo.
Na wanazuoni ni warithi wa mitume,sasa wewe ili kauli yako tuijadili,tuambie nani aliye kutangulia katika hilo.
Elimu ni amana,na amana huwa inarejeshwa kwa watu wake.
Hii kauli haibadilishi muktadha wa aya na maana yake.
Ndio nataka uniambie marejeo yako ni wapi,ili tumjadili aliye kutangulia katika hili,yeye alipita mapito gani mpaka kufikia hitimisho hilo.
Kadhia ni rahisi sana.
Nataka,nije nikujibu lile swali lako la kuhusu Wanazuoni ni kina nani.