Dunia inazungukaje?

Dunia inazungukaje?

nimekusudia hiyo aya ya Qurani.

kwa hyo unataka kuhamisha mada sio..?

Qurani ndio nimeinukuu kwanza kabla ya alfarsiy.

unataka kusemaje..?
Sihamishi mada bali nataka uwe makini na unacho kiandika na uwe unajua una andika nini.

Mada za kielimu hujadiliwa kielimu,kuanzia katika lugha mpaka marejeo.
 
Sihamishi mada bali nataka uwe makini na unacho kiandika na uwe unajua una andika nini.

Mada za kielimu hujadiliwa kielimu,kuanzia katika lugha mpaka marejeo.
wewe ndo katika wanaosema ukicheza bao ukasema nakula hapa, nasafiri ilhali umefunga unafungua sioo ?

hhaha..
 
wanachuoni wakubwa wana sifa zipi ambazo zitatufanya tuone kuwa huyu adallah saleh ni kijanachuoni kidogo...?

Kwanza kabisa unatakiwa kujua Elimu inaenda kwa kurithiwa.

Wanachuoni wakubwa wana sifa zifuatazo.

1. Kudumu katika elimu ya dini kwa muda mrefu.
2. Kuandika vitabu.
3. Kupewa ijaza kwa kutambuliwa na wanachuoni wakubwa. Yaani wewe hapo ulipo huwezi kutuambia Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni,bila kutupa kauli ya mwanachuoni mkubwa anae sema ya kuwa Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni.
4. Lazima awe anawasomesha watu dini na kuwalea katika elimu kwa muda mrefu.
5. Awe na maarifa mapana juu ya Qur'aan na Sunnah na kufata ufahamu wa wema wa walio tangulia.

Kwa uchache hizo ni sifa wanazuoni.
 
Nimeishia form four ila napenda kujua haya mambo,hivyo ukija na porojo ooh huna shule kasome utapoteza muda tu,tujadili hili suala.
Kuhusu jua na mwezi hivi bila shaka vinazunguka na nadharia yake iiko madhubuti kueleweka.lakini hii ya dunia kuzunguka imekaaje mbona inakanganya sana wadau?
Hii dunia kama inazunguka tena kwa spidi kubwa sana inakuwaje wale ambao wanatoka nje ya dunia wakirudi hurudia pale pale tu hata hawatui pengine?
Yaani muweke sisimizi kwenye tufe alafu jaalia pale alipo ndo anatoka duniani anaenda mbali katika sayari zinginee.jaalia umempaisha sasa alafu alipotoka katika anga ya dunia ile dunia(tufe)likawa linazunguka kwa spidi kali sana.umepata picha?.
Sasa je ili arudi na ile kasi ya dunia yenyewe kuzunguka naweza kutua pale pale kweli?
Hawa wanaopaa wannafanyaje mpaka wanaarudi pale pale walipotokea?
Naomba tueleweshane nipo hapa kujifunza wadau.sitaki kejelii
Mokaze
Shark
AL - ANBIYAA - 33
Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea.
YA-SIN - 39
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe
YA-SIN - 38
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
Sent using Jamii Forums mobile app
na f4 itakuwa ya masomo ya art. Kuzunguka kwa dunia zamani nilikuwa syllabus ya shule ya msingi jiografia.
 
iweke aya sio unaandika tu ukajua umejibu.

nimetaka aya ambayo imeeleza hivyo.

jibu lako sijalielewa kwa sababu hakuna aya.

nimeomba maneno matupu..?
Huko nyuma nilikwambia ya kuwa huo sio msingi katika misingi ya kutafsiri aya ya Qur'aan ndio maana nikakwambia hivi angalia mtiririko wa aya na uangalie muktadha wa aya na vipi ilivyofasiriwa.

Mathalani ukisoma sura ya 55 aya ya 33 unaweza kuniambia aya ina zungumzia wapi Duniani au Ardhini ?
 
Bado una ruka ruka,nataka unipe aya inayo onyesha Dunia inazunguka.


Hapo inaonesha utoto umekujaa, hivi wewe una umri gani??, inawezekana tunajadiliana na mtoto!!!.

Katika hiyo aya 21:33, jua na mwezi vimetajwa kwamba vinazunguka kwa kuelea katika njia yake "falakin"--- sasa dunia siku zote imeambatana na mwezi, (AU KWA UBISHI WAKO NA HILI UKATAE KWAMBA MWEZI NA DUNIA HAVIJA AMBATANA/ MWEZI NI SATELLITE YA DUNIA ), sasa kama mwezi unazunguka katika falaki ni wazi hata dunia itakuwa inaelea ikizunguka kupitia falaki hiyohiyo ya mwezi, ni jambo la akili ndogo kuweza kujua jambo hili, isitoshe usiku na mchana vimetajwa kwenye hiyo aya hapo Allah anataka tujue kwamba licha ya dunia kuogelea na kuzunguka kwenye falaki yake pia hujizungusha ndipo tunapata usiku na mchana.

Katika aya 38: 29, Allah anatunasihi kwa kusema: " Na hiki kitabu tumekutetemshia kimebarikiwa ili WAZINGATIE aya zake na wakumbushwe WENYE AKILI.

Qur'an ni kitabu cha watu wanaotumia akili.

Kstika sayansi, Nguvu za uvutano, the universal gravitation zinatii kanuni hii;-

F= GMm/r² ambapo, F ni nguvu ya uvutano kati ya vitu viwili katika suala letu ni kati ya jua na dunia iliyoambatana na mwezi., M ni mass ya jua, m ni mass ya dunia na r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, ili dunia iliyoambatana na mwezi vibakie katika falaki yao ni lazima kuwepo na balancing force/counter force hivyo basi ni lazima vizunguke /revolve along the orbit na hivyo kutengeneza counter force/ centripetal force;


F=mrw² , ambapo m ni mass ya dunia, r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, w ni angular velocity ya dunia ikiambatana na mwezi kwenye falaki yake vinapolizunga jua.

Kama kusingekuwa na hiyo conterforce basi dunia ingevutwa na jua kwa force ile pale juu kabisa na ingetumbukia kwenye jua kama kwamba jiwe umelitupia kwenye bwawa la maji, lakini kumbuka moto wa jua ni nuclear reaction, joto lake kwenye kiini ni temperatute tskriban 1,000,000 °C, hivyo dunia haiwezi kufika kwenye uso wa jua kabla haijawa mvuke.

Hiyo ndiyo sayansi kiduchu tukuhusiana na mzunguko wa dunia kuzunguka jua, kwani kuna sayansi zaidi ya hiyo.

Qur'ani ni kitabu mujarabu licha ya sisi wenyewe Waislamu kukipuuza, mtume atasema; yaa rabbi inna qaumi takhadha hadha alqur'an mahajuurah, Ewe mola wangu hakika watu wangu wameifanya hii Qur'an kitu kilichoachwa/cha kupuuzwa/kisichofaa.

Zurri unataka kuondoa uzuri wa Qur'an, labda unataka uzuri wa vitabu vingine ambao haupo utamalaki,🤣🤣
 
Huko nyuma nilikwambia ya kuwa huo sio msingi katika misingi ya kutafsiri aya ya Qur'aan ndio maana nikakwambia hivi angalia mtiririko wa aya na uangalie muktadha wa aya na vipi ilivyofasiriwa.

Mathalani ukisoma sura ya 55 aya ya 33 unaweza kuniambia aya ina zungumzia wapi Duniani au Ardhini ?
yani kwa kuwa aya zote zimetaja milima ndo unazibambanisha tu sio.

nimekuuliza tokea mwanzo je hayo mawingu yaliyotolewa mfano yatatembea siku ya kiama..?

tatizo sio kufasiri aya kwa aya tatizo je zinauhalisia.

nimekuambia nipe tafisri ya mtume mwenyewe kafaisri vipi kuondoa mgogoro mana huyo ndiye mualimu wetu.

na sahaba je ?
 
Kwanza kabisa unatakiwa kujua Elimu inaenda kwa kurithiwa.

Wanachuoni wakubwa wana sifa zifuatazo.

1. Kudumu katika elimu ya dini kwa muda mrefu.
2. Kuandika vitabu.
3. Kupewa ijaza kwa kutambuliwa na wanachuoni wakubwa. Yaani wewe hapo ulipo huwezi kutuambia Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni,bila kutupa kauli ya mwanachuoni mkubwa anae sema ya kuwa Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni.
4. Lazima awe anawasomesha watu dini na kuwalea katika elimu kwa muda mrefu.
5. Awe na maarifa mapana juu ya Qur'aan na Sunnah na kufata ufahamu wa wema wa walio tangulia.

Kwa uchache hizo ni sifa wanazuoni.
kabla ya yote naomba uniambie hasa hyo namba 3 kwa ushahidi upi au kwa mujibu wa nani..?

alafu unaporuia kusema eti awe amekubaliwa na wanachuoni wakubwa hapa ndo sifa hii ?

hao wanachuoni wakubwa wanasifa gani ?

sasa nakuliza sifa za wanazuoni wakubwa wewe unasema "lazima wawe wamekubaliwa na wanazuoni wakubwa ?

yani nakuuliza tunamjuaje mtu ambae anakula sana wewe unasema tena awe anakula sana ?

katika sifa zote ulizotaja sheikh abdallah saleh MashaAllah anazo na mema yake yanaonekana mpaka hivi kesho.

namba 3 hiyo hujatakja sifa bali umerudia neno hilo hilo..

bado hakuna mashiko ya kumtoa sheikh abdallah saleh katika wanachuoni wa africa mashariki..
 
Kwanza kabisa unatakiwa kujua Elimu inaenda kwa kurithiwa.

Wanachuoni wakubwa wana sifa zifuatazo.

1. Kudumu katika elimu ya dini kwa muda mrefu.
2. Kuandika vitabu.
3. Kupewa ijaza kwa kutambuliwa na wanachuoni wakubwa. Yaani wewe hapo ulipo huwezi kutuambia Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni,bila kutupa kauli ya mwanachuoni mkubwa anae sema ya kuwa Shaykh Abdullah Saleh ni mwanachuoni.
4. Lazima awe anawasomesha watu dini na kuwalea katika elimu kwa muda mrefu.
5. Awe na maarifa mapana juu ya Qur'aan na Sunnah na kufata ufahamu wa wema wa walio tangulia.

Kwa uchache hizo ni sifa wanazuoni.
kwani hayo maarifa mapana wewe unayapimaje ?

kwani kufasiri Qurani kunataka uwe na maarifa mapana kumbeeee...?
 
Huko nyuma nilikwambia ya kuwa huo sio msingi katika misingi ya kutafsiri aya ya Qur'aan ndio maana nikakwambia hivi angalia mtiririko wa aya na uangalie muktadha wa aya na vipi ilivyofasiriwa.

Mathalani ukisoma sura ya 55 aya ya 33 unaweza kuniambia aya ina zungumzia wapi Duniani au Ardhini ?
niambie wewe mimi sijasrma kitu kuhusu hiyo aya.

aya yetu ya 88 annaml ndo tunayoizungumzia sasa ukileta aya, ingine unataka kutoka kwenye reli.

nimetaka aya ambayo Allah anajisifia ufundi wa kuumba alafu hilo liwe linamaanisha kiyama ?

bila shaka haipo hiyo Aya.
 
Hapo inaonesha utoto umekujaa, hivi wewe una umri gani??, inawezekana tunajadiliana na mtoto!!!.

Katika hiyo aya 21:33, jua na mwezi vimetajwa kwamba vinazunguka kwa kuelea katika njia yake "falakin"--- sasa dunia siku zote imeambatana na mwezi, (AU KWA UBISHI WAKO NA HILI UKATAE KWAMBA MWEZI NA DUNIA HAVIJA AMBATANA/ MWEZI NI SATELLITE YA DUNIA ), sasa kama mwezi unazunguka katika falaki ni wazi hata dunia itakuwa inaelea ikizunguka kupitia falaki hiyohiyo ya mwezi, ni jambo la akili ndogo kuweza kujua jambo hili, isitoshe usiku na mchana vimetajwa kwenye hiyo aya hapo Allah anataka tujue kwamba licha ya dunia kuogelea na kuzunguka kwenye falaki yake pia hujizungusha ndipo tunapata usiku na mchana.

Katika aya 38: 29, Allah anatunasihi kwa kusema: " Na hiki kitabu tumekutetemshia kimebarikiwa ili WAZINGATIE aya zake na wakumbushwe WENYE AKILI.

Qur'an ni kitabu cha watu wanaotumia akili.

Kstika sayansi, Nguvu za uvutano, the universal gravitation zinatii kanuni hii;-

F= GMm/r² ambapo, F ni nguvu ya uvutano kati ya vitu viwili katika suala letu ni kati ya jua na dunia iliyoambatana na mwezi., M ni mass ya jua, m ni mass ya dunia na r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, ili dunia iliyoambatana na mwezi vibakie katika falaki yao ni lazima kuwepo na balancing force/counter force hivyo basi ni lazima vizunguke /revolve along the orbit na hivyo kutengeneza counter force/ centripetal force;


F=mrw² , ambapo m ni mass ya dunia, r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, w ni angular velocity ya dunia ikiambatana na mwezi kwenye falaki yake vinapolizunga jua.

Kama kusingekuwa na hiyo conterforce basi dunia ingevutwa na jua kwa force ile pale juu kabisa na ingetumbukia kwenye jua kama kwamba jiwe umelitupia kwenye bwawa la maji, lakini kumbuka moto wa jua ni nuclear reaction, joto lake kwenye kiini ni temperatute tskriban 1,000,000 °C, hivyo dunia haiwezi kufika kwenye uso wa jua kabla haijawa mvuke.

Hiyo ndiyo sayansi kiduchu tukuhusiana na mzunguko wa dunia kuzunguka jua, kwani kuna sayansi zaidi ya hiyo.

Qur'ani ni kitabu mujarabu licha ya sisi wenyewe Waislamu kukipuuza, mtume atasema; yaa rabbi inna qaumi takhadha hadha alqur'an mahajuurah, Ewe mola wangu hakika watu wangu wameifanya hii Qur'an kitu kilichoachwa/cha kupuuzwa/kisichofaa.

Zurri unataka kuondoa uzuri wa Qur'an, labda unataka uzuri wa vitabu vingine ambao haupo utamalaki,[emoji1787][emoji1787]
mkuu kama wa kuelewa angeelewa hii aya ambayo hata sheikh Abdallah saleh kasema kwamba dunia inszunguka..

ingemtosha Aya inayosema MILIMA INAKWENDA KAMA YANAVYOKWENDA mawingu.

anasema aya inahusu kiyama kwa mujibu wa tafsiri za wanazuoni wakati huo huo aya iko wazi imetplea mfano wa mawingu ambayo yanakwenda katika nyakati zetu ambazo sio za kiama.

kwa maana kam mfano wa mawingu kwenda ni wa nyakati hizi kabla ya kiama basi na milima kwenda ni nyakati hizi.
 
Hapo inaonesha utoto umekujaa, hivi wewe una umri gani??, inawezekana tunajadiliana na mtoto!!!.
Nakukunbusha tu,kwanza tangu jana nilikuambia unithibitishie ya kuwa Dunia inazunguka kwa mujibu wa Sayansi najua hili huliwezi na nitakuuliza pia maswali maana naona umeingia kwenye mambo ya "Universal Gravitational Force" nakuja huko,namalizia hapa kwanza. Umenukuu aya tangu jana lakini nimekuonyesha ya kuwa haionyeshi ya kuwa dunia inazunguka,lakini kwa uchache wako wa maarifa hulioni hilo na unataka kulazimisha maana ambazo hazina asili.

Utoto hausaidii,zaidi unachotakiwa ni wewe kupambana na hoja zangu na kuzojibu.
Katika hiyo aya 21:33, jua na mwezi vimetajwa kwamba vinazunguka kwa kuelea katika njia yake "falakin"--- sasa dunia siku zote imeambatana na mwezi,
Kuambatana unako dai wewe sio kweli sababu Mwezi una njia na unafata amri ya Allah,na nani amekwambia kwamba Dunia siku zote imeambatana na mwezi ? Swali kwenye njia au kwenye mwendo ?

Naendelea ....
 
(AU KWA UBISHI WAKO NA HILI UKATAE KWAMBA MWEZI NA DUNIA HAVIJA AMBATANA/ MWEZI NI SATELLITE YA DUNIA ),
Haya maneno amekwambia nani ? Na unaweza kuthibitisha ukweli wake kwa kutumia misingi gani ?

Mwezi ni huu,anasema Allah aliye juu :

5. Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na nuru, na akaupimia vituo ili mjue idadi ya miaka na hisabu. Mwenyezi Mungu hakuviumba hivyo ila kwa Haki. Anazipambanua Ishara kwa watu wanao jua. ( Yunus : 5 )

Huo ndio mwezi hayo uliyo yasema yanataka ithibati.
sasa kama mwezi unazunguka katika falaki ni wazi hata dunia itakuwa inaelea ikizunguka kupitia falaki hiyohiyo ya mwezi,
Acha uvivu toa ushahidi wa maneno haya,usileta habari za kama A ana tembea na B anatembea basi A ni sawa B. Huu ni uvivu wa kufikiri na kutumia akili vibaya.

Nani amekwambia hayo maneno na umeyapata wapi ?
isitoshe usiku na mchana vimetajwa kwenye hiyo aya hapo Allah anataka tujue kwamba licha ya dunia kuogelea na kuzunguka kwenye falaki yake pia hujizungusha ndipo tunapata usiku na mchana.

Sasa huku unakoelekea unaenda kukufuru kaka,naona unaikataa aya ya Qur'aan inavyoelzea ni namna gani usiku na mchana unapatikana.

Allah aliye juu anasema :

5. Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku. Na amefanya jua na mwezi vitumike. Kila kimojapo kinakwenda kwa kipindi kilicho wekewa. Jueni mtanabahi! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe! ( Azumar : 5 )

Hivi ndivyo usiku na mchana unavyopatikana.

Hivi hu ujinga na utoto bado uko nao,hizi tunaziota "Fitina za uongo wa Sayansi" tatizo hizi nadharia za Sayansi huwa mnashindwa kuzihoji na kujja Ukweli,sasa mimi huku nilitoka kitambo sana,sasa nipo kwenye haki,ukweli na uhalisia.

Naona najadiliana na mtu ambae Sayansi haijui wala Qur'aan haijui,nakushauri ungekomea hapo naona unazidi kukosea na kuonyesha ujinga wako wapi ulipo.

Naendelea kukufundisha sasa,maana nimeona nilikupa nafasi ya kujadiliana na mimi kimakosa,kumbe hujui mambo mengi sana.

Naendelea .....
 
Katika aya 38: 29, Allah anatunasihi kwa kusema: " Na hiki kitabu tumekutetemshia kimebarikiwa ili WAZINGATIE aya zake na wakumbushwe WENYE AKILI.

Qur'an ni kitabu cha watu wanaotumia akili.

Kwenye ufunuo ulio wazi akili haitumiki,sasa wewe Allah aliye juu ameshasema ni vipi usiku na mchana unapatikana,wewe kwa ujinga wako na ujuaji na kuvutiwa na story za wana sayansi unakuja kusema usiku na mchana unapatikana kwa dunia kuzunguka ? Hapa unakuwa unapingana na aya ya wazi na hii ni kufuru.

Tumia akili kuyafanyia kazi maandiko na ufikiri kwa usawa sio unafikiria kwa kufata nadharia za kubahatisha zilizojengeka katika misingi ya majaribio na kubadilika badilika.

Naendelea .....
 
F= GMm/r² ambapo, F ni nguvu ya uvutano kati ya vitu viwili katika suala letu ni kati ya jua na dunia iliyoambatana na mwezi., M ni mass ya jua, m ni mass ya dunia na r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, ili dunia iliyoambatana na mwezi vibakie katika falaki yao ni lazima kuwepo na balancing force/counter force hivyo basi ni lazima vizunguke /revolve along the orbit na hivyo kutengeneza counter force/ centripetal force;


F=mrw² , ambapo m ni mass ya dunia, r ni umbali kutoka katikati ya jua kuja hadi katikati ya dunia, w ni angular velocity ya dunia ikiambatana na mwezi kwenye falaki yake vinapolizunga jua.

Unajua nimehuzunika sana,mpaka nikawa nawaza huyu mtu nimjibu au nisimjibu ?

Naomba unijibu maswali yafuatayo.

1. Hivi unaweza kunithibitishia kuhusu uhalisia wa hii nadharia ?
2. Tungamo ya Dunia na Jua unaipimaje ? Yaani ili kujua uzito wa kitu unatakiwa uwe na nini ?
3. Umbali wa jua na dunia unaupataje ? Yaani ili uujue wewe umbali kutoka Ubungo mpaka Kariakoo huwa unazingatia votu gani ? Hapa nimekufafanulia tu ili ujibu swali vizuri.
4. Huyo Mwanasayansi alijuaje kama kuna nguvu ya mvutano kati ya vitu viwili hivyo na alitumia kifaa gani kujua hilo ?
5. Katikati ya jua alifikaje na kujua kwamba hapo ndipo katikati ya Jua ?
6. Katikati ya jua ni wapi na katikati ya dunia ni wapi ? Je ili kujua katikati ya viwili ni sharti uwe katika viwili hivyo au unakadiria ? Kama unakadiria ni Ukweli wa nadharia hiyo ?

Ukijibu maswali hayo,nitakuuliza mengine.

Naendelea .....
 
Kama kusingekuwa na hiyo conterforce basi dunia ingevutwa na jua kwa force ile pale juu kabisa na ingetumbukia kwenye jua kama kwamba jiwe umelitupia kwenye bwawa la maji, lakini kumbuka moto wa jua ni nuclear reaction, joto lake kwenye kiini ni temperatute tskriban 1,000,000 °C, hivyo dunia haiwezi kufika kwenye uso wa jua kabla haijawa mvuke.

Sasa umejuaje hilo wakati jambo lenyewe ni nadharia na hali hiyo ya mvutano haijawahi kutokea ?

Hivi unajuaje ukweli wa jambo ambalo halijawahi kutokea ?

Kaka utakuja kuulizwa kwanini hukuitumia akili yako vizuri.

Nani alikwambia jua lina kiini na joto ridi lake ni 1,000,000 deg C ? Walipima joto hilo kwa kutumia kifaa gani na nani alikuwa wa kwanza katika hilo ?

Kama hakuna aliyefika huko vipi ujengee hoja jambo ambalo haliwezekani ?

Haya yote unayo yanukuu ni nadharia tu,ambazo hata wao walio kuandikia haya hawawezi kuyathibisha.

Nilicho kiona kwako ni kuwa :
1. Unavutiwa sana "Story" za wana Sayansi pasi na kuhoji,na huu ni utumwa wa kujitakia na unasabbishwa na :
2. Uvivu wa kufikiri au
3. Kuwaamini sana Wana Sayansi au
4. Hujaisoma sayansi ukaielewa.

Namalizia .....
 
Zurri unataka kuondoa uzuri wa Qur'an, labda unataka uzuri wa vitabu vingine ambao haupo utamalaki,🤣🤣

Uzuri wa Qur'aan uko pale pale,na uzuri wa Qur'aan hautegemei nadharia za Sayansi kunogesha,hiki ni kitabu ambacho ni muongozo kwa watu na hakitegemei kupewa nguvu na nadharia za uongo za Wanasayansi.
Qur'ani ni kitabu mujarabu licha ya sisi wenyewe Waislamu kukipuuza, mtume atasema; yaa rabbi inna qaumi takhadha hadha alqur'an mahajuurah, Ewe mola wangu hakika watu wangu wameifanya hii Qur'an kitu kilichoachwa/cha kupuuzwa/kisichofaa.
Uwe unanukuu matini ya kiarabu au kuweka tarjama hivi unakuwa unapoteza maana ya aya,kwani unaandika kinyume na ilivyo matini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom