Kaka naomba ujibu maswali yangu tu,mbona rahisi sana.
Sasa kama ni maswali rahisi kwanini uniulize???, umenitega??🤣🤣
Sasa kaka ni mwendo wa kutegana na sio mwendo wa kuelimishana!!!, imekuwa ligi???🤣 kutafuta nani kashinda na nani kashindwa???.
Basi Umeshinda na mimi nimeshindwa. Nadhani umeridhika kaka, tuendelee na maisha.
Ila usiibeze sayansi hata kama "ilikupiga" wewe iheshimu tu, hiyo touch yako ni matokeo ya sayansi.
Kwaheri kaka, nakwenda kutafuta riziki ya watoto.
[/QUOTE]
Kwanza sijakutega,ila nimekuonyesha ya kuwa hizo nadharia mnazopewa unatakiwa uwe unazihoji na ujue ukweli wake na ujue mipaka yake.
Pili,unatakiwa usome Tafsiri za aya za Qur'aan kutoka kwa wanazuoni kabla ya kuitafsiri kwa mtindo wa kisayansi,kwani lazima ukosee. Sababu unaweza kukosea na kuifasiri kwa mtazamo wa Wanasayansi kwa kukataa maana ya kweli ya aya na kufanya hivi unakufuru kama alivyosema Shaykh Ibn Baz,alipokuwa anazungunzia ya kuwa Dunia,haizunguki kisha akasema akitokea mtu akasema ya kuwa Jua halitembei,wakati kuna aya za wazi zinazo onyesha Jua linatembea,huyo anakuwa amekufuru.
Tatu,mimi si sishindani,ndio maana huwa naweka ushahidi kisha upambanenao.
Nne,siibezi Sayansi sababu mimi ninaishi humo yaani field yangu na taaluma ysngu ni moja ya tawi la Sayansi,ila kuishi humo hakunifanyi nisihoji juu ya Sayansi,na ninacho kifanya mimi ni kuwa Sayansi ifate Qur'aan na hivi ndivyo wanazuoni wetu wanasema na ndio haki.
Tano,nilichokiona kwako ni kuwa wewe ni mshabiki na mpenzi wa Sayansi ndio maana kuna mengi huyajui hasa misingi yake ndio maana hata kuitetea unashindwa. Hili ni tatiz kubwa sana,na wanazuoni wetu husema "Ukinyimwa misingi ya elimu fulani,ni sawa na kuharamishiwa elimj hiyo,yaani kunyimwa elimu hiyo". Yaani hitaijua hakika yake.