Dunia inajua mlima Kilimanjaro upo Kenya

Dunia inajua mlima Kilimanjaro upo Kenya

Tanzania imekuwa na mikakati mingi ya kutangaza vivutio vya utalii huku pesa nyingi zikitumika, ila jambo la kushangaza bado sekata hii haijatangazika ipasavyo nje ya Tanzania. Hapa tunapaswa kujiuliza ni kipi kinasababisha vivutio vya utalii vikose mvuto ilihali bado mataifa ya nje yanaendelea kujitangaza kwa kutumia vivutio vyetu? Au tunatumia njia mbovu za kujitangaza? Au wahusika wa hiyo sekta hawawajibiki ipasavyo? Ukiangalia hapo chini utaona jinsi mapesa yalivyotumika
Waziri Nyalandu atanua na Aunty Ezekiel Marekani kwa fedha za Wizara ya Utalii
Serikali yatenga Bilioni 2.7 kutangaza utalii ndani na nje ya nchi - DEWJIBLOG
Bi. Flaviana Matata Ateuliwa Kuwa Balozi wa Kutangaza Utalii wa Tanzania Nje ya Nchi. | Ministry of Natural Resources and Tourism
Vanessa Mdee aahidi kutangaza utalii wa Tanzania | lukwangule entertainment
BODI YA UTALII TANZANIA YAZINDUA MKAKATI WA KUTANGAZA UTALII KIMATAIFA - HARAKATI ZA MTANZANIA
 
mtoa mada....hebu lete habari kamili kiongozi!hiyo habari inasemaje???maana mlima kilimanjaro unaambaa aamba mpaka pande za kenya,tatizo haupandiki ukitokea upande ule wa jirani labda yeye kafia pande hizo za kenya
images

Na wanavyouweka kwenye ndege zao pia ikoje?
 
Mimi nilijua wangu peke yao ndio hawajui kumbe hata Waafrika wenzetu hawajui. Waziri wa Wizara husika unatumbiaje? .
Kama Waziri ameshindwa basi JPM ingilia kati tumechoka onewa na Wakenya
 
2168671d3d7f1f4733ca6d0fa7c90738.jpg


Naomba tuamke watanzania katika hili binafsi sijapendezwa hata kidogo Mimi sikuwai kufuatilia hizi habari japo zilivuma sana lakini hili gazeti limenitisha kidogo, wakuu wa nchi ni vizuri kupitia na kufanya kazi.

Kama mambo yenyewe kabla ya huo muunganiko ni hivi..vipi kama tukiungana?
Mh. Rais naomba ulichungulie hili swala kwa ukaribu (kikulacho ki nguoni mwako)

Maswali ya msingi kwa watanzania;
1. Kwanini taarifa iseme Kenyan mount?
2. Je serikali ya Kenya kwa habari kama hii lini iliwahi kukanusha?
3. Je sisi kitu gani Dunia inatutambua kwa kutusisngizia kama chetu lakini sio?

Viongozi wetu kama mtaliachia hili bila kusema chochote basi watanzania tumelogwa (huo ni mtazamo wangu)
Haituhusu! Sisi tunasubiri Watalii Matajiri!
 
Kwa kawaida watanzania tuna urithi Mwingi sana kinacho tuharibu ni siasa zetu tunaziendesha kwa chuki na kupandikiziana sumu tumejaa unafiki na kuendekeza vyama vya siasa kuliko hata maendeleo .
Leo hii mtu wa chadema akimkuta mtu wa ccm Ana matatizo hawezi kumsaidia hata mtu wa ccm akimkuta wa upinzani Ana matatizo hawezi kumsaidia yaani tunafika point tunachukia mpaka nchi yetu Huyu aliyetuloga watanzania atafutwe kwa udi na uvumba
you know who fights for their country kid? damn rubes, that's who...kama unaipigania nchi nakutakia mafanikio mema, ila wajanja tushashtuka siku nyingi
 
images

Na wanavyouweka kwenye ndege zao pia ikoje?

hata ethiopia airlines na klm wameandika,kuna gesti zina majina ya miji ya marekani...new york,chicago,las vegas...haina shida hiyo sana sana tulitakiwa tuwazunguke,mfano rais angeenda(au hata mwakilishi) ktk mkutano AU kule kigali aseme anawashukuru sana majirani kenya kwa kuutangaza mlima wetu kilimanjaro katika ndege zao!wakenya ni wajanjawajanja tu sasa tulitakiwa kuutumia ujanjaujanja wao kujinufaisha nao!sisi tunalala sana
 
Tafakari, chukua Hatua !

Nani anajali Utalii ?

Tukiendelea hivi,

Ni miaka mingine mitano ya kupoteza !!
 

Attachments

  • 1468914885314.jpg
    1468914885314.jpg
    36.2 KB · Views: 44
Duh, nimeipenda hiyo...lakini sidhani kama huyo Waziri wa utalii anapitia humu JF...mimi nakushauri tafuta namba ya Wizara ya Utalii na uwapigie na ikibidi mpigie Waziri mwenyewe Prof. Maghembe au Katibu Mkuu Mj. Gen. Gaudence Milanzi...ila namwamini zaidi Maj. Gen. Milanzi anaweza akachukua hatua haraka kwa kuwaagiza vijana wake wa wizara lakini Prof. sina hakika naye...
Yaani kama Hao mawaziri hawapo humu basi tunatwanga maji kwenye kinu Hao wanao itwa wasaidizi hawafikishagi hizi taarifa yaani ni bure kabisa
 
hata ethiopia airlines na klm wameandika,kuna gesti zina majina ya miji ya marekani...new york,chicago,las vegas...haina shida hiyo sana sana tulitakiwa tuwazunguke,mfano rais angeenda(au hata mwakilishi) ktk mkutano AU kule kigali aseme anawashukuru sana majirani kenya kwa kuutangaza mlima wetu kilimanjaro katika ndege zao!wakenya ni wajanjawajanja tu sasa tulitakiwa kuutumia ujanjaujanja wao kujinufaisha nao!sisi tunalala sana
Bado tumelala
 
Back
Top Bottom