Dunia inajua mlima Kilimanjaro upo Kenya

Correction: South Africa-Climber Dies story

2e111d17d2034977bf3c83f84c8bc757.jpg

JOHANNESBURG (AP) — In a story July 18 about a South African climber dying while trying to summit Mount Kilimanjaro, The Associated Press reported erroneously that the mountain is in Kenya. It is in Tanzania.
 
Haa Hao Watahangaika Kusema Upo Kenya Sijui Nchi Gani Ila Ukweli Ni Tanzania Itabaki Hivyo Nakuna Namna Wapigwe Tu Kwa Kufanya Usahihi Wa Habari
 
Tuzubae mara ngapi... Kwan kuna kiongozi wetu hata mmoja aliewahi kusimama na kusema kua hilo ni uongo.. Wapi waziri/wizara ya maliasili na utalii.. Au hizo post za wakenya huwa hawazioni, je wakenya wanavotangaza kua mt kmnjaro upo kenya viongoz wetu hawajui.
Hii nchi alieturoga mbona kashakufa muda mrefu
 
Vitu na mali zote za nchi yetu vitarudi na kujulikana ni vya Tanzania. Tuipe muda serikali ya awamu ya tano na mabalozi wetu nje ya nchi waitangaze nchi kweli huko marekani ni wachache wanao ijua Tanzania. Mabalozi Wafanye kazi ya ziada kwani wasingoji ujio wa viongozi wetu ndio wajitutumue.
 
Una uhakika kwamba wanapandia Kenya ? Njia gani wanaitumia ? Naomba kueleweshwa tafadhali
Kama ulikuwa hujui, ni kwamba watalii wengi wanaopanda mlima kilimanjaro wengi wao huwa break ya kwanza wanafanya utalii huko Kenya halafu ndo wanakuja Tanzania kupanda mlima kilimanjaro kwa sababu wenzetu wakenya wanautangaza sana huu mlima kuliko sisi ingawa huwa hawasemi upo kwao bali huwa wanasema mlima mrefu kuliko zote Africa upo urefu mdogo kutoka mbuga zao, na hii ni kweli, kumbuka sio kila mtu anaijua geography ya Africa, mfano mzuri mwingine kwa hapa Tanzania ni mbuga ya serengeti ambayo ipo mkoa wa Mara, lakini watalii wengi ukiwauliza watakwambia ipo mkoa wa Arusha kwa sababu watalii wengi wanakwenda serengeti kupitia mkoa Arusha lakini hii haiondoi uhalisia kuwa mbuga ya serengeti ipo mkoa wa Mara. Kwa haya maelezo nahisi utakuwa umeelewa neno "kupitia" nadhani hili ndilo neno lililokuchanganya zaidi ukadhani nimeandika "wanapandia" Kenya
 
Watendaji wetu hawasomagi hizi, wanaweza chukua hata mwezi mzima hawajarespond.
Hii ilitakiwa iwe imeshakemewa kwa kelele za hali ya juu.
Imagine mpo kwenye umati wa watu hawafu MC anamtambulisha wife wako kwamba ni mke wa mtu mwingine??????
Halafu wewe unachekelea!!!!
Kisha unasema "akipendwa au asipopendwa" mimi naishi. Kwi kwi kwi
 
Kama ulikuwa hujui, ni kwamba watalii wengi wanaopanda mlima kilimanjaro wengi wao huwa break ya kwanza wanafanya utalii huko Kenya halafu ndo wanakuja Tanzania kupanda mlima kilimanjaro kwa sababu wenzetu wakenya wanautangaza sana huu mlima kuliko sisi ingawa huwa hawasemi upo kwao bali huwa wanasema mlima mrefu kuliko zote Africa upo urefu mdogo kutoka mbuga zao, na hii ni kweli, kumbuka sio kila mtu anaijua geography ya Africa, mfano mzuri mwingine kwa hapa Tanzania ni mbuga ya serengeti ambayo ipo mkoa wa Mara, lakini watalii wengi ukiwauliza watakwambia ipo mkoa wa Arusha kwa sababu watalii wengi wanakwenda serengeti kupitia mkoa Arusha lakini hii haiondoi uhalisia kuwa mbuga ya serengeti ipo mkoa wa Mara. Kwa haya maelezo nahisi utakuwa umeelewa neno "kupitia" nadhani hili ndilo neno lililokuchanganya zaidi ukadhani nimeandika "wanapandia" Kenya
Kwa hilo nakubaliana na wewe, wengi hutokea huko ila nilidhani nao pia wanapandisha kule
 
Board ya Utalii ni kama haipo maana haya matatizo ya kushindwa kutangaza utalii wa nchi yetu yamelalamikiwa muda mrefu. Nilichukua nakiona ni board kufanya vikao nje ya nchi na kujinufaisha wao tu na sio nchi. Kwenye utalii kunahitaji Mkono wa raisi kuleta mabadiliko na sio waziri. Sasa kazi tu.
 
Hivi kweli Tanzania itaendelea kulifumbia macho hili swala mpaka lini? Inatia aibu sana tena sana tu serikali ina tubana kwenye kodi alafu maswala nyeti kama haya ambayo ndio yana changia pato kubwa kwenye uchumi wetu ndio yana puzwa.
 
Sie yetu maneno tu, siku wakisema kiswahili ni cha kenya utaona tutakavyotokwa povu, kanga na bakora mkononi kwenda kuwa suta.
 
Na hamu kweli kweli mzee wa "SPENDED" aandike barua kwenda AP kuomba wa ombe msamaha na kusahihisha taarifa hii
 
Watanzania tumeegemea siasa tumesahau vingine vyote vya muhimu.hivi tutakua hivi mpaka lini, mawaziri wanaohusika kimya si watumbuliwe?
 
Yaani nikua nimejipanga nikagawe dose huko mtandaoni kufungua nimekuta wamecorrect wana bahati sana ilikua nimuwashie moto huyo muandishi hatari.
 
Back
Top Bottom