Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

Dr. Slaa aomba ukimbizi Canada

maneno yote aliyosema Gwajima dhidi ya Slaa kumbe ni kweli tupu- cheza na wote lakini usicheze na mtumishi wa mungu
 
Aiseee anajiandaa kuanzisha chama chake? He he he mazito haya, kwanini asirudi CCM tu maana kadi anayo amsaidie magufuli,
msaada wake ni kwa ajili ya ustawi wa Taifa Hili.... Ww subiri kolabo ya Prof Lipu na Dk Bastola ujue kuwa kinachofanywa ni hatari na hakuna anayeweza kukizuia
 
Ukiona mtu Mzee ambae aliwahi kupata mafanikio na amani hapo kabla, na sasa anaishi maisha yake ya uzee katika hali ya mahangaiko pasipo na amani basi basi jua huyo mzee ana LAANA.
 
baadhi ya vyombo vya habari vya hapa nchini siyo vya kuamini au vya kuttumia kama source wengine hawana weledi hata kidogo wa uandishi bali wa be driven na wanasiasa. hapa nchini naona gazeti moja tu anagalau linajitaidi kuandika RAIA MWEMA
Naona unakariri tu...RAIA MWEMA nalo ni Gazeti..!! lina tofauti gani na Mzalendo
 
Chezea Ccm wenye,Washamtumia na kumdampo.Sasa anaona aibu mke keshakula nyumba.Afadhali apotelee huko huko maisha yake yote.
Watanzania hawamwitaji tena.

Mungu mkubwa, mwaka jana muda kama huu mlikuwa mnampamba kwa mapambio hatare leo mtu akisoma post zenu anaweza zimia kama hawajui vile, manake msala na jumba bovu mnatupia watu wengine. Raisi wa mioyo yenu leo amekuwa si lolote. Tulikuwa tunawaambia siasa hazifiki mbali mlituangushia kila aina ya matusi leo. Ndio wengine wanaagiza popcorn tu wala hawathubutu kuwa jibu. Ila nyie nouma
 
Mwanangu Dr. Slaa cyo level yako hata mwk. wako taifa analijuwa hilo.
Nandiyo maana hadi leo chama hakijapata katibu mkuu hata wa kumsogelea kwa asilimia 6% tu hajapatikana cdm. Ni Mungu amempa uwezo huo na simwingine ni mungu wake.
Na kwalevo ya Dr awezi kuja cdm kuomba msamaa huyu jamaa anamisimamo sana, nadiyo maana kasema choo kime jaa mavi yamepakuliwa na kuletwa chumbani, leo ishajionyesha.




Nyinyi ndiyo mliomfanya leo hii awe mkimbizi,hivi mlishindwa kumshauri kabla ya kuchukua mke wa mtu amchunguze huyo mke kama ni asset au liability?
 
Bila shaka Dr. Slaa anaelewa michezo inayochezwa. Itakuwa ajabu kama hajui kile kinachoitwa "siasa ni mchezo mchafu" ni nini hasa. Kuhusu CDM sioni itapata faida gani kutishia uhai wake labda kama chama kina zero intelligence. Nachoona ni wale "waliommiliki" Dr. na kumfadhili wakati akiigeuka CDM, kuhamia Serena hotel na kuzungukia vyombo vya habari kuiponda CDM na Lowasa ndio wenye manufaa makubwa kwa kifo au kudhurika kwake kimwili. Faida kuu mbili ni, kwanza, kuwaaminisha watu kuwa ni "maadui wake wapya: CDM na Lowasa ndio wamefanya hivyo. Pili, ni "kumzima" asijeropoka yasiyotakiwa baada ya kumaliza kumtumia. Dr. anatakiwa kutumia intelligence yake vizuri sana katika hilo.

Kosa kubwa alilofanya Dr. ni kutotumia busara alipopewa tenda na watu wenye nia mbaya na "mikono michafu" waliotaka kuhujumu upinzani na kummaliza adui yao Lowasa. Yeye alimuona tu adui/"fisadi" Lowasa na kukerwa na CDM kumteua kuwa mgombea. LAKINI hakuona uovu na malengo batili ya waliompa tenda. Shortsightedness. Alitakiwa aone kuwa hawa ni watumia fursa tu; watu wa mikakati; kwamba ikibidi wanaweza "kumzima" waliyemtumia asije akaleta nuksi baadaye. He should be more smart on these kinds of moves. Jazba haitakiwi kabisa.

Siamini kama suala la nyumba ndilo linamkimbiza. Kama ilivyosemwa huko nyuma, alipewa mshiko wa kutakata. Labda kama wenye kusema hivyo wana"enjoy" kumsanifu tu. Nahisi amepoteza mwelekeo wa maisha na kushindwa kuona ni vipi atarejea kuishi Tz baada ya yote yaliyotokea. Labda pia mwisho wa visa umefika. Hivyo inabidi aombe uraia kwenye nchi yenye uwezekano mkubwa wa kupata. Huyu ni mtu aliyezoea harakati na mazingira ya Tz. Sijui ataweza vipi kuishi nje permanently.

Naamini kwa Sana adui mkubwa wa Slaa ni ccm kuliko chadema
Chadema kwa Sana Slaa sio ishu Tena ...alishawaumiza kwa namna flan na uchaguzi is over ....Ila ccm wanna hasira kwa Sababu project Slaa haikufanikiwa ...Pengine kwa mikakati mobovu ya handlers wenyewe ....Ila Sheria ya kutimika ni kutupwa au kuuliwa Kama ukishindwa au hata some extent ukifanikiwa Ili usiseme kweli .....na dr Slaa Kama msomi anajuwa Hilo
Scerio kama ya Sasa ambako Lipumba anawabip CuF ...sidhani Kama kwa dr Slaa itatakiwa kwa kuwa yeye ndio alikuwa target
 
L
Habari za kutoka magazetini leo asubuhi itv zimesema kuwa Dr. Slaa ameomba ukimbizi huko Canada kwa madai kuwa maisha yake yamo hatarini Tanzania!

Swali: Ni nani huyo anayetishia uhai wa Dr.Slaa?
LOWASA
 
Inawezekana kweli mahana bila yeye ccm wasingeshinda kizembe kama vile.
 
Hihihiiii mtaalamu wa saikolojia alione hili.
DuppyConqueror
Sasa mtaalam wa psychology tena akahudumiwe na wataalam wengine? Ama kweli mganga hajigangi!! Mzee wa watu mafuta ya Chrisma yanamtesa maskini!! Kazee kanaona aibu kurudi Tz kataweka wapi uso wa kenyewe huku Lowassa kaliyemsema ni liability anaendelea kunawiri tu huku UKAWA ikiingiza mjengoni wabunge lukuki na kushika majiji karibia yote!!
 
Kwanza huku wana UKAWA wengi wanamuonea huruma
alivyoingizwa mkenge na Magufuli

Sasa watu wanao kuonea huruma wataku dhuru vipi?
Hata mimi mwana CCM namwonea huruma sana Dk Slaa sikutegemea maisha yake yatasinyaa kiasi cha kuanza kukimbia kimbia kuomba nchi ya kuishi ndani ya muda mfupi kiasi hiki, nawaombeni tumuombee!!

Na kama Magufuli kuna alichomwahidi angemtekelezea padre wake hakuwajua wanasiasa alidhani ni wachungaji wenzie.
 
Haka sio kampango kama kale ka gavana wa kipindi kileeeeee aliekufa bila mazishi
 
Duuuu,ndio maana kuna watu walikuwa wanasisitiza kuna maisha baada ya uchaguzi
 
Back
Top Bottom